Efatha Ministry-Ihumwa Dodoma.

Efatha Ministry-Ihumwa Dodoma. Tunapatikana Mtaa wa Bwawani,Ihumwa.Panda daladala pale sabasaba Dodoma ushuke Flemingo Jeshini,utao

Kwa wanaotoka Dar es salaam,Huduma ya Efatha Ihumwa ipo kingoni mwa barabara kuu ya Dar es salaam kuja Dodoma;kilomita 16 kutoka mjini Dodoma,shukia Flemingo jeshini.

Mchungaji Witness John aki*sign daftari la wageni jioni ya leo ila sasa sio mgeni bali ni Mchungaji wa kituo cha Efatha ...
28/06/2017

Mchungaji Witness John aki*sign daftari la wageni jioni ya leo ila sasa sio mgeni bali ni Mchungaji wa kituo cha Efatha Ihumwa.Tunamshukuru Mungu kwa kutupa mchungaji,HALLELUYA.

26/06/2017

KUTOKA KATIKA MAKTABA %YA KITUME NA KINABII%
SOMO:NIA MBILI
{sehemu ya II}
-Unapopata changamoto unatumia maneno yapi?Ya Nia ya Mbinguni au nia ya kuzimu?
-Ukiwa na Nia ya Mbinguni,utaona dhambi na ulilie Bwana akusaidie k**a mwizi wa kuumeni mwa Bwana pale Kalvari msalabani.
-Lazima ujue unayemwamini.
-Zaa hata katika vifungo,Bwana Yesu anazaa katika saa mbaya,akiwa kwenye mti wa msalaba na maumivu makali.
-NIA MBILI NI HATARI SANA.
-Uliapa kumtumikia Bwana Yesu maisha yako yote,unafanya hivyo?unatubu? umebadilika?
-Lazima ufanye uliyoyasema.
*k**a ni nadhiri futa.
-Lazima ufuate Bibilia
*Fungu la kumi ni la Bwana.
-Jifunze na kufanya ya Mungu.
*******Wafilipi 2:5*******
-Hamna njia ya mkato,lazima kila mmoja katika wokovu awe na nia ya Kristo ndani yake.
-Nia ya Kristo haipendi ubinafsi.
******Yakobo 1:7-8******
-Aliye na nia mbili husitasita.
-Lazima usimame na uliyoyasema.
-Fisha nia ya dunia.
-Mbinguni watakusaidia ukikubali sio ukijihesabia haki.
-Mtu aliyekaa katika uwepo wa Mungu na haoni kasoro yake ni HATARI.
+++++++++Amen++++++++++++++
***********&&&&&&&************
I.C.T. Efatha Ihumwa.

26/06/2017

%%%KUTOKA KWENYE%%% %MAKTABA YA KITUME NA% %%%%%%KINABII%%%%%
%%%%%%%%%%%%%%%%%{Tar 29/6/2014}sehemu ya I
SOMO:NIA MBILI
-Bibilia inafundisha watu kuwa na nia moja tu,hayo ndiyo mapenzi ya Mungu.
***Petro wa 1,3:8-12***
-Katika nia moja tutaona nguvu ya kuhurumiana,kusameheana,kupendana.........ambako ni kutumika katika Bwana.
*Tunapofanya hivyo tunarithi baraka za Mungu wetu.
-Jifunze na ukubali kuwa na nia ya Kristo maana inaelezea yalimo ndani ya Mungu.
*Ukiwa na Nia ya Kristo utania anayoyania Kristo;anayoyania Kristo ndiyo anayoyania Mungu.
*****Wafilipi 2:5*****
-Katika nia yako unatakiwa kuwa na sheria ulizopewa na Bwana,roho yako isiongozwe na sheria za kidunia maana si salama.
*****Waebrania8:10*****
-Bwana Mungu anawapigania,anawatetea na kuwapa msaada wale wenye nia ya wokovu wake.
-Mtu mwenye nia mbili atakwama maishani kwa kuwa hawezi kumshinda shetani.
*****Yakobo 1:7-8*****
-Unapaswa kushinda vita vya maisha na Mungu atakuwa upande wako ikiwa unasikia na kufanyia kazi unachoambiwa,hapo unaonyesha kuwa na nia moja katika Bwana.
*******Ufunuo 1:3*******
-Unasoma kupitia macho.
-Unasikia kupitia masikio.
*Mtu anayekaa mbele za Bwana,katika uwepo wa Bwana,akatoka bila kuona kasoro aliyo nayo,ana nia mbili na anajihesabia haki;ni vigumu mtu huyu kubadilika maisha yake kwenye eneo kolofi.
*Nia mbili zinafanya kazi,Nia ya Kristo na nia ya shetani,zitambue uzishughulikie.
-Yesu alituokoa tutoke katika nia mbili.
-Lazima ufishe nia zako zooote ufuate NIA YA MBINGUNI.
-Lazima ujifunze kusamehe,usishindwe kusamehe.
*Lazima usamehe kwa gharama zote.
*Asiyesamehe hana tofauti kubwa na shetani.
*Ukimwombea mtu ina maana unampenda.
*Asiyesamehe hana uwezo wa kuwaleta watu kwa Yesu.
-Utaratibu wa Bwana ni wewe umtumikie mtumishi mwenzako naye akutumikie.
********&&&&&&&&&*********
Somo litaendelea..........
I.C.T. Efatha Ihumwa

Saa ya ukombozi Bwana yupo kazini,kweli ufalme wake upo mahali hapa.
25/06/2017

Saa ya ukombozi Bwana yupo kazini,kweli ufalme wake upo mahali hapa.

Mtumishi Elizabeth Shauri akifundisha hapa Efatha Ihumwa Dodoma muda huu.SOMO:UPENDO
25/06/2017

Mtumishi Elizabeth Shauri akifundisha hapa Efatha Ihumwa Dodoma muda huu.
SOMO:UPENDO

 Mtumishi Veronica Gabriel akiongoza ibada hapa  Efatha Ihumwa Dodoma.Maandalizi ya moyo ni ya mwanadamu.
25/06/2017


Mtumishi Veronica Gabriel akiongoza ibada hapa Efatha Ihumwa Dodoma.Maandalizi ya moyo ni ya mwanadamu.

Mchungaji Bonita kutoka makao makuu ya huduma ya Efatha mkoa wa Dodoma,Kisasa akifundisha muda huu hapa Efatha Ihumwa.So...
18/06/2017

Mchungaji Bonita kutoka makao makuu ya huduma ya Efatha mkoa wa Dodoma,Kisasa akifundisha muda huu hapa Efatha Ihumwa.
Somo:HURUMA YA MUNGU

Mtmsh Elizabeth Shauri akiongoza ibada muda huu hapa Efatha Ihumwa
18/06/2017

Mtmsh Elizabeth Shauri akiongoza ibada muda huu hapa Efatha Ihumwa

Kazi zinaendelea kwa NGUVU ZA MUNGU MKUU WA EFATHA.HALLELUYA
15/06/2017

Kazi zinaendelea kwa NGUVU ZA MUNGU MKUU WA EFATHA.HALLELUYA

13/06/2017

%&KUTOKA KWENYE MAKTABA YA&%
%%%%%&KITUME NA KINABII&%%%%
SOMO:YESU NDANI YAKO
{Lilifundishwa 22/6/2014}
MTMSH:WILBERT BASSANA{Mchngj kiongozi Shinyanga}
*Yoh 15:4-8
-Omba njia zako za rohoni zifunguke ili malaika watakaotumwa wakufikie.
-Kuna kumpokea Yesu na kuishi ndani yake na Yeye kuishi ndani yetu.
-Tukikaa ndani ya Yesu ni ili tukaweze yote katika yeye atuwezeshaye.{Wafilipi 4:13}
-Walio wa Mbinguni hawana msamiati wa kushindwa.
-Kushindwa huanza kwa kupungukiwa.
-Tabia huwa ulivyoamua.
-Yesu akikaa ndani yako,mwonekano wa Kiungu utapatikana.
-Dhambi ni aibu.
*Luka24:13
-Macho ya mtu asiye na Yesu moyoni mwake hufumbwa,atakuwa{Bwana Yesu}pamoja nao lakini hawatajua.
*Wale wawili walikuwa na Bwana Yesu lakini hawakumtambua.
*Walifunguka macho baada ya Yesu kuingia ndani yao.
-Lazima uwe na amani wakati wote.
-Ufalme wa Mungu kwa kawaida una utaratibu wake.
*Nje ya utaratibu,Mungu hatendi kazi.
OMBI:BWANA YESU NAOMBA UJIFUNUE KWANGU
-Hufai kuuliza utasemaje,Yesu Bwana akiwa majibu yapo.
*Ambia mlima NG'OKA,utang'oka.
-Bwana Mungu ana hesabu ya nywele zako,wewe mwenyewe za kwako na hujui hesabu zake,sasa asijue matatizo yako?Ni nini cha kwako hajui??
-OMBI:BWANA YESU,YATOSHA,WEWE KUWA MGENI KWANGU,YATOSHA.
-Utamshindaje shetani na silaha zake mwenyewe?una chuki,wivu n.k.
*Hata ukinena kwa lugha,hayo ni mapambo tu,chuki ukiwa nayo lazima ushughulikie,ukishindwa kushughulikia shetani hutamshinda.
*Bwana Yesu anasema kaeni ndani yangu nami ndani yenu sio chuki ikae ndani yenu.
*Utazaa sana Yesu akiwa ndani yako.
-Bwana Yesu hakuwa anapatikana usiku,alikuwa ana shughuli mbalimbali kwa ajili ya huduma mfano maombi milimani.
*Watesi wake hawangemk**ata k**a asingejipatiana kwao.
-Adam alishindwa na wewe ni mzawa wake,wewe ni k**a yeye tu.
*Unafanana na babako.
OMBI:OMBA USIFANANE NA BABAKO.
+BOMOA SURA YA BABAKO KWENYE SURA YAKO.
*Mizimu itakupotea.
*Ndoa ya Adamu itakupotea.
*Kutokufanikiwa kutakutoroka.
-Bwana Yesu anaumba yasiyokuwepo.
*Alifanya kuumba Gethsemane.
*MSALABA UNAOTEMBEZWA NA WATU K**A UNA NURU SHETANI HAWEZIKUMPATA MMOJA AKIWA NAO.{watu huvamiwa wakiwa na misalaba shingoni au mikononi}
*Anayekusumbua mpeleke Gethsemane,mtundike na misumari mikononi.
# Ukidhamiria kubadilika itakuwa.
I.C.T.-EFATHA KITUO CHA IHUMWA

13/06/2017

KATIKA MAKTABA YA@ @@ NA KINABII@@@
SOMO:FURAHA YA WOKOVU
{{{{{{elimu ya kubomoa dini}}}}}}}
•Ilikuwa ibada ya kuwapokea watoto wa imani.
-Luka 15
-Mafarisayo na masadukayo ni wale viongozi wa dini,wale ambao leo wanazuia watu kuokoka.
-Dini haiwezi kukusaidia kumjua Mungu maana haina maarifa.
-K**a hauna uhusiano mwema na Mungu kuponyeka kwa mgonjwa mikononi mwako ni 'ishu'.
-Yesu alikuchagua uje Efatha,uzae matunda na ili ukiomba akusikie.
-Watoza ushuru ni wale waliokataliwa na jamii.
-Unapookolewa wewe ni wa thamani mno.
-Mungu aliamua kukutafuta maana wewe ni wa thamani.
-Bila toba hutafika Mbinguni.
-Yesu akiingia ndani yako wewe ni mkuu.
-K**a tungekuwa tunaokoka tukifa,Yesu hangekuja duniani,angetusubiri huko huko tukifa anatuokoa.
-Yesu duniani hakuwa na usalama na alipitia mazingira magumu;iweje apitie hayo k**a wokovu ni baada ya kifo.
-Usiseme hela ni zako maana Mungu alisema kuwa mali na vyote ni vyake.
-Bwana Yesu anakuangalia moyoni unavyomwazia.
-Utabarikiwa ili ufanye kazi ya Mungu kiurahisi.
*Ukipewa gari litumie kuwaleta uliowashuhudia kanisani.
*Nyumba yako igeuze kanisa dogo.
-Duniani faida kubwa ya kutoka nayo ni kumpokea Yesu.
-Mtu akishakufa,ibada ya wafu HAITAM*OKOA.
-K**a Mbinguni wanaacha shughuli zao mmoja akiokoka duniani,wewe mbona unataka ufe na dhambi zako.
-Hutajuta kwa Yesu.
-Umepewa kibali.
-Hutakuwa k**a ulivyokuwa.
-Viongozi wa dini wana shida kuwa Bwana Yesu ananisikiliza.
-Sisi Efatha hatuamini kufa kwa ajali.
*Ukiingia kwa basi,fahamu kila mtu kuanzia muda huo yupo salama humo ndani.
-Ukimheshimu Mungu,atakuheshimu.
-Walio kwenye dini wamesikia Yesu ila hawamfahamu huyo Yesu.
-Musa alishika nyoka mkiani akageuka mti,ndivyo na sisi tutakavyoukausha uchawi.
-Iwa mwaminifu kwa Mungu,hutakufa kabla ya kazi k**a musa.
-ukimwi sio ugonjwa hatari,balaa ni dhambi alioifanya mtu ili aupate ukimwi.
-Kifo kipo ndani yako lazima ufanye juhudi kukishinda.
Lazima nijenge tabia ya kutubu ili malaika waje,Roho Mtakatifu aje,Bwana Yesu aje, Mungu Baba aje na Mbinguni niingie.
==> I.C.T. Huduma ya Efatha Ihumwa,,Dodoma

06/06/2017

%KUTOKA KWENYE MAKTABA YA%
-------KITUME NA KINABII-------
SOMO:Lilifundishwa siku ya mwisho ya semina ya Ukombozi-Julai 2015
¶MAELEZO KUHUSU ROHO MTAKATIFU WA MUNGU÷
-Ana majeshi.-Yoh 14:16-31
*Andiko hili linathibitisha kuwa Roho Mtakatifu yupo.
-Roho wa Mungu ana Roho nyingi zitendazo kazi.
-Isaya anazungumzia Roho 7 ambazo Ufunuo unaziita macho 7 ya Mungu.
-Mithali16:4~wabaya pia wameumbwa kwa kusudi.
-Mwanzo 1:4~Mungu akatenga giza na nuru.
*Katika maisha yetu lazima tutenge kilicho cha nuru na kilicho cha giza;kilicho cha nuru hicho tufanye na cha giza tusifanye.
*Mwanzo 3:22-25~kujua mema na mabaya kulimpelekea mtu kufukuzwa,alichanganya mwanga na giza,kabla ya hapo alikuwa mtakatifu alivyokusudiwa.
*Giza lina kundi lake(utawala wa chini)
*Nuru ni utawala wa kati.
*Roho ni utawala wa juu.
¶WAKUU WA GIZA KAZI YAO NI÷
{Wakuu wa giza ni wachawi,waganga wa kienyeji,wapiga ramli,wanajimu,wenye mapepo ya utambuzi,wafanya mazingaombwe.}
i}Kukufanya usiwe na maamuzi yoyote kuhusu Mungu
-Waliokoka wanakuwa wapo wapo tu.
-Ukitangaza maombi kwa mfano,huyu hana maamuzi huyahusu au yupo mtaani muda wa ibada.
ii}Kufanya mapenzi ya Mungu kimwili.
-Wiki inaisha hajafanya ya Mungu.
¶MKUU WA ANGA KAZI YAKE NI÷
i}Kukuangalia kokote unakoenda na kutoa taarifa kwa wakuu wa giza na mapepo ili wakudhibiti.
-Walokole wengi wanashindwa kufanikiwa kwa sababu huyu huwazuia wasifanye mapenzi ya Mungu.
-Lazima uuweke ufalme wa Mungu kwanza na haki yake utapewa+mengine uzidishiwe.
-Kumb la torati 28:1
*Lazima kusikia,kutunza kuyafanya maagizo yake naye atanitukuza duniani kote.
-Kituo kikuu cha Mungu duniani ni kanisa.
*Akisema mtmsh,lazima ufanye ni agizo.
-Baraka zitakujilia,hutazitafuta.
-Mambo hayaendi kwa kuwa umedhibitiwa.
ii}Anahakikisha umekufa kiroho.
-Kiroho wanaanza kufa alafu ndipo wanalala.
*Anakuua kiroho alafu anahakikisha umelala.
iii}Kukuchelewesha.
** #*** #** #** #** #** #** #** #** #*** #*
-Efeso 5:14~Amka,baada ya kuamka,Roho Mtakatifu anakufufua,alafu Yesu atakuangazia nuru yake alafu Rum 8:1{huna hukumu upo katika Kristo}alafu wanakuagiza ukaangaze{Isaya 60:1}
*Dan 12:3~Hawa hawakubali kufa kiroho ndiyo maana watang'aa.
-Efeso 2:13-Yesu alibomoa kiambaza ili ukaribie.
*Mkuu wa anga anakufuatilia kwa kuwa aliye na Kristo sio wa kawaida duniani.
-wakuu wa giza wanapewa taarifa na mkuu wa anga.
*mkuu wa anga anakuua kiroho alafu anawapa wakuu wa giza na mapepo taarifa ili wakushambulie kimwili.
hali hii Roho Mtakatifu na Bwana Yesu wanatuombea alafu Roho Mtakatifu anaingia mtumishi mmoja wa Mungu anaonyeshwa yanayokutesa afu anakupigania.
-Isaya 52:1~Amka Sayuni{mpendwa/mlokole}
-K**a hauna nguvu hauwezi kushinda
{Matendo 1:8}
*Nikiwa na nguvu nitashinda.
-Isaya 9:6
*Tunapewa Mungu mwenye Nguvu ili atusaidie.
*Yesu wetu sio wa show ni mwenye nguvu.
¶JINSI YA KUFANYA÷
i}Kuomba nguvu
-Usipowashinda hawa{mkuu wa anga na wakuu wa giza}huwezi kumpinga shetani.
-mkuu wa anga ni mfalme kwa hiyo ili kumshinda tunahitaji nguvu za kifalme.{Efeso 4:13}
-KAZI YA MUNGU INAENDA KWA MAJIRA NA NYAKATI.
-Lazima kuukomboa wakati ili÷
{i}Nimshinde,nikichelewa atanishinda.
{ii}Anajua majira ya Mungu kufanya kazi na mimi kwa hiyo baraka zangu atachukua.
-Mungu anaokoa na kukomboa,kukombolewa ni lazima usisikilize injili ya wainjilisti ya wokovu tu jua pia kuna Ukombozi.
-Usiwe mwepesi wa kutoa fedha yako kwa yeyote ambaye Roho wa Bwana hajakushuhudia umpe.
-Mtu anaweza kuwa anapigwa na Mungu hivyo na wewe ukimchangia pengine atibiwe hasira ya Bwana ikakuwakia.
-Usiwape wanaoombaomba mitaani bila ridhaa ya Roho Mtakatifu maana wengine ni mizimu kutoka kuzimu.
*Ukimpa mzimu hela yako ni zindiko kuzimu,unageuka mchawi au unakuwa kiloriti huelewi kwa nini.
-Hazina yako ilipo ndipo na moyo wako ulipo.
*Ukitoa kwa mchawi utapokea ya huko kwenye uchawi.
-Kila cha kwako kinafaa kumtumikia Mungu.
-Wafilipi 3:10-14
*Paulo anashughulikia yaliyopita.
*shetani anakukumbusha yaliyopita mfano huwezi wewe mjinga n.k.dawa ni KUSAHAU.
-Usiseme ulitukanwa siku ile sahau kaza mwendo fanya ulichoitiwa.
-mkuu wa anga haui mtu mpaka ajiue mwenyewe.
-Kufa au kuishi kuko katika ulimi wako.
-Efeso 3:16-17~Angalia Mungu katika upendo wake ndiyo uweze kusahau ya zamani.
¶SILAHA ZA MKUU WA GIZA KUKUMALIZA NI÷
i}Mwendo wako
2Tim 4:7
*Paulo alikuwa na mwendo.
*Paulo alikuwa na mwendo MZURI.
MWENDO MZURI ni pale mmoja anapoweza kuangalia majira na nyakati.
ii}Mwenendo~Kolosai 1:4-5
-Hapa maana yake ni jinsi unavyomaanisha,kujali na kuzingatia mambo ya Ufalme.
**-**-**-**-**AMINA-**-**-**-**-**-
I.C.T. EFATHA IHUMWA.
'share' tafadhali.....

Address

Bwawani, Ihumwa
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Ministry-Ihumwa Dodoma. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share