18/07/2026
Kwanini ni muhimu kutoa sadaka?
Sadaka nimatoleo ya ibada, yanayo tolewa na waumini kwa lengo la kuonyesha utiivu na utekelezaji wa maandiko katika eneo hili la matoleo.
Katika maandiko Matakatifu, kwaeneo kubwa zaidi, Biblia inamtaka muumini kuwa mwaminivu na muadilivu katika kutekeleza maagizo ya Mungu katika maandiko haya matakatifu.
Moja ya maagizo ya Mungu kwa wanadamu, ni pamoja na kushika Amri 10 za Mungu, mfano, usiue. Hii nimoja ya onyo ambalo Mungu amemuonya mwanadamu duniani, hasa mwanadamu anae mwamini.
Kadhalika Sadaka ni matoleo ya ibada, ambayo Muumini atamtolea Mungu mbele ya kiongozi wa dini ama madhabahu ya anapo abudia.
Sadaka hii hutumika kununua chakula na maendeleo mengine ya nyumba ya ibada pamoja na wanao husika kusimamia mahali hapo, ambao ni watumishi wa Mungu mahali hapo.
Swali sadaka hii itakusaidia nini?
Sadaka inaruhusu kupokea baraka toka kwa mtu aliye barikiwa, yaani kupata sehemu ya baraka toka kwa mtu ambae Mungu amesha m'bariki.
Hivyo kwakutoa sadaka kanisani, mfano kanisa la RC, sadaka itakuruhusu kupokea baraka katika mfumo wa kanisa hilo, kuanzia parokia uliyo toa matoleo yako na kuenda hadhi shinani.
Kadhalika katika makanisa mengine, na hata kwa watumishi unao wajua na ukapata kibali machoni mwao, ikiwa utatoa matoleo yako kwao piya, utapokea sehemu ya baraka toka kwa watu hao ambao unaamini Mungu amewababriki katika nafasi yao.
Hii ni kwawatoaji.
Kadhalika kunawapokeaji wa sadaka.
Mtu anaye pokea sadaka ama unataka kupokea sadaka, kunamambo kadhaa unapaswa kusimamia.
Kwanza ama ujiunge na mtandao wa kanisa fulani, ama ufwate namna Roho wa Bwana anavyo kuongoza, ili utambue mahali utakapo simama ili kuwaonyesha wengine ile karama Mungu amekukarimia, ili kwakazi zako wapendwa wa Mungu wakutunze kwa matoleo yao.
Hivyo nakusihi kutokumuone wivu mtumishi wa Mungu yoyote yule kwa sadaka anayo pewa, kwani hakuna anaye toka sadaka ya bure, kila anaye toa sadaka anajua kwanini ametoa, hasa wanao toa sadaka kubwa wanajua uzito wa sadaka zao.
Badala ya kumuonea wivu ama chuki, nivyema ukasoma elimu ya Roho pengibe ukatambua kuwa hakuna ujira wabure, na k**a ukitambua wala hakuna siku utatamani sadaka kubwa kushindwa nguvu ya kharama uliyo karimiwa.
Barikiwa sana kwa kusoma nakuelewa mafundisho ya wa kiroho