26/01/2026
SOMO: ONYO – ACHA KIBURI NDUGU YANGU
Neno la Mungu linatupenda sana, ndiyo maana halinyamazi tunapoishi katika dhambi. Mungu hataki mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba ya kweli. Kiburi kimekuwa chanzo kikubwa cha watu wengi kuendelea kukaa kwenye dhambi wakijifariji kuwa “Mungu ni mwenye rehema” pasipo kuacha maovu yao.
Biblia inasema:
“Mungu huwapinga wenye kiburi, bali huwapa neema wanyenyekevu.” (Yakobo 4:6)
1. Kiburi humfanya mtu akatae onyo
Mtu mwenye kiburi hasikii, hashauriki, na haonywi. Anapoambiwa ukweli, huchukia badala ya kutubu. Ndiyo maana watu wengi wanaendelea kuishi katika:
Uzinzi
Uongo
Uasherati
Usagaji
Ushoga
na dhambi nyinginezo
Wanasema: “Huo ni wakati wa sasa” au “Kila mtu anaishi hivyo”
Lakini Neno la Mungu halibadiliki.
“Ole wao waitao uovu wema, na wema uovu.” (Isaya 5:20)
2. Mungu anaongea wazi kuhusu dhambi
Biblia haisemi kwa siri, inasema waziwazi.
“Msidanganyike; waasherati, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala watu waliolainika, wala walawiti, hawataurithi ufalme wa Mungu.”
(1 Wakorintho 6:9–10)
Hili si tusi, hili ni ONYO LA UPENDO. Mungu anakupa nafasi leo uache dhambi kabla ya hukumu haijafika.
3. Toba ya kweli ndiyo njia pekee
Toba si kusema “samahani” kwa mdomo, bali:
Kuacha dhambi
Kuchukia dhambi
Kujitenga na mazingira ya dhambi
Kumrudia Mungu kwa moyo wote
“Tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.” (Matendo 3:19)
Usiseme: “Nitabika baadaye”
Kesho si yako.
4. Unapokutana na ujumbe huu – amua kubadilika
Hii posti si ya bahati mbaya. Mungu anakuita leo:
Acha kiburi
Acha kujitetea
Acha kuhalalisha dhambi
Chagua wokovu
“Leo ukiisikia sauti yake, usifanye moyo wako kuwa mgumu.” (Waebrania 3:15)
Ndugu yangu, Mungu anakupenda lakini anachukia dhambi. Neema haikupi ruhusa ya kuendelea kukaa kwenye dhambi, bali inakupa nafasi ya kutoka kwenye dhambi.
👉 Chagua toba
👉 Chagua utakatifu
👉 Chagua uzima wa milele
✍️ Mtumishi Moses
Nimeandika na kuposti, sambaza kwa wengine ujumbe huu ufike mbali.