20/10/2025
SOMO:- UWEZO
ANDIKO:- ISAYA 43:2
Upitapo katika maji mengi
nitakuwa pamoja nawe;
na katika mito,
haitakugharikisha;
uendapo katika moto,
hutateketea; wala mwali
wa moto hautakuunguza.
KIINI- UWEZO WA KUKABILIANA NA
NYAKATI NGUMU
(I) UTANGULIZI
Kila binadamu hupitia vipindi viwili
maishani:
(a) KIPINDI CHA MAFANIKIO NA
FURAHA
(b) KIPINDI CHA MAJARIBU NA
MACHUNGU.
ONA:-
-Siri si kuepuka nyakati ngumu, bali kujua namna ya kuzishinda.
-Isaya anatukumbusha jambo kuu: Mungu hakusema hatutapitia majini, bali amesema “nitakuwa pamoja nawe unapopita.”
-Hii ndiyo nguvu ya waamini si kukosa misukosuko, bali kuwa na Mungu ndani yake.
(II) NYAKATI NGUMU SI ISHARA YA
KUSHINDWA
-Watu wengi wanapopitia magumu hudhani Mungu amewaacha, kumbe Mungu yupo kazini.
-Ndugu wa Yusufu walitaka kuua ndoto yake , akauzwa utumwani lakini huko ndiko alipopandishwa cheo; Mwanzo 50:20 “Ninyi mlikusudia mabaya juu yangu, lakini Mungu alikusudia mema.”
-Danieli aliingia kwenye tundu la simba, si kwa sababu Mungu hakuwepo, bali ili ulimwengu ujue kwamba Mungu anaokoa.
Ukweli wa Kuchukua:-
Kila mtihani una nafasi ya ushuhuda. Mungu anatumia nyakati ngumu kutengeneza nguvu mpya ndani yako.
(III)- NAMNA YA KUKABILIANA NA
NYAKATI NGUMU
1. KAA IMARA KWENYE NENO LA MUNGU
Mathayo 7:24–25 “Kila asikiaye maneno haya na kuyatenda ni k**a mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba juu ya mwamba.”
ONA:-
-Upepo unapovuma, Neno ndilo
mwamba.
-Usijenge imani yako juu ya hisia,
jenga juu ya ahadi za Mungu.
2. OMBA HATA K**A HAUONI MAJIBU MARA MOJA
ONA:-
-Maombi hayambadilishi Mungu, lakini yanambadilisha mtu anayeomba;
Luka 18:1 “Wapaswa kuomba siku zote wala wasikate tamaa.”
-Mungu anapochelewa, hajachelewa anakutayarisha.
3. USIRUHUSU HOFU ITAWALE
-Shetani hupenda kutumia hofu kukupofusha usione wokovu.
2 Timotheo 1:7 “Kwa maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu, ya upendo na ya moyo wa kiasi.”
-Usikubali sauti ya hofu izime sauti ya matumaini.
4. ZUNGUKWA NA WATU WENYE
IMANI
-Kuna nguvu katika ushirika sahihi.
Mhubiri 4:9–10 “Afadhali wawili kuliko mmoja; maana wakiporomoka, mmoja atamwinua mwenzake.”
-Wakati mwingine unahitaji tu mtu wa kukushika mkono na kukuambia, “Utafanikiwa!”
(IV)- KILA JARIBU LINA KUSUDI LA
KIFALME
ONA:-
-Kabla ya taji, kuna vita.
-Kabla ya ushuhuda, kuna maumivu.
Warumi 8:28 “Tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao kwa mema.”
-Mungu anaweza kutumia magumu uliyonayo leo kuwa daraja la kukuinua kesho.
Note:-
-Kuna nyakati Mungu anaondoa dhoruba;
-lakini mara nyingine anamsaidia baharia aweze kuvuka mawimbi salama
(V)- KUMBUKA
-Nyakati ngumu si mwisho wako, ni mwanzo wa sura mpya ya ushindi.
-Mungu anasema leo: “Usiogope, nitakuwa pamoja nawe.”
-Uwezo wa kukabiliana na nyakati ngumu upo ndani yako kwa sababu Roho Mtakatifu anakaa ndani yako.
Zaburi 30:5.... “Kilio cha usiku ni cha muda mfupi, lakini furaha huja asubuhi.”
By.
Rev.Missionary Emmanuel F.Kitaly
(CHINI YA KANISA LA TAG VICTORY KAONGWA MJI MWEMA)
👇 Bonyeza viungo hapa chini kuungana nami moja kwa moja:
📺 YouTube:
👉 Rev. Missionary Emmanuel F. Kitaly
📘 Facebook (Page/Share):
👉 Jiunge / Share Posts
👉 Rev. Missionary Emmanuel F. Kitaly
💬 WhatsApp Group:
👉 Jiunge na Victory Mission Global
📞 Kwa Ushauri, Maombi na Maombezi
📲 +255 754 478 929
Kwa Ushuhuda,Sukrani,Sadaka,kuwezesha huduma.+255754478929
LIPA NAMBA VODA - 51260374
( JINA- EMMANUEL KITALY)
VICTORY MISSION GLOBAL (VGM)