rifqtz

rifqtz Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from rifqtz, Religious Center, Dar es Salaam.

SIFA ZA HIJABU YA KISHERIA (صفات الحجاب الشرعي)Assalamu Alaykum warahmatullah wabarakatuh.Hijabu si mavazi tu ya kitamad...
31/05/2026

SIFA ZA HIJABU YA KISHERIA (صفات الحجاب الشرعي)

Assalamu Alaykum warahmatullah wabarakatuh.

Hijabu si mavazi tu ya kitamaduni, bali ni ibada na utii kwa Allah (Subhanahu wa Ta'ala). Ili hijabu ikidhi vigezo vya kisheria na kukubaliwa, ni lazima iwe na sifa zifuatazo kwa mujibu wa Qur'ani na Sunnah:

1. Kufunika Mwili Mzima (استيعاب جميع البدن)

Hijabu ya kisheria ni lazima isitiri mwili wote wa mwanamke isipokuwa kile kilichovuliwa (k**a mikono na uso kwa baadhi ya wanachuoni).

Dalili:

Allah Amesema:

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ قُل لِّأَزْوَاجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَاءِ الْمُؤْمِنِينَ يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِن جَلَابِيبِهِنَّ ۚ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يُعْرَفْنَ فَلَا يُؤْذَيْنَ ۗ وَكَانَ اللَّهُ غَفُورًا رَّحِيمًا

"Ewe Nabii! Waambie wakezo, na binti zako, na wake za Waumini wajiteremshie nguo zao (jilbāb). Hivyo ni karibu zaidi kuweza kutambulikana (kuwa ni watu heshima) wasiudhiwe. Na Allah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu."

(Al-Ahzab: 59)

──────────────────

2. Isiwemo Pambo Ndani Yake (أن لا يكون زينة في نفسه)

Nguo yenyewe ya hijabu isilete mvuto au kurembwa kwa namna inayovutia macho ya wanaume wa kando (ajnabiy).

Dalili:

Allah Amesema:

وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ

"...Wala wasidhihirishe mapambo yao..."

(An-Nur: 31)

──────────────────

3. Iwe Nzito Isiyoonyesha Ndani (أن يكون صفيقا لا يشف)

Nguo haitofanya sitara ikiwa ni nyepesi kiasi cha kuonyesha rangi ya ngozi au mwili wa mwanamke.

Dalili:

Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema:

سيكون في آخر أمتي نساء كاسيات عاريات... لا يدخلن الجنة ولا يجدن ريحها

"Watakuwepo mwisho wa umma wangu wanawake waliovaa nguo lakini wako uchi... Hawataingia Peponi wala hawatasikia harufu yake."

(Hadithi ya Muslim)

──────────────────

4. Iwe Pana Isiyobana (أن يكون فضفاضا غير ضيق)

Lengo la hijabu ni kuzuia fitna, hivyo nguo inayobana na kuchora maumbo ya mwili haikidhi sifa ya hijabu.

Dalili:

Mtume (صلى الله عليه وسلم) alimwambia Usamah bin Zaid kuhusu nguo nene aliyompa mke wake:

مُرْهَا فَلْتَجْعَلْ تَحْتَهَا غِلَالَةً، فَإِنِّي أَخَافُ أَنْ تَصِفَ حَجْمَ عِظَامِهَا

"Mwambie aweke nguo ya ndani chini yake (hiyo nguo nene), kwani mimi nachelea isichore ukubwa wa mifupa yake (umbo lake)."

(Hadithi ya Ahmad na Al-Bayhaqi)

──────────────────

5. Isitiwe Marashi wala Manukato (أن لا يكون مبخرا مطيبا)

Mwanamke haruhusiwi kutoka nje akiwa amejipaka manukato kwenye mwili au nguo zake kwa namna inayovutia watu.

Dalili:

Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema:

أَيَّمَا امْرَأَةٍ اسْتَعْطَرَتْ فَمَرَّتْ عَلَى قَوْمٍ لِيَجِدُوا مِنْ رِيحِهَا فَهِيَ زَانِيَةٌ

"Mwanamke yeyote atakayejipaka manukato kisha akapita mbele ya watu ili wasikie harufu yake, basi huyo ni mzinifu."

(Hadithi ya Abu Musa Al-Ash'ari)

──────────────────

6. Isifanane na Mavazi ya Wanaume (أن لا يشبه لباس الرجل)

Ni haramu kwa mwanamke kuvaa mavazi yaliyohusishwa mahususi kwa wanaume.

Dalili:

لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الرَّجُلَ يَلْبَسُ لِبْسَةَ الْمَرْأَةِ، وَالْمَرْأَةَ تَلْبَسُ لِبْسَةَ الرَّجُلِ

"Mtume (صلى الله عليه وسلم) amemlaani mwanamume anayevaa vazi la mwanamke, na mwanamke anayevaa vazi la mwanamume."

(Hadithi ya Abu Hurairah)

──────────────────

7. Isifanane na Mavazi ya Wanawake wa Kikafiri (أن لا يشبه لباس الكافرات)

Mavazi ya mwanamke wa Kiislamu yanatakiwa kuwa na utambulisho wake wa kiimani na yasifanane na nembo au mitindo maalumu ya makafiri.

──────────────────

8. Isiwe Nguo ya Umaarufu/Kujionesha (أن لا يكون لباس شهرة)

Kujiepusha na nguo inayovaliwa kwa lengo la kujivunia, kujionyesha, au kuwa tofauti na watu ili tu kupata umaarufu au sifa.

Dalili:

Mtume (صلى الله عليه وسلم) amesema:

مَنْ لَبِسَ ثَوْبَ شُهْرَةٍ فِي الدُّنْيَا أَلْبَسَهُ اللَّهُ ثَوْبَ مَذَلَّةٍ يَوْمَ الْقِيَامَةِ

"Mwenye kuvaa nguo ya umaarufu (kujifakhiri) hapa duniani, Allah Atamvisha nguo ya udhalili Siku ya Kiyama."

(Hadithi ya Ibn Umar)











31/05/2026
UCHOCHEZI WA VYOMBO VYA HABARI: HATARI KWA JAMIIVyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuelimisha, kuhabarisha na ku...
30/05/2026

UCHOCHEZI WA VYOMBO VYA HABARI: HATARI KWA JAMII

Vyombo vya habari vina nafasi kubwa katika kuelimisha, kuhabarisha na kujenga uelewa ndani ya jamii. Hata hivyo, pale habari zinapotolewa kwa upendeleo, upotoshaji au kwa lengo la kuchochea hisia za watu, matokeo yake yanaweza kuwa mabaya kwa jamii, taifa na hata ulimwengu kwa ujumla.

Mwandishi wa habari mwenye weledi anatakiwa kuhakikisha anawasilisha taarifa kwa usahihi, uadilifu na uwiano, bila kueneza propaganda, kuibua chuki au kuchochea migogoro. Habari sahihi hujenga umoja, lakini habari za uchochezi huweza kuvunja mshik**ano wa kijamii, kuharibu biashara, kuleta sintofahamu na hata kusababisha migawanyiko na mapigano.

Katika mafundisho ya Kiislamu, uchochezi na upotoshaji wa habari ni mambo yanayokatazwa. Uislamu unatufundisha kuthibitisha habari kabla ya kuzisambaza na kuzungumza kwa haki na ukweli. Hivyo, vyombo vya habari vya Kiislamu vinapaswa kuwa mfano bora wa uadilifu, busara na uwajibikaji katika kuelimisha jamii na kutafuta suluhu pale kunapotokea migogoro au sintofahamu.

Jamii yenye habari za kweli ni jamii yenye amani. Tuwe waangalifu na tunachosoma, tunachosikiliza na tunachosambaza.

Je, wewe unaonaje nafasi ya vyombo vya habari katika kujenga au kuharibu jamii? Tuandikie maoni yako.

KITABU SALAMA CHA DUAKitabu cha Hisnul Muslim kilichoandikwa na Sheikh Sa’id bin Ali bin Wahf Al-Qahtani ni miongoni mwa...
28/05/2026

KITABU SALAMA CHA DUA

Kitabu cha Hisnul Muslim kilichoandikwa na Sheikh Sa’id bin Ali bin Wahf Al-Qahtani ni miongoni mwa vitabu muhimu sana kwa kila Muislamu. Kina dua na nyiradi sahihi kutoka ndani ya Qur’an na Sunnah kwa usalama wa dini na maisha yetu ya kila siku. 🤲✨

Ndani yake utapata dua nyingi sahihi na zenye manufaa makubwa, mbali kabisa na mambo ya kishirikina k**a uchawi, kuroga, matambiko na kafara. Hayo si mafundisho ya Uislamu bali ni njia za upotevu na hasara kubwa mbele ya Allah سبحانه وتعالى.

Muislamu wa kweli anatakiwa ashik**ane na dua sahihi na amtegemee Allah pekee, si waganga wala hirizi.

📚 K**a unahitaji kitabu hicho, andika kwenye comment:
👉 “KITABU”

KIONGOZI MCHAMUNGUKila mwenye akili anatambua kuwa uongozi na mamlaka ni neema na mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu Subh...
28/05/2026

KIONGOZI MCHAMUNGU

Kila mwenye akili anatambua kuwa uongozi na mamlaka ni neema na mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Ta’ala. Hakuna anayepata nguvu, heshima na uwezo isipokuwa kwa idhini yake Allah. Na mwisho wa kila mwenye mamlaka ni kurejea kwake Mola wake kwa hesabu.

Ndiyo maana viongozi wa haki huongozwa na hofu ya Allah, unyenyekevu na kujitahidi katika ibada. Allah Subhanahu wa Ta’ala ametufundisha ndani ya Qur’an kuwa Yeye humpa mamlaka amtakaye na humvua amtakaye. Hivyo, uongozi wa kweli haujengwi kwa kiburi wala dhulma, bali kwa uadilifu, ibada na kumuogopa Mwenyezi Mungu.

Historia ya Uislamu imejaa mifano ya viongozi waliomtegemea Allah katika kila jambo. Mtume ﷺ, na Maswahaba wake na wema waliotangulia ni mfano nzuri wa viongozi wamchao Allah. Kwasasa Viongozi k**a Ibrahim Traoré wamekuwa mfano wa kuigwa kwa kusimama kidete katika kutetea watu wao huku wakionyesha unyenyekevu na kumtegemea Mwenyezi Mungu.

Kiongozi anayemkumbuka Allah katika mamlaka yake huwa karibu na haki, huruma na uadilifu. Na taifa lenye viongozi wanaomuogopa Allah huwa na matumaini ya amani, maendeleo na baraka.

“Mwenyezi Mungu humpa ufalme amtakaye na humvua amtakaye.” — Qur’an 3:26

28/05/2026

Eid Mubarak

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when rifqtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share