Tikeysu Media

Tikeysu Media Wasilisho la taarifa ya mkuu wa shule kuvamia kituo cha uandikishaji. Utangulizi
Ni taarifa ya habar

17/10/2024

Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, ametoa wito wa kualikwa mara moja kujiunga na NATO wakati akiwasilisha "mpango wake wa ushindi" kwa bunge la Ukraine ili kumaliza vita dhidi ya Urusi. Mpango huo unalenga kuhamisha mapigano kwenye ardhi ya adui na kuweka shinikizo kwa Kremlin, huku pia ukipendekeza matumizi ya silaha kubwa zisizo za nyuklia ili kuzuia uchokozi zaidi wa Urusi. Zelensky pia alisisitiza haja ya kuondoa vikwazo vya matumizi ya makombora ya masafa marefu kutoka nchi za Magharibi. Wakati huo huo, Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz alisisitiza umuhimu wa kumaliza vita kwa kushirikiana na Ukraine. Katika uwanja wa mapambano, vikosi vya Ukraine vimedai kudungua droni nyingi za Urusi zinazolenga Kyiv na miji mingine, huku mashambulizi yakiendelea.

17/10/2024

DODOMA: Wakili Peter Madeleka akielezea mwendelezo wa Shauri la jinai lililofunguliwa na Wakili Paul Kisabo dhidi ya Fatma Kigondo kutoka katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Dodoma, amesema wamemuelekeza Hakimu anayesikiliza Shauri hilo, Nyambuli Tungaraja kusaini Hati ya Mashtaka ili Mtuhumiwa asomewe tuhuma zake popote alipo

Mtuhumiwa Fatma ambaye hakufika Mahak**ani hapo ikidaiwa anaumwa, anatuhumiwa kuratibu ubakaji na ulawiti wa kundi dhidi ya mwathirika anayetambulika kwa jina la “Binti wa Yombo Dovya”

Soma https://jamii.app/AfandeUpdates

17/10/2024

Mara nyingi Wanawake hukumbana na mtazamo hasi kutoka kwa jamii, hasa kwenye michakato ya Kisiasa ambapo nafasi za uongozi zimekuwa zikihusishwa zaidi na Wanaume

Utamaduni huu unawapa Wanaume nafasi zaidi katika maamuzi huku Wanawake wakionekana k**a Wasaidizi au Walezi wa Familia, hali inayoleta changamoto kwao kuingia katika Siasa

Tukumbuke, Haki ya kushiriki katika Siasa ni ya kila mtu, bila kujali jinsia. Tunatokaje hapa?

Mjadala https://jamii.app/UshirikiWaWanawakeSiasaTz

17/10/2024

PWANI: Baada ya kuk**atwa kwa Watuhumiwa wanne wa Taasisi ya Mikopo ya OYA, leo Oktoba 16, 2024 wamefikishwa Mahak**a ya Wilaya ya Kibaha wakituhumiwa kwa mauaji ya kukusudia ya Juma Said Seif (45), Mkaazi wa Kitongoji cha Mbagala Mlandizi yaliyotokea Oktoba 7, 2024

Wakili wa Serikali, Monica Mwela amewataja Watuhumiwa hao ni; Abdallah Felix Wendiliwe (32) Mkaazi wa Janga Mlandizi, Emmanuel Joshua Olala (24), Dastan John Charles (23) na Christopher John Charles (23) wote Wakaazi wa Kilangalanga, Mlandizi

Hakimu Mkazi Mfawidhi, Emmaneli Lukumai amesema ushahidi wa kesi hiyo iliyosomwa kwa mara ya kwanza bado haujakamilika, hivyo kesi hiyo imehairishwa hadi Oktoba 30, 2024, ambapo Watuhumiwa wote wamerudishwa rumande

Soma https://jamii.app/MkopoOYA

17/10/2024

USWISI: Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akifungua Mkutano Mkuu wa 149 wa IPU uliofanyika Geneva, Uswisi amewasisitiza Wajumbe wa Bunge hilo kumuamini na kumpa nafasi afanye kazi yake na waache kufikiria dhana ya Ukoloni kwa wanaofikiria hiyo

Amesema hayo baada ya baadhi ya Wajumbe kukosoa uamuzi wake wa kufanya ziara Urusi na kukutana na Rais Vladimir Putin

Mkutano huu umehudhuriwa na takribani Washiriki 1,500 wakiwemo Maspika, Naibu Maspika, Wakuu wa Misafara na Wabunge, na unatarajiwa kuhitimishwa Oktoba 17, 2024 kwa kutoa maazimio muhimu yatakayolenga kutatua changamoto za Kimataifa zinazoikabili Dunia kwa sasa

Soma https://jamii.app/PCUTulia

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA CHADEMA WAJISALIMISHA ACT-WAZALENDO." Tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za...
17/10/2024

KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA CHADEMA WAJISALIMISHA ACT-WAZALENDO.

" Tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, Vijiji na Vitongoji vyama vyetu vya Upinzani vipo hoi kiuchumi. Sisi CHADEMA tumekubaliana na wenzetu wa ACT wazalendo katika uchaguzi huu wa serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji tutasimamisha mgombea mmoja wa upinzani. Hii ndiyo njia pekee ya kushindana na CCM kwenye huu uchaguzi wa Novemba, 2024". Ndug. Freeman Mbowe Mwenyekiti wa CHADEMA akiongea na waandishi wa habari leo tarehe 16 Octoba, 2024. Mikocheni, Dar es Salaam.

17/10/2024

📍Netherlands, The Hague

Tazama Mhe. Caroline Chipeta, Balozi wa Tanzania nchini Netherlands akielezea namna alivyofungua akaunti ya Twiga Diaspora Banking na kupata NBC Visa Debit Card papo hapo.

Karibu Ubalozini, Groot Hertoginelaan 28, The Hague tukufungulie akaunti hii na upate nafasi ya kubenki bila mipaka, yaani unajisikia upo home hata ukiwa ughaibuni.

17/10/2024

Ndugu mteja wa Benki ya NBC, sasa unaweza kutuma au kupokea pesa bila kuwa na akaunti. Tumekutelea mbinu ya kurahisisha miamala kwa ndugu jamaa na marafiki.

Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwa Wakala wa NBC ukiwa na namba yako ya NIDA na Namba ya simu ya mpokeaji tu.

Wasiliana nasi kupitia 0800711177 (BURE) kwa msaada zaidi.

17/10/2024

Timu yetu imewasili Netherlands kukukaribishwa na Mhe. Balozi Caroline Chipeta, tayari kuanza kutoa huduma ya Twiga Diaspora Banking kwa Watanzania waishio Netherlands na Kanda ya Ulaya.

Huduma zetu za Twiga Diaspora Banking zitapatikana kuanzia leo tarehe 14 na 15 Agosti Ubalozini, Groot Hertoginelaan 28, The Hague.

Aidha huduma hizi pia zitapatikana pia tarehe 16 na 17 Agosti 2024 wakati wa Bonanza la Serengeti, Sportpark Wanica, Mellis Stokelaan 117, 2541 GA, The Hague.

Karibuni sana.

Address

Kinyerezi
Dar Es Salaam
1224

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tikeysu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share