The Catholic Diocese of Bukoba

The Catholic Diocese of Bukoba Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from The Catholic Diocese of Bukoba, Catholic Church, bukoba, Bukoba.

MHASHAMU ASKOFU MTEULE - JOVITUS FRANCIS MWIJAGEHongereni wana Jimbo Katoliki Bukoba na Kanisa zima, BIKIRA MARIA MAMA W...
19/10/2023

MHASHAMU ASKOFU MTEULE - JOVITUS FRANCIS MWIJAGE

Hongereni wana Jimbo Katoliki Bukoba na Kanisa zima, BIKIRA MARIA MAMA WA HURUMA, UTUOMBEE.

Mahafali & Uzinduzi wa Shule ya Bweni ya Sekondari (Ishozi Sacred Heart Secondary School)A: MAHAFALI- Mahafali ya Tano (...
23/09/2023

Mahafali & Uzinduzi wa Shule ya Bweni ya Sekondari (Ishozi Sacred Heart Secondary School)

A: MAHAFALI

- Mahafali ya Tano (5)
- Wahitimu 16
- Maaskofu
+Method Kilaini A/Admn
+D. Rwoma Emeritus
Mapadre:
Fr Revocatus Mwemezi PP
Fr Gratian Rweyendera
Fr Jovitus Mwijage
Fr Hilarius Kamanzi
Wengine::
Fr Delphinus Rwehumbiza (Mhazini)
Fr Delphinus Ngaiza (Masomoni)
Fr Revocatus Mwemezi
Fr Richard Tiganya

- Masista & Mabruda

B: Uzinduzi wa Shule ya Bweni ya Sekondari (Ishozi Sacred Heart Secondary School)

-Imezinduliwa rasmi leo Tarehe 23 Sept, 2023 na Mhashamu Askofu Method Kilaini
- Tayari shule inao wanafunzi wa kidato cha kwanza idadi yao ni 25
- Wapo pia vijana wa Pre-Form One wanaojiandaa kuingia form One mwakani

23/09/2023

MAHAFALI - RUTABO SEMINARI

Waseminarista wa Seminari ndogo ya Mt. Yohane Bosco Rutabo (Rutabo Seminari) leo wametimu masomo yao ya msingi wakiwa wahitimu 49.

Aliyeongoza lbada ya Misa Takatifu ni Fr Samwel Muchunguzi - Makamu Msaidizi wa Kitume, Jimbo Katoliki la Bukoba. Mgeni rasmi alikuwa ni Omulangila Lambert.

Wahitimu wote 49 wameruhusiwa kuendelea na malezi ya Upadre huko Rubya Seminari. Kutoka Rubya Seminari alikuwepo Fr Reginald Kashakuro kuwapokea wahitimu.

SAKRAMENTI YA KIPAIMARA, UZINDUZI WA KANISA LA KIGANGO & SAKRAMENTI YA NDOA - PAROKIA YA KASHOZI, JIMBO KATOLIKI BUKOBAM...
16/09/2023

SAKRAMENTI YA KIPAIMARA, UZINDUZI WA KANISA LA KIGANGO & SAKRAMENTI YA NDOA - PAROKIA YA KASHOZI, JIMBO KATOLIKI BUKOBA

Mhashamu Askofu Method Kilaini ametoa Sakramenti ya Kipaimara kwa wakristu wapatao 350, kuzindua Kanisa la Kigango Kilima (Parokia ya Kashozi) na Kubariki Ndoa (Jozi 3).

Baba Paroko, Padre Samuel Muchunguzi pamoja na wasaidizi wake (Padre Africanus Bigirwamungu & Padre Vedastus Rugaijamu) wanawashukuru wote waliowezesha sherehe hii pamoja na ujenzi wa Kanisa la Kilima, Parokia ya Kashozi, Jimbo Katoliki Bukoba.

WAZEE NI HAZINA!!! Ugeni, ugeni!Mafrateri 52 wa Jimbo Katoliki la Bukoba, pamoja Mkurugenzi wa miito wa Jimbo Katoliki l...
14/09/2023

WAZEE NI HAZINA!!!

Ugeni, ugeni!

Mafrateri 52 wa Jimbo Katoliki la Bukoba, pamoja Mkurugenzi wa miito wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Padre Edson Mtembei, watembelea mapadre wazee katika kituo chao cha watakatifu Oscar na Wilbard, kilichopo katika Parokia ya Kagondo.

Matembezi hayo yaliambatana na Adhimisho la Misa Takatifu la Kutukuka kwa Msalaba lililoongozwa na Paroko wa Parokia ya Kagondo, Padre Medericus Kyaruzi, akisaidiana na Askofu Mstaafu wa Jimbo la Bukoba, Mhashamu Askofu Desiderius Rwoma, Padre Edson Mtembei pamoja mapadre wazee.

Mafrateri walishirikishana mengi na mapadre hao wazee wakichota hekima, ujuzi, uelewa, maadili, historia, na ustaarabu wa Maisha ufaao kwa padre katika ujana wake na katika muda wote wa kumtumikia Mungu. Mapadre wazee wamewasisitiza vijana hao kuwa karibu zaidi na Yesu Kristo pamoja na kumpenda Bikira Maria ili waweze kustawi vema katika utume na kuwa kweli mbegu, chumvi na mwanga kwa ulimwengu.

Aidha, wazee wameeleza furaha yao ya kuona kuwa kazi aliyoiacha Kristo ambayo nao waliishiriki bado zina watu wenye nia ya kuziendeleza, yote kwa ajili ya kukuza na kueneza ufalme wa Mungu duniani. Baada ya Adhimisho la Misa na mawaidha ya wazee, burudani zilifuata pamoja na kidedea kikali kutoka kwa mafrateri kwa nia ya kuwachangamsha wazee na kuwashirikisha furaha za vijana.

Mapadre wazee waliopo katika kituo hicho kwa sasa ni:
1. Msgr. Deogratias Rweyongeza
2. Pd. Gotfried Kamala
3. Pd. Thomas Tibainuguka
4. Pd. Potentine
5. Pd. Odilon Kajwahura
6. Pd. Audax Rutakyamirwa
7. Pd. Leopold Mushuga
8. Pd. Edward Furahisha

IBADA YA MISA TAKATIFU"Kila tuulapo MKATE huu na kukinywea KIKOMBE hiki, twangaza ufufuko wa BWANA mpaka atakapo kuja te...
08/09/2023

IBADA YA MISA TAKATIFU

"Kila tuulapo MKATE huu na kukinywea KIKOMBE hiki, twangaza ufufuko wa BWANA mpaka atakapo kuja tena" (1 Kor 11:26)

27/08/2023

KUSIMIKA & KUBARIKI TABERNAKULO - KANISA KUU JIMBO KATOLIKI BUKOBA

TABERNAKULO - KUBARIKI & KUSIMIKALeo Tarehe 27 Agosti, 2023 Mhashamu Askofu Method Kilaini amebariki na kusimika Taberba...
27/08/2023

TABERNAKULO - KUBARIKI & KUSIMIKA

Leo Tarehe 27 Agosti, 2023 Mhashamu Askofu Method Kilaini amebariki na kusimika Taberbakulo yenye hadhi ya Kiroma katika Kanisa Kuu la Jimbo Bukoba.

Tunamshukuru Mhashamu Askofu Novatus Rugambwa na wote walioshiriki katika kupatikana kwa Tabernakulo hii, Mungu awabariki.

JUBILEI YA MIAKA 70 YA KUZALIWA YA MA. GRETURDA EMMANUEL MUKARUGILIRWALeo Mhashamu Askofu Method Kilaini ameshiriki kati...
25/08/2023

JUBILEI YA MIAKA 70 YA KUZALIWA YA MA. GRETURDA EMMANUEL MUKARUGILIRWA

Leo Mhashamu Askofu Method Kilaini ameshiriki katika Jubilei ya Ma. Greturda Emmanuel Mukarugilirwa anayetimiza miaka 70 ya kuzaliwa, Kijiji Kitwe, Parokia Itahwa, Jimbo Katoliki Bukoba.

Mhashamu Askofu Method Kilaini amembariki na kupongeza juhudi zake alizowekeza katika malezi ya watoto wake sita akiwa bila baba yao. " Hata nikiwa mzee, mzee mwenye mvi, Ee Mungu usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, na kila atakayekuja uwezo wako" (Zab 71:18).

Address

Bukoba
Bukoba
99

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Catholic Diocese of Bukoba posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share