Ev. Kidifu Joseph Jr

Ev. Kidifu Joseph Jr Gospel

JE, UMEANDIKWA JINA LAKO KATIKA KITABU CHA MBINGUNI??.Ndugu yangu moja ya jambo la msingi kabisa kwa ustawi wa Roho yako...
21/08/2025

JE, UMEANDIKWA JINA LAKO KATIKA KITABU CHA MBINGUNI??.

Ndugu yangu moja ya jambo la msingi kabisa kwa ustawi wa Roho yako sio kufurahia majina yako kuandikwa ukutani au vitabu vya starehe za dunia hii.

Yesu aliwaambia wanafunzi kwa Luka 10:20 kuwa "Wasifurahi kwa kuwa pepo na kuzimu zinawatii, Bali wafurahi kwa kuwa majina yao yameandikwa mbinguni"!

Yesu hakukurupuka kusema maneno haya, anajua mtu akiwa hajaandikwa katika kitabu za mbinguni huyo ni hasara na ni wakutupwa motoni.

Ufunuo wa Yohana (Rev) 20:15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

Ndugu yangu jitahidi sana majina yako yaandikwe katika kitabu cha mbinguni.

Majina yako yanaandikwaje????

Majina yako yanaandikwa hivi.

1. Amua kutubu kabisa maovu yako mbele za Mungu kwa moyo wako wote.

2. Amua kabisa kubadilisha mfumo wote wa maisha yako, Anza kuhudhuria ibada za kweli katika makanisa ya kipentekoste bila kutegea wala kuruka ibada.

3. Amua kuacha kwenda katika sehemu ambazo ndio zinakupelekea kuwa muovu na kuzidi kumkosea Mungu.

4. Amua kupata marafiki wapya wenye uelewa na wanao mpenda Mungu, hiyo itakusaidia kudumu kwa Mungu na kuzidi kulitunza jina lako katika kitabu cha Mungu.

K**a jina lako halijaandikwa katika kitabu cha Mungu unao wajibu wa kuamua leo kumfuata na kumrudia Mungu kwa njia ya Toba ya kweli.

Nakusalimu katika pendo la Yesu Kristo.

Ev. Joseph Kidifu Jr.

Mungu anapokupa maelekezo halafu usiyafanye kwa vitendo yale maelekezo hana kitu kingine cha kukusaidia.Eliya aliambiwa ...
22/04/2024

Mungu anapokupa maelekezo halafu usiyafanye kwa vitendo yale maelekezo hana kitu kingine cha kukusaidia.

Eliya aliambiwa atoke aende sarepta kwa mama mjane, lakini angeamua kubaki pale angekufa kwa njaa maana Mungu alishamaliza siku za Eliya kuhudumiwa na kunguru. Hata usafiri wa kuondoka pale kando ya mto hakupewa bali aliambiwa aondoke hapo.

Ibrahim mwenyewe aliambiwa aondoke katika nchi ya baba yake tena Ibrahim aliambiwa mpaka atakaoambiwa hakupewa hata uelekeo k**a alivyopewa Eliya.

Lakini kwa Imani Ibrahim alifuata maelekezo ya Mungu, ukuu wako na mafanikio yako vinategemea vile unamsikia Mungu na kutii kwa vitendo yale maelekezo aliyokupa Bwana.

Ukiyapiga teke matendo nakuambia kwa jina la Yesu Kristo hautapiga hatua yoyote kwenye maisha yako na kwenye huduma yako.

Mafanikio yako na ustawi wako umefungwa kwenye kusikiliza maelekezo kutoka kwenye kinywa cha Mungu na kuyatekeleza kwa vitendo na sio kwa maneno ya midomoni.

VITENDO VIMEBEBA HATUA ZAKO ZA KUOGEZEKA.

Nakusalimu kwa jina la Yesu.

Ni kwa amani tu.

Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Bethel.
0755438142

MUNGU HUFANYA KAZI PAMOJA NA WATU.Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo. 1 Wakorintho 3:9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja...
08/03/2024

MUNGU HUFANYA KAZI PAMOJA NA WATU.

Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo.

1 Wakorintho 3:9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.

Kuna vitu Mungu hawezi kukupa hata ukifunga siku 365 ikiwa hutaamua kuanza kufanya wewe mwenyewe.

Chochote unachokiomba kwa Mungu kinahitaji vitendo vyako ili Mungu avifanye vitokee kwako.

Mungu hataweza kufanya peke yake, Neno lake linasema yeye hufanya kazi pamoja na sisi (watu)!

Unahitaji vitendo ili kile Mungu amekufunulia kwa Neno au Mawazo kiwe dhahiri kwako.

Warumi 8:28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

Bado Neno la linasisitiza kwamba Mungu hufanya kazi na wale wampendao, ni kweli unampenda ni kweli unamuamini lakini usipoinuka kufanya kwa vitendo yale amekufunulia Imani yako imekufa nafsini mwako.

Ibrahim aliambia atoke katika nchi ya baba yake, asingetoka pengine asingempata Isaka na mali yake ingepungua.

Alifunuliwa aondoke hakung'ang'ana aliondoka alitii maelekezo ya ufunuo aliousikia.

Unataka kufanikiwa, unataka kuongezeka basi kile Mungu anakufunulia kwa Neno lake yakupasa ukifanye kwa vitendo ili Mungu akidhihirishe kwako.

Mungu akusaidie uanze kufanya kwa vitendo chochote kile ambacho Mungu amekufunulia katika jina la Yesu Kristo.....

Umebarikiwa na Bwana.
Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Bethel
0755438142

Isaya 66:9 Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema BWANA; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Ase...
07/03/2024

Isaya 66:9 Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema BWANA; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako.

Mungu akikuletea wazo kwenye ufahamu wako hilo lazima lizalishe faida haliwe kukufunga au kukufanya upate hasara.

Nakuombea katika jina la Yesu Kristo kila wazo lililopita kwenye ufahamu likazaliwe kwa uhalisia wake.....

Katika jina la Yesu Kristo chochote kinachokuzuia usifanikishe wazo kukiachie na kikao mbali na uwezo wako wa kuzalisha kwa jina la Yesu Kristo.

Roho ya kupuuzia na kusitasita inayokufunika ili mradi tu lile wazo usilifanyie naamuru kwa mamlaka niliyopewa vikuachie na vikae mbali na mikono yako na miguu yako na ufahamu katika jina la Yesu Kristo....

Roho ya kukumwamisha naondoa katikati yako katika jina la Yesu Kristo usizuiwe.

Wazo lako lizae kwa jina la Yesu Kristo.
Mipango yako ifanikishwe katika Yesu Kristo.

MUNGU HAWEZI KUKUPA WAZO HALAFU LIISHIE NJIA, KILA WAZO LA MUNGU ANALOPITISHA KWAKO LIFANIKIWE KATIKA JINA LA YESU KRISTO...

KWA ANAYEAMINI ANDIKA AMEN AMEN KWENYE COMMENT NAWE KWA IMANI UTAVUKA.

Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Bethel

Follow this link to join my WhatsApp group: https://chat.whatsapp.com/CHdc9RDZoupGoEwOfH7l02GUSA LINK HAPO KUJIUNGA NA G...
29/02/2024

Follow this link to join my WhatsApp group: https://chat.whatsapp.com/CHdc9RDZoupGoEwOfH7l02

GUSA LINK HAPO KUJIUNGA NA GROUP WHATSAPP, HILI NI GROUP KWA WAOMBAJI NA WENYE MAHITAJI MBALIMBALI.

KARIBU HAPA NDIO MAHALI PAKO SAHIHI.

Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Nyikani

NAMNA VIUNGO VINAWEZA KUKUFANIKISHA AU KUFUNGA MAFANIKIO YAKO.Haleluya haleluya mtu wa Mungu, nakusalimu kwa jina la Yes...
29/02/2024

NAMNA VIUNGO VINAWEZA KUKUFANIKISHA AU KUFUNGA MAFANIKIO YAKO.

Haleluya haleluya mtu wa Mungu, nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo.

Karibu tujifunze neno la Mungu, leo Mungu ametupa kibali cha kujifunza kuhusu VIUNGO.

Adui anatumia viungo hivi hivi tulivyonavyo kuweza kuzuia hatima ya mtu, na Mungu anatumia viungo hivi hivi tulivyonavyo ili kuweza kumfanikisha mtu.

Viungo ambavyo tutaviangalia kwenye somo letu ni viungo vifuatavyo.

KICHWA, MIGUU NA MIKONO.

1. KICHWA.

Kichwa kinawakilisha hatima yako. Adui akitaka kushambulia hatima yako basi atashambulia kichwa chako.

Kichwa kimebeba viungo vingine k**a akili, macho, masikio na ulimi.

Kwahiyo ninaposema kichwa nimewakilisha na hivyo viungo vingine ambavyo vimeshikiliwa na kichwa.

Mhubiri 2:14 macho yake mwenye hekima yamo kichwani mwake, lakini mpumbavu huenda gizani; ila hata hivyo nikatambua ya kwamba ni tukio moja la mwisho liwapatalo wote sawasawa.

Macho ya mwenye hekima yako kichwani mwake, macho ya mwenye hekima hakimbilii gizani, kichwa chenye akili nzuri hakikimbilii kutenda maovu, bali hukimbilia kwa Mungu mahali pa Nuru.

Zaburi 140:7 Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.

Mungu asipokifunika kichwa , kichwa kinakosa nguvu, kichwa kinakosa kinga, kichwa kinavamiwa na kutumiwa na shetani atakavyo...

Mungu ni nguvu zetu sisi tulio katika Bwana, ametufunika vichwa vyetu tusienende katika Giza, ametufunika na nguvu za Roho Mtakatifu ili tuzidi kutulia nuruni na pendoni mwake...

Ndugu kichwa kikimkosa Mungu, kinampata shetani na mapepo yake, yaani muda wote kichwa kinawaza ulevi, kinawaza uzinzi na uasherati kwasababu hakijafunikwa na nguvu za Mungu bali kimefunikwa na giza (shetani) kwahiyo mawazo yatazunguka ya kishetani shetani tu, mawazo ya kumkosea Mungu na sio kumlingana Mungu wala kumsogelea Mungu.

Watu ambao vichwa vyao vimezungukwa na shetani muda wote wanawaza mambo ya gizani, ni tofauti kabisa na ambaye kichwa chake kimezungukwa na nguvu za Mungu, mtu aliyezungukwa na nguvu za Mungu atawaza muda wa MAOMBI, muda wa kusoma NENO LA BWANA, atawaza muda wa kukusanyika kumfanyia Mungu ibada. N.K.

MPENDWA KATIKA BWANA.

OMBA NGUVU ZA MUNGU ZIKIFUNIKE KICHWA CHAKO.

2. MIKONO

Mikono inawakilisha uwezo wa mtu kuzalisha (kuzaa)!

Kuna mikono ya aina mbili.
Kuna mikono ya baraka na mikono ya laana.

Mikono ya baraka ni mikono ambayo inauwezo wa kuzalisha.

Mikono ya laana ni mikono ambayo haina uwezo wa kuzalisha, ni mikono ya uharibifu.

Mikopo ya uharibifu huwa inategwa yaani mtu anategewa mikono ya uharibifu, kila anachogusa kinaharibiwa, au yaani hawezi kufanikisha jambo lolote zuri lazima tu ataliharibu.

Danieli 11:16 Maana ajaye kupigana naye atatenda kadiri apendavyo, wala hapana mtu atakayesimama mbele yake; naye atasimama katika nchi ya uzuri, na uharibifu utakuwa mkononi mwake.

Na uharibifu utakuwa mkononi mwake, kwahiyo hii roho ya uharibifu ni mtu anasemewa na watu wengine kwamba uharibifu ukae katika mikono yake na hii ndio wengi wameangukiapo.

Mithali 3:16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.

Shetani anajua siri iliyoko katika mikono, mikono inaweza kukupa maisha marefu au mafupi na mikono inaweza kukufanya masikini au tajiri.

Mkono wako wa kuume (kulia) kiroho unawakilisha wingi wa siku zako za kuishi na mkono wa kushoto unawakilisha utajiri na heshima.

Unaweza kukuta mtu anaota ndoto ameng'atwa na nyoka mkono wa kulia au kushoto, k**a umewahi kuota ndoto yoyote unang'atwa mkononi basi ujue shetani anawinda kati ya wingi wa siku zako za kuishi au utajiri na heshima unavyotakiwa kuvipata.

Katika mikono yako ndani yake kunaweza kukawa na mkono wa Mungu au mkono wa shetani, utajua kwa matokeo ya mikono yako.

Kutoka 17:11 Ikawa, Musa alipouinua mkono wake, Israeli walishinda; na alipoushusha mkono wake, Amaleki walishinda.

Mikono ya Musa iliwapa ushindi wana wa Israel, Musa akiinua mikono wana wa Israel wanashinda lakini akishusha mikono amaleki wanashinda, kwasababu ndani ya mikono ya Musa kulikuwa na mkono wa Mungu ambao uliwapa ushindi wana wa Israel.

Wachawi wanaweza kumloga mtu, badala ya kuwa na mkono wa baraka wa Mungu mtu anakuwa na mkono wa uharibifu na kutokufanikiwa.

Hii mikono ndio mikono ambayo Mungu anatumia pia kupitisha uzima, miujiza na uponyaji kwa watu wake.

Marko 16:18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Mikono ya watumishi wa MUNGU huwa imebeba mikono ya Mungu ndani yake.

Ndio maana watumishi wanaweza kuweka mikono yao kwa wagonjwa na wagonjwa wakapata afya.

K**a mtumishi wa Mungu amefungwa mikono yake hawezi kumuombea mtu akapona au kufunguka k**a amefungwa na pepo.

Mikono ya Musa ilitenda ajabu nyingi na ishara nyingi pale misri kwasababu ndani yake kulikuwa na mkono wa Mungu.

TORATI 34:11-12, KUTOKA 3;20.

OMBEA MIKONO YAKO IFUNGULIWE K**A IMEBEBA UHARIBIFU.

3. MIGUU.

MIGUU inawakilisha utawala au mamlaka yako.

Luka 10:19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Tunakanyaga kwa miguu, maana miguu imebeba mamlaka.

Miguu inakupa kutawala, miguu inakupa mamlaka, nguvu zote za shetani NENO la Mungu linasema tutazikanyaga.

Maana yake ukikanyanga unakuwa juu yake, huwezi kukanyaga halafu ukawa chini ya ulichokikanyaga.

Warumi 16:20 Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi.

Maana yake ni kwamba Mungu ametupa kumtawala shetani, shetani hawezi kuwa juu ya mtu aliyemuamini Mungu, hawezi kuwa juu ya mtu wa Mungu.

Zaburi 22:16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu.

Shetani akitaka kukuweza au akitaka kukuharibu atashughulika kwanza na kuizuia miguu yako, akiweza kuiongoza miguu yako basi shetani anakuwa amekushinda.

Ili akushinde anakufunga kwanza miguu, lakini Mungu naye akitaka kukuinua ataifungua kwanza miguu yako...

Naiamuru miguu yako ifunguliwe kwa jina la Yesu Kristo....

Kuna miguu mizuri na miguu mibaya pia.

MIGUU mizuri ni ipi???

Na

Miguu mibaya ni ipi???

Warumi 10:15 Tena wahubirije, wasipopelekwa? K**a ilivyoandikwa, Ni mizuri k**a nini miguu yao wahubirio habari ya mema!

Miguu mizuri ni miguu inayopeleka habari njema kwa watu, miguu inapeleka habari za kufunguliwa kwa watu waliofungwa, habari za uponyaji kwa wagonjwa, Habari za kutuliwa mizigo ya dhambi.

Zaburi 8:6 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.

Mungu ameweka mamlaka ya vitu vyote katika miguu.

Kwahiyo Mungu akitaka kukupa kutawala anafungua miguu yako, miguu ikifunguka tayari umepewa vitu vyote chini yako.

MUAMBIE MUNGU AKUFUNGUE MIGUU YAKO UTAWALE....

Katika ulimwengu wa Roho unaweza kuwa na mguu unaoteleza, mguu ambao hauwezi kutunza vitu au watu.

Zaburi 17:5 Nyayo zangu zimeshik**ana na njia zako, Hatua zangu hazikuondoshwa.

Hold up my goings in thy paths, that my footsteps slip not.

2 Samweli 22:37 Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Wala miguu yangu haikuteleza.

Thou hast enlarged my steps under me; so that my feet did not slip.

Nyayo zako zishik**ane na Mungu, zisiteleze kwa jina la Yesu Kristo.

Umebarikiwa.

Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Nyikani.

12/04/2023
WALA HAWAMJUI BWANAHosea 5:4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawa...
15/09/2022

WALA HAWAMJUI BWANA

Hosea 5:4 Matendo yao hayatawaacha kumgeukia Mungu wao; maana roho ya uzinzi imo ndani yao, wala hawamjui Bwana.

Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo mtu wa Mungu.

Ninalo Neno la Mungu kwako wakati huu, Mungu anatupenda watu na kwa kudhihirisha kuwa anatupenda alimtoa Yesu Kristo aje afe hapa duniani ili atupate na atufanye mali yake.

Hilo la uhai wa Yesu Kristo halikutosha, Yesu mwenyewe alivyoona amefufuka na imempasa kwenda mbinguni kwa Mungu Baba akaona atatuacha peke akaamua kutuletea Roho Mtakatifu the invisible Man kutuongoza na kutufanya imara kila iitwapo leo.

Lakini kuna watu wanakataa kumgeukia Mungu, k**a wewe ni mmoja wa watu hao ujumbe huu ni wa kwako!

Kizazi hiki kimefunikwa na roho ya uzinzi na ukahaba, kuna watu wanaona uzinzi na uasherati ndio maisha yenyewe ya kwenda na wakati!!

Sikia nikuambie k**a unadhani uzinzi na uasherati ni jambo la nyakati (season) unajidanganya, hii moja ya kazi za shetani kuzidi kujiongezea idadi ya wafuasi wataochomwa pamoja naye!!

Kataa hiyo kitu, uzinzi na uasherati ni ushetani huo, shetani mwenyewe yumo humo katika uzinzi.

Usiseme siku hizi ni kawaida leo unalala na huyu na kesho unalala yule, napenda nikuambie unazini wewe na hilo kosa mbele za Mungu!

Unayejiuza na unayenunua mapenzi sikia nikuambie huyo ni shetani anawafanyisha dhambi ili msije mkamjua Mungu.

Shetani amewawekea roho ya uzinzi ndani yenu ili muone kawaida, ili miili yenu iwake moto kusudi tu muendelee kumkosea Mungu na msije kumjua Mungu.

Kuna wanawake wanajiuza wamegeuza viungo vyao biashara, wamegeuza viungo ndio kazi zao, sikia shetani amepofusha akili yako usione k**a ni kumkosea Mungu bali uone ni kazi k**a kazi nyingine na biashara k**a biashara nyingine, unapigwa na unatumiwa shetani vibaya, Mungu anataka uvitumie viungo vyako kwa ajili ya haki na sio uovu!!

Sikia naongea na mtu mmoja anayetamani sana kuacha tabia za uzinzi lakini anashindwa, unashindwa kwasababu shetani mwenyewe ndio amekaa ndio yako, hutaweza kumtoa kwa utashi wako na akili zako au mawazo yako!!

Ili shetani atoke ndani yako unamhitaji Yesu Kristo akae ndani yako, unamhitaji Yesu Kristo akufungue katika vifungo hivyo!!

Shetani anaogopa mtu mwenye Yesu Kristo ndani yake, haogopi akili zako wala mawazo yako wala maneno yako!!

Marko 1:24 akisema, Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je! Umekuja kutuangamiza?

Kwahiyo ili utoke kwenye kifungo cha uzinzi na ukahaba unamhitaji Yesu Kristo, yeye atakutoa humo!!

Najua unataka sana kutoka huko, lakini nakuambia kwa akili na mawazo yako hutaweza!!

Muamini Yesu Kristo na UOKOKE yeye atakutoa kwenye kifungo hicho cha uzinzi!!

HUTAWEZA KUMJUA MUNGU K**A BADO UNAISHI MAISHA YA KUENDEKEZA UZINZI NA KUPENDA UZINZI, KUPENDA UZINZI NI PEPO!!

Ni mimi mtumishi wa Mungu
Ev. Joseph Kidifu Jr
Kutoka Nyikani

Kwa maombi na maombezi
Text/Calls/WhatsApp: 0755438142

Marko 2:17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bal...
26/08/2022

Marko 2:17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.

Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo mtu wa Mungu.

Ninalo neno kwako wakati huu, nalo ni hili!!

Wakati ujio wa Yesu Kristo ulimwenguni ukiwa na kusudi kuu la kuwaokoa wanadamu kutoka mautini (dhambini) na kuwapeleka uzimani!

Sikiliza Yesu Kristo hakuja kulazimisha watu wote wamuamini, wanaomuamini ndio wanaokuwa wake!

Sikiliza Yesu Kristo hakulazimishi na wala hakulazimisha mtu amuamini au amsaidie, wote waliosaidiwa na kuponywa na Yesu ni kwasababu wao wenyewe walitaka kuponywa na Yesu Kristo na waliamini Yesu Kristo anao uwezo wa kuwaponya!!

Wasiotaka kuponywa, hashughuliki nao, bali anashughulika na wale wanaotaka uzima na kusaidiwa na Yeye.

Wewe usifuate mkumbo, usifuate upepo, sikia hakuna anayejua maumivu yako zaidi yako mwenyewe, hakuna anayejua kuugua kwako zaidi yako!!!

Amua kujisaidia mwenyewe, k**a ukoo wako hawaamini katika Yesu Kristo na wakusaidie kuyatua maumivu yako, la k**a hawawezi kuyatua maumivu Yesu Kristo anakuambia umuamini yeye akutue na akumpuzishe maumivu yako!!

Sikia hakuna aliye mzima wa afya anayemtafuta daktari, bali wote wanaotamfuta daktari ni walio hawawezi, ni wale wenye matatizo!!

Wewe una matatizo unawasilikiza watu wanakuambia usiende huko hatuamini na hatufungamani, usiwakilize hao hawakupendi, wanaokupenda watahitaji kuona unakuwa na nguvu k**a zao, njoo kwa Yesu Kristo akuponye, njoo kwa Yesu Kristo akuondolee maumivu, njoo kwa Yesu Kristo akuondolee uchungu!!

Umehangaika siku nyingi imetosha, umemaliza mali yako uliyoitegemea utapata uzima hata mali imeisha hujapona umekata tamaa ya maisha, sikia hii ni habari njema kwako inuka sasa amua kuja kwa Yesu Kristo daktari wa kweli akuponye na akuweke huru mbali na mateso!!

Usiishi kwa mateso, usiishi kwa kukata tamaa ya kuishi, usijitamkie kufa, usijitamkie kujinyonga, wanakuambia haiwezekani hawakupendi hao, Yesu Kristo anakuambia yeye anaweza, wewe unamhitaji daktari Yesu usikate tamaa Yesu Kristo yupo na alikuja kwa ajili ya watu waliokata tamaa k**a wewe, alikuja kwa ajili ya watu wanaoteseka k**a wewe, alikuja kwa ajili ya watu wenye maumivu k**a yako muamini na CHUKUA HATUA YA KUSOGEA KWAKE ATAKUPONYA NIAMINI MIMI MTUMISHI WAKE NAKUAMBIA UKIAMINI MSIBA WAKO UTAKWISHA, UKIAMINI MAUMIVU YAKO YATAKWISHA.

Nikupe ushuhuda huu!!

Mwaka jana tulipomaliza huduma mkoa fulani na rafiki yangu katika huduma mtumishi mwenzangu tulisafiri mpaka mkoani mbeya!!

Tulipofika tukaenda kufanya huduma ya maombi na maombezi nyumbani kwa mama mmoja.

Yule mama ana miaka zaidi ya mitatu hatembei, miguu inamuuma inavimba kwa muda mrefu!!

Yule mama alikuwa ni mfanyabiashara, na tayari alikuwa ameshafikia hatua ya kupata order nyingi kabla kabla hajamaliza mzigo anakua na order za kutosha Tu!!

Yule alianza kupata shida ya miguu, kwasababu alijua anazo fedha akaenda hospitali akawa anapangiwa tarehe za kwenda na kubadilishiwa hospitali hadi muhimbili alifika na appointment za madaktari bingwa alikuwa nazo hadi mali yake ikaisha akawa hawezi tena kufika hospitali!!

Siku tumefika kumuombea nyumbani kwake, akalipuka pepo, kumbe wajanja wamebeba nyota yake ya biashara wanajitarisha wao kupitia nyota yake, tukakemea mapepo yule mama akafunguliwa pale pale akaanza kusema miguu imekuwa myepesi na imesinyaa, tukamuambia tatizo lilianzia kwenye biashara yako, watu waliona unapiga hatua kubwa akasema ni kweli kabisa!!

Nataka nikuambie ndugu yangu, ukiona tatizo limekuzidi kipato na limechukua muda mrefu kukuachia, hilo sio tatizo la kawaida, matatizo mengine ni roho ya kukufilisi, ni umasikini kwako na kwenye nyumba yako!!

NAKUAMBIA LEO MUAMINI YESU KRISTO AKUPONYE, ATAKURUDISHIA MIGUU YAKO, ATAKUREJESHEA UZIMA (AFYA) YAKO, ATAKUREJESHEA UZIMA WA BIASHARA YAKO, ATAKUREJESHEA MWILI WAKO, ATAKUREJESHEA AKILI ZAKO NA MENGINE MENGI.

MUAMINI YESU KRISTO YEYE NDIYE DAKTARI WA MAGONJWA SUGU.

MUAMINI YESU KRISTO YEYE NDIYE BINGWA WA KILA KITU.

CHUKUA HATUA BADO HUJACHELEWA NDUGU YANGU.

Ni mimi.

Ev. Joseph Kidifu Jr
Prayerline: 0755438142

Kutoka Nyikani
26.08.2022

Kornelio alitoa sadaka kwa watu na kuomba, ni SADAKA NA MAOMBI, ndipo akaletewa ujumbe kuwa SADAKA ZAKE NA MAOMBI YAKE Y...
25/07/2022

Kornelio alitoa sadaka kwa watu na kuomba, ni SADAKA NA MAOMBI, ndipo akaletewa ujumbe kuwa SADAKA ZAKE NA MAOMBI YAKE YAMEFIKA KWA MUNGU. (MATENDO 10;1-4)

Kuna kitu cha kujifunza hapa ambacho ni SADAKA LAZIMA IAMBATANE NA MAOMBI, Sasa wewe kazana kutoa na huombi, au kazana kuomba na hutoi, maombi yenye kumfikia Mungu na kujibiwa na Mungu SIRI YAKE IKO KWENYE KUTOA NA KUOMBA.

ELIYA WAKATI ANATAKA KUMDHIHIRISHA MUNGU WA KWELI KUMBUKA SADAKA ILIKUWEPO NA BAADA YA KUANDALIWA ELIYA AKAOMBA MUNGU ASHUKE NA BAADA YA MAOMBI MUNGU ALISHUKA.

UNATAKA KUMSIKIA MUNGU ANAKUJIBU BASI SADAKA NA MAOMBI HAVIPASWI KUTENGANA, VIFANYE VYOTE UTAKUTANA NA MUNGU.

Ev. Joseph Kidifu Jr

LAKINI MSIPOTUBU MTAANGAMIA.Luka 13:3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.Nakusalimu ...
05/04/2022

LAKINI MSIPOTUBU MTAANGAMIA.

Luka 13:3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

Nakusalimu kwa jina la Yesu Kristo mpendwa katika Bwana.

Leo nimepata neema ya kukufikishia ujumbe kwa habari ya Toba, tutaangalia umuhimu wa kutubu dhambi.

Kaini aliambiwa na Bwana ya kwamba dhambi iko mlangoni inamuotea, nayo imemtamani lakini aliambiwa yampasa aishinde.

Mwanzo 4:7 K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Kuna mambo matatu hapa Kaini alitahadharishwa na Bwana.

✓Dhambi iko mlangoni
✓Dhambi ina muotea
✓Dhambi inamtamani

Nami nakuambia maneno haya haya ambayo Bwana alimuambia Kaini,

Dhambi siku zote iko mlangoni kwako, inawezekana mahali ulipo nayo iko hapo hapo. Lakini yakupasa uishinde!

Dhambi inakuotea, kila siku, kila siku saa dhambi inakunyemelea, vishawishi ni vingi vinakujisogeza kwako, dhambi yenyewe unachokitaka kutoka kwako ni wewe umkosee Mungu ili ipate nafasi ya kukuangamiza na kuvurunga baraka/njia zako!

Dhambi inakutamani, ndio dhambi inakutamani utende ili umkosee Mungu ukaangamie, ili umkosee Mungu ukawe na mwisho mbaya. Lakini yakupasa uishinde mtu wa Mungu.

Kwanini kutubu, na kwanini Yesu Kristo alisema usipotubu utaangamia!??

✓Toba inaondoa uharibifu ndani ya maisha ya mtu.

✓Toba inaondoa laana ndani ya maisha ya atubuye.

✓Toba inakufutia na kugeuza hukumu mbaya iliyosomwa kwa maisha ya mtu.

✓Toba inakupa haki iliyowekwa juu yako.

Watu wa Ninawi walitangaza kuingia katika mfungo ili kutubu na Mungu alisikia toba yao akaghaili uharibifu aliokuwa umeukusudia juu ya Ninawi.

Yona 3:5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.

Yona 3:6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.

Watu wa Ninawi walivyotubu wakapewa haki ya uzima wao.

Bathomayo kipofu alipotubu, Yesu akampa haki yake ya kuona.

Marko 10:47 Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu.

Ni kweli dhambi imekusonga,

Ni kweli imekung'ang'ania,

Ni kweli dhambi imefanya makazi ndani yako,

Ni kweli dhambi umefanikiwa kukuk**ata.

Lakini ninalo Neno kwako, Tubu dhambi na maovu yako yote kwa dhamiri ya kuacha na kuzichukia, Mungu ni mwaminifu sana atakuondoa katika utumwa huo.

"Yesu alisema, Lakini usipotubu, Utaangamia"

Kutoka Nyikani
Ev. Joseph Kidifu Jr
0755438142

Address

Kaliua

Telephone

+255755438142

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ev. Kidifu Joseph Jr posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Ev. Kidifu Joseph Jr:

Share