God's Kingdom on Earth Ministry

God's Kingdom on Earth Ministry we teach the word of God and discuss faith relating staffs.

20/01/2025

MWAKA 2025 NI MSIMU MPYA.
Mwanzo 8:11
[11]njiwa akamjia jioni, na tazama, alikuwa na jani bichi la mzeituni kinywani mwake, ambalo amelitunda, basi Nuhu akajua ya kwamba maji yamepunguka juu ya nchi.
Mwanzoni mwa mwaka huu niliwashirikisha ujumbe wa mwaka huu kutoka mwanzo 8:13 Ambapo tunaona Nuhu anatoka ndani ya safina baada ya mwaka mzima kupita.
Kuna mambo kadhaa nataka uyafahamu kwa uhakika kuhusu msimu mpya, na tutajifunza mambo hayo kwa kujibu maswali haya mawili;

1. Kwanini Nuhu, alimtoa njiwa kwenye dirisha ilhali yeye mwenyewe alikuwa nauwezo wa kuona nje ya safina kwa kutumia dirisha hilohilo?

Njiwa katika agano jipya ametumika k**a ishara ya Roho mtakatifu, pia katika mazingira ya Nuhu, ni wazi kuwa njiwa aliweza kuona umbali mrefu na eneo kubwa kuliko ambavyo Nuhu angeona.
Jambo la kujifunza hapa ni hili; Mwanzo wa msimu mpya unahitaji zaidi msaada wa Roho mtakatifu kuona zaidi ya pale uwezo wako unaishia. inawezekana Nuhu alikuwa anaona aridhi imekwisha kauka, lkn ili kujiridhisha akaamua kumtumia njiwa. Macho yetu ya kimwili na uwezo wetu wa kiakili unamipaka katika ulimwengu huu uliofungwa kwenye muda, lkn Tunaingia Rohoni na kuamua kushirikiana na Mungu na kumsikia yeye anachotuambia, tunafunguliwa kwenye mipaka ya kiulimwengu na hiyo inatusaidia kuepuka hasara.

Kwakuwa ni msimu mpya kwako, unapaswa kutazama kila fursa inayoonekana mbele yako kwa sura ya Mungu, weka matamanio yako pembeni na lenga zaidi kutafuta shauri la Bwana kwenye jambo husika. Unaweza kuelewa mtu kukaa ndani ya safina mwaka mzima! alikuwa na shauku kubwa sana ya kutoka nje, lkn alijidhibiti na kutafuta uhakika wa usalama wake akiwa huko nje anakotaka kwenda.
Unaweza kuwa ni msimu mpya kwako kwenye mahusiano, kwenye biashara, kwenye kazi yako, kwenye elimu yako, lkn ili ufanikiwe katika kiwango bora, unapaswa kushik**ana na mashauri ya Mungu.
2. Kwanini njiwa alikuja na jani la mzeituni?
Biblia inataja aina ya jani ambalo njiwa alirudi nalo sio kwa bahati mbaya, ukumbuke kuwa njiwa ni ishara ya Roho mtakatifu katika agano jipya.
Vile vile mti wa mzeituni, unamaana kubwa ya kinabii ndani ya biblia.
Kumbukumbu la Torati 28:40
[40]Utakuwa na mizeituni katika mipaka yako yote usijipake mafuta yake; kwa kuwa mzeituni wako utapukutika.
Hapa Biblia inatuambia k**a mzeituni ukipukutisha majani yake maana yake mafuta hayatakuwepo, na kitu kinachoweza kupelekea mizeituni ya nchi kupukutisha majani yake ni k**a Mungu hajairidhia nchi kwa sababu ya kutotii kwao. Hivyo, Njiwa alipokuja na jani la mzeituni ishara ya kwanza ilikuwa ni Mungu kuiridhia au kuikubali nchi. Hili ni jambo muhimu sana kujua mwanzo wa msimu mpya ni kitu gani unapaswa kufanya ambacho Mungu anakiridhia.
Vile vile Ubichi wa jani la mzeituni ni ishara kwamba kuna uwezesho wa kiMungu juu yako unapoanza msimu mpya, kumbuka hatuna mafuta ya mzeituni k**a zeituni itapukutisha majani yake, mafuta ya zeituni ni ishara ya uwezesho wa kiMungu (Upako).
Majani ya zeituni ni dawa, hii inatuashiria kuwa Mungu atakupa neno la uponyaji ili uponywe kutoka kwenye madhara yaliyoletwa na gharika kwa msimu uliopita.
Nuhu na familia yake walisaziwa maisha tuu, lkn walipoteza vitu vingi ndani ya kipindi cha mwaka mmoja. Haijalishi umepoteza nini, lkn tarajia neno la uponyaji kwa Bwana ndani ya msimu huu mpya.
Neno la Mungu analolituma kwako linakuja kukupa wazo la kufanya, kukupa uhakika wa mapenzi ya Mungu, kukupa upako utakao amsha Ari ya kulitekeleza ndani yako na zaidi sana litakuponya kutoka kwenye madhara uliyoyapata ya mwaka uliopita. Umebarikwa.

-2025
+255746283923

NDOA KATIKA SURA YA MUNGU.Mwanzo 2:21-23[21]BWANA Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubav...
01/10/2024

NDOA KATIKA SURA YA MUNGU.
Mwanzo 2:21-23
[21]BWANA Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
[22]na ule ubavu alioutwaa katika Adamu BWANA Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
[23]Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Maswali la kutafakari;
1: Adam aliwezaje kujua ikiwa Hawa ametolewa kwenye mwili wake wakati alilala usingizi mzito?
2: Je, Mungu alimfanya Adam kulala ili asishuhudie kile anacho kifanya?
A:Ikiwa ndivyo, inamaana lengo la Mungu halikufanikiwa kwakuwa alijua baada ya kuamka, sio?
B: Ikiwa sio, inamaana hicho kitendo cha Adam kulala usingizi hakikuwa na maana, kwakuwa Mungu anauwezo usio na mipaka angeweza kumuumba Hawa adamu akiwa macho bila kuathiri chochote, sio?
Hebu tuangalie andiko hili;
Mithali 18:22
[22]Apataye mke apata kitu chema;
Naye ajipatia kibali kwa BWANA.
Kabla ya Adam kuumbiwa Hawa alikuwa amezungukwa na wanyama, lkn biblia inasema alikuwa peke yake. K**a Mungu angemuumba mtu mwingine wa njinsia ya k**e kutoka kwenye mavumbi ya Aridhi na kumleta kwa Adam, bado Adam angekuwa peke yake.

Adam alipoamka kutoka katika usingizi wake na kumuona Hawa aliona nini? Alijiona yeye ndani ya mwanamke. Ndio maana aligundua kuwa mwanamke huyo ametokana na yeye.

Ili Adamu aweze kujiona yeye ndani ya Hawa, lazima ajijue yeye kwanza.
Hawa alipo mtazama Adam aliona nini? Aliona kipande kilicho pungua (Missing piece).
Kila mwanaume kabla ya kutafuta mwanamke wa kuoa, anatakiwa kujijua yeye kwanza, kwakuwa anaweza kuwa katikati ya wanawake wengi na akawa yuko peke yake k**a Adam. Fikiria Adam angemfanya Tembo kuwa msaidizi wake kwasababu ya umbo lake kubwa, asinge fanikiwa kwenye kusudi lake.
Mwanamke anaweza kuzungukwa na wanaume wengi, lkn asipokutana na mwanaume ambaye yeye(Mwanamke) ndio missing piece kwa huyu kijana, thamani yake katika hiyo ndoa itakuwa ndogo sana, that man can be fine without her.
Mungu anakusudia ndoa ifanye kazi k**a Single unit. Ndio maana Adam anasema tena kuwa mtu ataacha wazazi wake na kuungana na mwenzake nao watakuwa mwili mmoja. Hawa ni sehemu ya Adam iliyo boreshwa (modified).

Biblia inasema anaye pata mke kapata kitu chema, naye ajipatia kibali kwa BWANA.
Hiki sio kibali kwa ajili ya kila anaye oa au kuolewa, ni kibali kwa ajili ya anayeweza kuipata ile missing piece ndani yao ili waweze kuoperate kwenye ufanisi wao wa juu zaidi.

Ndoa k**a Single unit, inanguvu kubwa sana ya kuleta matatizo au suluhisho kwa ulimwengu huu. Adam na mke wake walituletea tatizo lililo gharimu maisha ya Yesu kristo ili kulitatua.

Mungu amewaumba wanawake kwa namna ya ajabu, wanapoingia kwenye maisha ya wanaume sahihi ni k**a kontena la materials yanayo hitajika kwa project.

Kuhusu usingizi wa Adam, Mungu anapo jifunua kwenye level fulani ya utukufu wake miili yetu huwa haiwezi kuhimiri, Yohana na Daniel pia walikutana na hiyo hali.
Pia Adam ni roho kabla ya mwili, mwili unaweza kulala lkn roho huwa hailali.
Mungu awabariki.
GKEMINISTRIES-2024.

24/05/2023

Vg

Address

Manzese
Dar Es Salaam

Telephone

+255719847423

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when God's Kingdom on Earth Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share