Ufalme wa Mungu

Ufalme wa Mungu Bali utafuteni Kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hayo yote mtazidishiwa( mathayo 6:33)

12/04/2026
Pasaka
05/04/2026

Pasaka

Asante sana mtu wa Tabora usiache kufika siku ya kesho na Mungu akubariki 🙏🙏
20/03/2026

Asante sana mtu wa Tabora usiache kufika siku ya kesho na Mungu akubariki 🙏🙏

Yohana 3:12 Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?❤️❤️TUKUTAN...
20/03/2026

Yohana 3:12 Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?
❤️❤️TUKUTANE TABORA✅✅

MTUMISHI ZINGATIA HAYA KABLA HUJAANZA HUDUMA1. Huduma inahitaji Uvumilivu. Usiwe mwepesi kukata tamaa.2. Haijalishi umea...
11/12/2025

MTUMISHI ZINGATIA HAYA KABLA HUJAANZA HUDUMA

1. Huduma inahitaji Uvumilivu. Usiwe mwepesi kukata tamaa.

2. Haijalishi umeanzaje lakini jiandae kwa nyakati za kupimwa na kujaribiwa katika huduma yako.

3. Huduma itachanua kwa kuzingatia kutembea na Mungu, uaminifu, kutochoka mapema.

4. Kila hatua ya huduma ina watu wake na marafiki wake. Kuna wakati watu fulani watakuja au wataondoka. Usiwe mwepesi kujisahau kwa wanaokuja au kulaani wanaoondoka kipindi chao kinapoisha.

5. Hakikisha huduma yako ina mlezi au msimamizi wa kiroho anayeweza kukukemea na kukukosoa na ukanyenyekea na kusikiliza.

6. Unapopata fursa ya kutumika mahali tumika kwa moyo na nguvu zote maana huwezi kujua hiyo fursa moja itakufungulia milango gani.

7. Usikimbilie kuiga wanachofanya wengine na kikawasaidia kwenye huduma zao, kabla hujatulia na kuomba uongozi wa Roho Mtakatifu k**a na wewe kitakufaa.

8. Kuna watumishi wengine wa Mungu kamwe hawatatambua wito wako wala kukukubali. Usipambane nao.

9. Kuna watumishi tena marafiki zako watabebea bango madhaifu yako na kamwe hawataangalia alichoweka Mungu ndani yako. Songa mbele.

10. Unahitaji kujijengea nidhamu ya hali ya juu katika Neno la Mungu na kujilinda na mawaa ili utumishi wako usiwe wa kulaumiwa.

11. Heshimu walio mbele yako kihuduma bila kujali umri wao.

12. Ushindani ni mkubwa. Kuwa na hekima, mbinu na shindana kwa msaada wa Mungu.

13. Katika huduma yako kitu kingine chochote kisiwe na thamani zaidi kuliko roho au nafsi ya mtu.

14. Ikimbie zinaa, pombe, tamaa (ya mwili, ya macho, ya mali), masengenyo, wivu na kiburi cha uzima.

15. Tunza sana siri zako na siri za waumini wako.

16. Kila mwaka kuna waumini wako unaowategemea sana wataondoka. Ila Roho Mtakatifu na vipawa alivyokupa havitaondoka.

17. Hakuna mjadala kuhusu Kufunga na Kuomba kila mara ili huduma yako ichanue.

18. Unyenyekevu utakuinua hata pale wengine wanapoona huna vigezo.

19. Usiendekeze sana kukaribishwa kwenda kuhudumia makusanyiko mengine kuliko kulihudumia kundi ambalo utalitolea hesabu.

20. Wapende na wajali washirika wako. Watie moyo, watembelee na ulizia maendeleo yao.

Injili ya endelea🔥🔥🔥
19/10/2025

Injili ya endelea🔥🔥🔥

2 Samweli 3:33 Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu?2 Samweli 3:34 Mikono ...
06/10/2025

2 Samweli 3:33 Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu?
2 Samweli 3:34 Mikono yako haikufungwa, Wala miguu yako haikutiwa pingu; Aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka. Na watu wote wakaongeza kumlilia.
🇹🇿🇹🇿

Miaka mingi iliyopita nilikutana na mtu ambaye nilikuwa nasikia sana habari zake mbaya.....na alikuwa akizungumzwa sana ...
13/03/2025

Miaka mingi iliyopita nilikutana na mtu ambaye nilikuwa nasikia sana habari zake mbaya...
..na alikuwa akizungumzwa sana ubaya wake na mtu mwingine ambaye nilikuwa namfahamu.

Ukweli ni kuwa hata mtazamo wangu juu yake uliathiriwa sana na ulikuwa “negative” mno...
..hata k**a nilikuwa simjui sana na kuwa karibu naye lakini tayari niliona ndani yangu simkubali...
..na nilishahitimisha kuwa ni mtu mwenye sifa zote mbaya nilizokuwa nazisikia.

Siku niliyokutana naye alikuwa amekuja kuniomba ushauri.

Nilipokutana naye hakujua kuwa nina taarifa zake nyingi sana nilizoambiwa...
..na watu ambazo zilinifanya hata kabla hajasema niwe nimeshamuhukumu na kumuona si mtu sahihi...
..lakini nilimpa nafasi ya kumsikiliza.

Alipoanza kuongea nilishangaa sana, katika mambo niliyoambiwa takribani 98% hayakuwa kweli.

Na cha ajabu zaidi alikuwa anapitia wakati mgumu sana...
..na alikuwa na vita nyingi sana katika maisha yake ambazo watu wengi sana walikuwa hawajui kabisa.

Alinieleza kuhusu maumivu yake...

Alinieleza kuhusu changamoto zake...

Alinieleza alivyobakia peke yake na kila mtu amemkimbia...

Alinieleza jinsi ambavyo hakuna mtu wa kumsikiliza...

Alinieleza ambavyo amekata tamaa kwa sababu ya maneno ya kuchoma moyo ya uongo ambayo kila siku yanasemwa juu yake n.k

Nilishikwa na huzuni Moyoni, nilimuomba msamaha:

Nilijifunza kuwa kabla HAUJAMCHUKIA mtu tafuta SABABU ya KUMPENDA.

Kabla HAUJAMSEMA VIBAYA tafuta SIFA ZAKE NZURI.

Nilijifunza kuwa kuna watu WANATESEKA na MANENO MABAYA...
..ambayo wewe Unayasema kwa KUJIFURAHISHA wenzako YANAWATESA.

USIMUHUKUMU MTU bila KUPATA NAFASI YA KUMSIKILIZA.

USIMCHUKIE mtu kwa MANENO YA WENGINE.

Kuna mtu ANAHITAJI kupona leo kwa UPENDO wako.

USIRUHUSU CHUKI na MANENO YAKO yawe chanzo cha YEYE KUKATA TAMAA.

Tafuta Mtu wa KUMGAWIA FURAHA na TUMAINI kwa MANENO YAKO na sio KUSABABISHA HUZUNI.

Kuna mengi unayoweza kuyaamini yakawa si kweli.

UWE CHANZO CHA FURAHA KWA MTU MWINGINE LEO.

USIHUKUMU kabla HAUJASIKILIZA.

USIAMINI kabla HAUJATHIBITISHA.

USITENGENEZE MSIMAMO kwa KUSIKIA kwa WENGINE TU.

GAWA FURAHA LEO!!

K**a umeipenda makala hii...

1. SHARE makala hii na mtu mmoja afurahi

Address

Kisasa
Dodoma

Telephone

+255752407591

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ufalme wa Mungu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Ufalme wa Mungu:

Share