rifqtz

rifqtz Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from rifqtz, Religious Center, Dar es Salaam.

KITABU SALAMA CHA DUAKitabu cha Hisnul Muslim kilichoandikwa na Sheikh Sa’id bin Ali bin Wahf Al-Qahtani ni miongoni mwa...
28/05/2026

KITABU SALAMA CHA DUA

Kitabu cha Hisnul Muslim kilichoandikwa na Sheikh Sa’id bin Ali bin Wahf Al-Qahtani ni miongoni mwa vitabu muhimu sana kwa kila Muislamu. Kina dua na nyiradi sahihi kutoka ndani ya Qur’an na Sunnah kwa usalama wa dini na maisha yetu ya kila siku. 🤲✨

Ndani yake utapata dua nyingi sahihi na zenye manufaa makubwa, mbali kabisa na mambo ya kishirikina k**a uchawi, kuroga, matambiko na kafara. Hayo si mafundisho ya Uislamu bali ni njia za upotevu na hasara kubwa mbele ya Allah سبحانه وتعالى.

Muislamu wa kweli anatakiwa ashik**ane na dua sahihi na amtegemee Allah pekee, si waganga wala hirizi.

📚 K**a unahitaji kitabu hicho, andika kwenye comment:
👉 “KITABU”

KIONGOZI MCHAMUNGUKila mwenye akili anatambua kuwa uongozi na mamlaka ni neema na mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu Subh...
28/05/2026

KIONGOZI MCHAMUNGU

Kila mwenye akili anatambua kuwa uongozi na mamlaka ni neema na mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Ta’ala. Hakuna anayepata nguvu, heshima na uwezo isipokuwa kwa idhini yake Allah. Na mwisho wa kila mwenye mamlaka ni kurejea kwake Mola wake kwa hesabu.

Ndiyo maana viongozi wa haki huongozwa na hofu ya Allah, unyenyekevu na kujitahidi katika ibada. Allah Subhanahu wa Ta’ala ametufundisha ndani ya Qur’an kuwa Yeye humpa mamlaka amtakaye na humvua amtakaye. Hivyo, uongozi wa kweli haujengwi kwa kiburi wala dhulma, bali kwa uadilifu, ibada na kumuogopa Mwenyezi Mungu.

Historia ya Uislamu imejaa mifano ya viongozi waliomtegemea Allah katika kila jambo. Mtume ﷺ, na Maswahaba wake na wema waliotangulia ni mfano nzuri wa viongozi wamchao Allah. Kwasasa Viongozi k**a Ibrahim Traoré wamekuwa mfano wa kuigwa kwa kusimama kidete katika kutetea watu wao huku wakionyesha unyenyekevu na kumtegemea Mwenyezi Mungu.

Kiongozi anayemkumbuka Allah katika mamlaka yake huwa karibu na haki, huruma na uadilifu. Na taifa lenye viongozi wanaomuogopa Allah huwa na matumaini ya amani, maendeleo na baraka.

“Mwenyezi Mungu humpa ufalme amtakaye na humvua amtakaye.” — Qur’an 3:26

28/05/2026

Eid Mubarak

28/05/2026
SIKU YA IDDI SI SIKU YA KUMUASI ALLAH…Iddi ni siku ya furaha, shukrani na kumtaja Allah kwa wingi. Ni siku ya kusherehek...
27/05/2026

SIKU YA IDDI SI SIKU YA KUMUASI ALLAH…

Iddi ni siku ya furaha, shukrani na kumtaja Allah kwa wingi. Ni siku ya kusherehekea baada ya ibada kubwa na masiku ya utiifu. Lakini si siku ya kuingia kwenye maasi na uchafu.

Si jambo jema kwa Muislamu kutoka nyumbani kwake kwenda sehemu za maovu; k**a vile vilabu, ulevi, kuchanganyika kiharamu kati ya wanaume na wanawake, au kufanya mambo aliyoyaharamisha Allah.

Inashangaza kuona kwamba jana tu tulikuwa kwenye ibada, dua, saumu na kutarajia msamaha wa madhambi ya miaka miwili… leo inakuaje rahisi kuingia kwenye maasi?

Je, una uhakika wa kuifikia kesho?
Je, unajua k**a ibada zako zimekubaliwa au zimekataliwa?

Hivyo basi, tusigeuze siku tukufu ya Iddi kuwa sababu ya kumuasi Allah. Hakika Iddi ni katika siku kubwa zinazopaswa kuheshimiwa, kutukuzwa na kutumiwa katika mema.

Sherehekea kwa amani, furaha na ndani ya mipaka ya Uislamu.

26/05/2026

Ubora wa siku ya ´Arafah

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when rifqtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share