25/03/2026
UBATIZO WA MAJI TELE
Siku hizi, wimbi la Wayahudi Kumkubali YESHUAH kuwa BWANA na Mwokozi wa Maisha yao limekuwa kubwa Sana, K**a Uonavyo katika Picha Wayahudi Wakibatizwa katika Mto ya Yordani;
Miaka ya nyuma, ilikuwa vigum kuona wimbi kubwa Namna hii ya Wayahudi Kumgeukia Mungu wao, na Kukubali kwamba YESHUAH ni Mwokozi wa Maisha yao, Hakika Utukufu kwa Mungu juu, Yeye Aliyemtoa YESHUAH kuja Kutafuta na Kuokoa kile kilichopotea!
Bila kujali Utaifa wa mtu wa Kabila yake, Yeye Kazi yake Kuu ni Kuokoa kile kilichopotea.
NI NYAKATI ZA MWISHO
Nasema ni Nyakati za mwisho kwa Sababu! Si kila Myahudi atakayeweza Kuokoa wakati wa thiki Kuu;
Japo Biblia inasema, Wakati Neema ya Mataifa itakapokoma, Na YESHUAH Kuchukua Kanisa, Neema ya Wokovu itawageukia Wayahudi.
Je! Neema itakapowageukia Wayahudi, Unadhani Wayahudi wote watakuwa tayari Kumkubali YESHUAH kuwa BWANA na Mwokozi wa Maisha yao?
Bila shaka, haitakuwa rahisi k**a ambavyo si rahisi wakati huu ambao Neema ya Wokovu bado ipo juu yetu Sisi Mataifa, Maana Dunia na mambo yaliyomo katika dunia, Ni matamu kwa watu wa dunia pia;
Kwa vile, Kumkubali YESHUAH Ni "Kuikana" Nafsi yako, katika Dunia hii yenye Maasi ya kila Namna hii!
Na Kumkataa YESHUAH ni "Kuikubali Nafsi" yako katika dunia, kwa maana ya kuwa tayari Kuipa Nafsi yako Mambo Maasi ya Dunia.
ISEMAVYO BIBLIA
(Luka 9:23-26) Nukuu:
[23] Akawaambia wote, "mtu ye yote akitaka Kukifuata, na 'Ajikane' mwenyewe, 'Ajitweke' Msalaba wake kila siku, Anifuate.
[24] Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake 'ataiangamiza', na mtu 'atakayeiangamiza' nafsi yake kwa ajili yangu 'atakayeisalimisha'.
[25] Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, k**a 'akijiangamiza', au kuipoteza mwenyewe?
▪︎ Kwa sababu kila atakayenionea haya Mimi na Maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika Utukufu wake na wa Baba na wa Malaika watakatifu.
▪︎ Nami nawaambia kweli: Wapo katika hawa wanaosimama hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata wauone kwanza ufalme wa Mungu".
Hakika, Vigezo na Masharti kuzingatiwa; Sababu kwa Nini Vigezo na Masharti vizingatiwe, ni Kwa Sababu Mungu alipotuumba aliweka ndani yetu hali ya Kuchagua!
1) Mabaya, au
2) Mema.
Wewe Unachagua nini kati ya moja na mbali?
Nataka ujue, Katika haya mawili, ni Jukumu langu Mimi, Kuchagua Mema ili nipate Mema;
Lakini pia, ni Jukumu lako wewe, Kuchagua Mema ili upate Mema.
▪︎ K**a utaamua Kuchagua Mema, hayo Mema yatakuwa yako,
▪︎ Na k**a utaamua Kuchagua Mabaya, huo Ubaya utakuwa wako.
Habari Njema ni kwamba, YESHUAH HAMASHIACH Bado Anaokoa, Ukiwa tayari, Sali Sala hii pamoja nami.
Ee YESHUAH HAMASHIACH, Mimi ni mwenye dhambi, na kwa muda mrefu nimeishi Maisha ya dhambi;
Mwokozi wa Ulimwengu, YESHUAH HAMASHIACH BWANA wangu, Naomba Unisamehe Dhambi zangu zote!
Kisha, Andika Jina langu Katika Kitabu cha Uzima wa Milele.
Sasa, Nakiri kwamba wewe ni BWANA na Mwokozi wa Maisha yangu, Ahsante kwa Kunisamehe, Ahsante kwa Kumipokea, Ahsante kwa Kunipa Haki ya Kuitwa Mtoto wa Mungu.
Ni Katika Jina Lile Lipitalo Majina yote, YESHUAH HAMASHIACH BWANA wangu, Nimeomba na Kuamini, Amen tena Amen.