21/02/2021
*NJIA TATU ANAZOZITUMIA SHETANI KUWAFUNGA WATU*
Sehemu ya 3.
Sehemu ya kwanza hadi ya pili tuliona mambo mawili anayoyatumia shetani kuwafunga watu
*1.Maneno*
*2.Makombora*
Leo tunamalizia sehemu ya mwisho
*3.SADAKA*
Watu wengi sana hawajui kazi ya sadaka kiroho
✔Sadaka katika ulimwengu wa roho ina umhimu mkubwa sana kwa upande wa Mungu na kwa upande wa shetani
📚KAZI KUBWA YA SADAKA KIROHO
*Ni Kumpatanisha mtu na Mungu au miungu*
Biblia inasema hivi👇
*◾2 Wakorintho 5:19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.*
Sehemu nyingine imeandikwa hivi👇
*◾Waefeso 2:16 Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.*
👆🏻Nachotaka kukuonyesha ni kuwa kwa njia ya damu ya Yesu tumepataniswa na Mungu aliye hai
Ni hivi Damu ya Yesu ni SADAKA ya Yesu aliyoitoa mbele za Mungu kwaajili ya wanadamu waliokuwa gizani.
*◾Waefeso 5:2 mkaenende katika upendo, k**a Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.*
Sehemu nyingine imeandikwa hivi👇
*◾Waebrania 9:14 basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?*
👆🏻Kwahiyo damu ya Yesu ni sadaka ya upatanisho kati ya wanadamu na Mungu maana dhambi ilitutenga na Mungu
NISIKILIZE VIZURI MPENDWA KAZI MOJAWAPO YA SADAKA NI KUMPATANISHA MTU NA MUNGU AU MIUNGU ITATEGEMEA UTAITOA WAPI
*-K**a sadaka unaitoa kwa Mungu aliye hai maana yake unaipatanisha nafsi yako na Mungu kwaajili ya jambo Fulani*
*-Na k**a unaitoa SADAKA yako kwa miungu maana yake unajipatanisha nafsi yako na mapepo*
Kuna watu mnaenda kwa waganga wa kienyeji au kuzimu kabisa mnatoa
*-Mbuzi au kuku wengine hutoa mpaka damu za watu😢 kwaajili ya kafara au matambiko ni hivi kwa kufanya hivyo unaipatanisha nafsi yako na mapepo*
*-Hata ukitoa Pesa bado unaipatanisha nafsi yako na mapepo unayotaka yakusaidie*
👉KWA MAANA NYINGINE NI KWAMBA UNAPOTOA SADAKA NI SAWA NA UNATOA NAFSI YAKO AU MAISHA YAKO KWA MAPEPO
Maana imeandikwa hivi👇
*👉Mathayo 6:21 kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako.*
🎤Yaani ulipoiweka hazina yako na moyo wako upo hapohapo
🎤Ukiweka hazina yako kwa Mungu na moyo wako utakuwa kwa Mungu
Na ukiweka hazina yako kwa mapepo na moyo wako utakuwa hapohapo kwa mapepo
*➡KWAHIYO UNAPOTOA SADAKA UNATOA MOYO WAKO NA UNATOA MAISHA YAKO PIA KUTEGEMEA NI WAPI UNATOA*
✔Wana wa Israel walikuwa wakitoa mbuzi na ndama wa dhabihu kwaajili ya dhambi zao kuonyesha kuwa mbuzi alibeba maisha yao mbele za Mungu wao kwaajili ya upatanisho👇
*👉Waebrania 9:13 Kwa maana, ikiwa damu ya mbuzi na mafahali na majivu ya ndama ya ng'ombe waliyonyunyiziwa wenye uchafu hutakasa hata kuusafisha mwili;*
*👉Waebrania 9:7 Lakini katika hema hiyo ya pili kuhani mkuu huingia peke yake, mara moja kila mwaka; wala si pasipo damu, atoayo kwa ajili ya nafsi yake na kwa dhambi za kutokujua za hao watu.*
Nachotaka kukufundisha ni kuwa shetani huitumia sadaka k**a njia moja Wapo ya kuwafunga watu
*👉Mapepo yanapopata sadaka ni rahisi sana kumuingia na kumfunga mtu*
✔Kuna watu mmefungwa nafsi zenu kwasababu nyakati zile za ujinga mliwahi kutoa sadaka kwa waganga wa kienyeji hamkujua kuwa mlikuwa mkitoa maisha yenu kuzimu
✔Au inawezekana maadui zako wametoa sadaka kukufunga wewe usiolewe, usifanikiwe kiuchumi, usipate mtoto, wanao wasifanye vizuri darasani, biashara yako isifanikiwe au usipate ajira
HABARI NJEMA NI KUWA IPO SADAKA YENYE UWEZO WA KUKULIPIA GHARAMA YA KUTOKA KIFUNGONI SADAKA HIYO NI DAMU YA YESU
*👉Wakolosai 1:13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;*
SADAKA HUSHINDWA NA SADAKA, ULIFUNGWA KWA SADAKA NA UTAFUNGILIWA KWA SADAKA PIA HIVYO TUMIA DAMU YA YESU KWA IMANI KUIKOMBOA NAFSI YAKO KUTOKA KIFUNGONI
PIA JIFUNZE KUITUMIA DAMU YA YESU MALA KWA MALA K**A SILAHA YAKO YA VITA DHIDI YA MAPEPO NA NGUVU ZA GIZA.
*👉Ufunuo 12:11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.*
📚Jinsi ya kuitumia damu ya Yesu
*(i)Weka imani ya kuwa damu ya Yesu ipo na inaweza kukusaidia*
*(ii) Kisha omba kwa kutumia damu ya Yesu unaweza ukaimwaga au kuipaka sehemu unayotaka nguvu za Mungu zikusaidie*
K**a ni kwenye uchumi unaweza ukasema "naimwaga damu ya Yesu kwenye uchumi wangu"
K**a ni kwenye ndoa unaweza ukasema *Naimwaga damu ya Yesu kwenye ndoa yangu"
Huu ni mfano tu kwahiyo jifunze sana kuitumia damu ya Yesu k**a silaha yako ya vita utakuwa mshindi siku zote
*MWISHO*
NAKUOMBEA MUNGU WA MBINGUNI AKUPE HEKIMA YA KUUINGIZA UJUMBE HUU KWENYE MATENDO KISHA UKAMZALIE MUNGU MATUNDA KWA JINA LA YESU
Mungu awabariki sana
Maombi, ushauri, neno na WhatsApp 0657117595
Mwl.Joseph Leonard