02/04/2026
SOMO; UFAHAMU WA ROHONI JUU BARAKA ILIYOPATIKANA MSALABANI KUPITIA DAMU YA YESU KRISTO NA FAIDA ZAKE
""PASAKA hii ni zamu yako ya kutoka utumwani na kwenye vifungo mbali mbali vya siri jifunze pamoja nasi""
A... Nini maana ya pasaka kibibilia!!?
PASAKA ni Jina la aina ya Sadaka na siyo sikukuu ya kula na kunywa K**a wengi wanavyofikiri!
1Korintho; 5:7
KUTOKA 12:1-13
B.... PASAKA ni siku au Mlango wa kutoka kwenye utumwa wa magonjwa-- vifungo--mateso/ magerwza ya kiroho/laana za kichawi nk. maana aliyekushikilia atahukumiwa na Bwana
KUTOKA 12:1-14
C... PASAKA ni Mlango wa ufufuo wa vilivyokufa maishani mwako; ndoa--uchumi-- afya-- kazi za mikono-- familia--ufugaji kilimo nk.
🔍 Maana ya Ufahamu wa Rohoni
Ufahamu wa Rohoni ni uwezo wa roho ya mwanadamu kupewa nuru na kuelewa mambo ya Mungu, ulimwengu wa roho, na ukweli wa ndani ambao hauonekani kwa macho ya kawaida.
Kwa lugha rahisi:
👉 Ni uelewa unaotoka kwa Roho Mtakatifu, sio akili ya kawaida (logic ya kibinadamu)
1--- Ufahamu juu ya damu ya Yesu Kristo iliyotoka kichwani kwa kutobolewa na taji ya miiba na faida zake (baraka za msalaba kutokea kichwani)
MATHAYO 27:/51-53
A... Damu hiyo ya kichwani;ilibeba nguvu au upako wa kuondoa laana na adhabu ya Mungu juu ya ardhi iliyolaaniwa kwa sababu ya dhambi ya kutokukutii sauti ya Mungu pale edeni
MWANZO 3:17
MATHAYO 27:29-31
B... Damu ya Yesu Kristo iliyotoka kichwani pia ilibeba nguvu au upako wa kuondoa adhabu ya kiuchumi/kifedha kwa sababu ya dhambi ya kutokutii Neno la Mungu na kulitekeleza
MWANZO 2:15-17
C... DAMU ya Yesu Kristo iliyomwagika kutoka kichwani ilibeba nguvu au upako wa urejesho wa nguvu ya ufahamu wa kimungu-- nguvu ya kiakili-- maamuzi ya kimungu na mawazo ya kimungu
KOLOSAI 3:1-3
Maana Kuna mambo adui huyafanya kwenye akili ili kubana akili-- ufahamu--maamuzi --mawazo na fikra za mtu wa ndani
2Kor; 4:3-4
2Kor; 11:3
Mwanz; 3:1-15
Kumbuka watu wenye ufahamu--maarifa akili za ubunifu ndiyo watu wanaolipwa mishara mikubwa duniani hivyo ni muhimu Pasaka hii ufufuke kiakili--kiufahamu-- kimaamuzi --kifkra na kimawazo; hizo ndizo faida ya damu ya pasaka iliyobeba baraka za msalaba na faida zake
""MAOMBI YA KIPENGELE HIKI"'
Ninakushukuru Mungu uliye Hai kwa kumtoa mwanao wa pekee; Yesu Kristo aliye Hai--- kwa ajili ya Kuitoa dhabihu na sadaka ya pasaka Kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu; na kila laana na Kila adhabu ya kutokulitii Neno lako juu ya ardhi mama iliyonizaa; ardhi mama ninayoishi na kuifanyia kazi/biashara nk. Ee Bwana nirehemu na kunisamehe mtumishi wako (taja majina yako K**a utambulisho wako wa kiroho) .......... maana damuni mwako nimepokea msamaha wa dhambi na Ukombozi tangu Leo; naialika na kuilekeza damu ya msalaba iliyotoka kichwani mwa Yesu iniondolee adhabu na laana ya kula kwa jasho -- laana ya michongoma na miiba toka Kwa Mungu; laana; Laana ya zuio la kiuchumi na kifedha laana iliyokaa kihalali ya juu ya uso wa ardhi mama iliyonizaa umeniondolea leo kwa sadaka ya pasaka sawa sawa na Neno lako la 1KOR 5:7
MWANZO 3:17 MWANZO 2:15-17 Na damu hii iliyomwagika kutoka kichwani pako inirejeshee nguvu ya ufahamu-- nguvu ya kiakili-- nguvu ya kimaamuzi -- nguvu ya kifikra na kimawazo ; inirejeshee tena utukufu wako ulioniondolea Kwa sababu ya dhambi ya asili ya babu yetu Adam wa kwanza; Yesu pia kwa Kuniondolea zuio la kiuchumi-- kupitia Damu ya msalaba toka kichwani mwa Yesu Kristo tangu Leo sitakula Kwa ajili jasho wala michongoma na miiba haitakuwa sehemu ya kazi ya mikono yangu
"" WAEFESO 1:7
Sali Sala hiyo Kwa Imani Kisha kesho nitakuletea faida ya pili kutokea msalabani kutokana na damu na maji yaliyotoka ubavuni mwa Yesu;
Imeletwa kutoka madhabahu ya JEHOCIFONA MINISTRIES chini ya mpakwa mafuta wa Bwana; Apostle & Prophet Jackson Nelson Nyantamba pia unaweza kuwasiliana Moja Kwa Moja kwa 0764-3043-42 kwa msawali na majibu zaidi