YODAE

YODAE YODAE ni kifupi watumishi Yusufu, Yoshua, Daniel na rafikize, Eliya, Elisha, Esta na Mjombae. YODAE ipo kwa wakristo kuishi maisha Matakatifu ya Ushindi

Nikiyatazama maendeleo ya teknolojia naogopa mnoChangamoto ya ukosefu wa ajira itakuwa kubwa zaidi sababu ya kazi nyingi...
05/01/2026

Nikiyatazama maendeleo ya teknolojia naogopa mno

Changamoto ya ukosefu wa ajira itakuwa kubwa zaidi sababu ya kazi nyingi kuchukuliwa na AI..hata kazi za ndani tu Sasa zinachukukiwa na mashine nyingi ndogondogo za kufua, kupika, kufanya usafi n.k SEMBUSE KAZI ZA KITAALAMU ambazo mifuko inaendana nazo zaidi?

Changamoto ya usalama kutokana na kuongezeka kwa zana nyingi zenye kuweza kukata vitu kwa haraka mfano cordless chainsaw, grinder n.k matumizi ya drone yanavuka vizuizi vikubwa.

Kukupa kwa vyakula bandia; vyakula vilivyolazimishwa kukuzwa k**a kuku, matunda mengi k**a vile matikiti, nyanya, mahindi, maparachichi, mbogamboga n.k

Kuongezeka kwa bidhaa feki; teknolojia inarahusisha kunakili(kucopy bidhaa) siku hizi Leo toleo Bora la bidhaa fulanj kesho unakuta toleo lenye muonekano uleule lakini sio halisi.

Elimu bandia; kutakuwa na elimu iliyopatikana mitandaoni lakini ikiwa k**a halisi! Walimu na wanafunzi watategemea sana AI kupata taarifa na maarifa .

Mwisho lakini si kwa umuhimu PICHA, VIDEO NA SAUTI si ushahidi wa uhakika Tena kwa sababu watu wanaweza kubuni.

Nitaendelea kuwakumbusha athari mbaya kabisa ya teknolojia.

Jenerali
Safarini

CHUKI=====Leo nahitaji kuwashirisha kuhusu  . Tukiangazia maana ya chuki ni hisia zinazohusisha kutopenda kitu, Jambo au...
31/03/2024

CHUKI
=====
Leo nahitaji kuwashirisha kuhusu .
Tukiangazia maana ya chuki ni hisia zinazohusisha kutopenda kitu, Jambo au mtu. Chuki ni kinyume cha upendo.

Historia ya chuki;
----------------------------
Chuki ina historia ndefu mno kwani Kwa mara ya kwanza imeonekana wakati dunia ikiwa na watu 4 Tu. Mwanzo 4:6-8
[6]BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
[7]K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
[8]Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua.
Biblia inayoonyesha chuki ilianza lini na watu wakiwa wangapi, TAFAKARI KIDOGO walikuwa watu 4 Tu duniani yaani hata wangewana hii dunia kila mmoja angepata robo LAKINI bado chuki ikajipenyeza

Nini chanzo cha chuki
-------------------------------------
Chuki ina vyanzo vingi lakini kibali ni chanzo kikubwa maana hata chuki ilipoonekana Kwa mara ya kwanza chanzo Ilikuwa kibali. Chuki ya Esau Kwa Yakobo ni Kibali, chuki ya Wana wa Yakobo kwa Yusufu Ilikuwa ni KIBALI
Chuki ni kinyume cha upendo hivyo sababu zozote zinazosababisha upendo zikiondoka ndio sababu za chuki.
Hata ukiona watu wanachukiana sababu ya mapenzi ujue mmoja kapata kibali mwingine makosa.
Vyanzo vingine vya chuki ni kutofahamiana vema; usipomfahamu mtu vizuri ni rahisi kujenga chuki ikiwa atakuwa na matendo usiyoyapenda lakini ukimfahamu utatumia nafasi hiyo kubaini sababu ya matendo hayo
wivu; mtu kumwonea wivu mtu mwingine huzalisha chuki
Uzushi; hii hutokea pale mtu anasikiliza maneno ya uzushi juu ya mtu mfano anaambiwa Jenerali ni mwizi. Basi mtu atamchukia Jenerali Kwa sababu amesikia ni mwizi.
Itikadi Kali za kiimani; mtu atamchukia mtu Kwa sababu tu haamini juu ya kile anachokiamini mfano wazee wa Mila kuwachukia wakristo sababu T
tu hawashiriki sehemu ya Mila zao. Na mkristo anamchukia mzee wa Mila Kwa sababu zilezile.
PAmoja na vyanzo tajwa vya chuki pia chuki hutakuwa vizuri kwenye UNAFIKI Na hutekelezwa Kwa unahisi Kwa HILA

CHUKI HUFANYWA NA NANI?
-----------------------------------------------
Chuki hufanywa na binadamu yeyote; chuki haichagui kimo, unasaba, rangi, ushirika WA kazi n.k
WATU WENGI HUFIKIRI CHUKI INAPASWA KUFANYA NA MTU WA MBALI KWA MTU KINASABA, KIDINI, KIELIMU N.K huu ni upotoshaji mkubwa kwani tumeona chuki ilianzia Kwa binadamu wenye unasahau wa damu na walikuwa 4 Tu.

Chuki huweza kutokea katika familia, shuleni, mahali pa kazi, mahali pa ibada na kadhalika.
Chuki haichagui kitu chochote Bali yenyewe hufuata tu maandalio ya moyo.

Hivyo basi tufahamu chuki hutokea popote na mara nyingine bila sababu yoyote. Ukiona unachukiwa mshukuru Mungu kwamba kumbe wewe ni binadamu na umezungumwa na binadamu.
Watu wengi wanaweza kuvumia chuki bali wanaochukiwa na ndugu zao na marafiki wa karibu huumia mno. Hata biblia haijawa kimya juu ya chuki kwa watu wa nyumbani 1 Timotheo 5:8;
[8]Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.
Na ndio sababu nimeona tushirikishane.

Chuki ina athari mbaya na za kidumu. Kwanza Sigmund Freud anasema chanzo cha migogoro yote duniani ni mapenzi. Mapenzi hayawezi kuleta ugomvi isipokuwa inapozalishwa chuki.

Hata migogoro inayosababishwa na mivutano ya KIDINI bado dini imekuwa mwamvuli tu, kwani ikiwa Mimi ni mkristo nikahubiri Injili yangu Safi watu wasikubaliane nami kuna sababu gani ya kuwachukia hata kupigana??? Jibu ni chuki ni hulka ya binadamu. CHUKI ILIZALIWA KABLA YA UYAHUDI UKRISTO NA UISLAMU, CHUKI ILIZALIWA KABLA YA UWEPO WA MADOLA DUNIANI YAANI KABLA YA UWEPO WA MIPAKA YA NCHI NA WAFALME WAKE.

Ukiona rafiki yako anakuchukia mkumbuke Yesu akivyosalitiwa na Yuda
Ikiwa ndugu zako basi jua chuki Kwa ndugu ilianzia kwenye Eden.
Binadamu ndio sababu ya chuki hivyo tunalazimika kila mmoja kushinda chuki na uruhusu upendo utawale..

Mwl Kapagi

  na Aina zakeUpendo ni hisia za ndani za kumgusa, kumjali kuathirina kumpenda mtu au kitu. Kwanini tujifunze Aina za up...
14/02/2023

na Aina zake
Upendo ni hisia za ndani za kumgusa, kumjali kuathiri
na kumpenda mtu au kitu.
Kwanini tujifunze Aina za upendo kanisa! Hii ni Kwa sababu Kwanza upendo ndio lugha ya biblia/agano. Mungu aliupenda ulimwengu akamtoa mwanae, mwana kukubali ukihitaji Upendo, wafuasi kumfuata Yesu inahitaji upendo, na Bwana Yesu kuwapokea wafuasi wake inahitaji upendo. Yoh 3:16
Upendo ndio umeliathiri kanisa Kwa chanya na hasi, kanisa limethiriwa vibaya na upendo Kwa waamini kushinda kutofautisha Aina za upendo, sababu za upendo na mazingira ya upendo.

1. AGAPE ( charity or unconditional love)

Ni Upendo wa ukarimu na usiokuwa na masharti, Upendo wa kujitolea bure bila kutegemea faida.
️Ni Aina ya upendo wa kiroho Kwa Kristo ndiye wa Kwanza kuonyesha upendo huu yalijitoa kufa ili tuweze kupata ondoleo la dhambi zetu, aliteswa kwa ajili yetu .
Yohana 3:16

2. EROS (Sexual love)
Eros ni Upendo unaohusishwa na tamaa ya mapenzi ya kingono, kijinsia, kimwili. Ni Upendo wenye shauku na hamu ya kingono. Mifano ya upendo huu ni Kwa Daudi Kwa Mkewe Uria alipokuwa anaoga (2sam 11:2-4 )na pia mwanae Amnoni alipofanya mapenzi na Dada yake Tamari. (Soma 2 Samweli 13) Sulemani ndiye mwathirika Sana wa upendo huu hata akaoa wanawake wengi na kuimba nyimbo nzuri za mapenzi hasa wimbo ulio Bora.Wimbo Ulio Bora 1:15
Tazama, u mzuri, mpenzi wangu,
U mzuri, macho yako ni k**a ya hua.
Chanzo kikubwa cha migogoro duniani ni upendo huu. Uimara na udhaifu wa kanisa na Imani unaathiriwa na upendo huu. Familia nyingi zinaegemea upendo huu. Upendo huu Una nguvu ya kujenga na kubomoa. Hata majasusi wanatumia upendo huu kushinda mipango Yao. Licha ya kwamba unapigwa kupuo na kanisa lakini ni muhimu mno kufanywa kuwa mjadala wa muhimu kila mara.
3. PRAGMA
️ Ni Aina ya upendo ambao unatokana na kudumu pamoja na kuaminiana katika jukumu moja. Pia ni upendo unaochochewa na kuaminiana Kwa muda mrefu pamoja na kuvumiliana. Upendo huu unaweza kuwa baina ya watu 2, mtu na watu n.k. lakini mara nyingi umeonekana mahali pa kazi, kanisani, machimboni na shuleni( watumishi au wanafunzi wakikaa muda mrefu huishi Kwa upendo mkubwa kuliko ndugu) mdo 2:43-47
Pia upendo huu inaonyeshwa na Yakobo alipomtumikia Laban miaka Saba ili ampate Raheli. Mwanzo 29: 15-30.
Ukweli ni kuwa Eros amejiweka jirani zaidi na upendo huu, ukikosea kidogo Tu yeye anaingia. Na vijana wengi wamepotezwa na upendo huu kwani wanashindwa kuvumiliana.

4. Philia. (Friendship love)
Ni aina ya upendo wa kirafiki. Wagiriki waliamini kuwa Aina hii ya upendo huwa haina mvutano wa shauku ya kimwili K**a ilivyo kwa Romantic love (eros).
Mifano mikubwa ya upendo huu ni
i. upendo wa Yonathan na Daudi, Biblia Inasema Yonathan alimpenda Daudi K**a anavyoipenda Roho yake mwenyewe. (1 Samweli 18- 20)
ii. Daniel, Shadraka, Meshaki na Abdnego Dan 2:17

5. STORGE (Family love)
Ni aina ya upendo wa kindugu au familia. Ni upendo wa mzazi kwa Mtoto. Pia inaweza kuwa ndugu na ndugu. Upendo unakuwa na nguvu wenye nasaba. Sababu kuu ya upendo huu ni undugu na ikiwa undugu ukavunjika Kwa sababu yoyote pia upendo utavunjika. Upendo wa Yusufu kwa ndugu zake (Mwanzo 45: 1-15)
ni mfano mkubwa wa upendo huu. Wakati mwingine upendo huu unaweza kutumika vibaya sababu unakuwa na chembechembe za ubaguzi mfano wa Isaka na Rebeka Kwa watoto wao Esau na Yakobo. Mwanzo 25:28
Basi Isaka akampenda Esau, kwa sababu alikula mawindo yake, na Rebeka akampenda Yakobo.
Wazazi wabaguzi ni chanzo cha migogoro katika familia
Kwenye Aina zote za upendo Eros ni backbencher wakati wote anategea makosa ajiingize
Mwl Kapagi

WEWE NI MTI KANDO YA VIJITO VYA MAJI.++++++++++++++++++++++++++++ZABURI 1Mst 3 " Naye atakuwa k**a mti uliopandwa kandok...
06/06/2021

WEWE NI MTI KANDO YA VIJITO VYA MAJI.
++++++++++++++++++++++++++++
ZABURI 1
Mst 3 " Naye atakuwa k**a mti uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, wala jani lake halinyauki, na kila alitendalo litafanikiwa."
Bwana yesu asifiwe eeh upendwaye sana.
Mwimba Zaburi anasema Mtu anayeitafakari sheria ya Bwana, na si kutafakari tu bali inampendeza. Sheria mama ya Bwana ni neno lake takatifu. Unapokuwa mkristo ni lazima uwe mfuasi wa neno kwa kuwa uliitwa na kufanywa mkristo kwa neno, tunaokolewa kwa neno na is kwa hadithi nyinginezo.
Kabla hatujaona nini kinatokea baada ya kutafakari na kupendezwa na neno la Mungu ni vema tukaangalia tofauti ya mti ulio kandokando ya vijito vya maji na ulio nje kabisa ya maji.
Nenda Moshi, Mbeya hasa Rungwe, Iringa, na Kule kanda ya ziwa utakutana na kijani kibichi majira yote kwa sababu miti inapata maji na chakula wakati wote. Ukitembelea Dodoma utakuona mimea imekauka hata majira mvua haina kitu.
Mpenzi kuitafakari sheria ya Bwana kunakufanya upate mahitaji yako wakati wote wa uhitaji, kutafakari neno ni kumkaribia Bwana yesu ambaye ni maji ya uzima nasi ni matawi kwake. Anatupatia maji na chakula kwa wakati.
Kwanini unafadhaika k**a mti wa jangwani? Mbona huna matunda yoyote katika kazi yako, katika masomo yako, katika biashara zako? huna matunda k**a mti ulio mbali na vijito vya maji.
Mkaribie leo Bwana yesu kwa neno lake, mwendee kwa hoja takatifu yeye ni maji ya uzima atakujazi kwa kila hitaji lako.
Ni maombi yangu usiku huu Bwana aikumbuke bidii yako katika wokovu hatimaye uzae matunda katika huduma, kazi yako, biashara yako, masomo yako n.k
KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, AMENI

TUNAISHI KWA Imani++++++++++++++MWL. KAPAGI. P.KEBRANIA 10:38-39Mst 38 “lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye...
06/06/2021

TUNAISHI KWA Imani
++++++++++++++
MWL. KAPAGI. P.K

EBRANIA 10:38-39

Mst 38 “lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisitasita, roho yangu haina furaha naye.”

39 “Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu.”

Bwana Yesu asifiwe,
Mpendwa ulipokubali kumkiri Yesu Kristo kuwa Bwana mwokozi wa maisha yako moja kwa moja uliingia katika kundi la wenye haki wake na kwamba unaweza kurithi kutoka kwake. Wewe ni mwenye haki tena ni mshindi kwa kuwa yeye mwenye aliushinda ulimwengu.

Haleluya….
Bwana aliyetukomboa anasema mwenye haki wake ataishi kwa imani, maana yake pasipo imani hataweza kuishi…unajua kwanini? Kwa kuwa aliitwa kwa imani hiyo hivyo kujitenga na imani ni kujitenga na Kristo. Na huyo mwenye haki akionekana kusitasita Bwana hana furaha naye.
Elewa katika famila mtoto ambaye hana uhakika na haki zake katika familia itakuwa vigumu kwake kusogelea urithi, itakuwa ngumu kwake kuomba haki zake…wakati wenzake watakuwa wakifurahia mali za familia yeye atakuwa mwenye huzuni kwa maana amejitenga kwa wasiwasi wake juu ya haki yake katika familia yake.
Bwana hana furaha na mtu mwenye kusitasita kwa kuwa hataweza kuzirithi Baraka za Kristo, hataweza kuingia mbinguni, hataweza kushuhudia matendo makuu ya Mungu kwa kuwa tu hana imani thabiti.

Mwisho Biblia inasema lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea (baada ya kusita ni kupotea), bali miongoni mwao walio na imani na si imani tu bali ya kutuokoa roho zetu.

Nakusihi eeh mpendwa tena upendwae sana Bwana amekufunilia siri hii uimarishe imani yako k**a mwenye haki ili upate kurithi haki zako kwa Bwana, urithi Baraka, uzima na matendo makuu ya Mungu.

Nakutakia Jumapili ya ushindi, iwe siku ya kuimarisha imani yako, imani yako isiwe na mashaka tena na Kristo.

Soma hii
22/12/2019

Soma hii

"Kabla ya kubadilika ni lazima uchukue jukumu kamili kwa tabia yako. Acha kutoa vijisababu. Acha kulaumu wengine. Hiyo ni sehemu ndogo ya mabadiliko ambayo Mungu anafanya kupitia kwako." Joyce

KUONESHA UPENDO................................Kuna namna nying watu huonesha upendo wao kwa wawapendao.....Leo nimegund...
01/03/2018

KUONESHA UPENDO................................
Kuna namna nying watu huonesha upendo wao kwa wawapendao.....Leo nimegundua upendo wa kweli huonekana kwa "KUTOA"... Yoh 3;16.Yesu alitolewa kuwa sadaka kwaajili dhambi zetu.upendo ulimgharimu ajitoe afe ili atutoe katika utwamwa wa dhambi..

Kiwango unachojitoa kwa muda,Mali,mawazo,maneno yako, kutumia vipaji,maombi nk. kwaajili ya Mungu kitaonesha ni kwa kiasi gani unampenda Mungu.lakini pia hata huyo unaempenda aaaa.............
Tunaweza kujipima Leo ,Mara nyingi tunaweza KUTOA kipaumbele ktk tuvipendavyo au tuwapendao

Tutawashirikisha hisia na mawazo,mipango na maono yetu na mengine..Toa kipaumbele chako kwa Mungu hutajuta.....mshirikishe yooooooote ,hata unalowaza sasa hiv atakushauri na kukuonesha njia utakayoiendea............."..MUNGU NI PENDO"

Lakini yeye aijua njia niendeayo;Akisha kunijaribu, nitatoka k**a dhahabu.Ayubu 23:10
06/09/2017

Lakini yeye aijua njia niendeayo;Akisha kunijaribu, nitatoka k**a dhahabu.
Ayubu 23:10

Katika mipango yote midogo kwa mikubwa mtegemee Mungu... Mtangulize yeye!!! Wakati unapopuuza kumshirikisha Mungu ama ku...
06/09/2017

Katika mipango yote midogo kwa mikubwa mtegemee Mungu... Mtangulize yeye!!! Wakati unapopuuza kumshirikisha Mungu ama kutokana na udogo wa jambo au uwezo wako wa kulikabili ndio wakati anaotumia Ibilisi kukwamisha na kukurudisha nyuma!!!

Katika mambo yote yanayokupata Mungu akishirikishwa, kila kitu kinakaa sawa!!! Katika dhiki na shida Mungu anajua!!! Katika kulala mapangoni, kukimbizana, kukosa utulivu na Amani MUNGU ANAJUA, ANAJUA MPANGO WAKE KWAKO!!

Yeremea 29:11(naisimamia tangu nilipoitwa) inasema 'Nayajua mawazo niwawaziayo ninyi, ni mawazo ya amani wala si mabaya, ili kukupa tumaini siku zenu za mwisho.

Usipuuze Mungu ana nguvu mno, kuna wakati unabanwa kweli ukihisi umeachwa hapana katika huo uchochoro na mkwamo Mungu anautumia kwa mpango... Ana kuchelewesha kidogo ili ufike Salama na kwa mafanikio

Nakutakia Maisha ya Ushindi
Jenerali Kapagi

Address

0685306666
Kilwa

Telephone

+255685306666

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when YODAE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to YODAE:

Share