22/03/2026
KANISA LA EAGT CENTRAL DODOMA, IBADA YA JUMAPILI TAREHE 22/03/2026
MUHUBIRI: MCHUNGAJI DONALD CHOGO
SOMO: BARAKA ZINAZO BUBUJIKA.
BWANA anataka kuachilia baraka kwa watu wake jumapili ya leo.
Mwanzo 26:18-23
"Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye. Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika..."
Unaweza ukawa mtu wa thamani katika ulimwengu wa roho lakini bado kuna vitu atui anakunyang'anya.
Kila kitu lazima kibubujike
○Baraka isiyoisha
○Amani isiyoisha
○MUNGU atufanyie nafasi
K**a Mungu hajakubariki hata k**a uwe na upako wanamna gani ndoto ZAKO haziwezi kutumia.
Tamani Mungu akufanyie nafsi
MUNGU ni yule yule habadiliki aliye tenda kwa Ibrahim,Isaka na Yakobo anaweza Kutenda kwetu maana yeye ni Mungu wa maagano.
Kutoka 33:1
"BWANA akanena na Musa, Haya, ondokeni, katokeni hapo, wewe na hao watu uliowaleta wakwee kutoka nchi ya Misri, waende nchi hiyo niliyomwapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, niliposema, Nitakipa kizazi chako nchi hii; "
Zaburi 26:7
"Ili niitangaze sauti ya kushukuru, Na kuzisimulia kazi zako za ajabu."
Mwenye haki wa Mungu
●Haachwi na Mungu
●Analindwa na Mungu
●Anatetewa na Mungu
●Anapendwa na Mungu
MUNGU wetu habadiliki hata kidogo yeye ni Mungu wa maagano alitenda kwa wengine hata kwako anaweza Kutenda.
KUMBUKUMBU LA TORATI 7:9
"Basi jueni ya kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu; "
Kunawakati huhitaji kuomba vitu ila vitu tu vinatokea ukiwa unatamka vitu vinatokea
VITU VYA KUZINGATIA ILI BARAKA ZAKO ZITOKEE.
1 . Endelea kuwaleta watu ndani ya Yesu
2 .Endelea kutembea katika mapenzi ya Mungu
3 .Linda utakatifu wako.