Efatha Church Chamwino Ikulu

Efatha Church Chamwino Ikulu Ukurasa huu unalenga kutangaza injili ya Yesu Kristo ili kuwafanya wengi wageuze nia zao na kurudia Bwana na Mwokozi wa ulimwengu

16/12/2023
Esta 4:13-15 “ Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijidhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa...
15/10/2023

Esta 4:13-15 “ Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijidhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa mfalme, zaidi ya Wayahudi wote. Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; walakini ni nani ajuaye k**a wewe hukuujia ufalme kwa ajili ya wakati k**a huo? Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai,”

Esta alikuwa ni mke wa mfalme (Malkia) alikuwa ana kila kitu alichokihitaji katika maisha yake lakini baada ya Mungu kusema naye juu ya Wayahudi hakuwa na amani mpaka Wayahudi wakawa salama. Inaweza kuwa Mungu amefungua mlango kwa ajili yako ili kuingia katika nyumba ya mtu mmoja ambaye hamjui wala kumuheshimu Mungu, au unafanya kazi katika kampuni ambayo mtu huyo hamjui Mungu au unaishi katikati ya watu ambao hawamjui Mungu, hiyo ni sababu au njia ya wewe kumuwakilisha Mungu hapo.

Lakini walokole wengi wamechagua kuridhika na kutokufanya chochote kile katika maisha hayo, Mungu amekuweka hapo ili umuwakilishe na kuwabadilisha hao watu, usiikumbatie amani yako pekeyako bali tamani watu wengine wapate kumjua Mungu kwa maana Mungu amekuchagua uwe hapo kwa kusudi maalumu nawe yakupasa kulitimiza hilo kusudi.

Mungu anasema usiitafute amani yako binafsi na ukaacha kinachowatokea wengine, kataa kushikilia amani yako pekeyako au amani ya familia yako tu, kijiji chako, majirani zako, kataa kuwa na amani juu ya magonjwa ya watu wengine, usiruhusu maisha yako yakakufanya uache kile ambacho wengine wanapitia bali simama mpaka umuone Mungu akifanya jambo katika maisha ya watu wengine.

Wakristo wengi changamoto yao ni kuwa wakiokoka na wakaipokea amani wanafurahia hiyo amani yao pekeyao hawajali maisha ya watu wengine, Mungu amekuponya, amekubariki, amekupa familia nzuri ili uweze kumuwakilisha Yeye na kuwafanya wengine wapate kumjua Yeye. Esta alikuwa na kila kitu lakini Mungu akasema naye kwa kupitia kinywa cha Mordekai ili aweze kuw

MCHUNGAJI MICHAEL KYAZEE KUTOKA UGANDA SOMO: KUWA SALAMA NA KUWA MAKINI KATIKA MASUALA YA KIROHOAyubu 1:1-6 “Palikuwa na...
15/10/2023

MCHUNGAJI MICHAEL KYAZEE KUTOKA UGANDA

SOMO: KUWA SALAMA NA KUWA MAKINI KATIKA MASUALA YA KIROHO

Ayubu 1:1-6 “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu. Kisha walizaliwa kwake wana saba, na binti watatu. Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu,…….”

Ayubu alikuwa na familia na mali nyingi sana lakini pia kikubwa alikuwa anamcha Mungu.

Ayubu 1:6 -7 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.”

Mkutano huu haukuwa duniani bali mbinguni, huu ulikuwa ni mkutano wa kiungu ambapo Mungu alikuwa anajadili mambo yanayohusu dunia.
Mungu alikuwa anatoa ushuhuda kuhusu habari za Ayubu, ya kuwa ni mcha Mungu, ndipo Mungu akamuuliza ibilisi unatoka wapi? Akasema “Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo”

Hii inamaana unapaswa kujua kuwa tunaishi huku duniani mahali pa vita, ibilisi yupo na anatembea kwa maana hiyo tunapaswa kuwa makini katika kuenenda kwetu ili tuweze kuwa salama.

Ayubu 1:9-10 “Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.”

Kuna vitu vitatu ambavyo Mungu alivifanya kwa Ayubu:-
• Mungu aliweka uzio (ukigo) uliomzunguka Ayubu,
• Mungu aliweka uzio katika nyumba ya Ayubu (kwa wote walio nyumbani mwake).
• Uzio wa mali zake

Hii inamaana kuwa kuna maeneo matatu katika maisha yetu ambayo yanahitaji kuwekewa ulinzi (ukigo) wa kiroho, maeneo hayo ni:-
• Wewe mwenyewe unahitaji ulinzi wa kiroho

• Nyumba yako (watu wa nyumbani mwako)

• Vile unavyomiliki

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA 1 Yohana 5:14-15 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu saw...
11/10/2023

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

1 Yohana 5:14-15 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na k**a tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba.”

Je! Unajua kuwa wewe ni mapenzi ya Mungu? Mapenzi ya Mungu nini basi? Ni wewe kuokolewa, hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwetu sisi wanadamu; je! Wewe umezaliwa mara ya pili (umeokoka) k**a jibu ndiyo basi chochote ulichomuomba Mungu amekupa, je! Umeomba chochote kwake? K**a umeomba ondoa mashaka yote kwa maana tayari Mungu amekupa. Kwa nini hauoni sasa hivi? Kwa sababu bado haupo eneo la kutendea kazi.

UKIRI:
• Baba weka shauku ndani yangu ya kukuabudu wewe, kukutii, kukutumikia, siku zote za maisha yangu.

• Bwana nipe kuwa mtii na kupitia utii nipe kuwa mtoaji, chochote unachonipa ukifikia wakati wa kutoa nipe kutoa kwa uaminifu.

MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO CHA PRECIOUS KATIKA NGAZI YA CHETI CHA USIMAMIZI WA THEOLOJIA NA UONGOZI MATUKIO KATIKA PICHA...
10/10/2023

MAHAFALI YA KWANZA YA CHUO CHA PRECIOUS KATIKA NGAZI YA CHETI CHA USIMAMIZI WA THEOLOJIA NA UONGOZI

MATUKIO KATIKA PICHA

PICHANI NI MAANDAMANO YA KITAALUMA YA WAHITIMU, WANATAALUMA, MGENI RASMI NA BODI YA CHUO WAKIINGIA KATIKA UKUMBI WA MAHAFALI YAKIONGOZWA NA BRASS BAND

NENO LA SIKU.Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.Tarehe 10/10/2023Marko 5:25-34 “Na mwanamke mmo...
10/10/2023

NENO LA SIKU.

Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.

Tarehe 10/10/2023

Marko 5:25-34 “Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona………..”

Huyu mwanamke aliyetokwa na damu hakuwa hana msaada, rafiki, mume wala mtoto, alikuwa hana tumaini, alikuwa mpweke kwa muda wa miaka kumi na mbili, madaktari walifanya udaktari wao lakini hakupona.

Mwanamke huyu alikuwa katika uhitaji mkubwa kwa sababu alitumia fedha zake zote kwa ajili ya kujitibia, kwake hakukuwa na kilichosalia bali Imani yake kwa Mungu pekee. Lakini siku moja alisikia kelele ndipo akauliza ni kelele za nini? Akaambiwa Yesu anapita huyu mwanamke alijadili katika nafsi yake, akajiambia “lazima uamke maana hii ni nafasi pekee uliyonayo na ukiikosa utakufa na ukiipata utaishi”.

Huyu mwanamke aliamua kuchukua hatua ya kumwendea Yesu kwa sababu alikuwa amechoshwa na hali yake, akijiambia “k**a nikifa basi nitakufa nikiwa najaribu kuishi” ndipo akachukua hatua ya kumwendea Yesu na kwa kupitia Imani yake akaponywa, Yesu hakumwombea yule mwanamke bali kwa Imani na neno la yule mwanamke lilimfanya yeye apokee uponyaji wake.

Inatosha kusema kuwa una Imani sasa ni wakati wako wa kutendea kazi Imani yako, maneno yoyote unayotamka katika Imani mara zote yanawezeshwa na Mungu ili yapate kutimia kwa sababu Imani inatoka juu kwa maana hiyo unapotamka kwa imani unaiamrisha mbingu ishuke na kutendea kazi lile neno ulilolitamka.

K**a unataka kuona miujiza kwa haraka tamka neno kwa imani utapata muujiza kwa haraka zaidi ya kuomba.

Naitwa Wema Emmanuel, napenda kumshukuru sana Mungu kwa matendo yake makuu katika maisha yangu, nilipita katika kipindi ...
09/10/2023

Naitwa Wema Emmanuel, napenda kumshukuru sana Mungu kwa matendo yake makuu katika maisha yangu, nilipita katika kipindi kigumu sana wakati nikiwa Mkoa wa Arusha, kwani nilikwenda kule kufanya kazi nikitokea Mkoa wa Dar-es-salaam, lakini baadae nilipoteza kazi yangu nikakaa kwa muda wa miaka miwili bila kazi nikiwa katika nyumba ya kupanga. Ilifika mahali nikaona mambo yamekuwa magumu sana ndipo nikaamua kumuaga Mchungaji kuwa nataka kurudi Dar es salaam, lakini Mchungaji akaniambia kuwa nisiondoke, kazi ipo Arusha na hata mume wangu yupo hapa hapa Arusha nilimuitikia tu amina.

Nakumbuka siku moja ilikuwa ni ibada ya live (mbashara) kutoka Mwenge, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira akasema kuwa mwenye ufahamu hatafuti kazi ila kazi inamtafuta, nililishikilia hilo neno; ulipofika usiku nikaomba sana, ilipofika asubuhi nikapigiwa simu kuwa kuna mtu anataka nikamfanyie kazi yake, nikaenda kufanya ile kazi lakini cha ajabu ni kuwa nilipata pesa nyingi ambazo ni za mshahara wa miaka yote miwili ambayo nilikuwa sina kazi. Baada ya kuifanya kazi ya yule mtu akaniambia wewe ndio nataka uwe muhasibu wa kampuni yangu, japo sikusomea kazi ya uhasibu lakini kupitia ile kazi niliyoifanya ikanipa kazi nyingine. Namshukuru sana Mungu wangu kwa maana sasa ile pesa niliyokuwa napata kwa mwezi k**a mshahara sasa naipata kwa wiki k**a posho tu mbali na mshahara. Pia Mungu amenipa mume mzuri naweza kusema kuwa yote haya nimeyapata kwa sababu toka nimeingia Efatha nimekuwa mwaminifu kwenye swala la matoleo na kushuhudia wengine habari za wokovu. Kwa kipindi chote cha miaka miwili nilipokuwa sina kazi nilitumia muda wangu kupita na mitaani na kushuhudia watu habari za wokovu na kuwaleta kwa Yesu, namtukuza sana Mungu kwa matendo yake makuu kwangu.

Naitwa Shukuru Erick natoka nchi ya Congo eneo la Kivu, napenda kumshukuru sana Mungu kwa kuniokoa, ilikuwa ni ombi lang...
09/10/2023

Naitwa Shukuru Erick natoka nchi ya Congo eneo la Kivu, napenda kumshukuru sana Mungu kwa kuniokoa, ilikuwa ni ombi langu nipate mahali sahihi pa kuabudia, namshukuru Mungu kwa maaana amenionyesha mahali sahihi.

Pia napenda kumshukuru sana Mungu kwa maana kupitia mimi kuokoka Mungu amefanya jambo kubwa sana katika maisha yetu. Mke wangu alikuwa kila akipata mimba anajifungua kwa upasuaji, siku moja nikiwa namuomba Mungu anipe mahali sahihi pa kuabudia nikaingia kwenye mtandao nikaona mahubiri katika page moja ya Efatha Church Sharon yameandikwa Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, baada ya kusoma yale mahubiri nikavutiwa sana na nikatamani kujua k**a hilo kanisa linapatikana Congo. Nilituma ujumbe mfupi kuuliza na baada ya kitambo kidogo Mchungaji wa kanisa la Efatha Arusha alinipigia simu na akajitambulisha kwa Jina la Mchungaji James Nyansika na alinipa maelekezo namna ya kuipata Efatha kule Congo. Naweza kusema haikuwa rahisi kutokana na umbali lilipokuwa kanisa la Efatha lakini Mungu alifanya maajabu yake na Leo Mimi ni Mchungaji wa Efatha kule Congo Kivu Kusini na nina kanisa lenye watu wengi.

Nakumbuka ilikuwa ni mwaka 2022 ulikuwa ni mwaka wa maachilio, nikamwambia Mungu kuwa mimi na familia yangu tunataka kuachiliwa. Baada ya kupata maana ya neno Efatha kuwa ni funguka nikamwambia Mungu mke wangu amefungwa maana kila akibeba ujauzito lazima ajifungue kwa kupasuliwa ( operation) nikamsihi Mungu amfungue, nilifunga siku tatu kavu nikimuomba Mungu amsaidie mke wangu ajifungue salama, namshukuru sana Mungu kwa maana niliona maajabu sana kwani mke wangu alijifungua salama kabisa, mtoto wa kiume na nilikuwa nimeweka nadhiri kuwa akiwa wa kiume nitampa jina James Nyansika Jina la Mchungaji aliyesababisha niijue Efatha ili iwe alama ya mwanzo wa safari yangu ya wokovu ndani ya Efatha. Mtoto wangu Sasa ana mwaka mmoja, amekuwa mtoto wa muujiza na kwa umri wa mwaka mmoja anaongea na kutembea, namshukuru sana Mungu kwani sasa mimi na familia yangu tunaam

ASKOFU CHARLES KARIUKIMungu ana vyote ambavyo unavihitaji, hivyo mpe shukrani ili afungue mbingu kwa ajili ya yale unayo...
09/10/2023

ASKOFU CHARLES KARIUKI
Mungu ana vyote ambavyo unavihitaji, hivyo mpe shukrani ili afungue mbingu kwa ajili ya yale unayoyahitaji, funguo yako ya kufungulia hayo unayoyahitaji ni kumshukuru Yeye ili aweze kumimina yale aliyokukusudia katika maisha yako.
Mshukuru Mungu kwa yale anayoenda kuyafanya.
MAOMBI:-
• Omba Mungu akupe haja ya moyo wako.
• Omba Mungu afunue yale yaliyo jificha katika maisha yako,
• Ee Mungu wangu ninafungua ukurasa mpya leo na wewe, naomba utamalaki katika maisha yangu na katika hatima yangu ya kiungu.

TANGAZO:Ikiwa Mimi ni mtu wa Mungu, umaskini nenda UTAJIRI njoo. Ikiwa Mimi ni mtu wa Mungu, magonjwa na maradhi nenda, ...
06/10/2023

TANGAZO:
Ikiwa Mimi ni mtu wa Mungu, umaskini nenda UTAJIRI njoo.
Ikiwa Mimi ni mtu wa Mungu, magonjwa na maradhi nenda, UPONYAJI njoo.
Ikiwa Mimi ni mtu wa Mungu, kushindwa nenda, USHINDI njoo.
© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira

MAOMBI YA UMILIKI: Kuanzia leo UKAMILIKI vya kwako, kwa ajili ya watoto wako na wajukuu zako, ardhi mimea, mazao na kila...
06/10/2023

MAOMBI YA UMILIKI:

Kuanzia leo UKAMILIKI vya kwako, kwa ajili ya watoto wako na wajukuu zako, ardhi mimea, mazao na kila utakachokifanya kikakubali, kila utakachofuga kikaongezeke. Bwana akakupe KUZAA matunda, ukajenge nyumba za kupendeza, ukawe na nyumba za kupangisha, ukawe na nyumba za biashara.

Bwana akakupe fedha mifukoni mwako.
Mungu akakupe wahesabu watakaohesabu mali zako, ukawe na wafanya kazi wa kufanya kazi nyumbani mwako, kuanzia sasa ukawe na ustawi na kuongezeka sana, asiye na mtoto akapate mtoto asiyeolewa akaolewe. Kuanzia sasa ukawe na mwendelezo ukapate kumiliki, usiwe na kifo cha mapema, magonjwa yakakae mbali na wewe, ajali iwayo yoyote haikuhusu. Adui yoyote atakayeinuka akanyamazishwe kabla hajakukaribia; chochote kilicho kinyume chako kiwe ni hali ya hewa, vyakula au maji kuanzia leo nawapatanisha navyo.

K**a unauadui na utajiri, mafanikio au fedha leo nakupatanisha navyo kwa jina la Yesu, pesa ikafanye makao kwako. Kuanzia leo Mungu akakupe KUMILIKI fedha za mataifa mengine.

Kuanzia sasa ukapate chakufanya, ukawe mtendakazi pamoja na Bwana wa mabwana.

Bwana AKAKUTUMIE kwa ajili ya utukufu wake, Bwana AKAKUINUE kwa utukufu wake,
Bwana AKAKUPIGANIE kwa utukufu wake
Bwana AKAKULINDE kwa utukufu wake
Bwana AKAKUNEHEMESHE kwa utukufu wake,
Bwana AKAKUPE kibali kwa utukufu wake.

Kuanzia sasa utaitwa HERI, ndugu zako watakuonea wivu lakini wataishia kukuheshimu kwa sababu Bwana amekufanya kuwa kimbilio la wengi, nenda ukawe; amen.

Kuanzia sasa ongea kile unachotaka kuona katika maisha yako k**a vile ulivyosikia usibadilishe hata mafuriko yaje usibadilike. Kuanzia leo ukawe na kibali popote unapokwenda.

© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Precious Centre Kibaha

Address

Chamwino Ikulu
Dodoma

Telephone

+255768710868

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Chamwino Ikulu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church Chamwino Ikulu:

Share