Mt Marko P. Kabanga

Mt Marko P. Kabanga Catholic church at the service of God's people

Kanisa Katoliki katika huduma ya watu wa Mungu

26/04/2026

Shukrani baada ya watoto 266 kupewa kipaimara

Mambo ya Kipaimara Jumamosi 25/04/2026 katika adhimisho la Mt somo wa parokia
26/04/2026

Mambo ya Kipaimara Jumamosi 25/04/2026 katika adhimisho la Mt somo wa parokia

Maisha yanakuwa na maana na uzuri wa kweli pale tunapomfuata Kristo Yesu, kwani wito si mzigo bali ni mpango wake wa upe...
26/04/2026

Maisha yanakuwa na maana na uzuri wa kweli pale tunapomfuata Kristo Yesu, kwani wito si mzigo bali ni mpango wake wa upendo na furaha anaotushirikisha kila mmoja wetu. Katika Parokia, familia, na jumuiya za kitawa tunapaswa kuunda mazingira yanayoruhusu miito kuchanua, tukifahamu kuwa sote tunatembea pamoja k**a Jumuiya. Kuna umuhimu wa kusindikizana kidugu kwa sala kila mara ili kusaidia wale wanaopokea wito wa Mungu kuweza kuukubali kwa furaha na ujasiri. Dominka Njema!

Kristo Yesu anapoingia katikati yao anawauliza swali moja, “Ni maneno gani mnayosemezana hivi mnapotembea?” Yesu anawaul...
19/04/2026

Kristo Yesu anapoingia katikati yao anawauliza swali moja, “Ni maneno gani mnayosemezana hivi mnapotembea?” Yesu anawauliza Mnazungumza nini? Si kwa sababu hajui, bali ili kuwapa nafasi ya kutoa machungu, hofu, na majonzi yaliyokuwa yamejaa mioyoni mwao. Hii inatufundisha kuwa Kristo ni msikilizaji mkuu ambaye anataka tushiriki naye mahangaiko yetu ya kila siku. Kristo anakuja kwetu kila siku, anataka tumweleze yote yanayotusibu k**a hawa wanafunzi walivyomwelezea Yesu masikitiko, hofu, huzuni, kukata kwao tamaa. Kristo anakuja kwetu kila saa ya maisha yetu. Anatupa nafasi ya kumweleza yale yote tunayopitia katika maisha, huenda ni misiba, changamoto za maisha, migogoro ya familia, ni kukata tamaa, udhaifu wetu, mahangaiko yetu ya kila siku katika maisha nk. Ni kweli zipo nyakati tunapitia na hatuoni kabisa tumaini tena. Mara kwa mara katika misiba, katika changamoto kubwa tunaweza kuona namna huzuni inavyojaza mioyo yetu, wakati mwingine tunashindwa kuelewa Neno lolote. Kristo anataka tuseme naye, anatusikiliza. Dominika njema!

14/04/2026
Katika Dominika hii ya huruma ya Mungu, tunakumbushwa kwamba Bwana wetu Yesu Kristo mfufuka anakuja kwetu katika kila ny...
12/04/2026

Katika Dominika hii ya huruma ya Mungu, tunakumbushwa kwamba Bwana wetu Yesu Kristo mfufuka anakuja kwetu katika kila nyakati ya maisha yetu. Sisi sote kwa namna mbalimbali tuna milango iliyofungwa katika maisha yetu, mioyo iliyofungwa na huzuni, hofu, chuki, visasi, mashaka ya wakati ujao, aibu, fedheha na kushindwa, hofu na aibu ya dhambi na udhaifu wetu wa zamani, maumivu na vidonda katika historia za maisha yetu. Dominika hii inatukumbusha kuwa Huruma ya Mungu ina nguvu ya kupenya pale ambapo binadamu hawezi kufika. Hata k**a tumejifungia kiasi gani, Yesu hangojei tuwe sawa ili atutembelee bali anakuja hapo hapo tulipo, katika udhaifu wako na wangu, ili akupate, ili anipate.
Mara nyingi tunadhani kuwa madonda yetu (makosa ya zamani, kuumizwa na watu, au kufeli) ni alama za kushindwa. Dominika hii ya Huruma ya Mungu inatufundisha kuwa madonda yetu yanaweza kuwa chanzo cha nuru mpya ndani mwetu. Tunapopata huruma ya Mungu, yale makovu yetu ya zamani yanakuwa ushuhuda wa jinsi Mungu alivyotuokoa.
Dominika njema!

Baada ya kuadhimisha: Mateso na Kifo cha Bwana wetu Yesu Kristo, katika siku hii mtakatifu, tunaadhimisha Ufufuko wake k...
05/04/2026

Baada ya kuadhimisha: Mateso na Kifo cha Bwana wetu Yesu Kristo, katika siku hii mtakatifu, tunaadhimisha Ufufuko wake kutoka wafu k**a alivyosema. Tunamshangilia, “Kristo Mfufuka, tumaini la Ufufuko na Uzima wetu” Ufufuko wa Bwana wetu Yesu ni msingi wa Imani yetu, k**a anavyotuambia Mtume Paulo, “Kama Kristo asingalifufuka basi Imani yenu ni bure” (1 Kor 15:14).
Pasaka Njema!

29/03/2026

DOMINIKA YA MATAWI MUGANZA

Address

Kabanga Mission
Kasulu
41

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mt Marko P. Kabanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share