New hope

New hope Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from New hope, Religious organisation, kwembe, Dar es Salaam.

Page hii ni kwaajili ya kuhubiri neno la Mungu na kuwapa watu tumaini kwamba yapo maisha baada ya haya ya duniani ykwamba yatupasa kuikimbia ghadhabu ya Mungu nakumuishi Kristo ili tuufikilie uzima wa milele.

09/10/2022

Hongera kwa kwenda ibadani .Mungu akubariki.

21/02/2021

*NJIA TATU ANAZOZITUMIA SHETANI KUWAFUNGA WATU*

Sehemu ya 3.

Sehemu ya kwanza hadi ya pili tuliona mambo mawili anayoyatumia shetani kuwafunga watu

*1.Maneno*
*2.Makombora*

Leo tunamalizia sehemu ya mwisho

*3.SADAKA*

Watu wengi sana hawajui kazi ya sadaka kiroho

✔Sadaka katika ulimwengu wa roho ina umhimu mkubwa sana kwa upande wa Mungu na kwa upande wa shetani

📚KAZI KUBWA YA SADAKA KIROHO

*Ni Kumpatanisha mtu na Mungu au miungu*

Biblia inasema hivi👇

*◾2 Wakorintho 5:19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.*

Sehemu nyingine imeandikwa hivi👇

*◾Waefeso 2:16 Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.*

👆🏻Nachotaka kukuonyesha ni kuwa kwa njia ya damu ya Yesu tumepataniswa na Mungu aliye hai

Ni hivi Damu ya Yesu ni SADAKA ya Yesu aliyoitoa mbele za Mungu kwaajili ya wanadamu waliokuwa gizani.

*◾Waefeso 5:2 mkaenende katika upendo, k**a Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.*

Sehemu nyingine imeandikwa hivi👇

*◾Waebrania 9:14 basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?*

👆🏻Kwahiyo damu ya Yesu ni sadaka ya upatanisho kati ya wanadamu na Mungu maana dhambi ilitutenga na Mungu

NISIKILIZE VIZURI MPENDWA KAZI MOJAWAPO YA SADAKA NI KUMPATANISHA MTU NA MUNGU AU MIUNGU ITATEGEMEA UTAITOA WAPI

*-K**a sadaka unaitoa kwa Mungu aliye hai maana yake unaipatanisha nafsi yako na Mungu kwaajili ya jambo Fulani*

*-Na k**a unaitoa SADAKA yako kwa miungu maana yake unajipatanisha nafsi yako na mapepo*

Kuna watu mnaenda kwa waganga wa kienyeji au kuzimu kabisa mnatoa

*-Mbuzi au kuku wengine hutoa mpaka damu za watu😢 kwaajili ya kafara au matambiko ni hivi kwa kufanya hivyo unaipatanisha nafsi yako na mapepo*

*-Hata ukitoa Pesa bado unaipatanisha nafsi yako na mapepo unayotaka yakusaidie*

👉KWA MAANA NYINGINE NI KWAMBA UNAPOTOA SADAKA NI SAWA NA UNATOA NAFSI YAKO AU MAISHA YAKO KWA MAPEPO

Maana imeandikwa hivi👇

*👉Mathayo 6:21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.*

🎤Yaani ulipoiweka hazina yako na moyo wako upo hapohapo

🎤Ukiweka hazina yako kwa Mungu na moyo wako utakuwa kwa Mungu

Na ukiweka hazina yako kwa mapepo na moyo wako utakuwa hapohapo kwa mapepo

*➡KWAHIYO UNAPOTOA SADAKA UNATOA MOYO WAKO NA UNATOA MAISHA YAKO PIA KUTEGEMEA NI WAPI UNATOA*

✔Wana wa Israel walikuwa wakitoa mbuzi na ndama wa dhabihu kwaajili ya dhambi zao kuonyesha kuwa mbuzi alibeba maisha yao mbele za Mungu wao kwaajili ya upatanisho👇

*👉Waebrania 9:13 Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili;*

*👉Waebrania 9:7 Lakini katika hema hiyo ya pili kuhani mkuu huingia peke yake, mara moja kila mwaka; wala si pasipo damu, atoayo kwa ajili ya nafsi yake na kwa dhambi za kutokujua za hao watu.*

Nachotaka kukufundisha ni kuwa shetani huitumia sadaka k**a njia moja Wapo ya kuwafunga watu

*👉Mapepo yanapopata sadaka ni rahisi sana kumuingia na kumfunga mtu*

✔Kuna watu mmefungwa nafsi zenu kwasababu nyakati zile za ujinga mliwahi kutoa sadaka kwa waganga wa kienyeji hamkujua kuwa mlikuwa mkitoa maisha yenu kuzimu

✔Au inawezekana maadui zako wametoa sadaka kukufunga wewe usiolewe, usifanikiwe kiuchumi, usipate mtoto, wanao wasifanye vizuri darasani, biashara yako isifanikiwe au usipate ajira

HABARI NJEMA NI KUWA IPO SADAKA YENYE UWEZO WA KUKULIPIA GHARAMA YA KUTOKA KIFUNGONI SADAKA HIYO NI DAMU YA YESU

*👉Wakolosai 1:13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;*

SADAKA HUSHINDWA NA SADAKA, ULIFUNGWA KWA SADAKA NA UTAFUNGILIWA KWA SADAKA PIA HIVYO TUMIA DAMU YA YESU KWA IMANI KUIKOMBOA NAFSI YAKO KUTOKA KIFUNGONI

PIA JIFUNZE KUITUMIA DAMU YA YESU MALA KWA MALA K**A SILAHA YAKO YA VITA DHIDI YA MAPEPO NA NGUVU ZA GIZA.

*👉Ufunuo 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.*

📚Jinsi ya kuitumia damu ya Yesu

*(i)Weka imani ya kuwa damu ya Yesu ipo na inaweza kukusaidia*

*(ii) Kisha omba kwa kutumia damu ya Yesu unaweza ukaimwaga au kuipaka sehemu unayotaka nguvu za Mungu zikusaidie*

K**a ni kwenye uchumi unaweza ukasema "naimwaga damu ya Yesu kwenye uchumi wangu"

K**a ni kwenye ndoa unaweza ukasema *Naimwaga damu ya Yesu kwenye ndoa yangu"

Huu ni mfano tu kwahiyo jifunze sana kuitumia damu ya Yesu k**a silaha yako ya vita utakuwa mshindi siku zote

*MWISHO*

NAKUOMBEA MUNGU WA MBINGUNI AKUPE HEKIMA YA KUUINGIZA UJUMBE HUU KWENYE MATENDO KISHA UKAMZALIE MUNGU MATUNDA KWA JINA LA YESU

Mungu awabariki sana

Maombi, ushauri, neno na WhatsApp 0657117595

Mwl.Joseph Leonard

12/02/2021

Ikimbie kuzim na jehanamu! Unaweza!! Wakatini sasa Tubu.

06/02/2021

Hallelujah!!!

Tukimtumaini Yesu hatatuacha hata tukipitia magumu kiasi gani,,,,Ee ,Yesu uso wako utembee nasi peke yetu hatuwezi.

22/10/2020

Hallelujah!

Mathayo 21:21-22
Tunapopeleka maombi yetu kwa Mungu yatupasakuamini ya kwamba Mungu yupo na anasikia vile tuombavyo.

Kwaiyo tunatakiwa kujua mioyoni kwmba Yale tuombavyo yanakwenda kutokea na inatupasa kuyaona katika roho kwamba yamekwishatokea na tuyapokee rohoni bila kuruhusu mashaka yoyote.
Marko 11:22-23

Kuna mifano inayoonyesha kwamba Mungu yupo na anaweza kufanya lolote.
Mfno: Musa alitumia fimbo kupasua bahari ya
Shamu

: Yeriko ilianguka kwa maombi

:Yesu mwenyewe alifanya miujiza mingi ya kuponya watu na hata kufufua.

💯Tumwamini Mungu halafu tuombe kwa Imani yeye ni mwaminifu atafanya.

Yesu naakubariki Sana, Amina.

17/07/2016

An organization which brings hope to poor children and to others

19/06/2016

matumain mapya

Address

Kwembe
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when New hope posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to New hope:

Share