21/12/2022
MASOMO YA BIBLIA
SOMO LA 3: SIRI YA MSALABA (SEHEMU YA 2)
Katika somo lililopita [somo la 2: 👉 https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=108770145421065&id=100088642391653&mibextid=Nif5oz] tuliona “Siri ya Msalaba” na jinsi maneno ya Yesu katika Yohana 12:32 ambapo alizungumza juu ya kuwavuta “watu wote kwangu,” yanahusu fidia, bei inayolingana, ambayo alikuja kutoa, k**a alivyosema: “Kwa maana hata Mwana wa Adamu alikuja … kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi” (Marko 10:45). Hawa “wengi” tuliwaona pia wanamaanisha ulimwengu mzima wa wanadamu: “Kwa maana kuna Mungu mmoja na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, Mwanadamu Kristo Yesu, ambaye alijitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wote ” (1 Timotheo 2:5, 6) .
Hii fidia au bei inayolingana ilikuwa kwa ajili ya mtu mmoja—Adamu—ambaye kupitia yeye ulimwengu wote umerithi hukumu ya mauti. Biblia inasema hivi kwa uwazi: “Kwa maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na ufufuo wa wafu uliletwa na mtu. Kwa maana k**a ambavyo katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watahuishwa” (1 Wakorintho 15:21,22).
Katika somo lililopita tulijifunza bei ya fidia ambayo Yesu alitoa. Sasa tutazungumzia matokeo yake au, kwa maneno mengine, kazi ya fidia. Ilikuwa kupitia mtu mmoja Adamu kwamba jamii yote ilihukumiwa kufa, lakini kupitia dhabihu ya “Adamu wa pili,” mwanadamu wa pili mkamilifu, jamii yote itakombolewa kutoka katika mauti: “Hivyo katika Kristo wote watafanywa kuwa hai” Hii inaitwa kanuni ya mmoja kwa mmoja.
Kanuni ya "Mmoja kwa Mmoja".
Hebu tuone jinsi kanuni hii inavyofanya kazi: “Tena yaweza kusemwa ya kuwa, kwa njia ya Ibrahimu, hata Lawi apokeaye sehemu ya kumi alitoa sehemu ya kumi; kwa maana alikuwa katika viuno vya baba yake, hapo Melkizedeki alipokutana naye.” (Waebrania 7:9,10). Lawi alikuwa mmoja wa wana kumi na wawili wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu. Kwa hiyo Lawi alikuwa kitukuu wa Ibrahimu. Lawi alikuwa kichwa au baba wa kabila la Walawi ambao walichaguliwa kumtumikia Mungu katika Hema. Hawakupata sehemu katika nchi ya ahadi. Walipokea “zaka,” au sehemu ya kumi, kutoka kwa makabila yaliyosalia kwa utegemezi wao. Lawi mwenyewe hakuwahi kutoa zaka, alipokea tu. Lakini andiko la Waebrania latuambia kwamba Ibrahimu alipotoa “zaka” kwa Mfalme Melkizedeki, inaweza kusemwa kwamba Lawi (ambaye bado alikuwa hajazaliwa na “ akiwa katika viuno vya Ibrahimu”), ingeweza kusemwa kuwa alitoa zaka pia. Hii ndiyo kanuni ya "mmoja kwa mmoja".
Wanadamu wote “katika Adamu” wanachukuliwa kuwa walifanya dhambi na hivyo kuja chini ya hukumu ya mauti wakiwa bado hawajazaliwa na “ wakiwa katika viuno vya Adamu” wakati babu yao Adamu alipofanya dhambi katika bustani ya Edeni. Lakini wakati bei ya ukombozi, ya fidia inapolipwa kwa ajili ya Adamu, ulimwengu wote pamoja na Adamu unaachiliwa kutoka katika hukumu hiyo ya mauti iliyokuja juu ya Adamu na jamii yote ya kibinadamu. Huu ndio Mpango Mkuu wa Mungu kwa wanadamu wote: “Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa hiari yake, bali kwa sababu yake yeye aliyeutiisha katika tumaini; kwa kuwa uumbaji wenyewe nao utawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata uingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu” (Warumi 8:20,21). Hii inaonekana k**a lugha ya ajabu.
Hebu tusome tena: “Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa hiari yake, bali kwa ajili yake yeye aliyeutiisha katika tumaini” (Warumi 8:20). Neno “uumbaji” linarejelea jamii yote ya wanadamu. Waliwekwa “chini ya ubatili” au kwa maneno mengine, walipokea hali ya dhambi na mauti ya kurithi. Hilo lilifanywa “si kwa kupenda” kwa sababu kila mwanadamu hakupewa chaguo wala kushauriwa kuhusu jambo hilo. Ilifanyika kwa matumaini "yake Yeye" akimaanisha Mungu mwenyewe na mpango wake. Hiki kinarejelea kipindi ambacho “k**a katika Adamu wote wanakufa.”
Huenda wengine wakauliza, “Je, ni sawa au ni haki kwa Mungu kufanya hivi?” Kwa kweli hutokea mara kwa mara wakati wazazi hata kabla mtoto hajazaliwa, hufanya mipango kuhusiana na shule, kazi, na mafunzo bila kuuliza maoni ya mtoto. Maamuzi kwa maslahi ya mtoto hufanywa na wazazi. Hivyo na Mungu ambaye ni “ Baba ” wa viumbe vyote k**a ilivyoandikwa: “Kwa sababu hiyo nampigia magoti Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa” (Waefeso 3:14,15). Ndiyo, Mungu anao mpango wa ajabu kwa watoto wake wa kibinadamu.
Tunaona mpango huo wa ajabu tunapoendelea kusoma: “Kwa sababu uumbaji wenyewe nao utawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu hata uingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu” (Warumi 8:21). Ukombozi huu ni kupitia dhabihu ya fidia msalabani. “Uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu” unafafanua wokovu ambao Mungu atatoa kwa wanadamu wote kutoka katika hali hii ya dhambi na mauti.
Je, Hili Litatokeaje?
“Kwa maana hili ni jema, na lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu ambaye anataka watu wote waokolewe na kupata kujua yaliyo kweli” (1 Timotheo 2:3,4). Haya ni mapenzi ya Mungu kwa ulimwengu! Kwa ujumla maneno “kuokolewa” yanadhaniwa kumaanisha “kuchukuliwa kwenda mbinguni.” Ikiwa hiyo ndiyo maana hapa, lingekuwa jambo la kipuuzi kwa Mungu kuwachukua wanadamu wote katika hali yao ya kimaadili ya sasa kwenda mbinguni. Kando na hayo, ufahamu wa jumla kuhusu wokovu ni kwamba kwanza, mtu huja kwenye ujuzi wa ukweli na kisha “kuokolewa.” Hapa suala limebadilishwa! Kwa nini?
Mapenzi ya Mungu ni kwamba kwanza “watu wote waokolewe.” Hii inarejelea hali ambayo wanadamu wote wako nayo sasa, yaani, mauti au hali ya kuhukumiwa. Kupitia fidia watu wote “watafanywa kuwa hai”: “Nina tumaini kwa Mungu, ambalo hata hao nao wanalitazamia, ya kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia” (Matendo 24:15). Huu ndio kweli kuu ya ufufuo wa wafu wote.
“Ufufuo” ni fundisho la Biblia ambalo halijulikani kabisa ndani ya dini zingine zote. Ingawa dini zingine zinaweza kusema juu ya uhai baada ya kifo kupitia kuzaliwa upya kupitia tumbo la uzazi k**a katika Uhindu na Ubudha, au maisha katika “paradiso” ya kiroho k**a inavyofundishwa na Waislamu na hata Wakristo. Fundisho la Biblia la ufufuo ni tofauti sana. Biblia inanena jinsi Mungu kwa kutumia nguvu zake kuu za kimungu anavyoweza kuwarudisha kwenye uhai wale waliokufa na kuwa katkutokuwepo tena. Nguvu za Mungu zitarejesha kila mtu akiwa na mwili na akili k**a wakati alipokufa. Ni muujiza wa ajabu!
Wazee watafufuliwa katika hali ya uzee k**a wakati walipokufa; vijana watafufuliwa katika hali hiyo hiyo. Hata watoto wadogo na wachanga watafufuliwa wakiwa wadogo na wachanga k**a walivyokufa.
Neno la Kigiriki lililotafsiriwa ufufuo ni anastasis (Strong's Greek #386) na maana yake ni "kufufuliwa" au "kusimama tena." Kwa hiyo “ufufuo” kwa kweli haurejelei tu urejesho mkuu na wa kimuujiza kwa hali ya kuishi, bali pia kurudishwa kwa hali kamilifu ambazo Adamu aliwahi kufurahia. Ufufuo ni mchakato unaoanza na hali ya "kuamka kutoka kwa wafu".
Kwamba wote watafufuliwa kutoka kwa wafu inafundishwa wazi na Yesu: “Msistaajabie neno hili; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake nao watatoka” (Yohana 5:28) Hakika ni jambo lisilosadikika na la ajabu! Yesu anazungumza kuhusu siku kuu ya “kufufuka kwa wafu.” K**a vile leo wakati “k**a katika Adamu wote wanakufa” kipindi hicho kitakuwa utimizo wa “vivyo hivyo katika Kristo wote watahuishwa.”
Hili ni fundisho linalofundishwa katika Agano la Kale pamoja na Agano Jipya. Huu hapa ni mfano mmoja: “Wafu wako wataishi, waamke na kuimba, ninyi mkaao katika mavumbi kwa maana umande wenu ni k**a umande wa mimea, na nchi itawatoa wafu” (Isaya 26:19). Ni wazi sana: wafu wataamka kutoka kwenye “mavumbi.” Tunasoma tena: “Na wengi wao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka” ( Danieli 12:2 ). Iko wazi sana!
Maagizo Yanafuatia Ufufuo
Hivyo Mungu atafanya watu wote “waokolewe” kutoka katika mauti kwa njia ya ufufuo wa wafu. Kisha kuna hatua inayofuata katika mapenzi ya Mungu: : “… na kupata ujuzi wa kweli” (1 Timotheo 2:4). Wanadamu walishakufa wote katika dhambi na “wataamshwa,” “kufanywa kuwa hai,” katika hali iyo hiyo. Ni lazima basi wakombolewe kutoka katika dhambi. Hilo linawezekanaje? “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli” (Yohana 17:17). "Kutakasa" au "kusafisha" kutoka kwa hali na tabia ya dhambi hufanywa kupitia kweli.
Ujuzi wa neno la Mungu na kweli husababisha utakaso kutoka katika njia za dhambi kwa kutii neno la kweli. Baadhi ya mifano ni k**a lugha mbaya, ubinafsi, udanganyifu, uwongo n.k. Lakini pamoja na wafu wote “kuamka,” huu “ujuzi wa kweli” lazima ufunika ulimwengu wote. Hilo litatimizwaje? Hili ndilo jibu: “Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa Bwana, k**a maji yaifunikavyo bahari” (Habakuki 2:14). Ulimwengu wote utajawa na maarifa ya Neno la Mungu na Neno hilo ni Biblia!
Tunaona tena jambo lile lile likithibitishwa: “Kwa maana dunia itajawa na kumjua Bwana, k**a maji yaifunikavyo bahari” (Isaya 11:9). Njia ya kufanya hivi iko mbele ya macho yetu! Leo taarifa na maarifa hupitishwa katika kila nyumba kupitia redio, televisheni, intaneti, DVD, CD, nk. Vitabu vimebadilishwa na mawasilisho ya sauti-ya-kuona. Teknolojia hii imetengenezwa tu katika miaka 70 hadi 80 iliyopita. Hii inaonyesha jinsi tulivyo karibu na wakati huo wenye baraka. Hakika ufahamu wa jinsi aya hii itakavyotimizwa katika ulimwengu wetu mkubwa na wenye aina mbalimbali unazidi kuwa wazi siku baada ya siku. Ni k**a kuamka asubuhi moja na kutoka nyumbani mwetu na kukuta kamera, taa, magari ya kubebea jenereta, viti, lakini hakuna watu hata kidogo. Mtu angefikiria nini? Ah, kutakuwa na upigaji filamu hivi karibuni. Vifaa hivyo vyote kwa kawaida husababisha kufikia hitimisho hilo.
Vivyo hivyo leo. Kukiwa na teknolojia nyingi za kustaajabisha za kupeleka habari mbali zaidi papo hapo, wakati umekaribia ambapo “dunia itajawa na kumjua Bwana, k**a vile maji yaifunikavyo bahari.” Kuhusu wakati huo mtukufu imeandikwa: “Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao” (Yeremia 31:34). Hivyo wote watakuja kwenye ujuzi wa kweli na kupata fursa ya kutakaswa au kusafishwa kutoka katika dhambi zao.
Lakini mtu anaweza kuuliza, “Iko wapi nafasi ya walio hai na waliokufa?” Swali zuri! Hili ndilo agizo la Mungu kwa Adamu na Eva katika Edeni: “Mungu akawabarikia, akawaambia, Zaeni, mkaongezeke; na kuijaza nchi” (Mwanzo 1:28, NIV ). Amri ya Mungu haikuwa kuijaza zaidi bali “kujaza dunia”
K**a vile muuzaji wa tiketi za ukumbi wa michezo anavyojua wakati wa kuacha kuuza tiketi wakati tiketi zimeuzwa za kutosha kujaza viti, Mwenyezi anajua wakati wa kukomesha kuzaliana ili kutojaza zaidi dunia. Vile vile wakati kwenye kituo cha kujaza petroli mhudumu anapoagizwa "kujaza tanki," haijazi zaidi. Hakika Mungu mtakatifu na Mwenyezi angefanya vivyo hivyo.
Idadi ya watu duniani kwa sasa ni karibu watu bilioni 7. Mwanzoni mwa miaka ya 1800 ilikuwa bilioni 1. Kadirio la idadi ya watu wote waliowahi kuishi ni karibu bilioni 100. Sasa fikiria ukubwa wa Australia. Ni zaidi kidogo ya kilomita za mraba milioni 7.6 (mita za mraba trilioni 7.6). Ikiwa watu wote bilioni 100 wangewekwa Australia, kila mtu angekuwa na trilioni 7.6 ikigawanywa kwa bilioni 100 au mita za mraba 76 kila mmoja. (Wale wanaoishi New York City wana mita za mraba 94 leo.)
Kuna ulimwengu mzima wa kutoshea watu hawa wote. Australia, hata hivyo, ina 5% tu ya ardhi ya sayari yetu. Hakika Mungu amepanga vyema kujaza mandhari nzuri ya dunia hii na kila mtu ambaye amewahi kuishi!
Siku ya Hukumu ya Ulimwengu
Sasa, tunafikia mstari usioeleweka kwa kiasi kikubw: “Wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima; na wale waliofanya mabaya kwa ufufuo wa hukumu[†] ” (Yohana 5:29— “NIV inasema “wahukumiwe”).
//[[†] Neno la kiswahili “hukumu” ni tafsiri ya maneno mawili tofauti ya kiingereza: condemnation na judgment. Tafsiri ya kwenye Yohana 5:29 ni ya neno “condemnation” ambayo ina makosa. Neno sahihi la kiingereza iliyotakiwa kutumika kwenye Yohana 5:29 ni “judgement” ambayo tafsiri yake hata hivyo bado ni “hukumu”. Hivyo msomaji anatakiwa kuzingatia muktadha ili kutambua ni neno gani la kiingereza limetafsiriwa hukumu]//
Je, ufufuo wa wafu ambao wamefanya maovu ni ili tu wahukumiwe au kuhukumiwa? Je, kifo cha Yesu hakileti tumaini kwa ulimwengu maskini? Sivyo kabisa: “Kwa maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu; bali ulimwengu uokolewe kupitia yeye” (Yohana 3:17). Ulimwengu wote tayari uko chini ya hukumu ya mauti. Mungu alimtuma mwanawe ili kuokoa ulimwengu kutoka katika hiyo hukumu, sio kuhukumu ulimwengu ambao tayari umeshahukumiwa. Hukumu juu ya ulimwengu ni hukumu ya mauti pamoja na mateso na huzuni zake zote.
Neno lililotafsiriwa "hukumu" (KJV) au "kuhukumiwa" (NIV) katika Yohana 5:29 linatokana na neno la Kigiriki krisis ambalo lina maana sawa na neno la Kiingereza "crisis." Inamaanisha “wakati wa hukumu” au “dharura.” Huenda ikasemekana kwamba mtu fulani katika Kitengo cha Wagonjwa Mahututi cha hospitali aliingia katika “hali ya hatari,” yaani, katika hali ambayo kuishi au kufa hutegemea. Vivyo hivyo ulimwengu wa wanadamu “waliotenda maovu” huinuka katika “ufufuo wa hali ya hatari” au “ wa hukumu.” Hiyo ndiyo itakuwa siku ya hukumu ya ulimwengu!
Haya ndiyo tunayoyasoma juu ya hiyo “siku ya hukumu”: “Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemweka; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo hayo kwa kumfufua katika wafu” (Matendo 17:31). Katika siku hiyo ya hukumu mwamuzi aliyewekwa rasmi ni Bwana Yesu Kristo, ambaye kwa hiari alitoa uhai wake kwa ajili ya wokovu wa ulimwengu wote!
Je, hii “siku” ya hukumu ni ya kudumu kwa saa 24 tu? Hebu tupate jibu: “Lakini, wapenzi, msisahau neno hili moja, ya kwamba siku moja kwa Bwana ni k**a miaka elfu, na miaka elfu ni k**a siku moja” (2 Petro 3:8). Siku pamoja kwa Bwana sio masaa 24 bali miaka elfu moja! Hivyo tunaona “siku ya hukumu” ya ulimwengu hudumu miaka 1,000.
“Na wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele ” (Danieli 12:2). Neno milele linatokana na neno la Kiebrania olam, neno linalomaanisha "kudumu kwa zama" k**a katika kipindi cha wakati. Haina maana ya milele! “Dharau” inahusu kuwekwa wazi kwa kashfa na ufisadi na udanganyifu wote uliofanywa na watu wote. “Kwa maana hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana. Basi, yo yote mliyonena gizani, yatasikiwa nuruni; na hayo mliyoyanena masikioni mwa vyumbani, yatatangazwa juu ya dari za nyumba” (Luka 12:2,3). “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya” (Mhubiri 12:14).
Hii itakuwa “siku” ya hukumu iliyoje. Hebu wazia siri zote za ufisadi miongoni mwa watu binafsi, familia, na mataifa zikijulikana!
Sasa na tuone picha nyingine ya fidia ya Yesu: “Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria” (Wagalatia 4:4). Yesu alizaliwa akiwa Myahudi ikimaanisha “alizaliwa chini ya” sheria! Yesu ndiye pekee aliyewahi kushika torati kikamilifu na hivyo kupata thawabu yake. Uzima ndio zawadi inayotolewa na Torati: “Basi mtazishika amri zangu, na hukumu zangu, ambazo mtu akizitenda ataishi kwazo; mimi ndimi BWANA” (Mambo ya Walawi 18:5); “Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo” (Wagalatia 3:12).
Yesu alipata haki za uzima wa milele wa kibinadamu zilizotolewa na Torati, kisha akazitoa: “Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila mkate huu, ataishi milele; mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu” (Yohana 6:51). Yesu alidhabihu haki hizo za uhai wa kibinadamu kwa ajili ya “uzima wa ulimwengu.” Hivyo twasoma hivi kuhusu fidia ya Yesu : “Kwa maana Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa fidia kwa ajili ya wote, itakayoshuhudiwa kwa majira yake” (1 Timotheo 2:5,6). Yesu hakutoa kamwe haki zake za maisha k**a kiumbe wa roho wa mbinguni bali k**a mwanadamu, mwanadamu Kristo Yesu! Ni k**a kumiliki nyumba London na nyingine New York. Pindi moja ya nyumba inapotolewa au kuuzwa haiwezi kurudishwa tena. Hivyo na Yesu. Alikuwa na haki za maisha ya mbinguni, na haki za maisha ya binadamu au duniani! Naye alitoa dhabihu haki zake za maisha ya kibinadamu, asizichukue tena!
Sasa Bwana si mwanadamu tena bali ni roho au kiumbe wa mbinguni k**a ilivyoelezwa na mtume Petro: “Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu, akiuawa katika mwili, bali alihuishwa katika roho” (1 Petro 3:18). Kwa hiyo Bwana Yesu sasa ni kiumbe wa rohoni aliyetoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu pamoja na haki zake za uhai k**a fidia ya Adamu (taz. 2 Wakorintho 5:16). Hivyo Bwana anathibitisha kwamba ulimwengu hautamwona tena, kwa kuwa yeye si mwili tena: “Bado kitambo kidogo na ulimwengu hautaniona tena” (Yohana 14:19).
Uzao wa Yesu
Hatimaye tunaona kipengele kingine kinachohusiana na Bwana wetu Yesu na fidia yake : "Atauona uzao wake , atazidisha siku zake" (Isaya 53:10). “Uzao” unarejelea watoto wa Yesu! Yesu angeweza kuoa. Si vibaya kufanya hivyo (taz. Waebrania 13:4). Da Vinci Code, kitabu cha kubuni, kinadai Yesu alimuoa Mariamu Magdelene. Lakini Yesu alichagua kutooa mtu yeyote. Badala yake aliifanya jamii ya Adamu kuwa “uzao” wake na atakuwa “Baba yao wa Milele” katika ufufuo (Isaya 9:6). Ndiyo maana Isaya 53:10 inasema ataona uzao wake. Ulimwengu una mwokozi mzuri k**a nini!
Hivi karibuni dunia yote itajawa na utukufu wake: “Ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba” (Wafilipi 2:10,11).
Katika wakati ufaao ambapo wote watafanywa kuwa hai tena katika ufufuo wa wafu na kuambiwa kweli hii kuu, wote watamsifu Bwana kwa ajili ya upendo wake mkuu na dhabihu, na kuliabudu jina lake takatifu!
Amina!
K**a unataka kupata masomo yaliyotangulia bofya hashtag hapa chini
Contacts (Mawasiliano):
https://wa.me/+255757411482
https://www.facebook.com/profile.php?id=100088642391653
https://chat.whatsapp.com/K1SVIkrX6Ni7jJcL7PgXwX
https://instagram.com/fredrick.elia
https://www.facebook.com/fredrick.elia.33
http://www.linkedin.com/in/elia-fredrick-507558251
https://www.bibletoday.com