21/04/2021
USIKUBALI KUTOLEWA MBUZI WA KAFARA
Mwanzo 9:24-27 "Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea, akasema, na alaaniwe Kanaani, atakuwa mtumwa kabisa wa ndugu zake. Na akasema, atukuzwe BWANA MUNGU wa Shemu, na Kanaani awe mtumwa wake. MUNGU akamnafisishe Yafethi, na akae katika hema za Shemu; na Kanaani awe mtumwa wake". Kosa la Hamu la kuuchungulia uchi wa Baba yake, lilimgharimu na kumfanya mtoto wake alaaniwe, maana Kanaani ni mtoto wa Hamu. Kanaani akafanyika kuwa mtumwa wa ndugu zake.Ukisoma katika Biblia utaona Kizazi cha Kanaani kilivyoijaza Africa, yaani walizaliana Africa, na Kizazi cha Shemu na Yafethi Ulaya, ndipo Mataifa ya Ulaya yakaonekana MAKUBWA yana NGUVU na Baraka Tele, alafu Africa tukawa watumwa, mataifa yetu yakaonekana hayana nguvu, mpaka tupate misaada Toka Ulaya. Ni kwa Sababu Hamu alitolewa Mbuzi wa kafara, alifanya kosa lililomfanya ashuke chini na ndugu zake kupanda juu. Maana tunaposema kuwa kuna MATAIFA MAKUBWA YENYE NGUVU NA MATAJIRI, ina maanisha kuna mataifa ya chini, mataifa maskini na dhaifu. Ina maana haya mataifa yametolewa kuwa mbuzi wa kafara. Ili kiwepo kitu bora lazima kiwepo kitu dhaifu ili kilicho bora kionekane. Ili awepo mshindi wa kwanza lazima wawepo waliofeli ili mshindi wa kwanza apatikane. Hawa waliofeli wametolewa mbuzi wa kafara kwa ajili ya Mshindi wa kwanza. Ili wawepo watu wanaofanya vizuri, ni lazima wawepo wanaofanya vibaya ili wanaofanya vizuri waonekane. Usikubali kutolewa Mbuzi wa kafara, kwa kosa la Hamu ndugu zake waliinuliwa! Kwa makosa ya ususi wako unamfanya mwingine aonekane kuwa msusi maafuru, k**a hayupo yeye watu hawasuki! Mtu anaulizia, fulani yupo? Akiambiwa hayupo anarudi bila kusuka, je wengine Siyo wasusi? Lazima kila mtu aonekane kuwa bora, na inawezekana kila mtu kuwa bora. Hata Mataifa ya Africa yaliyo mengi yameshainuka na kuwa bora, na inawezekana Kila Taifa kuwa bora, ni mipango na utendaji kazi ukiwepo ubunifu na ujuzi au utaalamu. Inawezekana wanafunzi wote kuwa bora, ndiyo maana nafasi ya kwanza inaweza ikashikiliwa na watu 3, hivyo wakijitahidi wote wanaweza kuwa namba 1 asiwepo wa 2 wala wa 3. Kuna Shule unakuta karibu wote wamepata Division 1. Hivyo hilo linawezekana wote kuwa bora. Kuna mashindano ya urembo yanaweza kufanyika majaji wakachanganyikiwa wasijue yupi anastahili kuwa kwanza, yupi anastahili kuwa wa pili. Hivyo inawezekana wote kuwa bora. Mtu mmoja anapoimba sana kuliko wote, akashangiliwa yeye peke yake, ina maana hao wengine walioimba wanaonekana hamna kitu, maana wangeimba vizuri wangekonga mioyo ya watu. Usikubali kuonekana hamna kitu. Mtu anapohubiri sana au kufundisha akapendwa sana kiasi kwamba akihama watu wanahama naye, ina maana wengine wanaonekana hamna kitu, wangekuwa na kitu watu wasingehama, maana watu wana tabia ya kuwafuata watu badala ya kumfuata MUNGU. Hivyo ni lazima kila mtu asimamie nafasi yake IPASAVYO ili kuonekana bora. Wanaposifia kuhusu mke mwema au mume mwema, ina maana kuna wake bomu na wame bomu. Mtu anapoitwa mfanyakazi bora, kuna wasio bora! Mtu anapoitwa Kiongozi bora, kuna kiongozi asiye bora, watu wanatamani hata ajiuzuru au afukuzwe. Mtu anaposifiwa ni muumini mzuri mtiifu, kuna waumini pasua kichwa! Ni mbuzi mwenye mapembe hata viongozi wa dini wanalia! Wanaumia. Kiongozi yoyote wa dini anapenda waumini wake wawe wazuri watiifu wenye Tabia njema, na Siyo wenye kuaibisha. Inawezekana watu wote kuwa bora, k**a ni mke mwema usifiwe wewe! K**a ni mume mwema usifiwe wewe! K**a mtoto bora usifiwe wewe! K**a ni mama bora usifiwe wewe! K**a ni baba bora usifiwe wewe! K**a ni jirani mzuri usifiwe wewe! K**a ni mchungaji mwema usifiwe wewe! K**a ni muumini mwema mfano wa kuigwa usifiwe wewe! K**a ni Kiongozi bora usifiwe wewe! K**a ni mfanyakazi bora usifiwe wewe! K**a ni Mwinjilisti mzuri uwe wewe! K**a ni Mwalimu mzuri uwe wewe! K**a ni mpishi mzuri uwe wewe! K**a ni mtangazaji bora uwe wewe! K**a ni mwandishi bora uwe wewe! K**a ni msusi bora uwe wewe! Katika jitihada za kila mtu kuutafuta ubora wake, basi tutajikuta wote tunakuwa bora. Na ubora unakuja kwa kuwa na bidii na kujituma, na kufanya kila kinachohitajika kwenye Sekta yako. MUNGU akubariki, akujalie kuwa bora.