18/10/2024
Vijana rafiki wapendwa, kila mnachopanda mtakivuna pia.sasa ni wakati wenu wa kupanda. Mavuno yatakuwaje? mwapanda nini? Kila neno msemalo, kila tendo mtendalo ni mbegu ambayo itazaa matunda mema au mabaya, nayo italeta furaha au huzuni kwa mpandaji. K**a ilivyo mbegu iliyopandwa.Ndivyo yatakavyokuwa mavuno. MUNGU amewapa nuru kubwa na mibaraka mingi. Baada ya nuru hiyo kutolewa baada ya hatari kuonyeshwa dhahiri mbele yenu, mambo yanabaki juu yenu. Namna mnavyofaya na nuru ambayo mnapewa na MUNGU italeta furaha ama huzuni. Ninyi wenyewe mnajitayarishaia mwisho wenu wenyeweβ. EG White- 1 kutayarisha njia sura ya 35:1 uk.212.
Kila neno msemalo kila tendo mtendalo ni mbegu ambayo itazaa matunda mema au mabaya. Nayo italeta furaha au huzuni kwa mpandaji. Nataka uelewe kuwa kutowaza sahihi tu kwa dakika moja, kutenda jambo dogo tu ambalo si la haki, kunaweza kubadiri mkondo wa maisha yako yote; Ninyi wenyewe mnajitayarishia mwisho wenu.
Muda mfupi unaotumika katika kupiga maisha ujanani, rafiki zangu vijana wapendwa, utatoa mazao ambayo yatafanya maisha yako yote yawe machungu, saa moja ya kutowaza sahihi, mara unapokubali kuingia katika jaribu, waweza kubadilisha mkondo mzima wa maisha kwenda mwelekeo usio sahihi. Unao ujana mmoja tu, hebu ufanye kuwa wenye manufaa. Upitapo katika eneo moja huwezi kurejea na kurekebisha makosa yako. Shetani huwa anajigeuza na kuwa mfano wa malaika wa nuru ajapo kwa vijana na majaribu yake yanayohadaa na huwa anafanikiwa kuwashinda, hatua kwa hatua kutoka katika wajibu waoβ
Ni kweli shetani ajapo kwa vijana na majaribu yake tena yanayohadaa anafanikiwa kuwashinda. Ni wengi ambao shetani amewashinda kwa tamaa za mwili, kwa ulevi wa pombe, ulafi, na kwa kutowatii wazazi wao. Vijana hawa ambao ndio hufanya familia, taifa na kisha mataifa, wengi wao wamearibika kiasi kikubwa. Katika Mataifa mbalimbali hata vijana wanavyoongea tu ushuhudia jambo hili na wengine wanaongea k**a mazezeta, wenyewe wakijiita kuwa ni masela; huu wote ni upotevu wa maadili.
MUNGU anahitaji maisha ya ujana juu ya vijana tulio nao katika nyumba zetu na kanisani, maisha yao yawe kielelezo: - Kielelezo katika usemi
usemi
- Kielelezo katika mwenendo
- Kielelezo katika upendo
- Kielelezo katika imani
- Kielelezo katika mavazi, uvae kwa kujistiri. Maandiko yanaendelea kuonya ifuatavyo:-
βMtu awaye yote asiudharau ujana wako,bali uwe kielelezo kwao waaminio,katika usemi na mwenendo na katika upendo na imani na usafiβ. 1 Timotheo 4:12.
Ili ujana wako usidharauliwe uwe kielelezo katika mwenendo, usemi, upendo, kielelezo katika imani, utakuwa na ujana wenye manufaa. Lakini k**a mwenendo wako ni wa ovyo, usemi ni waovyo, watu hawataacha kukudharau. Je wewe kijana unaesoma kitabu hiki ulichonacho mkononi mwako, mwenendo wako ukoje? Je, watu wanavyo kutazama wanaona kielelezo katika imani na usafi? Habari gani juu ya usemi wako, Maana katika siku hizi za mwisho kuna lugha zinazotumika mitaani ambazo zinaonyesha upotovu wa maadili. Zifuatazo ni baadhi ya lugha zinazotumiwa na vijana lakini ni upotofu wa maadili cha ajabu hata vijana Wakristo nao wamepotoka.