PAG Lango la Mbinguni Kahama

PAG Lango la Mbinguni Kahama LEAD PASTOR 👉 Pastoryuda Zacharia

Pentecostal Assemblies of God (PAG)
Lango la Mbinguni kahama (The GATE OF HEAVEN)

Mwanzo 28:
(Genesis)

17___hapa ni nyumba ya Mungu, napo ndipo lango la mbinguni. -----------
____and this is the gate of heaven!

MARIAMU MAGDALENE – IBADA ILIYOMGHARIMU KILA KITUKatika Injili ya Yohana 12:3–6, Mariamu Magdalene (mara nyingi huhusish...
27/04/2026

MARIAMU MAGDALENE – IBADA ILIYOMGHARIMU KILA KITU

Katika Injili ya Yohana 12:3–6, Mariamu Magdalene (mara nyingi huhusishwa na tendo hili la kujitoa) alimimina manukato ya thamani kubwa juu ya miguu ya Yesu na kuyafuta kwa nywele zake. Harufu yake ikaijaza nyumba yote.

👉 Ilikuwa ya gharama kubwa, yenye thamani ya mshahara wa mwaka mzima.
👉 Ilikuwa ya wazi, kila mtu aliona.
👉 Ilikuwa ya unyenyekevu, alipiga magoti miguuni Pake.

Lakini si kila mtu aliyefurahia hilo.

Yuda Iskariote alisema,

👉 Yohana 12:5
Kwa nini mafuta haya hayakuuzwa kwa dinari mia tatu, na kupewa maskini?

Maandiko yanaongeza kuwa hakusema hivyo kwa sababu aliwajali maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi na ndiye aliyekuwa akishika mfuko wa fedha.

👉 Yuda aliona upotevu.
👉 Yesu aliona ibada.

Wakati Yuda akihesabu gharama, Mariamu alionyesha upendo wake.

Yesu akajibu,

👉 Yohana 12:7
Mwache… ameweka haya kwa ajili ya siku ya kuzikwa kwangu.

Mariamu alielewa kile ambacho wengine hawakuelewa—Yesu anastahili kilicho bora zaidi.

Ibada ya kweli daima itaeleweka vibaya na baadhi ya watu. Lakini upendo unapokuwa wa kweli, hauzuiliki.

Vunja chupa yako ya alabasta. Acha kujitoa kwako kuseme zaidi kuliko lawama.

Kile unachomimina kwa ajili ya Yesu hakipotei kamwe.

👉 Marko 8:38 (KJV)
Kwa maana mtu atakayenionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.

Kwa gharama yoyote, mfuate Yesu jinsi ulivyo. Usione aibu kamwe kukiri upendo Wake. Amekutendea jambo kubwa. Usijali watu watasema au kufikiria nini kuhusu kujitoa kwako Kwake. Yesu anakuelewa kuliko mtu yeyote.

Je, utampa kila kitu?

Utukufu wote uwe kwa Mungu 🙏

KWANINI UNATAKIWA KUWAHI IBADANI?    Kuwahi kufika kanisani (ibadani) si tu suala la muda — ni suala la heshima, nidhamu...
14/02/2026

KWANINI UNATAKIWA KUWAHI IBADANI?



Kuwahi kufika kanisani (ibadani) si tu suala la muda — ni suala la heshima, nidhamu, na maandalizi ya moyo mbele za Mungu.

Hizi ni sababu muhimu kwa nini unapaswa kuwahi:

1. NI HESHIMA KWA MUNGU
Ibada ni kukutana na Mungu. siyo kukutana na waumini wenzako

Ukichelewa mara kwa mara, inaonyesha humweshimu Mungu,
Narudia Tena Ukichelewa mara kwa mara, inaonyesha humweshimu Mungu,

Injili ya Yohana 4:24 inasema:
“Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”

Kujiandaa mapema ni sehemu ya kumwabudu kwa heshima.

2. UNAJIANDAA KIROHO VIZURI
Ukifika mapema:
🛐Unapata muda wa maombi ya utulivu
💖Unatulia moyoni
💖Unamruhusu Roho Mtakatifu akuandae

😩Ukifika umechelewa mara nyingi unaingia ukiwa na haraka na mawazo mengi.

3. UNAPATA IBADA KAMILI YAANI IBADA YOTE BILA KUKOSA SEHEMU YOYOTE YA IBADA either NENO la msingi, Sunday school n.k

MKE wa Anania ambaye ni SAFIRA alikufa Kwasababu alichelewa kufika ibadani na hakujua k**a ule uongo wao umejulikna , angekuwepo wakati Mme wake anakufa Kwa huo Uongo huenda angetubu .... MATENDO 5:1....

Wakati mwingi kwenye makanisa ya kiroho mwanzo wa ibada ndio wenye:
🔥Maombi ya msingi
🔥Neno la utangulizi
🔥 Uwepo mzito wa Mungu
Watu wengi hupokea baraka zao mapema kabisa kwenye nyakati hizo.

4. NI NIDHAMU YA KIROHO
Nidhamu ya kuanza kwa wakati inaonyesha ukomavu wa kiroho.
Mhubiri 3:1 inasema:
“Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”
Mungu ni Mungu wa utaratibu.

5. UNAKUWA MFANO KWA WENGINE
K**a wewe ni kiongozi, mchungaji, au mtumishi watu wanakuangalia.
Kuwahi kunafundisha bila hata kusema.
Kwa ufupi:
Kuwahi kanisani ni:
Heshima kwa Mungu
Maandalizi ya moyo
Nidhamu
Njia ya kupokea zaidi

WAHI IBADANI, KARIBU PAG Lango la Mbinguni Kahama

Zaburi 22:(Psalms) 22. Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu. --------------- I will ...
07/09/2025

Zaburi 22:
(Psalms)

22. Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu.
---------------
I will declare Your name to My brethren; In the midst of the assembly I will praise You.

Pastoryuda Zacharia

   Pastoryuda Zacharia
25/07/2025


Pastoryuda Zacharia

Time to worship
08/07/2025

Time to worship

Pastoryuda Zacharia
03/07/2025

Pastoryuda Zacharia

03/07/2025
JESUS IS THE WAY COME TO HIM
03/07/2025

JESUS IS THE WAY COME TO HIM

Address

P. O. Box998 Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Telephone

+255672702144

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when PAG Lango la Mbinguni Kahama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to PAG Lango la Mbinguni Kahama:

Share

Category