Jerusalem Spiritual Transformation Church Kivule -Magole Area

Jerusalem Spiritual Transformation Church Kivule  -Magole Area Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Jerusalem Spiritual Transformation Church Kivule -Magole Area, Religious organisation, kivule, Dar es Salaam.

14/12/2018

LISTEN CAREFULLY THIS SONG AND BE FILLED WITH THE SPIRIT

09/12/2018

Tarehe: 9/12/2018 Na MT. Peter. Somo la Utangulizi: UTII. * Nini maana ya neno “utii”
Utii ni hali ya kutekeleza na kufanya kile kitu ambacho nimeamriwa au nimeagizwa nikifanye.
*Utii ndani ya mtu utampelekea kupatana na Mungu, na Mungu kuwa karibu na mtu sana.
* Mtu akikosa hali ya utii hata anapokosea / au anapotenda dhambi hakubali kosa,bali utafuta namna ya kuhalalisha alichofanya. (mfano mzuri ni mfalme Sauli).
* Hali ya kukosa utii ni miongoni mwa vitu vinavyotukosanisha sana na Mungu.
*Baraka za Mungu zinaambatana na mtu anayetii Sauti ya Mungu.
mfano: Ibrahim alibarikiwa na Mungu sababu ya utii aliokuwa nao, hata Mungu akamuita Ibrahimu rafiki yake.
YAKOBO 2:23
MWANZO 15
*Utii ndani ya mtu umjengea mtu heshima katikati ya jamii inayomzunguka.
*Ukimtii Mungu utawatii hata watumishi wake kwa kile wanachoelekeza.
LUKA 16: 19-31
*Utii unakuja ndani ya mtu pale mtu anapokuwa na nidhamu binafsi ndani yake katika Kweli ya Mungu.
*Nidhamu ikikosekana ndani ya mtu hujenga hali ya utii ndani ya mtu.
* Nidhamu ikikosekana ndani ya mtu uwa na hali ya mazoea hata anaopokuwa kwenye Uwepo wa Mungu.
* Ukimtii Mungu utaonyesha hali ya utii pia kwa jamiiinayokuzunguka (na si kuonyesha utii ukiwa kanisani tu).
* Utii ukiwa ndani yangu unaweza kupelekea watu wengine wasiomjua Mungu kuvutika na maisha yangu na kumgeukia Mungu.
* ( Tabia ya asili ndani ya mtu ataweza kuishinda / au kuiacha pale atakapokubali na kuamua kuikataa tabia hiyo, hata k**a ataonywa, atafundishwa, bado inahitaji maamuzi ya mtu kubadilika.
ISAYA 1:19,20
*Baraka za Mungu zinakuja katika maisha ya mtu pale anapokubali kutii Sauti ya Mungu.
*Utii ukiwa ndani ya mtu haijalishi anapitia mazingira gani, kamwe hawezi kubadilishwa msimamo alionao juu ya MUNGU.
* KUMBUKUMBU LA TORATI 28:1-......
* Mtu anapokosa hali ya utiii, ibilisi anaanza kuondoa kile ambacho Mungu amekupa taratibu.
* Kitu (dhambi) ambacho nakiona ni kidogo sana ndicho ambacho ibilisi anakitumia kumletea mtu uharibifu.
* Vile vile Mungu naye utumia mambo madogo tunayoyadharau kumuinua mtu.
*Utii ndani ya mtu umpelekea mtu kuwa na hali ya unyenyekevu.
* Utii ndani ya mtu umfanya mtu asiogope mazingira na kumfanya asimamie kufanya kile ambacho Mungu ameagiza.

11/11/2018

JERUSALEMU SPRITUAL TRANSFORMATION CHURCH
KIVULE AREA-DAR ES SALAAM.
12/11/2018
NA Mtumishi PETER
SOMO LA UTANGULIZI: MAJARIBU
YAKOBO 1:2
Imetupasa kufurahi pindi tunapopitia majaribu mbalimbali.
• Majaribu haimaanishi dhambi
• Majaribu ni kipindi ambacho kila mtu ambaye anaishi chini ya jua, iwe ameokoka au hajaokoka, iwe ametenda dhambi au hajatenda dhambi.
• Ingawa iko tofauti kati ya mtu ambaye ameokoka pindi anapopitia majaribu na mtu ambaye hajaokoka pindi anapopitia majaribu.
• Mara nyingi kwa mtu ambaye hajaokoka anapopitia majaribu umsababishia anguko kubwa sana.
• Kwa sababu kwa mtu
• Na kwa mtu ambaye ameokoka jaribu linapokuja, Mungu ufanya na mlango wa kutokea katika jaribu hilo.
• Kwa mtu aliyeokoka jaribu umfanya awe thabiti akistahimili
• Kuna majaribu ya aina tatu
1. Jaribu ambalo Mungu analiruhusu kwa mtu.
2. Jaribu ambalo ibilisi analileta kwa mtu.
3. Jaribu ambalo mtu anajiletea mwenyewe akivutwa na tamaa zake mwenyewe.


1. Jaribu ambalo Mungu analiruhusu kwa mtu
• Mungu wakati mwingine uruhusu majaribu yaje kwa mtu ili kumuimarisha.
• AYUBU 1
• Majaribu umfanya mtu apate uthabiti wa Imani pindi anaposhinda.
• Kabla Mungu hajampeleka mtu kwenye utukufu mwingine mara nyingi uruhusu majaribu kwa mtu ili kumfanya aimarike. Na vilevile ili kumfanya aweze kuendana na Baraka na kusudi lililopo mbele yake.
• Yusufu ili afikie maono yake Mungu alimpitisha katika majaribu mbali mbali, ikiwemo kuchukiwa na ndugu, kuuzwa kuwa mtumwa, kukufungwa gerezani.
• Katika maisha ya kawaida hakuna mwanajeshi anayepelekwa vitani k**a hajapitishwa katika mazoezi ya kumuimarisha, vivyo hivyo na mtu wa Imani lazima apitishwe kwenye majaribu ya kumuimarisha.

2. Jaribu linaloletwa na ibilisi kwa mtu
• Ibilisi huleta jaribu kwa mtu akiwa na lengo la kuharibu mahusiano ya mwanadamu na Mungu
• MWANZO 3
• Ibilisi utumia vitu ambavyo Mungu ametukataza tusivifanye kutujaribu na kutushawishi tuvifanye ili aweze kututenganisha na Mungu.
• Ibilisi utumia mwanya anaouachia mtu kumjaribu.
• Anachoogopa ibilisi ndani ya mtu si kwa sababu mtu anaomba sana, au anafunga sana, bali anachoogopa ni mahusiano mazuri aliyonayo mtu na Mungu.
• Ibilisi alilporuhusiwa kumjaribu Ayubu lengo lake lilikuwa ni ili Ayubu amkufuru Mungu na hivyo kuharibu mahusiano yake na Mungu.
• Ibilisi upata uhalali wa kumjaribu mtu pale anapoacha mwanya (mlango) kwa ibilisi.
• Mfano: - mlango wa ibilisi unaweza kuwa ni- hofu, hasira, uchungu, mawazo machafu, maneno machafu.


• YAKOBO 1: 13

3. Jaribu ambalo mwanadamu anajiletea mwenyewe akivutwa na tamaa.
• Tamaa iliyo ndani ya mtu ndiyo ambayo ibilisi uitumia kumjaribu mtu.
• YAKOBO 1:14.15

11/11/2018

JERUSALEMU SPRITUAL TRANSFORMATION CHURCH
KIVULE AREA- DAR ES SALAAM
TAREHE: 11/11/2018
NA Pastor STEVEN LAIZER
UJUMBE: NGUVU YA NENO LILILOTAMKWA
(The Power of a Spoken Word)
• MWANZO 1
• Nini ambacho kipo nyuma ya neno lililotamkwa?
• Kuna nguvu ya kujenga, kubomoa, kupanda, na kung’oa, kurekebisha au kuharibu kwenye kila neno linalotamkwa.
• (Inategemea nguvu hiyo inatoka wapi)
i. Nguvu ya kujenga, kupanda na kuumba kila kitu chema inatokana na Roho Mtakatifu ndani ya mtu.
ii. Nguvu ya kubomoa, kung’oa ma kuharibu inatoka kwa yule mwovu. (kwa sababu yeye ni muharibifu tangu mwanzo).
• ANGALIZO: Roho Mtakatifu vilevile anatoa nguvu ya kuharibu vitu ambavyo si sahihi kwenye ufalme wa Mungu.
• (kwahiyo si kila kinachoharibu kimetoka kwa adui lakini wakati mwingine kwa kutokulitii Neno La Mungu, Mungu anaruhusu uharibifu, lakini mtu akirejea anaondoa uharibifu)
• Nguvu ya Neno lililotamkwa lina uwezo wa kufufua chochote kilichokufa, na vilevile kina uwezo wa kufisha kilicho hai ambacho si sahihi ndani ya maisha ya mwamini.
• Anachotaka kukiona Yesu Kristo ni Imani na Muunganiko wa Roho Mtakatifu katika Neno linalotamkwa
• Kinachofanya nguvu ya Neno linalotamkwa isidhihirike ni kwa sababu wengi tunatamka neno likiwa halijachanganyikana na imani
• Lakini pia linaweza kuchanganyika na Imani lakini mahusiano kati ya mtu na Mungu hayako sawasawa.
• (Dhambi inajenga ukuta kati ya Mungu na mtu, uharibu mahusiano ya mtu na Mungu)
• Kinachofanya neno ulilotamka lisiwe na matunda ni asili ya nguvu iliyopo ndani mwako.
• je, unaamini katika Yesu Kristo, aliye chanzo cha nguvu.
• 2 WAFALME 7:1-…..
• Kujua ni wakati gani neno nililolitamka litatimia si juu yangu, ila mapaswa kuamini tu kuwa linafanyika sasa, wakati huohuo niliolitamka.
• 2WAFALME 13:14- …….
• Mimi ni nabii wa maisha yangu mwenyewe, yaani nina uwezo wa kujitabiria juu ya maisha yangu na ikawa hivyo hivyo sawa na nilivyotamka.
• Nyuma ya kila neno linalotamkwa kuna roho, inaweza kuwa roho chafu ya ibilisi au Roho Mtakatifu.
• Roho hiyo ndiyo inayolipa nguvu neno lililotamkwa.
• Upako ulio ndani ya mtu hauhitaji nguvu ya mtu ya mwilini kudhihirika, bali inahitaji maarifa ya Neno la Mungu ndani ya mtu ili kujua namna ya kuiachilia.
• Kila neno linalotamkwa kwa kinywa lina nguvu sipaswi kupuuza neno lolote linalotamkwa juu yangu haijalishi limetamkwa na mtu anayemcha Mungu au mtu asiye mcha Mungu.
• Neno ninalolitamka liwe ni jema ua baya lina madhara katika ulimwengu war oho, iwe ni madhara hasi au chanya.
• Natakiwa nitamke neno nikiwa na ufahamu kwamba hili ninalolitamka litakuwa na madhara Fulani, na itakuwa hivyo.
• Ufahamu ukiingia ndani ya mtu hofu uondoka.
• K**a sijajijua mimi ni nani, sijajua namna ya kutembea katika asili yangu na kujua namna ya kuumba vitu katika maisha yangu nitatembea na kuishi k**a mtumwa katika ulimwengu huu, ambao nimewekwa nitawale.
• Nguvu ya neno lililotamkwa nina uwezo wa kulibatilisha kwa Neno katika Roho Mtakatifu.
• Pale unapojaribiwa na kutamka maneno ya kuvunjika moyo/ au kukatisha tamaa, ibilisi anayashikilia na kukufunga kwa maneno yako mwenyewe.
• (ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo).
• Nguvu ya neno lililotamkwa litaandaa watu kwa ajili yako kesho, aidha ni wema kwa neno nililotamka jema, ama ni waovu kwa neno ovu nililolitamka.
• Neno ninalolitamka leo litanitambulisha kesho.
• Napaswa kutambua mimi ni nani na mamlaka yangu niliyonayo ni
• Mungu akitamka Neno natakiwa kuamini Zaidi ya ninavyotakiwa kuamini.
• Nguvu ya neno lililotamkwa lina uwezo wa kubadilisha kila kitu. (2WAFALME 13:14-…)
• Nabii Elisha ingawa alikuwa anaumwa bado maneno ya kinywa chake yalikuwa na nguvu.

08/11/2018

JERUSALEMU SPRITUAL TRANSFORMATION CHURCH
TAREHE: 4/11/2018
NA PASTOR STEVEN LAIZER
UTANGULIZI
Furaha ya wokovu ikiondolewa ndani mwangu hali ya kumuabudu Mungu katika Roho na Kweli inaondoka
SALA
ROHO MTAKATIFU NINAKUOMBA REJESHA NDANI MWANGU FURAHA YAKO YA WOKOVU.
UJUMBE: FURAHA YA WOKOVU(THE JOY OF SALVATION)
NINI MAANA YA FURAHA YA WOKOVU?
NA KWANINI FURAHA YA WOKOVU?
• Furaha ya wokovu ni shangwe inayoletwa ndani ya mtu baada ya kutolewa kwenye vifungu (utumwa) wa dhambi.
• Hapo furaha ya wokovu itastawi.
• YOHANA 8: 31-36
• Mtu aliyewekwa huru atakaa uweponi mwa Mungu kila wakati, ambaye hajawekwa huru hawezi kukaa kwenye uwepo wa Mungu kila wakati. Kwa sababu yupo chini ya utumwa.
• Dhambi ikitawala moyo wangu nitakuwa mtumwa wa ibilisi,
- hali ya furaha ya kukaa kwenye uwepo wa Mungu haitakuwepo wa ndani mwangu.
- Furaha ya kusoma Neno la Mungu haitakuwepo ndani mwangu;
- Furaha ya kukaa kwenye mapenzi ya Mungu haitakuwepo ndani mwangu;
- Furaha ya kumuabudu Mungu haitakuwepo ndani mwangu.
- Furaha ya kuomba na kufinga haitakuwepo ndani mwangu
• Dhambi ikiwa ndani ya mtu inamtumikisha mtu kutenda na kuelekea kule dhambi inamuelekeza, kwa sababu yupo chini ya utumwa.
• Wakristo wengi leo hawana furaha ya wokovu ndani ya mioyo yao, kwa sababu dhambi imeshachukua nafasi ndani mwao.
• Dhambi haiwezi kumfanya mtu kufurahia wokovu ndani mwake, sababu tayari ni mtumwa.
• Furaha ya wokovu ikiondolewa ndani ya mtu hataona umuhimu wa kumuabudu Mungu muda wote kila awakati.
• Bila kujali wokovu tulionao
- furaha ya wokovu ndani mwetu haiwezi kuimarika
- Hatuwezi kuleta furaha kwa wengine.
• ZABURI 51:12
• Furaha ya wokovu itakulazimisha- kusoma Neno, kufunga, kutenda mema, kuomba

KWANINI FURAHA YA WOKOVU ? (why the joy of salvation)
• Bila furaha ya wokovu siwezi kuomba katika ulimwengu wa roho.
• Furaha ya wokovu ina uwezo wa kumfanya mtu aache mambo mengine na kumuabudu Mungu.
• Furaha ya wokovu ina uwezo wa kunifanya niyakatae mapenzi yangu na kuyafuata mapenzi ya Mungu.
• Furaha ya wokovu itakufanya uwadharau wanaokudharau kwa sababu umebeba kusudi la Mungu ( yaani kuwapuuzia)
• Furaha ya wokovu ikiondolewa ndani mwangu hofu ya Mungu haitakuwepo ndani mwangu.
• Furaha ya wokovu itanifanya nione uthamani wa wokovu nilionao.
• Note: wokovu niliona ni wa thamani kuliko mimi mwenyewe.
• Furaha ya wokovu ikiondoka ndani ya mtu itamfanya mtu kuishi maisha ya kawaida tu, sababu haoni uthamani wa wokovu.
• NOTE: WOKOVU ni YESU KRISTO mwenyewe- WAEBRANIA 2:1-…….
• Tusipojali wokovu tuaishi maisha k**a watu wasioamini tukufanya mambo yale yale yanayofanywa na wasioamini ikiwepo kwenda kwa waganga, kwa sababu hatusikii tena sauti ya Mungu.
• 1SAMWELI 28:3-20
• K**a furaha wokovu iko ndani mwangu nitallipa gharama yoyot kulinda wokovu wangu udipotee.
• YUDA
• Kushindania Imani ya wokovu wangu ni vita, si suala jepesi/ rahisi.
• Kuwa mkristo anayetambua furaha ya wokovu ni kuwa shujaa na imara katika kila changamoto anayopitia.
• Furaha ya wokovu ndiyo inayoleta muunganiko na Roho Mtakatifu na mimi na kumfanikisha katika kila jambo.
• Furaha ya wokovu ndani mwetu lazima itunzwe ndani ya roho, mioyo na nafsi zetu.

• FURAHA YA WOKOVU INATUNZWAJE?
• Kwa kushika sheria za Mungu zilizopo katika Neno lake.
• WARUMI 12:2
• (maandalizi yangu sahihi ya leo kwenye maombi,kufunga, kujifunza Neno, kuutafuta Uso wa Mungu, ni kesho yangu njema)
• Natakiwa nijifunze kile ambacho hakifai nisikiweke moyoni mwangu, ili nisonge mbele.
• Mahusiano yangu na Mungu ni ya muhimu sana, haijalishi naenda kanisani kila siku, katika roho naweza kuwa nishamuacha Mungu, kwa tabia zangu.

• Furaha ya wokovu ni ya muhimu sana kuliko fedha na dhahabu.

*ZINGATIA: Wokovu wangu ni ramani yangu, nikiupoteza nimepoteza mwelekeo.
• Nisiruhusu chochote kinitoe kwenye mwelekeo wa ukweli, iwe ni marafiki, kazi, mali n.k.
• Maumivu yanayosababishwa na adui yasinifanye nikaacha asili yangu ndani mwangu
• Mishale inayorushwa na adui isinifanye nikaacha asili yangu ya Uungu niliyonayo, nitazame mbele.
• Pale ambapo nimetoa umakini wangu na muda wangu kwa adui yaani kumsikiliza adui ndipo ambapo nimempa adui nafasi. Muda wangu mwingi nitautumia kutafakari na kuzungumza juu ya maumivu ninayopitia.

29/10/2018

JERUSALEMU SPRITUAL TRANSFORMATION CHURCH.

KIVULE AREA-DAR ES SALAAM
NA
PASTOR STEVEN LAIZER

UTANGULIZI
• MARKO 6:1-6
• Maswali yasiyo namaana juu ya namna Mungu anavyotenda kazi au juu ya uweza wa Mungu yanatufanya tushindwe kupokea kutoka kwa Mungu.
UJUMBE : KUTOKUAMINI
• Mara nyingi sisi tunaomuamini Yesu Kriso tunashindwa kupokea muujiza tunaouhitaji kwa sababu ya kutokuamini ndani yetu, ambayo inaletwa na maswali juu ya Neno la Mungu na Nguvu ya Mungu.
• Unapokuwa na maswali juu ya Neno alilotamka Mungu unakuwa umeruhusu kutokuamini kukalia moyo wako, hivyo uwezo wa kuamini na kupokea kutoka kwa Mungu uondoka.
• Kuna wakati mwingine maswali yanaweza kuzalishwa na mazingira anayopitia mtu.
• Kuna maswali unaweza kuwa nayo ambayo yanakupelekea kumtafuta Mungu Zaidi na sio kukukatisha tamaa.
• Mfano: maswali aliyokuwa nayo Gideon WAAMUZI 6:11-24
• Kuna maswali ndani ya mtu yenye kuzalisha hali ya shauku ya kutaka kujua ujumbe wa Mungu.
• Maswali waliyokuwa nayo watu katika MARKO 6 yalikuwa yamechanganyika na dharau, ndio maana yalizalisha hali ya kutokuamini ndani mwao.
• Maswali yanayozalisha hofu juu ya utendaji kazi wa Mungu, yanakundolea uhalali wa kuwa mwann wa Mungu mwenye uwezo wa kupokea kutoka kwa Mungu.
• Kinachompelekea mtu awe na maswali yanayompelekea mtu kutokuamini ni upungufu wa Neno la Mungu ndani ya moyo wake.
• Ukifahamu Neno la Mungu hautakuwa na hofu juu ya utendaji kazi wa Mungu.
• Ukiwa na Maarifa ya Neno la Mungu, mazingira unayopitia hayatakufanya kuwa na hofu juu ya uwezo wa Mungu.
• (asiyeamini, tayari amekwisha kuhukumiwa).
• Hali ya kutokuamini inazaliwa ndani ya mtu pale mtu anapoacha kuutafuta Uso wa Mungu.
• Imani ndani ya mtu haiwezi ikakua k**a mtu hajafafanuliwa Neno la Mungu.
• ZABURI 119:130
• MATENDO 8: 26-….
• Hali ya kutokuamini inaingia ndano ya mtu pale ambapo mtu ameacha kusikia Neno la Mungu linalofundishwa kwa UKWELI.
• Maswali yasiyo na maana ya uwezo wa kukunyima;
- kupokea taarifa kutoka kwa Mungu
- kupokea muujiza unaohitaji kutoka kwa Mungu.
• Hali ya kutokuamini ina uwezo wa kumfanya mtu akamtukana Mungu/ akatamka chochote mbele za Mungu.
• Hali ya kutokuamini wakati mwingine uzalishwa na mazinginra ya mtu aliyonayo., ndio maana kuna umuhimu wa mtu kujitenga na watu ulionao kuutafuta uso wa Mungu.
• Mtu mwenye maarifa ya Neno la Mungu ataendelea kukaza mwendo hata k**a kuna kikwazo mbele yake.,hawezi kukatishwa na mazingira anayoyaona, ataendelea kusonga mbele.
• Hali ya kutokuamini inazalishwa na hali ya kutokutii Neno la Mungu.
• Kutokulitii Nneo la Mungu upelekea kina cha maarifa ya Neno la Munug na hali ya kuamini kutoweka ndani ya mtu.
• Zingatia: Kuna kulitii Neno na kuna kuliamini Neno. Hivi ni vitu viwili tofauti.
• Mtu anaweza akaliamini Neno, lakini asilitii

29/10/2018

KIVULE DAR ES SALAAM
TAREHE: 14/10/2018
Na.Pastor Steven Laizer
UJUMBE: NURU YA ULIMWENGU
MATHAYO 5:13, 14
• YESU KRISTO ni NURU iliyokuja kwetu kutuangaza sisi tuliomkubali ili sisi tuuangazie ulimwengu nuru hiyo.
• (Yohana 1:12)
• K**a haumwamini Yesu Kristo Nuru hiyo haiwezi kuwa ndani yako, na k**a hauna Nuru hauwezi kuangaza kwa sababu una giza, na giza haliwezi kuangaza.
• Swali la kujiuliza: k**a wewe ni nuru ya Yesu Kristo, je, unaangaza?
• Nuru ya Yesu Kristo ikiwa ndani mwangu, nikitembea matendo ya Yesu Kristo yataonekana dhahiri ndani mwangu.
• Matendo ya Yesu Kristo yakionekana ndani mwangu, nitakuwa na mvuto kwa wengi wasiomwamini Yesu Kristo.
Kwanini?
- Kauli zangu zitakuwa na nuru ya Yesu Kristo, zitaondoa giza kwenye kauli za giza za ibilisi.zinazoelekezwa kuharibu maisha yangu mimi na maisha ya watu wengine.

• Kauli yangu ikishakuwa na Nuru (ikivuviwa nuru), nikizungumza ni Yesu Kristo anazungumza, nikiamuru ni Yesu Kristo anaamuru.
• Kusudi la ibilisi kuleta giza kwenye maisha ya mwamini ni kumfanya mwamini kauli zake ziwe na giza, ni ili kuleta uharibifu kwenye maisha yake.
• Kusudi la MUNGU kumtuma Yesu Kristo ni ili sisi tung’ae.
• YOHANA 17:22
SALA:
ROHO MTAKATIFU NISAIDIE UFAHAMU WANGU, MOYO WANGU, AKILI YANGU, ROHO YANGU KILA WAKATI, IWE NA TAARIFA YA UHARIBIFU/GIZA ANALOTAKA KULETA IBILISI JUU YANGU. USIFANIKIWE JUU YANGU. AMEN.
• (Ibilisi siku zote ujitahidi kuzuia nuru ya mtu anayeamini asiangaze, sababu anajua wazi akiangaza wengi watabadilishwa na kumgeukia Mungu.
• Ninachotakiwa kufanya ili Nuru ya Yesu Kristo iangaze kwenye maisha yangu ni mimi kuamua kulijaza Neno la Mungu ndani mwangu na kukaa katika Neno hilo.
• Kwahiyo maamuzi ya kuangaza ni ya kwangu mimi, sababu tayari Mungu alishatuangaza kupitia mwanae Yesu Kristo.
• ISAYA 60:1-….
• UHALISIA (ASILI YANGU) wangu katika roho ni Nuru.
• 1YOHANA 1:5-7

BWANA YESU asifiwe wapendwa wangu katika KRISTO ninayofuraha kukubwa ,kukualika we we unayetufatilia kwenye ibada zetu z...
26/10/2018

BWANA YESU asifiwe wapendwa wangu katika KRISTO ninayofuraha kukubwa ,kukualika we we unayetufatilia kwenye ibada zetu zinaziendelea katika eneo la john fedha ambako tupo kwa muda,usikose ni ibada ambayo MUNGU atarejesha furaha ya wokovu ndani mwetu,injili ni uweza wa MUNGU uketao wokovu kwa watu wote ,njoo MUNGU akufundushe na kukuinua imani yako katika KRISTO YESU ,kwakua yupo pamoja nasi akilidhihirisha neno kwa ishara zitakazo fuatana nalo,shalom shalom,mbarikiwe nyote.

10/10/2018

TAREHE: 06/10/2018
UJUMBE: DHAMBI SEHEMU YA 3
 NI NAMNA GANI DHAMBI INAVYOMUINGIA MTU
• (Mara nyingi dhambi inatokana na mawazo ya mtu).
• Dhambi inamuingia mtu pale anaporuhusu mawazo machafu ndani ya moyo wake, hii ina maana roho chafu ya dhambi au inayomsukuma mtu kufanya dhambi inamuingia mtu pale anaporuhusu mawazo machafu kuingia ndani ya moyo wake.
• Wakati mwingine roho chafu ya dhambi/au inayomsukuma mtu kufanya dhambi inamuingia mtu kwa njia ya ndoto au kufanya maagano na mtu kwa njia ya ndoto pale ambapo mtu ametoa muda wake kutafakari mambo yasiyofaa au kukaa kusikiliza mambo yasiyofaa.
(kwanini? Kwasababu kwa kawaida mwanadamu anarithi kutokana na kile mtu anachosikia, anachoona)
• Roho chafu inapomuingia mtu ni rahisi ila kumtoka mtu si rahisi, kuna gharama kwa mtu kuipinga kwa kutoa nafasi ya kuliingiza Neno ls Mungu ndani yake.
• MITHALI 1:10
• Maamuzi ya kuishinda dhambi au ya kushindwa na dhambi ni ya kwangu mwenyewe.
• (WARUMI 7:14-…..)
• Ili kujitoa katika roho ya dhambi inahitaji maamuzi yangu ya kumpinga shetani na kuamua kukaa kwenye Neno la Mungu.
• Tunafundishwa kuhusu dhambi ili tupate ufahamu juu ya namna inavyomuingia mtu na na ni namna gani tunawet uizuia
• Dhambi vilevile inamuingia mtu kwa udanganyifu wa adui., kuna vitu ambavyo adui (ibilisi) anavitumia kukuvuta uingie wkenye dhambi.
• YAKOBO 2:
• (dhambi ni ukuta kati ya mtu anayemuamini Yesu Kristo na Mungu. Hata akiomba Mungu hamsikii
• DHAMBI 1: 28 (SOMA SURA YOTE)
• (Isaya 6:1-……)
• Wakati mwingine mtu mwenye kusudi la Mungu ndani yake pale anapotoa mwanya kwa adui kwa kutokutii amri za Mungu dhambi umuingia mtu ili kumkwamisha katika kusudi la Mungu ndani mwake.
• WAKOLOSAI 1:
• wakati mwingine ibilisi huleta mateso kwa mtu ili kumfanya mtu ametende Mungu dhambi.
• AYUBU SURA YA 1 NA SURA YA 2
• Ili kuimarisha upendo na mahusiano yangu na Mungu kuna gharama ya kulipa kuharibu vitu vyangu ambavyo naona ni vya thamani kwangu.

 NI NAMNA GANI MTU ANAWEZA KUPINGANA NA ROHO YA DHAMBI
• Nikishajua ni namna gani dhambi inamuingia mtu, basi ni rahisi kuizuia dhambi isikuingie, yaani kwa kuufunga mlango ambao dhambi inatumia kumuingia mtu.
• Tunashindwa kufunga mlango ambao dhambi inatumia kuingia kwa sababu hatuna mahusiano mazuri na Mungu.
• Dhambi ili iondoke lazima NENO LA MUNGU lenye nguvu ya kufukuza dhambi liingie ndani mwangu.
• WAEFESO 2:1-………….
• (Ninapokuwa katika dhambi maana yake nimekufa katika roho).
• *Nitaweza kupingana na roho ya dhambi kwa kuruhusu sheria za MUNGU zikae kwa wingi ndani ya moyo wangu.
• ZABURI 119:11
• *Nitaweza kushinda roho ya dhambi kwa kuacha kutenda matendo maovu mbele za MUNGU.
• ISAYA 1:15-20

30/09/2018

KIVULE-DAR ES SALAAM -TANZANIA

TAREHE: 23/09/2018
UJUMBE: DHAMBI NO.1
UTANGULIZI
• Miongoni mwa vitu vikubwa ambavyo mtu anayemuamini YESU KRISTO anatakiwa kufurahia na ni:
- Kukemewa kuhusu dhambi.
- Kukaripiwa na kuonywa juu ya dhambi.
- Kufundishwa na kuelekezwa namna ya kushinda dhambi.
Kwanini?
Dhambi inayomtenganisha mtu na Yesu Kristo.
(TIMOTHEO 4:13)
(Baraka za mwamini zinakuja pale anapoamua kumtii Yesu Kristo).
Tabia ya dhambi inamuotea mtu: na inamtamani mtu.
• Roho Mtakatifu umfunulia na kumfundisha mtu kuhusu dhambi na kumpa mtu nguvu ya kushinda dhambi.
• Maswali ya kujiuliza:
Dhambi ni nani?
Na ni nani anayempa nguvu huyu dhambi.
Jibu: ni ibilisi
• Dhambi ni nini?
Dhambi ni roho chafu ya ibilisi inayodhihirisha matendo yake kwa kutumia vitu na tabia mbalimbali za kibinadamu.
• Dhambi kwa maana nyingine ni tunda la roho chafu (ibilisi) ambalo linazaliwa ndani ya mtu pale anapoach akuitii Sauti ya Mungu (NENO LA MUNGU).
• ZINGATIA
• Makosa yangu yasinifanye niukimbie Uso wa Mungu, lakini yanifanye nione sababu ya kumsogelea Mungu Zaidi.
• Makosa yasinitoe kwenye uwepo wa Mungu bali yawe sababu ya kunipeleka Zaidi kwenye uwepo wa Mungu.
• Dhambi ni roho ya giza ndio maana utakuta mtu anapambana dhidi ya dhambi leo, ila kesho yupo kwenye dhambi tena, kwa sababu hajatoa nafasi ya kutii Neno la Mungu.
• Ibilisi anajua mtu anashinda dhambi kwa kutii Neno la Mungu, (ndio maana anaweza kutumia pia Neno la Mungu kumjaribu mtu ili akosee pale anapojua mtu anatii Neno La Mungu).
• Dhambi ni roho chafu ya ibilisi inayofanya kazi kwa kutumia watu na vitu vinavyoonekana.
• Dhambi ni roho, nitaweza kupambana na roho hiyo kwa kuamua kuingia rohoni.(Roho upambana na roho)
• Mtu anakuwa roho pale anapolijaza Neno la Mungu ndani mwake ma kuwa k**a Roho Mtakatifu anavyotaka, kwa kuomba, kwa kufunga na kwa kujinyenyekesha kwa Mungu.
• Yesu Kristo alituonyesha mfano wa wazi wa kufunga, kuomba, na kuskesha ili kumtafuta Mungu na kuishinda dhambi.
• Ndio maana Yesu Kristo ingawa alikuwa katika mwili huu wa dhambi, hakutenda dhambi.
• Watumishi wote wa Mungu adui wao mkubwa ni dhambi (ibilisi)., sababu wanajua kitendo wakikosea tu, wanapoteza mamlaka yao kwa ibilisi, hawataweza kumtiisha tena/ kumkemea.
• Dhambi wakati mwingine utumia udhaifu wa mtu au mawazo ya mut kumshambulia mtu.
• Ufahamu na maarifa juu ya Neno la Mungu vina nguvu ya ajabu ya kuweza kumpiga ibilisi k**a nimeamua kuruhusu Neno la Mungu likae ndani mwangu.
• Hata k**a naomba kwa juhudi kiasi gani k**a sina maarifa ya Nneo la Mungu na mahusiano mazuri na Mungu nijue wazi tayari ibilisi ameshanishinda.
• Biblia inasema mpingeni ibilisi katika uthabiti wa Imani.
• Imani haiwezi kuwa thabiti k**a sina maarifa ya Neno la Mungu ndani mwangu.
• Inahitaji maarifa ya NENO LA MUNGU ndani ya mwamini kuamuru vitu na vikatokea.
• Bila maarifa ya Neno la Mungu watu uangamia.
• MWANZO 4:5-…..
• Dhambi ni roho giza inafanya kazi katika ulimwengu wa giza na sio wa nuru.
• ZINGATIA:
K**a wewe una roho giza, inakuwaje ukemee ufalme wa giza? MATENDO 19:11-16
• Dhambi uondoa mamlaka ya Mungu katika maisha ya mwamini.
• Ndio maana mtume Yohana akasema aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi bali ujilinda asitende dhambi.
• 1YOHANA 3:9
• Katika suala la dhambi mtu hujilinda, yaani, ana uchaguzi aidha afanye au akatae dhambi.
• Na mtu uwa mtumwa wa yule aliyeamua kumtumikia, ikiwa ni utumwa wa dhambi kwa uangamivu wake mwenyewe, ama ukiw autumwa wa haki kwa wokovu wa roho yake mwenyewe.
• Dhambi ikimvaa mtu uondoa aibu na hofu ya Mungu ndani ya mtu.
• Dhambi (roho chafu ya giza) ina uwezo wa kupofusha ufahamu wa mtu asione k**a anakosea.
• Dhambi ikimvaa mtu umtawala mtu, anakuwa hana maamuzi yake tena, kwa kuwa dhambi umuongoza
• WARUMI 7:14-25
• Mimi nina maamuzi ya roho chafu kukaa mbali na mimi kwa kuamua kutii Neno la Mungu.
• Vilevile nina maamuzi ya roho chafu iniingie na kukaa ndani yangu kwa kuacha kutii Neno la Mungu.
• MWANZO 4:5-10
• Mara nyingi tunaisikia Sauti ya Mungu lakini moja ya changamoto kubwa tuliyonayo ni katika kutii maelekezo ya Sauti ya Mungu.
• Inahitaji Imani na utii wa Neno la Mungu ndani ya mtu ili aweze kutii Sauti ya maelekezo ya Mungu.
• Yesu Kristo akiona maamuzi ya mtu ya kukataa dhambi, ndipo umpa nguvu ndani yake ya kuishinda dhambi.
• (MITHALI 7:7-…)
• Roho ya dhambi ikishaingia ndani ya mtu, mtu uwa na tabia hizi:
- Hakubali kuonywa
- Ujiona yuko sahihi na anajua kila kitu.
- Ujihesabia haki.
• Ila kwa mtu mtiifu na mnyenyekevu akigundua tu amekosea papo hapo uingia magotini kumsihi Mungu rehema, uwa aanzi kujitetea.
• Mfano: Mfalme Daudi (Soma 2 SAMWELI Sura ya 11 na 12
• (Nisitumie udhaifu nilionao kuruhusu au kuhalalisha roho chafu ya dhambi initawale).
• Roho chafu ula katika tabia mbaya za watu ( tabia mbaya ni chakula cha roho chafu)
• Kile ambcho ndani mwako umekusudia kukifanya ikiwa ni cha Kimungu, Roho Mtakatifu atakithibitisha (kwa kupitia Neno lake).
• K**a ilivyo kwa matunda ya Roho Mtakatifu dhambi pia ina matunda ya roho chafu, ambazo ni:
- Ghadhabu
- Wivu
- Chuki
- Dharau
- Kutokutii
- Uchoyo
- Matukano/matusi
- Kiburi cha uzima
- Tamaa mbaya za mwili
- Utovu wa nidhamu
- uongo
- Kutokuamini n.k
• Miongoni mwa vitu ibilisi amewafunga watu in kuwazuia wasipate maarifa ya Neno la Mungu.
• WARUMI 1(Soma yote)

TAREHE: 30/09/2018
Mahusiano yangu na Mungu yakiimarika mahusiano yangu na Mungu pia yataimarika.
Kwanini?
Kwasababu mtu uanza kumpenda Mungu kwanza ndipo atapenda na wenzake pia
Mahusiano yangu na Mungu ni ya muhimu kuliko mahusiano yangu na mwanadamu yoyote yule.

UJUMBE: DHAMBI- SEHEMU YA .2

• DHAMBI NI UASI.
• Nini maana ya uasi?
• Hauwezi kuacha kitu ambacho haukijua,lakini pia hauwezi kuchukia kitu ambacho haukijui.
• Ibilisi hahitaji mtu anahitajiroho ya mtu, ukimkubali tu akak**ata fikira zako atakuongoza kufanya kile anachotaka ukifanye.
• Ibilisi uja kwa njia ya ushawishi ndio maana uitwa mjaribu.
• Ibilisi anaweza kukujaribu kwa kutumia au kupitia uhitaji ulionao.
• Ibilisi pia anaweza kukujaribu kwa kukuonyesha maono feki.
• Ibilisi utumia vitu na tabia za kibinadamu kumsahwishi mtu.
• YAKOBO Biblia inasema mtu ujaribiwa kwa tamaa zake mwenyewe uku akivutwa na uongo.
• Ibilisi umdanganya mtu kwa kutumia tamaa yake mwenyewe.
• Inahitaji maarifa ya Neno la Mungu na maongozi ya Roho Mtakatifu kutambua kwamba uyu ni ibilisi.
• Biblia inasema watu wangu wanangamia si kwa kukosa upako, bali kwa kukosa maarifa.
• K**a ambavyo Mungu anahitaji maamuzi yako kwa kutoa muda wako kufanya anachotaka ili
• Vivyo hivyo ibilisi anasubiri utoe maamuzi kwa kutoa muda wako kufanya anachotaka ili akuletee uharibifu.
• *DHAMBI NI UKUTA KATI YA MTU NA MUNGU, hii ina maana nikitenda dhambi katika fikra zangu, moyo wangu, na mwili wangu, nimejiwekea ukuta kati yangu na Mungu.
• (ndio maana Yesu Kristo ni Mpatinishi kati yetu na Mungu.)
• Nikitenda dhambi ninajiondolea haki ya kusikiwa na kujibiwa maombi yangu na Mungu.
• ISAYA 59:1
• *KUASI maana yake ni kukana wenzako na kuacha utaratibu mliojiwekea na kuingia upande wa adui., kwa hiyo unapoingia kule umepoteza haki ya kundi uliloliacha, na kundi uliloliacha haliwezi kukuacha ubaki salama sababu linajua wazi unafahamu siri za kundi husika kwahiyo unaweza kuzitumia kuleta uharibifu kwenye kundi lako uliloasi.
• Hali ya uharibifu ikishaingia ndani ya ufahamu wa mtu aliyemuasi Mungu hata akiambiwa ujumbe wa Mungu hawezi kuuelewa au kuukubali kwa sababu ya hali ya mazoea.
• (Mungu ana njia nyingi za kuzungumza na mtu)
• Unapotenda dhambi unajiletea mwenyewe uharibifu kwenye maisha yako.
• (Changamoto tulizonazo si sababu ya sisi kutenda dhambi, bali ziwe chanzo cha kumsogelea Mungu Zaidi).
• *Dhambi inapofusha macho ya mtu ya rohoni asione k**a ambavyo Mungu anaona; masikio ya rohoni asisikie k**a Mungu anavyosikia.
• *Dhambi inapofusha ufahamu wa mtu wa rohoni asiwe na uwezo wa kupambanua, kwamba hiki ni sahihi, na hiki si sahihi.
• (Mungu ametoa nafasi ya mimi kuchagua kati yay eye na ibilisi, ni nani nitamtumikia).
• Kitu cha kwanza ambacho natakiwa kuogopa sana ni mahusiano yangu na Mungu, natakiwa niwe makini sana yasiharibike, ni hatari.
• Biblia haisemi Mungu atakulinda na dhambi, bali inasema aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi bali hujilinda mwenyewe asitende dhambi.
• 1 YOHANA 2:15-………
• Yohana 8:41
• Moja ya adui mkubwa wa mtu anayeamini, si jirani yake au mtu mwezake, bali ni roho chafu ya dhambi ndani ya mtu.
• Zingatia:
• Ni rahisi sana kumkaribisha ibilisi ndani mwako, ila ni vigumu sana kumtoa, inahitaji neema.
• DHAMB NI UASI:
UASI ni kukimbia ufalme mmoja au ufalme wangu ambao nilizaliwa ( sisi tumezaliwa kwa Neno katika roho) na kuingia ufalme wa pili ambao unapingana n aufalme wangu.
Zingatia:
Kuna kukimbia ufalme na kuna kutekwa.
Mfano: roho chafu zinakuvizia wakati wa kulala, ama wakati ambao haujaomba, ama wakati ambao nimeacha kusoma Neno, ama kwa njia ya ndoto.
Mtu mara nyingi amuachi Mungu haraka, balia uanza kidogo kidogo, kwa kuanza kulipuuzia Neno la Mungu.
• Wengi wetu tunaishi maisha ya kinafiki tukijifanya tumeokoka wakati tayari rohoni tumeharibu mahusiano yetu na Mungu. Hapo hatumdanganyi mtu bali tunajidanganya wenyewe na kujiletea uharibifu wenyewe.
• Watumishi wa Mungu wameamriwa kukemea, kukaripia na kuonya na kurejesha kwa upole pale mtu anapoanguka dhambini, na si kuwahukumu au kuwatenga pale wanapokosea.
ZINGATIA
“Ogopa kukaa mahali hatari bila kuchukua tahadhari”.
Unapokuwa mkristo anayeishi maisha ya kawaida tu k**a mtu mwingine asiyeamini, ni hatari kwake, anaweza kupigwa.
• ISAYA 1:15-……
• Unapoingia katika kuomba hakikisha ndani mwako umeweka dhambi zako mbali nawe, yaani unaacha.
• Dhambi ni dhambi, hakuna tofauti ya dhambi na dhambi wala hakuna dhambi ndogo na kubwa.
• Mfano: anayesema uongo ni sawa sawa tu na anayezini.
• *kitendo cha kutenda dhambi maana yake umemtii ibilisi.
• *dhambi ni mujumuiko ya matendo yote yasiyo ya haki, yasiyo halali.
• *DHAMBI NI UHALALI WA ADUI (IBILISI) KUMKALIA MTU. (ni leseni ya makazi kwa mtu).
• Wajibu wa watumishi wa Mungu ni kufundisha watu yaliyo kweli, ila maamuzi ya kukaa katika kweli hiyo no maamuzi ya mtu.

MAMBO YA KUJIFUNZA
 NAMNA GANI ROHO YA DHAMBI INAMUINGIA MTU;
 NI NAMNA GANI MTU ANAWEZA KUPINGANA NA ROHO YA DHAMBI.
• LAZIMA UJUE SILAHA ZA ADUI NA MBINU ANAZOZITUMIA ADUI NDIPO UWEZE KUPIGANA NA ADUI
• UKIINGIA KUPINGANA NA ADUI KABLA YA KUJUA SILAHA NA MBINU ANAZOTUMIA ADUI LAZIMA UTAPIGWA.
 HAUWEZI KUIJARIBU ROHO K**A WEWE SI ROHO.
 NINAKUWA ROHO KWA KUPATA MUUNGANIKO NA ROHO MTAKATIFU

• WOTE WALIOUNGWA NA BWANA NI ROHO MOJA NAYE.

Address

Kivule
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jerusalem Spiritual Transformation Church Kivule -Magole Area posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share