22/01/2025
SIKU 42 ZA UTUKUFU UNAOONEKANA
MAOMBI YA MFUNGO,
JUMATANO, 22 JANUARI, 2025
SIKU YA 17: UPAKO WA ENHAKORE
ANDIKO LA MSINGI:
“Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, nalo lipo katika Lehi hata hivi leo.” — Waamuzi 15:19
UTANGULIZI:
Mungu akiingilia jambo la mtu, ushindi siyo jambo la kuuliza. Nimewafundisha watu jinsi ya kumfanya Mungu ahusike na mambo yao na kuwapa ushindi katika nyakati zote ngumu au nyakati za mashindano na majaribu. Biblia inazifunua kanuni nyingi k**a sadaka ya dhabihu, sadaka za kiagano k**a zaka na malimbuko, sadaka kwa ajili ya wahitaji, unyenyekevu kwa watumishi wa Mungu na watu wenye mamlaka, heshima kwa wazazi, shukurani, sifa kwa Mungu, na mambo mengine mengi. Lakini katika yote, hakuna njia inayofanya kazi haraka katika kumleta Mungu kwenye maisha yako k**a maombi na utii katika neno lake.
Maombi ni silaha kubwa sana ya mwamini, na lazima ifahamike kwamba mwamini hawezi kamwe kuishi maisha ya ushindi katika ulimwengu huu bila kuishi maisha ya maombi. Hatupaswi kuwa na maisha ya maombi k**a kitu cha ziada; maombi lazima yawe sehemu ya maisha yetu k**a vile kula chakula, kuoga, kulala, kujisaidia na mambo mengine ya lazima. Hakuna mtu ambaye anasema ana maisha ya kula, maisha ya kulala; kwa nini iwe na maisha ya maombi? K**a mtu atalala mara moja kwa siku au masaa matatu au kumi, haitapoteza ukweli kwamba hawezi kuishi bila kulala. Huu ndio mtazamo ambao mwamini anapaswa kuwa nao—kwamba hawezi kuishi kabisa, hawezi kamwe kuishi bila maombi.
Tuangalie jinsi Mungu alivyomsaidia Samsoni kuwapiga wanajeshi wa Wafilisti 1000 kwa utaya wa punda.
Waamuzi 15:14-17
¹⁴ Alipofika Lehi, Wafilisti wakapiga kelele walipokutana naye; ndipo roho ya Bwana ikamjia kwa nguvu, na zile kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa k**a kitani iliyoteketezwa kwa moto, na vile vifungo vyake vikaanguka mikononi mwake. ¹⁵ Naye akaona mfupa mbichi wa taya ya punda, akautwaa, akapiga watu elfu kwa mfupa huo; ¹⁶ Samsoni akasema, “Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, kwa taya ya punda nimepiga watu elfu.” ¹⁷ Ikawa, alipokuwa amekwisha kunena, akautupa ule mfupa wa taya mkononi mwake; na mahali pale pakaitwa Ramath-lehi.
Siri ya ushindi wa Samsoni ilikuwa ni ujio wa roho ya Bwana juu yake. Asingeweza kuyafanya haya kwa nguvu zake mwenyewe. Lakini baada ya ushindi huu, angalia kile anachosema; hamtukuzi Mungu. Anasema, “Kwa taya ya punda chungu juu ya chungu, kwa taya ya punda nimepiga watu elfu.” Samsoni alijua kuwa aliyemsaidia kufanya hayo ni Bwana, lakini hakumtaja kabisa; alijisemea yeye mwenyewe. Tunaweza kugundua kwamba Samsoni alijua kuwa ni Bwana aliyempa ushindi, kwa kuangalia maombi yake baada ya hapo.
Waamuzi 15:17-19
¹⁷ Ikawa, alipokuwa amekwisha kunena, akautupa ule mfupa wa taya mkononi mwake; na mahali pale pakaitwa Ramath-lehi. ¹⁸ Kisha akaona kiu sana, akamwita Bwana akasema, “Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu wasiotahiriwa.” ¹⁹ Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo.
MAARIFA YA KUSHIKA:
Kuna hakikisho katika Bwana kwamba anaweza kukushindia vita zako zote. Mungu anaweza kuja kwako kwa sababu ya agano lake na wewe, k**a tunavyoona alivyoacha roho yake ije juu ya Samsoni. Hatuoni Samsoni akiomba maombi yoyote ili Bwana ampe msaada kuwapiga Wafilisti, lakini tunaona kuwa Bwana alimtetea Samsoni kwa sababu alikuwa mkananishi wake, alikuwa na agano naye. Ndio, kuna baadhi ya mambo ambayo unaona Mungu anafanya kwako bila kuomba, lakini isikupe kiburi kwamba utafanya mengine bila maombi. Mtu ambaye haombi ili kupata fedha na mahitaji fahamu kuwa kuna kitu pia anapata kwa kuomba; usijilinganishe na mwingine. Unachopata wewe bila kuomba, mwingine anapata kwa maombi. Kuna watu wanapata watoto bila maombi, sadaka wala kuhangaika, lakini wengine watapata watoto kwa sadaka, maombi, na kulia mbele za Bwana. Kubwa katika yote ni kwamba yote hufanywa kwa utukufu wa Mungu na kwa hekima yake mwenyewe. Usiingie katika mtego wa kuiga maisha ya mtu; k**a mtu anaomba saa moja kwa siku na mambo yake yanaenda, haina maana wewe ukifanya k**a yeye mambo yataenda pia. Acha Roho Mtakatifu akupimie kipimo chako.
Samsoni anapobanwa na kiu, hasubiri tena roho wa Bwana aje juu yake na kumsaidia k**a ilivyotokea kwa Wafilisti. Anaamua kumwalika Mungu katika jambo lake. Nilikwambia kwamba tunaweza kuona kuwa Samsoni alijua wazi kuwa msaada wa kwanza alipata kwa Mungu, na tunaweza kuthibitisha hilo kwa kuangalia maombi yake.
“Wewe umetupa wokovu huu kwa mkono wa mtumishi wako; na sasa nitakufa kwa kiu, na kuanguka katika mikono ya watu wasiotahiriwa.”
Maombi haya yalikuwa ni ya kumchoza au kumsuta Mungu; hayana tofauti na maombi ya Musa wakati Mungu anataka kuwaua Waisraeli wote na kumwacha Musa na uzao wake. Musa aliongea maneno k**a haya.
Unachoweza kujifunza hapo ni kwamba tunapoomba, Mungu anahusika nasi moja kwa moja. Kwa mara nyingine, tunaona Mungu akifanya jambo na kumpa matokeo Samsoni. Hakuitwa mara ya kwanza, lakini alipoitwa hapa, alikuja na kufanya jambo.
“Lakini Mungu akapasua mahali penye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake ikamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo.”
— Waamuzi 15:19
Maana ya neno Enhakore ni KISIMA CHA MTU ALIYELIA, AU CHEMCHEM YA MTU ALIYEPAZA SAUTI YAKE.
Na kweli, Samsoni baada ya kumlilia Bwana, Bwana anapasua mahali penye shimo na kinachotoka hapo siyo tu maji, bali maji ya uzima, yenye uwezo wa kurejesha nguvu, kuleta burudani na kumfanya mtu apate nafasi na kuheshimiwa.
Katika yote unayopitia, umemwita Bwana? Umemlilia Bwana? Jibu likiwa hapana, basi mwite Bwana. Jibu likiwa ndiyo, basi mwite tena ukiwa na ufahamu huu mpya. Mungu atakupa majibu yenye uzito.
MWONGOZO WA MAOMBI:
Leo tutaomba k**a jana. Ni suala la mahitaji yetu. Hata hivyo, kutokana na ufahamu huu mpya, naamini utaomba kwa nguvu zaidi. Paza sauti yako k**a vile na Bwana atakutiririshia maji ya faraja na ushindi.
MISHALE YA MAOMBI:
• “Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?” — Warumi 8:32
1. i) Ee Bwana, ninayo mahitaji mengi kwenye maisha yangu, naamini huwezi kushindwa kunisaidia na kunivusha. Nivushe Bwana.
ii) Achilia wasaidizi wa hatma yangu kwa wingi, kutoka kila pande za ulimwengu waje na kuwa msaada kwangu.
iii) Ee Bwana, shughulika na maisha yangu, niondolee kila vikwazo vinavyojijia na kunisumbua kwa jina la Yesu.
• “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.”
— Warumi 8:26
2. i) Roho Mtakatifu, bado sijui kuomba inipasavyo kuomba, k**ata kinywa changu, akili, mwili, roho na nafsi yangu unifundishe kuomba.
ii) Bwana, nisaidie maisha yangu ya maombi, natamani kuomba bila kukoma, kuomba kwa usahihi na kuomba kwa muda mrefu. Rekebisha maisha yangu ya maombi.
iii) Roho wa Mungu, niombee mapenzi ya Mungu yatimizwe kwangu, niombee kwa kuugua, Bwana anayasikia maombi yako mno. Nisaidie kuomba.
• “Kwa kuwa k**a katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.” — 1 Wakorintho 15:22
Pata muda leo kuomba kwa ajili yako, unajua mahitaji yako, mwambie Bwana kwa imani atakupa.
MAELEKEZO:
• Maombi ni ya siku 42, tutafunga masaa 12 kila siku bila kunywa maji wala chakula. Tutafungua saa 12 jioni, na mwisho wa kula chakula ni kabla ya saa 03:00 usiku. Usile tena chakula baada ya hapo.
• Masaa ya kuomba na kusoma maandiko yaliyomo kwenye kila mwongozo ni kati ya 12:00 Asubuhi, 03:00 Asubuhi, 06:00 Mchana, 09:00 Alasiri, 12:00 Jioni, 03:00 Usiku, 06:00 Usiku, 09:00 Usiku.
• Watu wote tulioko Dar es Salaam tunakutana kujifunza Neno na kuomba kila siku za Jumatatu mpaka Ijumaa saa 10:30 Jioni mpaka saa 12:30 Jioni hapa kanisani Nations Altar Church (NAC) - Mbezi kwa MSUGURI. Unaweza kupiga simu 0716298890 ili kuweza kufika.
• Siku za Jumamosi na Jumapili tunakutana kuanzia saa 03:00 Asubuhi mpaka saa 08:00 Mchana kwa ajili ya Mafundisho na Maombi.
Prophet Jofrey Kaigarula
Nations Altar Church (NAC)
Mbezi Msuguri, Dar es Salaam, Tanzania.