St. Aidan Anglican Church-Airport

St. Aidan Anglican Church-Airport Kanisa la Anglikana Mtakatifu Aidano linapatikana dayosisi ya Dar es Salaam, achidikonari ya Ukonga.

08/08/2026

SALAMU ZA PONGEZI

Kutoka: Safina Anglikana Kwaya – Karakata
Kwenda: Rev. Can. Thomas H. Mwayela

PONGEZI KWA KUTEULIWA KUWA KATIBU MTENDAJI WA DAYOSISI YA DAR ES SALAAM

Kwa heshima na upendo mkubwa, sisi Safina Anglikana Kwaya kutoka Karakata, tunapenda kukufikishia salamu zetu za dhati za pongezi kwa uteuzi wako wa kuwa Katibu Mkuu Mtendaji wa Dayosisi ya Dar es Salaam.

Tunamshukuru Mungu kwa neema na kibali alichokupa hadi kufikia hatua hii muhimu katika safari yako ya utumishi. Tunaamini uteuzi huu ni ushuhuda wa uaminifu, bidii, hekima na moyo wako wa kujitoa katika kumtumikia Mungu na Kanisa lake.

Kwa upande wetu k**a Safina Anglikana Kwaya, tunajivunia kuwa sehemu ya historia yako. Kabla ya kufikia nafasi hii kubwa ya utumishi, uliwahi kuwa mwimbaji wa Kwaya ya Safina, na pia uliwahi kulitumikia kundi hili k**a Mwenyekiti wa Kwaya. Mchango wako, ushirikiano wako na moyo wako wa kulitumikia Kanisa kupitia huduma ya uimbaji vimeacha alama katika historia ya Kwaya yetu.

Leo tunapokuona ukipewa jukumu hili kubwa ndani ya Dayosisi, tunatambua kwamba safari yako ya utumishi imeendelea kukua, lakini msingi wa huduma ulioujenga katika maeneo mbalimbali, ikiwemo Safina Kwaya, unaendelea kuwa sehemu ya ushuhuda wako.

Tunakupongeza kwa moyo mmoja na tunakuombea Mungu akupe hekima, nguvu, afya, unyenyekevu na uaminifu katika kutekeleza majukumu haya mapya. Tunakuombea pia uwe chombo cha umoja, maendeleo na baraka kwa Kanisa na kwa watu wote ambao Mungu amekukabidhi kuwahudumia.

Hongera sana Rev. Can. Thomas H. Mwayela

Tunafurahi pamoja nawe, tunajivunia wewe k**a mmoja wa watu waliowahi kusimama katika safu za Safina Kwaya, na tunamtukuza Mungu kwa hatua hii mpya katika maisha yako ya utumishi.

“Mungu akubariki, akulinde na akupe hekima katika kila hatua ya utumishi wako mpya.”

Kwa niaba ya Safina Anglikana Kwaya – Karakata,
Tunakupongeza na kukutakia utendaji mwema na wenye baraka katika Dayosisi ya Dar es Salaam.

Hongera sana, Mtumishi wa Mungu!
Hongera Katibu Mtendaji wa Dayosisi ya Dar es Salaam!

SAFINA ANGLIKANA KWAYA – KARAKATA
“Tukiimba kwa ajili ya Mungu, tukihudumu kwa ajili ya watu.”

St. Aidan Anglican Church-Airport

Leo katika kumbukizi. Wanakwaya wa kwaya ya vijana kutoka kanisa la Anglikana Mt. Aidano Karakata wakiwa katika picha ya...
06/08/2026

Leo katika kumbukizi.
Wanakwaya wa kwaya ya vijana kutoka kanisa la Anglikana Mt. Aidano Karakata wakiwa katika picha ya pamoja. Injili ya Kristo inaenezwa kwa njia ya uimbaji pia.

06/08/2026

Bwana Yesu Asifiwe

Sisi Kwaya Ya Safina Kutoka Kanisa Anglikana Karakata Tunapenda Kuwafahamisha Kuwa Bado Album Yetu Iko Sokoni, Hivyobasi Kwa Wewe Mdau Wetu, Rafiki Yetu Na Mkristo Mwenzetu Katika Imani Tunapenda Kukukaribisha Kuungana Nasi Katika Ununuzi Wa Album Hii Ili Uendelee Kufanyika Baraka Katika Maendeleo Ya Kwaya Yetu Pamoja Na Ukuaji Wa Uimbaji Ndani Ya Kanisa Letu.

TAYO Day 2026.
04/08/2026

TAYO Day 2026.

Matukio katika picha wakati wa ibada ya kuadhimisha Sikukuu ya TAYO (TAYO Day) katika Mtaa wa Mt. Aidano Karakata. Ibada...
04/08/2026

Matukio katika picha wakati wa ibada ya kuadhimisha Sikukuu ya TAYO (TAYO Day) katika Mtaa wa Mt. Aidano Karakata. Ibada hiyo ilifanyika katika siku ya Bwana Jumapili ya tarehe 02/08/2026, katika picha ni baadhi ya vijana wakiongozwa na mwenyekiti wao Oliver John Mguye. Ibada iliongozwa na Kasisi wa Mtaa Rev. Fr. Leonard Msamati na mahubiri yaliongozwa na mtumishi wa Mungu Mwl. Edward John kutoka kanisa la Anglikana Kristo Mfalme-Kinondoni.

Matukio katika picha wakati wa ibada ya Jumapili tarehe 26/07/2026 kanisani Mt. Aidano Karakata. Ibada iliongozwa na Ask...
27/07/2026

Matukio katika picha wakati wa ibada ya Jumapili tarehe 26/07/2026 kanisani Mt. Aidano Karakata. Ibada iliongozwa na Askofu John Mwela (mstaafu) kutoka Dayosisi ya Southern Highland pamoja na mwenyeji wake Kasisi Leonard Msamati pamoja na wasaidizi wengine wakiwemo Lay Canon Samson Mwela, Mwinjilisti John Musai na Mwinjilisti Joyce Mtembezi. Katika ibada hiyo kulifanyika shukurani kutoka idara ya UMAKI ambao walikuwa wakiadhimisha sikukuu yao katika mtaa, kuwaingiza katika huduma UMAKI Juniors, Jumuiya ya Mt. Paulo kuchukua ushindi wa jumla katika Sadaka ya Merejesho ya kila mwisho wa mwezi pamoja na ubatizo wa waumini wapya wawili.
Karibu tuabudu pamoja kila siku ya Jumapili kuanzia saa 01:00 asubuhi hadi saa 04:00 asubuhi.

TAYO DAY! TAYO DAY! Karibuni katika siku ya kuazimisha sikukuu ya TAYO katika kanisa la Mt. Aidano Karakata.
24/07/2026

TAYO DAY! TAYO DAY! Karibuni katika siku ya kuazimisha sikukuu ya TAYO katika kanisa la Mt. Aidano Karakata.

01/06/2026

Jumuiya ya Mt. Paulo wakikabidhiwa kombe lao la ushindi.

Matukio katika picha wakati wa ibada ya Jumapili, jumuiya ya Mt. Paulo kutoka kanisa la Mt. Aidano waliibuka washindi wa...
01/06/2026

Matukio katika picha wakati wa ibada ya Jumapili, jumuiya ya Mt. Paulo kutoka kanisa la Mt. Aidano waliibuka washindi wa jumla katika tukio la sadaka maalum ambayo hutolewa kila mwisho wa mwezi.

Address

Anglican Church, DSM Diocese
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when St. Aidan Anglican Church-Airport posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share