Amaninafuraha.blogspot.com

Amaninafuraha.blogspot.com KUWAFIKIA WENGI KWA NENO LA KWELI NA KUTAFUTA KWA BIDII KUMFAHAMU MUNGU MUUMBA MBINGU NA NCHI. SIKU ZOTE YESU NI MWOKOZI WA MAISHA YETU NI MPONYAJI.

20/04/2026

Check out Stelius Sane’s post.

09/03/2026

Watch, follow, and discover more trending content.

09/03/2026

Wakati wanawake wanaadhimisha kilele cha siku yao March 8 tuliona na kishuhudia wakijinasibu na kujigamba kuonesha namna wamepiga hatua za kimaendeleo,kiuchumi lakini bado kulikuwepo na mazungumzo juu ya matukio ya kikatili ambayo wamekuwa wakifanyiwa.
Hoja yangu ni hii ni kwa nini bado hayo matukio ya kikatili yanatokea wakati wanathibitisha kuwa wamepiga hatua kubwa kiasi kwamba msemo wa hamsini kwa hamsini upo vizuri sana kwao.Jaribu kuwaza nami halafu turudi Bustani ya Edeni hapo mwanzo ilikuwaje?.Ni ukweli usiopingika kuwa tunafanyiana matukio ya kikatili kwa sababu tumeacha kanuni na taratibu alizoziweka Mungu toka mwanzo.Hata wanawake wakitaka kusimama na kutawala kwa nguvu na kwa njia zote amini kuwa kuna siku watapwaya. Nimezaliwa na mwanamke,nimeoa mwanamke,Mungu amenipa watoto wa k**e na kiume hivyo nawaheshimu na kuwathamini sana wanawake ila wasiookubali kurudi kwenye principles(kanuni) na taratibu za Mungu wataendelea kupotea,matokeo yake utasikia yule mama (mwanamke) wakati akiwa kwenye nafasi sehemu fulani mwanzoni alikuwa akifanya vizuri ila alikuja kuharibu sana na hata yeye ukimuliza atajibu hivyo hivyo.Hii ni vita ambayo ilianzia toka bustani ya Edeni hivyo wanawake inawalazimu kuwa makini sana na kurudi kwenye kanuni na taratibu alizowapa Mungu hapo mwanzo.
Mwanzo 3:15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino. Alipofanikiwa kwenye Bustani ya Edeni Shetani kumhadaa mwanamke hajaishia hapo bado ameendelea kufuatilia uzao wake na kuleta mbinu mbalimbali za kuwaondoa kwenye kusudi na mpango wa Mungu kwao.

23/02/2026

Anza siku ya kwanza ya wiki na Bwana Yesu Kwa kutamkia baraka, mafanikio na kuinuliwa ili wiki unayoianza ikawe ya ustawisho na kujibiwa. Usikubali kuanza kwa maneno ya kukatisha tamaa,ya kinyonge hapana anza kwa ushindi na ushujaa,nakutia moyo ukaikabili wiki Kwa ujasiri na ushindi Kila linalotokea litumie kufikia kilele cha mafanikio yako.
1 Mambo ya Nyakati 29:12
Utajiri na heshima hutoka kwako wewe, nawe watawala juu ya vyote; na mkononi mwako mna uweza na nguvu; tena mkononi mwako mna kuwatukuza na kuwawezesha wote.

13/02/2026
13/02/2026

Kwa NYAKATI na MAJIRA ya MUNGU hakuna wa # @

23/12/2025

Kuoa ama kuolewa ni jambo zuri tena jema na kila mmoja anatamani kuona ama kuolewa k**a hana tatizo lolote.Na wazazi nao wanapenda na kufurahia mtoto wao akioa ama akiolewa na hilo jambo la kuona ama kuolewa huwa ni la heshima kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki.
Lakini Leo mi nakuletea ujumbe wa muhimu na tena wa kutafakarisha.Mara nyingi watu wanapokutana na kupendana na kuamua kuoana taarifa hufika kwa wazazi,na viongozi wa kiroho ambao wao nao wanahusika kufungisha ndoa na pia wakati mwingine serikalini.Sasa hoja yangu ni hii mara nyingi wanaambiwa wakapime afya ili mambo mengine yaendelee cha ajabu ni kwamba wanapia tu HIV. Sasa hoja ni ni vyema Hawa watu wakikutana wanapoenda kupimwa HIV wapimwe pia akili na wanaohusika wanatakiwa kutambua kuwa kwa kadri wanavyoenda kushangilia wakati wa kufunga ndoa ndivyo pia inalazimu wazazi,ndugu na jamaa kushughulikia changamoto zao pale wanapochokana na kutaka kupeana talaka. Vikao vianze k**a ilivyokuwa vikao vya harusi,vikao vya kuanza hatua za kwenda kudai talaka vianze na siku ikitolewa hiyo talaka bado tufanye k**a tulivyofanya siku ya harusi.Japo sio furisho kwa Imani ya Kikristo kuachana,Yesu alisema haikuwa hivyo toka mwanzo.
Marko 10:4-8
Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha. Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
Ndiyo maana hoja yangu wanapotaka kuoana wapimwa kila kitu mpaka akili.
Ni namna nilikuwa nawaza juu ya namna watu wanapokutana na kupendana na kuoana kwa shangwe na nderemo lakini baada ya muda hao wapendanao wanaanza kuchokana.

06/12/2025

Hakika Mungu wetu ni mkuu sana amini ninachokuambia yaani ipo hivi unayesoma posti hii Mungu huyu mkuu hawezi kukusahau wewe mtumikie tu na usiwaangalie wanadamu maana watakuchosha na kukumiza ila huyu Mungu kamwe hawezi kukusahau.
Isaya 49:15
Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.

Tafuta kwa bidii uwezo wa uvumilivu ambao utakuwezesha wewe,kuendelea na roho ya kujifunza mpaka ujifunze jinsi ya kujif...
18/11/2025

Tafuta kwa bidii uwezo wa uvumilivu ambao utakuwezesha wewe,kuendelea na roho ya kujifunza mpaka ujifunze jinsi ya kujifunza kutoka kwa wengine na ndipo utafika mbali.
Usiwe mtu wa kulalamika,kunung'unika hapana kaa chii jifunze ndiyo ni kweli kuna wakati unakuwa na uchungu,maumivu hasira ila kaa chini jifunze na hapo Mungu atakupeleka mbali.na utaitwa ni mtu ambaye amestawi.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Amaninafuraha.blogspot.com posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share