PAGTanzania

PAGTanzania Kanisa la Kipentekoste lenye msingi na imani katika Neno la Mungu linaloundwa na ujumla wa makanisa mahali pamoja.

Pentecostal Assemblies of God (Tanzania)

This is a Pentecostal church based on faith in the Word of God, formed by a community of local churches. It was founded by missionaries from Canada under the missionary organisation called Pentecostal Assemblies of Canada, who began spreading the Gospel in Tanganyika in 1912, during which time some died of disease. Since then, the church has been growing a

nd increasing until now there are more than 2000 churches throughout the country. Kanisa la Kipentekoste lenye msingi na imani katika Neno la Mungu linaloundwa na ujumla wa makanisa mahalia pamoja. Lilianzishwa chini ya wamisionari kutoka Kanada wakiwa chini ya Shirika la kimisionari liitwalo Pentecostal Assemblies of Canada ambao walianza kueneza Injili Tanganyika katika miaka ya 1912 ambapo katika miaka hiyo wengine walifariki kwa magonjwa. Kuanzia wakati huo kanisa limekuwa likikua na kuongezeka mpaka sasa kuna makanisa zaidi ya 2000 nchi nzima.

16/07/2026
16/07/2026

πŸ‡ΉπŸ‡Ώ MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA NUSU MWAKA
ALHAMISI β€’ 16 JULAI 2026
πŸ™ Maombi kwa Ajili ya Taifa
πŸ“– 1. Ombea Rehema za Mungu kwa Taifa la Tanzania
"Ikiwa watu wangu... watajinyenyekeza na kuomba..."
πŸ“– 2 Mambo ya Nyakati 7:14 | Yeremia 14:20 | Danieli 9:8
πŸ“– 2. Waombee Viongozi wa Mihimili Yote
Mungu awajaze hekima, maarifa na hofu ya Bwana ili waongoze kwa haki na uadilifu.
πŸ“– Ezekieli 22:29–30
πŸ“– 3. Ombea Amani na Haki Vitawale Nchini
Tuombe taifa letu liendelee kuwa na amani, haki na utakatifu katika kila sekta.
πŸ“– Mithali 14:34 | Isaya 61:8
πŸ“– 4. Omba Baraka na Ulinzi wa Mungu kwa Tanzania
Mungu alibariki taifa letu, alipe maendeleo, na aliweke chini ya ulinzi wake daima.
πŸ“– Zaburi 33:12–14 | Yeremia 29:11 | Zaburi 127:1
"Heri taifa ambalo Bwana ndiye Mungu wake." β€” Zaburi 33:12

16/07/2026

πŸ™ MAOMBI YA KATIKATI YA MWAKA DPC
πŸ“… JUMATANO, 15 JULAI 2026
πŸ‘¨β€πŸ‘©β€πŸ‘§β€πŸ‘¦ KUOMBEA FAMILIA
"Bwana ndiye anapoijenga nyumba, wajengao wafanya kazi bure." β€” Zaburi 127:1
I. MSHUKURU MUNGU KWA ZAWADI YA FAMILIA
πŸ“– Zaburi 127:1–5
βœ… Mshukuru Mungu kwa zawadi ya familia na kwa kutufikisha hapa salama.
βœ… Mshukuru kwa ulinzi wake juu ya ndoa, watoto na wazazi wetu.
βœ… Mshukuru kwa rehema zake na uaminifu wake katika maisha ya familia zetu.
II. TUOMBE MUNGU ASHUGHULIKIE CHANZO CHA MATATIZO YA FAMILIA
πŸ“– Mwanzo 37:3–4
πŸ™ Omba Mungu aondoe kila mzizi wa upendeleo, wivu na chuki ndani ya familia zetu.
πŸ™ Omba arejeshe upendo, mawasiliano mazuri na msamaha katika nyumba zetu.
πŸ™ Omba atufanye kuwa watu wa upatanisho na amani k**a Yusufu.
III. TUOMBE MUNGU ALINDE FAMILIA ZETU NA KUTIMIZA KUSUDI LAKE
πŸ“– Zaburi 128:1–4; Mwanzo 50:20
πŸ›‘οΈ Omba Mungu alinde familia zetu na watoto wetu dhidi ya kila mpango wa adui.
πŸ›‘οΈ Omba atimize kusudi lake katika maisha ya kila mwanafamilia.
πŸ›‘οΈ Omba hofu ya Mungu itawale katika nyumba zetu.
IV. TUOMBE MUNGU ABARIKI NDOA, WATOTO NA UCHUMI WA FAMILIA
πŸ“– Warumi 12:2
πŸ’ Omba Mungu alinde na kuimarisha ndoa, awaongoze wanaotamani kuingia katika ndoa na kuwajalia wenzi wanaomcha Mungu.
πŸ‘Ά Omba awakumbuke wanandoa wanaotamani kupata watoto, awalinde watoto wetu na wawakuzie katika hofu yake. (Zaburi 127:3–5)
πŸ’Ό Omba Mungu afungue milango ya uchumi, abariki kazi za mikono yetu na atupe hekima ya kusimamia alichotukabidhi. (Kumbukumbu la Torati 8:18)
Karibu tuungane katika maombi ya pamoja tukiiweka familia mbele za Mungu. Mungu anaweza kuleta uponyaji, upendo, umoja na baraka mpya katika kila nyumba.
#2026

16/07/2026
16/07/2026

πŸ”₯ MAOMBI YA KUFUNGA NA KUOMBA KATIKATI YA MWAKA 2026
SIKU YA 2 | Jumanne, 14 Julai 2026

OMBI KUU: UAMSHO πŸ”₯

"Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?" β€” Zaburi 85:6
Leo tumwombe Mungu alete uamsho wa kweli ndani ya maisha yetu, familia zetu, na Kanisa Lake.

πŸ™ 1. Ombea Uamsho Ndani Yako na Ndani ya Kanisa
‒⁠ ⁠Uishi maisha ya utakatifu na kumcha Mungu (Matendo 10:1–2).
‒⁠ ⁠Uwe mtu wa maombi na ujitoe kikamilifu kwa Mungu na kazi Yake.
‒⁠ ⁠Umzalie Kristo matunda na ushiriki katika kulijenga Kanisa Lake (Matendo 9:31).
‒⁠ ⁠Uamsho wa kweli ulete ukuaji wa kiroho, umoja, na kuimarisha Kanisa la Kristo.

πŸ™ 2. Ombea Uamsho wa Karama na Vipawa
‒⁠ ⁠Mungu achochee na kuhuisha karama zilizo ndani yako (2 Timotheo 1:6–7).
‒⁠ ⁠Akupe ujasiri mpya wa kumtumikia kwa uaminifu (Matendo 3:6).
‒⁠ ⁠Aachilie roho ya maombi ndani yako na ndani ya Kanisa (Matendo 12:5).
‒⁠ ⁠Aondoe kila uovu na kila kizuizi kinachopinga kazi Yake (Matendo 13:6–12).

πŸ™ 3. Ombea DPC
‒⁠ ⁠Ombea moto mpya wa uamsho ushuke juu ya Dar es Salaam Pentecostal Church (DPC), viongozi wake, watumishi, idara zote, vikundi vyote vya huduma, na washirika wote.
‒⁠ ⁠Mungu aliwezeshe Kanisa kutimiza kusudi Lake kwa nguvu za Roho Mtakatifu, umoja, na upendo.

"Ee Bwana, tuhuishe tena, ili jina Lako litukuzwe kupitia Kanisa Lako." πŸ”₯πŸ™Œ

16/07/2026

ISHI MAISHA MAPYA πŸ“– Warumi 12:1–2 Mungu hakuita tu kubadili tabia zako, bali kubadilishwa kabisa ili ufanane na Kristo. K**a vile kipepeo hupitia mabadiliko makubwa kutoka kiwavi hadi kuwa kiumbe…

16/07/2026

πŸ™ MAOMBI YA KATIKATI YA MWAKA NA KUFUNGA πŸ™

Kanisa linakualika kushiriki katika Wiki ya Maombi ya Katikati ya Mwaka na Kufunga, itakayoanza kesho Jumatatu, tarehe 13/7/2026 hadi Jumamosi, tarehe 18/7/2026.

Ratiba ya Maombi:
πŸ—“οΈ Jumatatu – Ijumaa: Saa 11:00 jioni hadi saa 1:00 usiku
πŸ—“οΈ Jumamosi: Saa 4:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana

Hii ni nafasi maalum ya kulisogelea Mungu, kutafuta uongozi wake, kumshukuru kwa uaminifu wake, na kuomba neema, nguvu na mwelekeo kwa kipindi kinachokuja.

Tafadhali panga kuhudhuria vipindi vyote vya maombi na alika familia, marafiki na wengine tushiriki pamoja katika kumtafuta Bwana.

"Niitane, nami nitakujibu, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua." β€” Yeremia 33:3

16/07/2026

Address

Area D Plot No 30 Block No S
Dodoma

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when PAGTanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share