BIBLE STUDY

BIBLE STUDY Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from BIBLE STUDY, Religious organisation, Dar es Salaam.

SIPENDAGI SANA KU SHARE SHUHUDA ZA WATU NAWEKA TU HUU MMOJA ILI NIKUHAMASISHE MDADA UJIUNGE NA GROUP LETU LA WADADA UPAT...
15/02/2025

SIPENDAGI SANA KU SHARE SHUHUDA ZA WATU NAWEKA TU HUU MMOJA ILI NIKUHAMASISHE MDADA UJIUNGE NA GROUP LETU LA WADADA UPATE MAFUNDISHO YA KILA SIKU AMBAYO PIA SIWEZI KUWEKA HAPA,, JAPO BAADHI UTAYAPATA KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK Dadaz To Jesus

NAFASI ZIPO 15 TU WAHI MAPEMA, K**A NI KAKA MTUMIE MDOGO WAKO AJIUNGE, KUNA WATU WALINIPA WADOGO ZAO HAPAHAPA FB NI MASHAHIDI WA JINSI WAMEKUWA WA TOFAUTI KITABIA NA MWENENDO

HAYA LINK HII HAPA https://chat.whatsapp.com/HW6iZ6Ia7mJ3TJo4tQiz8d

15/01/2025

OGOPA SANA VITU HIVI VINAWEZA KUUHARIBU MOYO K**A HUJAKOMAA SAWASAWA

John 3:30
[30]He must increase, but I must decrease.
Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi kuzidi, bali mimi kupungua.

1. WATU WANAPOKUAMBIA UNA KITU KIKUBWA SANA
2.WATU WANAPOKUAMBIA WANAGUSWA SANA NA WEWE
3.WATU WANAPOKUAMBIA WEWE NI BARAKA SANA
4.UNAPOPEWA MAJINA MAKUBWA MAKUBWA YA KIUTUMISHI
5.WATU WANAPOKULETEA SHUHUDA ZA KUJENGWA KUPITIA WEWE.
6.WATU WANAPOKUSIFIA SANA

SI VIBAYA WATU KUSEMA NA PENGINE WANAYOYASEMA YANA UKWELI TENA SANA, WAKATI MWINGINE UNAWEZA KUWA UNAFANYA ZAIDI YA WANAVYOKUAMBIA

👊🏼CHUNGA SANA USIJE UKAHARIBU MOYO KWA SIFA ZA WANADAMU

📌SIFA ZINA NAFASI KUBWA YA KUMPELEKA MTU JUU ZAIDI IKIWA ZITAMFIKIA MTU SAHIHI, UHAYA WA KIROHO UNAHARIBU MOYO, BADALA YA KUMPELEKA MTU JUU UNAMPOROMOSHA TARATIBU NA BAADAE MTU HUYU ANAKWISHA KABISA YANABAKI MAZOEA

📌UNAPOPOKEA SIFA ZICHUKUE ZOTE MPE MUNGU HALAFU MOYONI MWAKO UBAKI PATUPU BILA SIFA HATA MOJA ITAKUSAIDIA SANA . SAHAU ZILE SIFA LAKINI USISAHAU WEWE NI NANI, FANYA TENA KWA BIDII ZAIDI SIFA ZITAKUJA MPE TENA YESU, KAMWE HUTAKUWA NA KIBURI WALA KUJIINUA, BAADA YA KUMPA YESU SIFA ZOTE KUMBUKA HUTABAKI NA KITU, UTARINGIA NINI?

📌UNAPOPEWA SIFA K**A WEWE NDIYE UMEFANYA ZIKATAE HAPOHAPO NA KUONYESHA KUWA NI MUNGU AMEFANYA. KADRI WEWE UNAVYOPUNGUA YEYE ANAINULIWA.

UNAJUA YESU ANAFANYAGA NINI ANAPOINULIWA JUU?
Ephesians 4:8
[8]Wherefore he saith, When he ascended up on high, he led captivity captive, and gave gifts unto men.
Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.
💥VIPAWA VILIPATIKANA BAADA YA YESU KUINULIWA JUU. KWA HIYO HICHO ULICHO NACHO NI MATOKEO YA YESU KUINULIWA JUU NA KITAENDELEA KUNG'ARISHWA ZAIDI YESU AKIINULIWA JUU
💥LAKINI YESU AKIINULIWA JUU UNAKUA MATEKA WA KWAKE, UNAJUA MAANA YA KUWA MATEKA? MAANA YAKE UNAKUWA UNAMILIKIWA NA YEYE, KILA KITU CHAKO IKIWEMO SIFA HIZO NI ZAKE, LAKINI UNAKUWA MATEKA PALE ANAPOINULIWA, ASIPOINULIWA NAANA YAKE UMEJITOA KATIKA UTAWALA WA KWAKE.

KUMAINTAIN VIWANGO VYA JUU VYA UTENDAJI NI LAZIMA YESU AINULIWE JUU, NA ANAVYOINULIWA JUU SANA NDIVYO ANAACHILIA MARADUFU.

WENGI WETU TUKIPATA SIFA NDIO KWANZA MABEGA YANAPANDA JUU NA TUNATAKA KUTREATIWA HADHI YA VIP, HATA UPOKEE SIFA ZA AINA GANI IKIFIKA MAHALI KWENYE HUDUMA MMEENDA KIKUNDI UMEOMBWA USUGUE SUFURIA NENDA, UKITAKIWA KULETEA WATU VITI PELEKA WATU WAKAE, WAKIKUTAKA UTANDIKIE WENGINE VITANDA WEWE FANYA, NA WAKATI MWINGINE USISUBIRI UAMBIWE

UNAJUA KWA NINI UNAWEZA KUKASIRIKA UKIPEWA MAJUKUMU FULANI NA UKAJIHISI UNADHARAULIWA? NI KWA SABABU YA ZILE SIFA, UMEZIPOKEA, UKAZIWEKA MOYONI NA KUJIMILIKISHA NA KUONA KUNA VITU HUSTAHILI KUVIFANYA LAKINI AMINI KWAMBA WAKATI WA KUDHIHIRISHWA KWAKO BADO NDIO MAANA WATAKUOMBA USAIDIE KUOSHA VYOMBO, KWA NINI? NI KWA SABABU BADO HUJAFIKA HIBYO VIWANGO VYA VIP..NYENYEKEA SANA SANA WAKATI WAKO UKIFIKA KILA KITU KITAJIPANGA MAHALI PAKE, WAKATI WA KUKETISHWA NA WAKUU HATUTAKUONA JIKONI UKIGOMBANIA UKOKO NA KIPORO CHA WALI, UTAHUDUMIWA PAMOJA NA WAKUU

SIFA NYINGI SI KIPIMO CHA KIWANGO CHA MTU KUKUA KWA SABABU WAPO PIA WANAOSIFIA KINAFIKI NA UONGO PIA. KIPIMO NI UKOMAVU WA KUFANYA KWA MUENDELEZO NA BILA KIKOMO BILA KURUHUSU MATOKEO MAKUBWA UNAYOYAONA YAATHIRI TABIA NA KUUHARIBU MOYO.

UTAKAPOWEZA KUHANDLE SAUTI HIZI ZINAZOSIKIKA MASIKIONI MWAKO ZILIZOJAA SIFA NA UTUKUFU ZISIUJAZE MOYO UNAPANDA HATUA, UNAONGEZA KUAMINIWA NA MUNGU KWA VITU VIKUBWA ZAIDI.

MAOMBI: BASI ATUKUZWE MUNGU ALIYEMKIRIMIA MWANAYE YESU UTUKUFU, NA SIFA NA HESHIMA NAYE AKAACHILIA VIPAWA NA KARAMA KWETU SI KWA AJILI YETU SISI BALI YEYE APATE KUTUKUZWA KWA KILA KAZI TUTENDAYO KUPITIA JINA LAKE. BASI SISI TU WATENDA KAZI TU NA HATUPASWI KUGUSA UTUKUFU WAKO MUNGU. TUJALIE UNYENYEKEVU KATIKA HALI ZOTE NA MAZINGIRA YOTE TUKIJUA KUWA WA KUHIMIDIWA NI YULE PEKEE ANAYEMPA KILA MMOJA KWA KADRI ALIVYOKUSUDIA. MIOYONI MWETU KUSICHIPUE KIBURI NA MAJIVUNO, BALI TUZIDI KUSHUKA SANA ILI UTUINUE WEWE NA SI KUJIINUA KWA MANENO YA WATU.

Matthew 6:13
[13] [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]

Ireen

15/01/2025

KUHUSU WENYE MPANGO WA KUTOA MIMBA

SHALOM,

NINA UJUMBE JUU YAKO WEWE AMBAYE UNA MPANGO WA KUTOA MIMBA NA PENGINE UNA MAUMIVU MOYONI KWA SABABU SIO TABIA YAKO LAKINI IMEKUBIDI TU PENGINE LABDA HALI YA MAISHA, MWANAUME PENGINE AMEIKATAA MIMBA, PENGINE UNASOMA NK.

LAKINI KUNA AMBAYE KWAKO NI KAWAIDA TU K**A KULA KARANGA, POLE SANA SIO WEWE NI ROHO YA IBILISI NDANI YAKO K**A VILE SHETANI ALIPOMVAA HERODE ILI AUE WATOTO. KILICHOKUA KINATAFUTWA PALE SI WATOTO BALI KUFUTA AGENDA YA UKOMBOZI KWA HIYO ANAYETOA MIMBA HAUI MTOTO TU BALI ANATUMIWA NA SHETANI KUUA HATIMA.

LAKINI WEWE AMBAYE UNADHANI KIUMBE KINATOKEA ILE SIKU ULIPOKUTANA NA MWANAUME, HIVYO UKITOA HUONI HASARA SANA

NAOMBA UJUE MTU ANA NAFSI, ROHO NA MWILI, PALE MIMBA INAPOTUNGWA MAANA YAKE NI KIUMBE AMBACHO KILIKUWA KATIKA ROHO KINAUVAA MWILI, INAMAANA ULE NI MWANZO TU KATIKA MWILI LAKINI MWENDELEZO WA MAISHA YA ROHONI YALIYOKUWA YANAENDELEA

Jeremiah 1:5
[5]
Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

JARIBU KUONA HAPA, MFANO MAMA YAKE YEREMIA ANGETOA MIMBA MAANA YAKE YEYE ANGEDHANI AMEUA KIJUSI TU LAKINI KUMBE AMEUA NABII WA MATAIFA

KABLA MTOTO YOYOTE HAJAWEKWA KWENYE TUMBO LA MAMA YAKE ANAWEKWA WAKFU KWAMBA HUYU NI NABII, NI MFANYABIASHARA MKUBWA, NI RAIS, NI MCHUNGAJI NK. KWA HIYO WEWE UNAWEZA KUDHANI KILICHOINGIA NI KIMIMINIKA TU KUMBE ANAINGIA RAIS KATIKA ROHO ILI AUVAE MWILI KUPITIA TUMBO LAKO UNAONA SASA.

HIKI KIUMBE HATA K**A KIMEINGIA KATIKA MWILI KUPITIA WATU WENYE HATIA HAINA MAANA KWAMBA MUNGU ANAFUTA KUSUDI LA KUKIWEKA WAKFU KABLA HAKIJAINGIA TUMBONI.

KUTOA MIMBA ACHILIA KWAMBA NI UUAJI WA KIUMBE KISICHO NA HATIA NA KWAMBA TUNAWEZA KUSEMA MWANADAMU HANA HURUMA, AMEKUA KATILI, LAKINI JUA KUTOA MIMBA NI ZAIDI YA KUUA KIUMBE KISICHO NA HATIA

TUKITAZAME HIKI KIUMBE KWA NAMNA YA ROHO, MUNGU AMEKUSUDIA MATAIFA YAFIKIWE, AMEKUSUDIA PENGINE AMEBEBA JIBU LA KIZAZI HIKI NA MENGINE MENGI AKATENGENEZA WAZO AKALIFANYIA KAZI NA AKASUKA MKAKATI MZIMA JUU YA HII ROHO INAYOKWENDA KUVAA MWILI KWA AJILI YA KUTEKELEZA AGENDA YA MUNGU, WEWE UKISHAONA KITUMBO KIMETUNA UNAKWENDA KUTAFUTA MESSO TUASSUME NI SHILINGI ZA KITANZANIA 20,000 UNAUA. YANI KWA MTAJI WA SHILINGI 20000 UNAHARIBU ROHO AMBAYO INGEWEZA KUOKOA MAMILIONI. HII NI BIASHARA, LAKINI BIASHARA KICHAA. NI KWELI UTABAKI FREE UTAENDELEA NA SHULE, WAZAZI WATAENDELEA KUKUINA K**A BINTI YAO MWEMA, NA PENGINE BOYFRIEND NDIYE ALIKUAGIZA UTOE HIVYO MTAENDELEA NA MICHEZO YENU SI UMESHASHUSHA MZIGI BHANA

ROHONI HII NI HASARA, HUJAUA TU KIUMBE KISICHO NA HATIA BALI UMESHINDANA NA MUNGU. HUJAUA KIJUSI HAPO, UNAMFANYA MUNGU ATENGENEZE TENA MPANGO MWINGINE KUREPLACE HUYU ULIYEMUUA, HIVYO JUA NI KUSHINDANA NA MUNGU HUKU. YAANI UNACHELEWESHA MALENGO YA MUNGU.

MTU YEYOTE ANAYEZALIWA KATIKA HALI YA DHAMBI ANAWEZA PIA KUBEBA KUSUDI KABISA HAIJALISHI MAZINGIRA ALIYOZALIWA,

WAPO WENGI WALIZALIWA KATIKA UZINZI SASA NI WATUMISHI WA MUNGU WAZURI, WAMEOKOKA WANAMPENDA YESU, WAPO AMBAO MAMA ZAO WALIBAKWA LAKINI WATOTO WAO WALIZALIWA WAKIWA WAMEBEBA HATIMA KUBWA SANA. USIANGALIE HALI NA MAZINGIRA, FIKIRIA KUHUSU MTU WA NDANI WA HUYO KIUMBE NDIPO UFANYE MAAMUZI.

Psalms 51:5
[5].
Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani.

MIMBA KUCHUKULIWA HATIANI HAIMAANISHI KWAMBA ATAKAYEZALIWA NAYE ATAISHI KATIKA HIYO HATIA. K**A NI HIVYO DAMU YA YESU INGEKUWA FASHION TU. LAKINI KWA DAMU HATA DHAMBI NYEKUNDU SANA ZINAKUWA NYEUPE.

UKISHABEBA MIMBA JUA SIO BAHATI MBAYA, KUBALI UNAYO NA HAKUNA NAMNA YOYOTE BALI KUZAA. TAYARI UMEPEWA DHAMANA YA KUHAKIKISHA HUYU KIUMBE ANAKUWA SALAMA KUANZIA TUMBONI NA AKISHAZALIWA PIA MAISHA YAKE NA USALAMA WAKE UPO MIKONONI MWAKO KWA KUMLINDA LAKINI KUMFUNDISHA KATIKA NJIA IMPASAYO MPAKA PALE KILE KILICHO NDANI YAKE KITAKAPODHIHIRIKA.

KUTENDA UOVU WOWOTE WA KUTOA UJAUZITO KWANZA HUTAISHI KWA AMANI, SIKU ZOTE HATIA HIYO ITAKUTAFUNA, HUTAISAHAU MAISHA YAKO YOTE, LAKINI UNAWEZA KUKOSA UZAO TENA KABISA, UKIJIONA BADO UNAENDELEA KUPATA JUA NI NAFASI YA UPENDELEO NA NEEMA ZA MUNGU TU KUKUAMINU TENA, SI MCHEZO HUU, WAPI WANAOWEZA KWENDA MPAKA ROUND TANO WANATOA TU NIKWAMBIE NI LAANA,

MUNGU HATAKI HATA ROHO MOJA IPOTEE, SASA UMEPOTEZA ROHO MOJA AU MBILI AU TATU AMBAPO HIZO ROHO NAZO ZINGEOKOA MAMILIONI, HAPANA HAIFAI

LAKINI K**A UMEWAHI KUFANYA HIVYO NA UNAHISI HUKUMU, NA HUTAKI TENA KUENDELEA SIKIA NIKWAMBIE HUWEZI MWENYEWE, SI UNAONA ULIPOTOA YA KWANZA UKASEMA SITARUDIA TENA UKALAMBA KIDOLE KABISA UKAKIPITISHA KWENYE SHINGO ILI TUAMINI HUTARUDIA? NI KWELI HUKUTAKA KURUDIA NA SI MAIGIZO LAKINI MBONA UMERUDIA?? LAZIMA UJUE UNALOTAKA KUFANYA HUWEZI KUFANYA NA UNAFANYA USILOTAKA KULITENDA KWA SABABU KUNA NGUVU ZINAENDESHA MAISHA YETU

NGUVU ZINAZOTUENDESHA NI MBILI, KWA MAANA HIYO K**A ULO UPANDE WA GIZA MAANA YAKE UTASUKUMWA KUTENDA YA GIZANI HATA K**A HUTAKI. SISI TULIOOKOKA TUNAENDESHWA NA NGUVU NYINGINE INAYOTUSUKUMA KUTENDA MEMA NDIO MAANA MIMI NAWEZA KUSEMA NINAWEZA KUISHI BILA KUFANYA ZINAA LAKINI WAKATOKEA WATU WAKASEMA HAPANA HAIWEZEKANI HIYO. WAKAKUTAZAMA WAKAKUTHAMINISHA WAKAONA HUWEZI LAKINI NI KWA SABABU KILA NGUVU INAWASUKUMA WATU WALIO CHINI YAKE KUTENDA SAWASAWA NA TARATIBU ZAKE.

HAUHITAJI CHOCHOTE UNAMHITAJI TU MUNGU ALIYE HAI, SIZUNGUMZII UISHIE KUTAJA MUNGU TU MAANA HATA WAUWAJI WANATAJAGA MUNGU NAMAANISHA KWAMBA AINGIE NDANI YAKO ABADILISHE MFUMO MZIMA WA MAISHA YAKO NA INAWEZEKANA KABISA UKATUNZA KIZAZI CHAKO MPAKA MUNGU ATAKAPOKUPA MTU SAHIHI,

INAUMIZA SANA WATOTO WADOGO TU SEKONDARY WAMESHACHOKONOLEWA VIZAZI, VIZAZI VINAPATA TAABU NYIE. MI NITASEMA TU LIWALO NA LIWE. KIZAZI NI SEHEMU NAYOWEZA KUIITA TAKATIFU MAANA NDIPO MUNGU ANAPITISHIA WABEBA KUSUDI WAKE NA NDIO MAANA HATA KATIKA NDOA IMEWAPASA WATU KUINGIA KATIKA HALI YA USAFI. 🥺

K**A UPO BINTI UNASEMA NIMECHOKA NA HAYA MAISHA NJOO TUZUNGUMZE

K**A UPO KIJANA UNASEMA HAYA MAISHA HAPANA YANI UMEGEUKA TBS YA KUKAGUA VIZAZI NA KIKA MAHALI UNAACHA MADHARA NA UMEKUWA UKILAZIMISHA WASICHANA KUTOA MIMBA YESU ANAKUOENDA MNO UNAWEZA KUWA MTU MPYA
WEWE MAMA AU BINTI UNAYEUZA DAWA ZA KIENYEJI WASICHANA WATOE MIMBA NAWE UKIACHA HIYO KAZI HARAM TUTAOKOA ROHO NYINGI
WEWE DAKTARI HUKUSOMA ILI UUE BALI WATU WAPONE. MUNGU ANAWEZA KUKUTUMIA KWA KAZI HIYOHIYO. NJOO PIA TUZUNGUMZE

0762020312
IREEN

KATIKA HUDUMAWITO:MTU ANAPEWA NA MUNGU NA SI WATU, NINI NAMAANISHA?KUNA WATU HUWA WANAWAPA WATU WITO KWA KUWATAZAMA MWON...
08/01/2025

KATIKA HUDUMA

WITO:MTU ANAPEWA NA MUNGU NA SI WATU, NINI NAMAANISHA?

KUNA WATU HUWA WANAWAPA WATU WITO KWA KUWATAZAMA MWONEKANO WAO, KUNA NAMNA WATU WANAKUONA WANAANZA KUKUITA FULANI, LAKINI MTU WA NDANI SI HUYO WATU WANAYEMWONA

KABLA HUJAPOKEA WITO WA WANADAMU LAZIMA UINGIE MAGOTINI PA MUNGU, UMUULIZE WAMEONA SAHIHI?

KUNA WATU WANA MACHO YA ROHONI ANAPOKUTAMKIA WEWE NI FULANI MAANA YAKE HATAZAMI MUONEKANO WA NJE BALI ROHO MTAKATIFU AMEHUSIKA

NDIO MAANA KUNA MTU ANAWEZA AKAMTAMKIA MLEVI KWAMBA WEWE NI MCHUNGAJI, LAKINI KWA NJE NI MLEVI

WATU WASIO WA ROHONI WATASHANGAA SANA KWA SABABU WAO WANAJUA UTAMBULISHO WA MTU KWA NJE LAKINI ROHO HUTOA UTAMBULISHO KWA KUANGALIA HATIMA YA MTU, KWAMBA HUYU MTU NI MLEVI KWELI LAKINI ALIPASWA/ANAPASWA KUWA MCHUNGAJI

SASA IPO HIVI
NINAAMINI WITO ULIO NAO NI MUNGU AMEKUPA

KWA KUWA MUNGU NDIYE AMEKUITA TEGEMEA MAADUI WA WITO WAKO

NITAZUNGUMZIA ADUI MMOJA AMBAYE NI FAMILIA/NDUGU
WAPO WENGI WAPO NJIAPANDA KWENYE KUTEKELEZA WITO WAO KWA SABABU YA NDUGU WA KARIBU NA FAMILIA HAWAWAELEWI

KUNA WATU WANA MAWAZO KWA SABABU TU KUNA WATU WA FAMILIA WANAUSEMEA VIBAYA WITO WAKE

SIKIA, HAKUNA MWENYE MAMLAKA YA KUUSEMEA WITO WA MWINGINE

HUJAITWA KWA AJILI YA WASIOKUELEWA, UMEITIWA WANAOKUELEWA NA NDIO WA KUFOCUS NAO

Matthew 10:34-39
[34]Think not that I am come to send peace on earth: I came not to send peace, but a sword.
Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
[35]For I am come to set a man at variance against his father, and the daughter against her mother, and the daughter in law against her mother in law.
Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
[36]And a man's foes shall be they of his own household.
na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
[37]He that loveth father or mother more than me is not worthy of me: and he that loveth son or daughter more than me is not worthy of me.
Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
[38]And he that taketh not his cross, and followeth after me, is not worthy of me.
Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
[39]He that findeth his life shall lose it: and he that loseth his life for my sake shall find it.
Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona. Thawabu

TUNAPOANGALIA HAPA TUNAONA WAZI, KUWA NA MAADUI WA WITO WAKO KUTOKA KWA FAMILIA YAKO ILISHASEMWA NA YESU MWENYEWE

NITAKUSHANGAA SANA UNA HUDUMA HALAFU UNATAKA NDUGU WAKUPENDE, WAPENDE NA WITO WAKO,

K**A UTAPATA WA KUKUPENDA NI SAWA LAKINI WENGI WETU FAMILIA HATA HAWANA HABARI YA TUNACHOKIFANYA LAKINI HAITUUMIZI TUNAWATAZAMA WALE TUNAOWAHUDUMIA NDIO NDUGU ZETU KATIKA BWANA

NITAENDELEA............

8/1/2025
Mwl Irene George
WADADA KWA YESU🔥🔥🔥

Bwana Yesu asifiweNaomba tujifunze kitu cha msingi sanaJob 22:21-22[21]Acquaint now thyself with him, and be at peace: t...
06/12/2024

Bwana Yesu asifiwe

Naomba tujifunze kitu cha msingi sana

Job 22:21-22
[21]Acquaint now thyself with him, and be at peace: thereby good shall come unto thee.
Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.
[22]Receive, I pray thee, the law from his mouth, and lay up his words in thine heart.
Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako.

💥 Hapa tunaona neno mjue sana Mungu, halafu amani kisha mema yatakujia

Hii ni hatua, na hatua haipaswi kuruka,

Ukiona una amani na hujamjua Mungu maana yake hiyo amani ina shida mahali, sio ya Mungu

Ukiona kuna mema yamekujia kabla ya kumjua Mungu maana yake hakutakuwa na amani ndani yake, ni hatua kwa hatua.

Mara nyingi watu husema amani ya Roho Mtakatifu iamue k**a shotcurt ya kufanya maamuzi yanayowabeba. Je hiyo amani imekuja ghafla? Hakuna amani ya ghafla, lazima umjue Mungu na mapenzi yake katika jambo husika ndipo utapata amani au hautapata amani kulingana na jinsi umemjua Mungu

Lakini kwa hakuna kikomo cha kumjua Mungu, ndio maana anasema mjue "sana"

Isingekuwa neno sana maana yake ingekuwa ruhusa kujua hata kwa uchache, lakini neno sana maana yake hakuna mwisho, ni endelevu, ni kwa bidii kubwa

HEBU TUANGALIE MFANO HUU

Sote tunajua smartphone

Wapo watu waliposhika smartphone kwa mara ya kwanza hawakuwa wanajua matumizi, pengine walikuwa wanatumia kupiga picha, kupiga cm na kutuma ujumbe, ni kwa sababu hawakujua kuwa kuna matumizi zaidi ya hayo, yapo matumizi tena yenye faida kuliko kupiga cm, smartphone inaweza kuwa soko, inaweza kuwa shule, mtu anaweza kupata huduma za kiroho kupitia cm lakini kwa mtu kutokujua na kutokujishughulisha kujua basi anaishia kufaidi cm yake kwa uchache.

KWA MAANA HIYO, HUYU MTU AMBAYE HAFUATILII KUIJUA CM YAKE ATAPITWA NA FAIDA ZILIZOPO KATIKA CM HIYO, LAKINI ATAPITWA NA WAKATI KWANI KILA WAKATI MATUMIZI YANAONGEZEKA, KWA HIYO HATA ANAYEJUA LAZIMA AWE MFUATILIAJI ZAIDI KUJUA MATUMIZI MAPYA YANAYOTOKEA KILA MARA.

TOFAUTI NA HAPO MTU ANAWEZA KUWA TU MMILIKI WA CM ISIYOMTATULIA CHANGAMOTO ZAKE

VIPO VITU MTU ATALIPIA BILA KUJUA ANAWEZA KUFANYA KWA KUTUMIA SIMU YAKE, NI KWA SABABU YA KUTOKUJUA. KUTOKUJUA KUNASABABISHA HASARA,

MTU ANAWEZA KUCHELEWA KUFANYA JAMBO KWA KUTOKUJUA TU KWAMBA SIMU INAWEZA KUMRAHISISHIA, TUNAONA HAPO GHARAMA ZA KUTOKUJUA KITU HATA K**A UNACHO,

TUNAYE MUNGU LAKINI HATUTAACHA KUONA HASARA K**A HATUTATAFUTA YALIYOMO NDANI YA MUNGU

Chukulia Mungu k**a simu yenye kila kitu, lakini kwa kutokujua vilivyopo ndani ya cm basi unakosa kutekeleza mambo yako,

Lakini kujua haitoshi, hivi k**a ukijua kuwa cm inaweza kuwa namna ya kukupatia wateja wa bidhaa zako na hujui unatafutaje wateja kupitia cm inakuwaje?

Kumbe kuna la kufanya baada ya kujua, ukishajua kitu unacho lazima ujifunze kukitumia

Tunapomjua Mungu lazima tukae chini kujifunza kuhusiana na yale tuliyoyajua kwa sehemu kuhusu yeye

Job 22:22
[22]Receive, I pray thee, the law from his mouth, and lay up his words in thine heart.
Uyapokee, tafadhali, mafunzo yatokayo kinywani mwake, Na maneno yake yaweke moyoni mwako.

: Hapa anazungumzia kupokea mafunzo

Tukishamjua Mungu lazima tukae tuanze kutafuta kwa undani wake zaidi habari zake, ndio maana nimesema neno sana ni suala la muendelezo, ni suala ambalo halina mwisho na ni kwa sababu Mungu hazoeleki kadri tunavyojifunza habari zake tunazidi kumwona katika namna tofauti

Leo ukimjua Mungu k**a mtoa chakula si kila siku unahitaji chakula, lakini namna atakayokupa chakula leo si k**a atakavyokupa kesho, ndio maana hatuzoelei namna ileile tunayoifahamu kuhusu Mungu

Shida ipo wapi?

Shida ni kuzungumzia amani kabla ya kujua

Shida ni kuyapokea mema kabla ya kumjua ili upate amani

Mema yanayokuja kabla ya kumjua Mungu hayatokani na Mungu

Mema yake huwa yanakuja k**a zao la kujuana nae na kuwa na ushirika wa ndani

Hebu tuangalie kuhusu mema

Psalms 23:6
[6]Surely goodness and mercy shall follow me all the days of my life: and I will dwell in the house of the LORD for ever.
Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Hapa tunaona kuwa wema na fadhili za Mungu ni jambo la uhakika, mema yanatufuata sio sisi kuyafuata😁

Katika ayubu anasema mjue sana Mungu ndipo mema yatakapotujia

Oh kumbe yanatakiwa yaje na sio sisi kuyafuata. Siku za leo watubwa Mungu tunateseka na maisha. Tunatafuta mambo mazuri kumbe formula ni kumjua sana Mungu kisha mema yanakuja yenyewe

Lakini anazungumzia kukaa nyumbani mwa Bwana milele

Huku nyumbani mwa Bwana ni katika uwepo wa Mungu

Katika uwepo wake ndipo tunamjua nankumfahamu zaidi

Asiyekuwa na Muda wa kukaa katika uwepo wa Bwana hawezi kuwa na amani, lakini mema hayawezi kumjia bali atapoteza muda mwingi kiyatafuta mema asijue mema yanakuja yenyewe, mema yanafuata wale walio ndani ya uwepo wa Mungu

Kwa maana hiyo ninaomba nikwambie kuwa jichagulie kipaumbele ukae uweponi mwa Mungu mema yakujie au ukayatafute mema kwa nguvu yakukoseshe muda wa kukaa uweponi mwa Mungu

Wakati tunapoyatafuta mema wenyewe yanatufukuza mbali na uwepo wa Mungu. Hawa pale bustani ya edeni alikuwa anatafuta mema kwa hiyo wakati anakula tunda alijua ni jambo jema kufanana na Mungu. Kumbe kutafuta yale tunayoyaona mema kunaweza kututoa uweponi mwa Mungu

Ni vyema mema yakujie ukiwa uweponi mwa Mungu na si kumwacha Mungu kwenda kuyatafuta yaliyo mema machoni pako

Yesu akubariki sana
Ireen

UJUMBE WA LEO UNASEMA KILA KITU NI MAANDALIZI📌Maandalizi ni hali ya kufanya matayarisho kwa ajili ya jambo fulani. Katik...
06/12/2024

UJUMBE WA LEO UNASEMA KILA KITU NI MAANDALIZI

📌Maandalizi ni hali ya kufanya matayarisho kwa ajili ya jambo fulani.

Katika maisha mambo mazuri huandaliwa, kila jambo kinalotokea bahati mbaya bila maandalizi hupotea bila taarifa. Yani ambacho hakikupitia mchakato wa kuandaliwa hupotea ghafla

Mchakato wowote unaokutana na maandalizi sahihi huwa unaleta muendelezo wa uhakika,

Mtu mwenye maandalizi ana taarifa sahihi za kuelezea mafanikio yake hatua kwa hatua na tunaweza kujifunza kutoka kwake,

✅Maandalizi ya jambo fulani huweza kuwa katika namna mbalimbali kulingana na aina ya jambo linatakiwa kufanyika.

💥Maeneo mbalimbali ya maisha yanahitaji maandalizi, mfano
-biashara
-ndoa
-elimu
-huduma
-safari
-kuanza siku yenye mafanikio pia ni maandalizi

Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwa mtu ywyote mwenye akili timamu katika maisha yake yote hakuna mahali ambapo hapahitaji maandalizi

HEBU TUGUSIE MAANDALIZI ENEO LA UWEZO

Yapo maono makubwa ndani yetu, zipo ahadi za Mungu maishani mwetu ni kubwa sana pengine kuliko uwezo wetu,

Tumwangalie mtu k**a Yusufu, anaota ndoto kubwa kuliko uwezo wake na kwa kuwa uwezo hauruhusu kufikia ile ndoto anaanza kuandaliwa kwa kujengewa uwezo, Yeye hakuwa anaendana na ile ndoto lakini alianza kupitia mitihani inayoendana na ndoto yake ili Yusufu sasa awe na uwezo unaoendana na kile anachokwenda kukifanya/ile ahadi ya Mungu/ndoto yake

Ili ndoto isiishie kuwa ndoto inahitaji maandalizi sahihi

Mungu huachilia rasilimali mahali penye uwezo kwa sababu hapendi hasara, Mungu hapendi na haendani na wazembe,

Tunaweza kujiuliza mbona kuna watu walipewa rasilimali na Mungu na wakafeli, hawa ni wale ambao walikuwa na uwezo na Mungu akawaamini lakini wakabweteka

Lakini unapaswa kujua kuwa Mungu anaachilia rasilimali kulingana na uwezo ulio nao na ndio utaamua kwa kiasi kipi ulete faida

Matthew 9:17
[17]Neither do men put new wine into old bottles: else the bottles break, and the wine runneth out, and the bottles perish: but they put new wine into new bottles, and both are preserved.
Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na k**a wakitia, vile viriba hupasuka, divai ikamwagika, na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya, vikahifadhika vyote. Msichana Arejeshewa Uhai na Mwanamke Kuponywa

Katika andiko hili tunaona ya kuwa kwa akili za kibinadamu tu hakuna mtu anaweza kuweka divai mpya katika viriba vikuukuu, ni kwa sababu viriba vitapasuka na divai itamwagika na ni hasara

Mungu anazo rasilimali zote za kutufanya tufikie hatima/mafanikio lakini lazima tulitie mchakato wa kuongeza uwezo ili kukwepa hasara.

Ni wazi kuwa tunapokwepa maandalizi kuna vitu tunakosa na vitu hvyo kukosekana maana yake tunaenenda kwa akili zetu na ndipo anguko hutokea

📌Lazima ujue kuwa tunashirikiana na Mungu kuelekea mchakato, Mungu ana nafasi yake nasi tuna nafasi yetu,

💥Nafasi ya Mungu ilishaachiliwa tayari kwa kiasi kikubwa maamuzi yapo mikononi mwetu

2 Peter 1:3-4
[3]According as his divine power hath given unto us all things that pertain unto life and godliness, through the knowledge of him that hath called us to glory and virtue:
Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
[4]Whereby are given unto us exceeding great and precious promises: that by these ye might be partakers of the divine nature, having escaped the corruption that is in the world through lust.
Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

Hapa tunaona kuwa uweza wa Mungu umetukirimia vitu vyote na Mungu ameachilia sehemu ya uungu ndani yetu, kwa kujua hivyo lazima k**a mwana wa Mungu utambue iko nguvu ya ndani inayokupa uwezo wa kuanzisha jambo na likafanikiwa

📌Lazima ujue kuwa tunashirikiana na Mungu kuelekea mchakato, Mungu ana nafasi yake nasi tuna nafasi yetu,

💥Nafasi ya Mungu ilishaachiliwa tayari kwa kiasi kikubwa maamuzi yapo mikononi mwetu

2 Peter 1:3-4
[3]According as his divine power hath given unto us all things that pertain unto life and godliness, through the knowledge of him that hath called us to glory and virtue:
Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
[4]Whereby are given unto us exceeding great and precious promises: that by these ye might be partakers of the divine nature, having escaped the corruption that is in the world through lust.
Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.

Hapa tunaona kuwa uweza wa Mungu umetukirimia vitu vyote na Mungu ameachilia sehemu ya uungu ndani yetu, kwa kujua hivyo lazima k**a mwana wa Mungu utambue iko nguvu ya ndani inayokupa uwezo wa kuanzisha jambo na likafanikiwa

HAYA NI KUHUSU YUSUF, KWA TAARIFA ZAIDI UTASOMA MWANZO 39 NA KUENDELEA

HEBU TUMWANGALIE DAUDI NAYE 1samwel 16

Daudi maandalizi yake ya kuwa mfalme hayaanzii ikulu, hayaanzii kwenye mifumo ya kisiasa au ya uongozi,

Maandalizi ya daudi yanaanzia nyikani, yaani mtu anayetakiwa aongoze watu anapimwa uwezo wake kwenye kuchunga wanyama, huyu daudi uwezo wake wa kuweza kuokoa kondoo wasiliwe na simba ndio maandalizi ya kuuendea ufalme imagine,

Kumbe wakati mwingine kuna mazingira ambayo ni tofauti na kusudi letu lakini ni njia ya kutuandaa kiuwezo kuendea kusudi,

Daudi kumuua simba na dubu hakuwa anaandaliwa kuwa mchunga kondoo mzuri, ilikua ni maandalizi ya kuwa mfalme,

Inawezekana hicho unachokifanya sasa sicho mwisho wako bali ni maandalizi na kuwekewa uwezo wa kufikia mambo makubwa zaidi, lazima ukae hapo kwa uaminifu na ushinde kila mtihani

Kumbe wakati mwingine kuna mazingira ambayo ni tofauti na kusudi letu lakini ni njia ya kutuandaa kiuwezo kuendea kusudi,

Daudi kumuua simba na dubu hakuwa anaandaliwa kuwa mchunga kondoo mzuri, ilikua ni maandalizi ya kuwa mfalme,

Inawezekana hicho unachokifanya sasa sicho mwisho wako bali ni maandalizi na kuwekewa uwezo wa kufikia mambo makubwa zaidi, lazima ukae hapo kwa uaminifu na ushinde kila mtihani

UWEZO
ni kitu cha kuonekana si kiti cha kuzungumza tu, daudi mbele za mfalme alikuwa na cha kuzungumza kuhusu simba na dubu, k**a hatupitii kipindi cha maandalizi hatuwezi kujua nguvu yetu ilo wapi

K**a Yusuf hakutafsiri ndoto kule gerezani angejulikanaje kwa mfalme? Kumbe kipindi cha maandalizi ni kizuri kutuandaa kujua uwwzo wetu, kupata cha kutufanya tuzungumzwe kwa wakuu, kwa wakuu hatujipeleki tunaitwa, Kinachotuitisha kwa wakuu sio kwa sababu tunatia huruma ni taarifa, k**a hakuna maandalizi na mchakato ambao ulikwisha kufanyika je ni taarifa zipi zinaweza kutubeba?

LAZIMA KUBORESHA UWEZO

UWEZO NDIO UNALETA KUAMINIWA,,

KWA NINI NI LAZIMA KUJIANDAA?

-Kuleta ufanisi, maandalizi yanaleta ufanisi katika utendaji kwa sababu hutoa nafasi kwa mtu kujifunza kabla ya kuamua kufanya jambo lakini inamtengenezea mtu utulivu

-Kuepuka mabadiliko yasiyotarajiwa, kuna watu ni wataalam wa kuanzisha vitu na kuacha kwa sababu ya changamoto ambazo hazikutarajiwa. kunapokuwa na maandalizi basi mchakato mzima huwa katika namna ambayo kila kinachohitajika kinafahamika lakini pia kwa kasoro zinazojitokeza huweza kushughulikiwa kwa usahihi

-Kutokurudia makosa, maandalizi hutupa muda wa kujifunza kwa wengine lakini kuboresha eneo la ufahamu ili kuepuka makosa ya kujirudia rudia

-Kufanya maamuzi sahihi, tofauti na mtu anayekurupuka ambaye anaweza kubadilisha maamuzi au kufanya maamuzi yasiyo sahihi kwa sababu ya pressurw, lakini mwenye maandalizi anajua dira hivyo hufanya maamuzi kwa kuzingatia maono, hawezi kuamua maamuzi ya kuumiza malengo yake

Kujiandaa humuwezesha mtu kuwa na muda wa kufanya tathmini na kujua mahitaji anayohitaji kukamilisha mpango kazi wake na kujua namna gani rasilimali zinahitajika

- Kuniamini, maandalizi yanatufanya tuwe na kujiamini na kutokuwa na hofu kwa sababu tuna uhakika
Mtu aliyesoma vizuri ana uhakika wa kufaulu mtihani, kadhalika ukijiandaa kwa lolote una uhakika wa kufaulu

Jiulize k**a tunaweza kuweka mikono juu ya wagonjwa wasipone na wengine wapone, vipi daudi angepata hofu kuwa lile jiwe lisipomuua goliath itakuwaje? Lakini utaona kuwa daudi hakuwa na hofu sababu ameshazoea ndio shughuli zake tangu kipindi anaandaliwa

Kwa maana hiyo hakuna kisichohitaji maandalizi na katika kujiandaa lazima kuwa na uwezo, uwezo huu tunao kutoka juu lakini ni lazima sisi wenyewe tujue kuwa uwezo wa Mungu unamhitaji mtu

Mungu anapoachilia nguvu yake lazima ikutane na mtu sahihi anayeweza kuifanyia kazi na kukubali io nguvu imuendeshe

KWA KUHITIMISHA NI KUWA TUNAISHI KULINGANA NA UWEZO TULIORUHUSU UFANYE KAZI NDANI YETU, K**A TUNAHITAJI KWENDA ZAIDI TUNAHITAJI KUONGEZA UWEZO NA NI MCHAKATO TUSIKWEPE MCHAKATO

WANAOKWEPA MCHAKATO HAWANA SHUHUDA, HAWANA CHA KUSIMULIA JUU YA MAFANIKIO YAO NA MAFANIKIO HAYO HUWA HAYADUMU

YESU ATUJALIE UWEZO,
KIRIBA KIKUUKUU KIKIWEKWA DIVAI KINAPASUKA

HAKIKISHA UNAKUA MPYA KILA SIKU, JENGA UWEZO UNAOFANANIA KESHO YAKO, KESHO NJEMA ITAKUFUATA KWA SABABU UNA MVUTO

BARIKIWA SANA NA BWANA YESU
HADI WAKATI MWINGINE

Ireen❤

🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥Tunamshukuru Mungu tulimaliza mkesha wetu salamaHongereni kwa kufika kwenye mkesha  WADADA KWA YESU Tunatoa ...
21/11/2024

🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Tunamshukuru Mungu tulimaliza mkesha wetu salama
Hongereni kwa kufika kwenye mkesha WADADA KWA YESU

Tunatoa shukrani zetu kwa watumishi ambao walihudumu siku ya mkesha
MUNGU AWABARIKI SANA
Asanteni kwa wote mliohudhuria naimani kila mtu alitoka na kitu kwa ajili ya maisha yake

Zaburi 115:18
Bali sisi tutamhimidi Bwana, Tangu leo na hata milele.

MUNGU AWABARIKI SANA 🙏🙏🙏🙏

Somo : *NGUVU ZA MUNGU*Saivi kuna wimbi kubwa la watu  utakuta wamejaa kwenye milima ya maombi wanafunga, wanajinyima, w...
12/11/2024

Somo : *NGUVU ZA MUNGU*

Saivi kuna wimbi kubwa la watu utakuta wamejaa kwenye milima ya maombi wanafunga, wanajinyima, wengine wamekondeana miili hadi huruma.

Ukiwauliza mbona hivyo? Unaombea nini hadi unakondeana hivyo?

Atajibu *"Ninatafuta nguvu za Mungu"*

Ukimuuliza nguvu za Mungu unataka za nini?

Atajibu "Nataka nikiombea watu wapone, Nikimtabiria mtu itokee kweli, Nikimlaani mtu alaanike hapohapo. Nikiwa nahubiri watu wabubujike, nikipita kati ya watu bila hata kuomba, mapepo yalipuke yenyewe. Niwe na upako mwingi, niwe na ushawishi"

Aiseee🤔
SIKIA

Hizo nguvu hata shetani anaweza kukupa.
Ni hatari sana kuzitaka nguvu za Mungu kwa mlengo usio wa kiungu.

Watumishi wengi wa Mungu waliotembea na nguvu za Mungu hawajawahi kujitaabisha kuzipata hizo nguvu, ila walizingatia sana kutembea na mtoa nguvu (Mungu)

Kuwa na nguvu za Mungu sio kitu kigumu. Focus na mtoa nguvu upate nguvu zake.

Ukitembea na Mungu sawasawa ni Automatic nguvu zake zinakujia.

Haijawahi kumsumbua shetani wewe kuwa na nguvu za Mungu ila inamsumbua sana shetani wewe kutembea vizuri na Mungu.

Na inamsumbua sana Mungu wewe kuzitaka nguvu zake huku ukimkataa yeye kwa matendo yako unayofanya sirini au hadharani.
Zaburi 105:4 Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote.

Kwenye hayo maandiko mawili cha kwanza ni kumtaka Bwana kisha kuzitaka nguvu zake.

Hawajasema zitakeni nguvu zake na mtakeni Bwana.

Lazima umtake BWANA kwanza ndipo utapata na nguvu zake

1 Mambo ya Nyakati 16:11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
Siku ile Yesu alivyofunga siku 40alikuwa na utiisho mkubwa sana na nguvu za Mungu zilimfunika. Sasa shetani walae hakuogopa alimtokea na kuanza kumjaribu.

Kilichompa ushindi Yesu ni utii aliokuwa nao kwa Mungu na sio nguvu za Mungu.

HEBU NIZUNGUMZE KIBONGO ITAELEWEKA KIRAHISI.

Yesu hakumshinda shetani kwa nguvu za Mungu, bali alimshinda kwa utii aliokuwa nao kwa Mungu anayetembea naye.

Angalia haya majibu aliyotoa wakati anajaribiwa.

1. Huwezi kunitega kwa chakula maana mtue ili aishi sio mpaka ale chakula bali hata kwa Neno litokalo kwa Mungu.

2. Imeandikwa usimjaribu Bwana Mungu wako, siwezi kujitupa chini kisa imeandikwa Mungu ataniletea malaika wanidake

3. Nenda zako shetani siwezi kukusujudia wala kukuabudu. Wakusujudiwa na kuabudiwa ni Mungu pekee, wewe unaniambiaje nikusujudie wewe eti ili unifanikishe. Qwendraa zako shetaaa

Ukimjua Mungu na kutembea naye, atakushindia kila jaribu la shetani.

Ila nguvu pekee hazitakusaidia mahali fulani, utajikuta unaingizwa chaka pamoja na kwamba unazo nguvu za Mungu.
Kuzipata nguvu za Mungu ni very simple. Yaani hata ukienda Nigeria kwa Tb Joshua utazipata.

Ila shughuli ipo kwenye kumpata Bwana.

Vijana wengi wenye kiu ya nguvu za Mungu kwa mlengo usio wa kiungu wamejikuta wakiangukia kwenye mtego wa shetani.

Shetani huchungulia tamaa iliyo ndani ya mioyo yao na kugundua hitaji lao kisha kuwapatia yeye hizo nguvu halafu mwishoni hao vijana wanajikuta wanazaa matunda ya shetani badala ya matunda ya roho. Matunda mengi wanayozaa ni uzinzi, kiburi, kujiinua n.k

Mkumbuke simoni mchawi aliyeokoka wakati wa kanisa la kwanza la mitume.

Ona petro alivyomjibu.
Matendo 8:23Kwa maana nakuona u katika uchungu k**a nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu.
For I perceive that thou art in the gall of bitterness, and in the bond of iniquity.

Huyu simoni mchawi alipookoka akaona kina petro wanafanya ishara na ajabu.

Simoni akataka kununua hizo nguvu kwa pesa kutoka kwa kina Petro.

Badala ya kumtaka Bwana yeye alizitaka nguvu kiasi cha kuwa tayari kuzinunua
Ni makosa kutaka nguvu badala ya kumtaka Bwana
Watu wapo busy kuzitaka nguvu.ila mtoa nguvu hawana habari naye kabisa
Yesu alitoa mwongozo sahihi wa namna ya kuzipata nguvu za Mungu, akisema

Matendo 1:8
Matendo ya Mitume 1:8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Zaburi 29:11 Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani.

UKITAKA KUFANYA MAKOSA anza kuzitafuta nguvu badala ya kumtafuta mwenye nguvu (Roho Mtakatifu)

Hapo utajikuta una nguvu lakini zitakugharikisha au utakuwa na nguvu na uwezo kutoka kwa Shetani.

Hata wewe unawweza kuwa na nguvu za Mungu za ajabu ikiwa utatembea na Bwana kwelikweli.

Ukitembea na Bwana, nguvu zitakuja zenyewe
Kazana kumtaka Bwana.
Kazana kutembea na Mungu.

Kazana kudumisha uhusiano mzuri na Mungu.

Kazana na Mungu

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BIBLE STUDY posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share