13/12/2019
MWANGAZA WA SIKU
Friday 13th of December 2019
*JIANDAYE KWA MAVUNO*
MATHAYO 9:35-38
36.*Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika k**a kondoo wasio na mchungaji.*
37.*Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. *
Matthew 9:37-38 NIV
[37] Then he said to his disciples, “The harvest is plentiful but the workers are few. [38] Ask the Lord of the harvest, therefore, to send out workers into his harvest field.”
Nyuma ya kila mafanikio hutanguliwa na maandalizi na mipango mahususi kuhusiana na mafanikio hayo.
Katika tafakari yetu leo Yesu anatukumbusha na kutupa changaMoto kwa habari ya kumvunia Bwana mavuno ambayo yapo tayari lakini wavunaji au watendaji ni wachache.
Ili tuweze kufanikiwa kumvunia Bwana,tunajitaji kumuomba Mungu atupe moyo wa Yesu aliokuwa nao kwa mavuno(watu walioko dhambini na waliotayari kupokea injili na kugeuka).
🔹*Tunahitaji Kuona K**a Yesu alivyoona.*
-Wakati wanafunzi wake wanaliona kusanyiko tu la watu,lakini Yesu aliona HITAJI KUBWA ndani ya mioyo ya hao watu
•Walichoka nakutawanyika k**a kondoo wasio na Mchungaji)
•Aliona utayari wao wakutubu na kuziacha njia zao mbaya lakini hakuona au walikuwepo watumishi wa chache waliokuwa tayari Kuwasaidia na kuwaongoza katika nia yao hiyo.
-Mungu anatutaka sisi tuliokwisha kuokoka tuwe sababu ya wengine kumjua Kristo.
🔹*Tunahitaji kuguswa au kujisikia ndani mioyo yetu kuhusu wenye dhambi K**a Yesu alivyojisikia*
-Alipowaona makutano ALIWAHURUMIA
•Hatuwezi kuifanya kazi ya kumvunia Bwana Mavuno bila kusukumwa na UPENDO wa Mungu ndani yetu ambapo ndani yake kunakuwahurumia maana si wao Bali wamefungwa na shetani na kutumikishwa bila ridhaa yao.
🔹*Tunapaswa kuchukua hatua K**a Yesu alivyochukua hatua*
-Aliamua kuwahudumia kiroho na kimwili(uponyaji wa magonjwa yote na mafundisho pia)
Katika Utumishi huu wakumvunia Bwana mavuno yaliyotayari huwa hatujipeleki au kujituma wenyewe K**a sehemu pengine ya moja ya ajira k**a ajira zingine HAPANA,bali ni lazima Mungu ahusike kututuma ndio maana tunatakiwa KUMUOMBA MUNGU ili awapeleke wavunaji ili katika Utumishi huu wasiwepo watumishi WAMISHAHARA bali wenye kujitoa kwa moyo hata bila posho lakini Wawe tayari kulitimiza kusudi la Bwana katika Mwito wao.Maranatha