Love Is Power Of God

Love Is Power Of God LOVE IS POWER OF GOD (L.P.G Dodoma Tanzania)
Senior Pastor: Apostle Roderick Ndone
� Mkonze Kibaoni.

Mwanzo 9:(Genesis) 6. Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu, maana kwa mfano wake Mungu ...
14/09/2024

Mwanzo 9:
(Genesis)

6. Atakayemwaga damu ya mwanadamu, damu yake huyo itamwagwa na mwanadamu, maana kwa mfano wake Mungu alimfanya mwanadamu.
---------------
"Whoever sheds man's blood, By man his blood shall be shed; For in the image of God He made man.

UKIITAJI KUA SALAMA ZINGATIA HILI, MUNGU HAJAWAHI SEMA UONGO

_INUKA HAPO ULIPO KWA JINA LA YESU KRISTO,KAZI YAKO IINUKE,NDOA YAKO IINUKE,UZAO WAKO UINUKE,HUDUMA YAKO IINUKE,NK,KWA J...
12/09/2024

_INUKA HAPO ULIPO KWA JINA LA YESU KRISTO,KAZI YAKO IINUKE,NDOA YAKO IINUKE,UZAO WAKO UINUKE,HUDUMA YAKO IINUKE,NK,KWA JINA LA YESU KRISTO AMENI* ._

MUNGU YUPO PAMOJA NAWEMUNGU akasema, “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe, na nitakupa faraja (raha).”[Kutoka 33:14 MUN...
06/09/2024

MUNGU YUPO PAMOJA NAWE

MUNGU akasema, “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe, na nitakupa faraja (raha).”
[Kutoka 33:14

MUNGU yupo na wewe kwa kusudi kwamba usiteseke, kila jambo lako liwe jepesi na kufanikiwa.

MUNGU hayupo na wewe tu ili ufike mbinguni, ni pamoja na kuhakikisha mambo yako yanakwenda k**a unavyopenda.

Hivi unajua kwamba MUNGU anafanya vitu kwa ajili yetu, yaani anatupenda kiasi kwamba anatamani kututendea kila tunalotaka.

Yupo tayari kabisa kutekeleza unayopenda wewe.

Inawezekana ikawa ni jambo dogo kiasi kwamba unaona huwezi kumwambia MUNGU, usifanye hivyo, mwambie kila kitu MUNGU, jenga ukaribu na Baba yako, hakuna anayeweza kukusaidia na kukupa raha k**a YEYE.

Ukizoea kumwambia MUNGU mambo madogo hata yale ambayo yapo kwenye uwezo wako, itakusaidia siku yanapokuja makubwa kuzidi uwezo wako. Imani yako itakuwa imejengeka kiasi cha kuweza kuamini kwamba MUNGU atanitendea kwenye hili kubwa.

MUNGU yupo na wewe popote ulipo, ili kukupa raha. Raha unaipata pale unapolindwa na kupata kila kitu chako kutoka kwa MUNGU Baba yako anayekupenda.
AMENI
UWE NA USIKU MWEMA

AMENI,
Apostle Rodrick Ndone L P G KIBAONI MKONZE DODOMA.

KIBARI CHA MUNGU
03/09/2024

KIBARI CHA MUNGU

IJAPOKAWIA INGOJEE, HAINA BUDI KUTIMIA (USIKATE TAMAA). Bwana YESU KRISTO asifiwe sana mpendwa, leo mtumishi Apostle Rod...
02/09/2024

IJAPOKAWIA INGOJEE, HAINA BUDI KUTIMIA (USIKATE TAMAA).

Bwana YESU KRISTO asifiwe sana mpendwa, leo mtumishi Apostle Rodrick Ndone anasema na wewe ambaye una ona ndoto yako ime chelewa kutimia. Nasema na wewe ambaye kila ukiangalia umri wako na muda ulio nao una ona ndoto zako zimeyeyuka!! Nasema na mtu mmoja ambaye amekata tamaa kwa sababu ya magonjwa nk!! Tumaini lipo, YESU KRISTO ni tumani letu, soma hapa,

Habakuki 2:2-3 neno la MUNGU linasema:

"BWANA akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma k**a maji.

Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia".

Katika neno hili tuna ambiwa itatimia kwa wakati ulioamriwa. Ukisoma kitabu cha Mhubiri 3:1 neno la MUNGU linasema:

"Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu".

Usikate tamaa, majira yako na muda wako wa kufurahi unakuja. Wewe umekusudiwa mema. MUNGU mwenyewe anasema katika

Yeremia 29:11:

"Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho".

Hapa ulipo sasa hivi unaona dunia haieleweki, unaona umefika mwisho, sasa mwisho wako ndiyo mwanzo wa MUNGU k**a hautakata tamaa. Huo unao uona ni mwisho wako ndiyo MUNGU anaona nwanzo na anaruhusu tumaini kuibuka.

MUNGU akikuinua, uwe na moyo wa shukurani.

Katika mapito yako yote usijinenee mabaya, usikiri kushindwa. Fahamu kwamba "kukata tamaa ndiyo silaha ya mwisho ya shetani na UVUMILIVU ndiyo kipimo cha kwanza cha MUNGU kwa mtu yeyote".

**********USIKATE TAMAA**********AMENI****************

Apostle Rodrick
0710111214

Apostle Rodrick anakuombea saizi ili utoke katika vifungo vinavyo haribu maisha yako.“Nguvu yoyote ya kichawi,inayoweka ...
02/09/2024

Apostle Rodrick anakuombea saizi ili utoke katika vifungo vinavyo haribu maisha yako.

“Nguvu yoyote ya kichawi,inayoweka kizuizi juu ya maisha yako, kazi yako, nyumba yako, maisha ya watoto wako, ndoa yako - ninaiamamuru iharibiwe, katika jina la YeYESU KRISTO Kila silaha ya uovu iliyoundwa dhidi yako - itoweke, katika jina la YESU KRISTO! Uwe huru kutoka kwa kila vifungo vya utumwa!,pokea Mafanikio katika kazi yako, katika ndoa yako, katika jina la YESU KRISTO!” AMENI.

Address

KIBAONI MKONZE DODOMA
Dodoma

Opening Hours

Thursday 15:00 - 18:00
Friday 21:00 - 05:00
Sunday 09:00 - 13:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Love Is Power Of God posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category