TAG NIA NJEMA Bagamoyo

TAG NIA NJEMA Bagamoyo This is the Pentecostal church. We WORSHIP God in truth and spirit.

NI WEEK MPYA TUMEIANZA.Kumbuka uzima na mauti uko katika uwezo wa ulimi wako …Kiri maneno haya kwa imani nayatakuwa yako...
11/05/2026

NI WEEK MPYA TUMEIANZA.

Kumbuka uzima na mauti uko katika uwezo wa ulimi wako …

Kiri maneno haya kwa imani nayatakuwa yako .

Kumbuka analitazama neno na kulitimiza .

· Itakuwa week yangu ya kupendelewa kila nitakapokanyaga kwa jina la Yesu.
(Kutoka 12:36)BWANA akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara.

· Malango yangu ya baraka yatakuwa wazi mchana na usiku katika week nzima kwa jina la Yesu .
Isaya 60:11
Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

· Week hii itakuwa ni week ya kukutana na watu walioandaliwa kwa ajili ya maisha yangu kwa jina la Yesu.
Isaya 43:4
Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na makabila ya watu kwa ajili ya maisha yako.

· Naitabiria week yangu itakuwa week ya kupendelewa na kukubalika kila nitakapoingia kwa jina la Yesu .
Mwanzo 39:21
Lakini BWANA akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza.

· Kila silaha
zitakazoinuka juu yangu hazitafanikiwa kwa jina la Yesu .
Isaya 54:17
Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa.

Itakuwa week yenye baraka kwa jina la Yesu .
Kumbukumbu 28:3
Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

Amen Amen !!

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

ANZA WIKI MPYA KWA NENO LA BARAKAZaburi 20:1-4[1]BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.[2]Akupel...
27/04/2026

ANZA WIKI MPYA KWA NENO LA BARAKA

Zaburi 20:1-4
[1]BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.
[2]Akupelekee msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni.
[3]Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako.
[4]Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kuyatimiza mashauri yako yote.

Shalom Kanisa la Bwana!
Ni siku mpyaa na wiki mpya ambayo kwa neema na huruma za Mungu tumepata kibali cha kuhesabiwa haki ya kuwa wazima, wenye afya na nguvu tele.

Kwa ushindi huu nami Natamka neno la baraka na mguso wa kipekee kwako na uzao wako kwa jina la Yesu.

Wiki hii ikawe wiki njema kwako, wiki ya kicheko kwako, ikawe ni wiki ya mpenyo wa kifedha usio wa kawaida kwa jina la Yesu.

Hakutakuwa na taarifa mbaya iwayo yoyote kwako na uzao wako na ndugu zako,
zitasikika taarifa njema saana za matendo makuu ya Mungu.

Natamka amani uzima na afya iwe juu yako na kwa watoto wako na uzao wako na ndugu zako kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth.

BWANA akaukumbuke utumishi wako na akakutane na haja za moyo wako sawasawa na neno lake hapo juu!!

BWANA YESU akayatimize mashauri yako yote sawasawa na neno lake,
WIKI HII IKAKUPOKEE KATIKA JINA LA YESU KRISTO.

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

Ukiona viashiria hivi kwenye maisha yako, tafadhali punguza/acha kila unachofanya kisha ongeza muda wa kukaa kwenye maom...
26/04/2026

Ukiona viashiria hivi kwenye maisha yako, tafadhali punguza/acha kila unachofanya kisha ongeza muda wa kukaa kwenye maombi,
Maana kuna jambo Mungu anataka kufanya na wewe, kaa Magotini kupata maelekezo.

A. Ukiona unapata sana msukumo wa kuomba Toba sana

B. Ukiona unasukumwa sana kuomba ndani yako na hujui uombe kitu gani.

C. Ukiona kuna ndoto unaiota sana na inajirudia sana.

D. Ukiona kuna jambo umeliona mahali, linakuumiza kiasi unatamani Mungu AFANYE kitu fulani ama ATOKEE mtu fulani afanye k**a unvyotamani wewe,
K**a upo kwenye hili maana yake wewe ndiye ambaye Mungu amemkusudia kufanya hilo jambo.
TAFADHALI RUDI MAGOTINI KWA MAELEKEZO ZAIDI.

E. Ukiona TUMAINI limefifia yaani mbele yako unaona giza.
RUDI MAGOTINI KUPATA NURU

F. Ukiona ni k**a hakuna mtu anayekupa majawabu sahihi ya unachokitafuta.
RUDI MAGOTINI UKAOMBE KWANZA.

G. Ukiona kuna mzigo umekujaa moyoni na unakuumiza juu ya mtu fulani, mahali fulani au nchi.
Yaani unasikia kuhangaika ndani yako, Tafadhali Rudi Magotini kwa muda mrefu.

Matakwa ya Mungu kwa mwanadamu, huwa yanadhihirishwa kwa Mungu kuachilia hali fulani ya kuugua(mzigo) ama ya tofauti na kawaida ya mwanadamu, k**a sehemu ya kumtaka huyo mtu afanye yanayopaswa,
Na siku zote hali hizi huwa zinatakwa la kumtaka mhusika aingie katika kuomba ili aeleweshwe asichokielewa, ama apewe maelekezo sawia.

Yeremia 20:9
"Nami nikisema, Sitamtaja, wala sitasema tena kwa jina lake; basi, ndipo moyoni mwangu kumekuwamo k**a moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia."

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

JITAHIDI SANA WATU HAWA WASIKOSEKANE KWENYE  MAISHA YAKO.Mtu anayeomba pamoja na wewe.K**A  DANIELI NA  WENZAKEMtu ambay...
23/04/2026

JITAHIDI SANA WATU HAWA
WASIKOSEKANE KWENYE MAISHA YAKO.

Mtu anayeomba pamoja na wewe.
K**A DANIELI NA WENZAKE

Mtu ambaye Unajifunza Vitu vingi kwake.
K**a Elisha kwa Eliya pia k**a Yoshua kwa Musa.

Mtu ambaye ni Msaada kwenye Maono uliyonayo.
K**A ANANIA NA PAULO

Mtu ambaye anaweza kukushauri na kukurekebisha kwa upendo na kwa hekima na ukamsikiliza.
K**a musa na mzee Yethro

Mtu anayeweza kutangulia mbele kusafisha njia ili wewe upite.
K**a Yohana mbatizaji na Yesu
KUNA MTU UNAMHITAJI YOHANA ILI MAMBO
YAKO YAENDE.

Mtu wa kukutia moyo kwenye hali mbaya unazokutana nazo kwenye maisha.
K**a Elisabeth kwa Mariamu

Mtu anayeweza KUUBEBA mzigo wako ama msalaba wako na kushiriki mateso yako.
K**a paulo na watu wa kanisa la korintho.

Mtu anayeweza kukupokea kipindi ambacho umekataliwa kabisa kabisa, yaani hawataki kukuona au kuiona hata sura yako.
K**a anania na paulo.

Mtu anayeweza kuziona fursa na akakuletea.
K**a wale wakoma walivyoleta habari njema kwa ndugu zao.
K**a petro baada ya kupata samaki akawaita na wavuvi wenzake.

Kimsingi maisha ya kila mwanadamu huwa yanahitaji watu kadhaa na muhimu kwaajili ya kuyafanya maisha yalete maana ama matokeo hitajika.
Na jambo hili anayelifanyaga huwa ni Mungu mwenyewe, Katika kuomba kwako jifunze sana kumwomba Mungu akupe watu hitajika katika Maisha yako, lakini pia akupe hekima ya kuishi na hawa watu ili usije ukashindwa kuishi nao mwisho wa siku ukabaki jangwani milele.

Isaya 43:4
"Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo NITATOA WATU KWA AJILI YAKO; NA KABILA ZA WATU KWA AJILI YA MAISHA YAKO."

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

MWANANGU, YULE MAMA HAKUMALIZA VIZURI SAFARI YAKE!Hivi ndivyo Mchungaji wangu, alivyoanza kunieleza kwa habari ya kifo c...
22/04/2026

MWANANGU,
YULE MAMA HAKUMALIZA VIZURI SAFARI YAKE!

Hivi ndivyo Mchungaji wangu, alivyoanza kunieleza kwa habari ya kifo cha mama mmoja tuliyekuwa tukisali naye.
Nilimfahamu mama huyu mara tu nilipookoka,
Kwa ufupi alikuwa ni mama mwenye kumpenda sana Mungu, aliyejali ibada na zaidi Mwana maombi mzuri.
Alikuwa ni mama ambaye ni mfano wa kuigwa kwa mambo mengi...
kwa jinsi ya kibinadamu naweza kusema alikuwa Mshirika mwaminifu.

Nimeabudu na mama huyu kwa takribani miaka 3, nilitengana na mama huyu kwa kwenda Mkoa mwingine.
Mwaka fulani niliporudi likizo, nilienda kanisani kwaajili ya ibada ya jioni,
nilipofika kanisani niliambiwa kuwa ibada ya jioni ile itafanyika kwa mama huyu kwani amefariki.

Moyoni mwangu nilihuzunika kupata taarifa ile, ila nilipata tumaini na kuamini kwamba maadam alikuwa ameokoka na endapo aliendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu wake basi atakuwa yupo na Bwana akifurahi. Ndipo nikaenda kuungana na washirika wenzangu, kwenda kuwafariji familia ile kwa kuondokewa na ndugu yao.

Kesho yake nilienda kwa Mchungaji wangu kumsalimu na pia kumpa pole kwa kupatwa na msiba huo... Baada ya kumpa pole kwa kuondokewa na mama huyo, ndipo alipoanza kwa kusema
‘Mwanangu, kwa kweli yule mama hakumaliza vizuri safari yake. Mungu ndiye ajuaye yuko wapi, ila nami k**a Mchungaji wake, nasikitika kusema hakumaliza vizuri’.

Kauli hii ilinishtua sana, nami nikamuuliza kwa nini unasema hivyo Pastor?,
Ndipo aliponiambia yote ambayo mama yule aliyafanya miezi kadhaa kabla ya kifo chake.

Baada ya Mchungaji wangu kunielezea maisha yote ya yule mama katika siku zake za mwisho, ndani yangu niliumia sana.
Naam niliumia kwa sababu kubwa mbili;

Moja ni namna nilivyokuwa namfahamu na kumpenda yule mama kutokana na juhudi na imani yake katika Bwana.
Mbili ni ufahamu nilionao kuhusu wapi mtu anakwenda k**a hakufa katika Bwana.
Maana imeandikwa "…Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao."
(Ufunuo 14:13)

K**a mtu hakufa katika Bwana (utakatifu) mahali anapokwenda panaitwa kuzimu.
Kuzimu ni mahali ambapo laiti mwanadamu angejua nini kinaendelea huko, si tu angemwamini Yesu, bali asingeleta mchezo kwenye wokovu na angeishi maisha ya utakatifu kuzidi maelezo,
Jambo moja ambalo nina hakika nalo ni hili, endapo mtu atakufa katika dhambi zake, bila kutengeneza njia au mahusiano yake na Mungu akali hai, basi huyo atakuwa amemaliza safari yake vibaya, na kuzimu ndipo mahali ambapo ataenda.

Mpenzi msomaji, najua watu wengi hawapendi kuambiwa ukweli huu, lakini ni vema uujue kabla hujafa, ili ujifunze kuishi maisha ya kumpendeza Mungu wako.
Biblia inasema
"Na k**a vile watu walivyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu"
(Waebrania 9:27).

Je wewe utamalizaje safari yako hapa duniani?, Je unajua kwamba kifo chako ndio mwanzo wa maisha mapya ya umilele?,
Naam, maisha hayo ni ama ya mateso milele (kuzimu kisha Jehanamu) au raha milele (mbinguni kisha Jerusalemu mpya).

Wapi mtu atataka kwenda baada ya kufa anapaswa kufanya maamuzi akiwa hai.
Naam si tu kuokoka bali kuishi maisha matakatifu, maana wapo wengi ambao waliokoka lakini baada ya kufa kwao wakajikuta kuzimu, na hii ni kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Mungu wao katika kutii amri zake.
K**a unafikiri kuwa Mkristo ni tiketi ya kukupeleka mbinguni siku ukifa, badilisha fikra zako mapema, maana, mbinguni hawaendi Wakristo, bali watakatifu, naam wale wayafanayao mapenzi ya Mungu hapa duniani,
Rejea Mathayo 7:21

Kwa maelezo ya Mchungaji wangu yule mama katika siku zake za mwisho alifika mahala pa kwenda kwa waganga wa kienyeji ili kupata msaada.
Nami moyoni mwangu nilijiuliza maswali mengi kwamba,
kwa nini alienda kwa waganga wa kienyeji kutafuta msaada?,
Je, ni kweli Mungu wake aliyemwamini siku zote alishindwa kumsaidia? Kwa nini aliruhusu Shetani amdanganye kiasi hiki, k**a Hawa alivyodanganywa? (Mwanzo 3:1-19).
Ndipo nikajua kuna mahali yule mama alimpa Ibilisi nafasi (Waefeso 4:27) na Shetani akatumia nafasi hiyo ili kuhakikisha mama yule anamaliza vibaya.

Nilipozidi kutafakari juu ya jambo hili, ndipo mawazo yangu yalipoingia moyoni mwangu na kunikumbusha kile ambacho Mtume Paulo aliwaambia Wagalatia akisema
"Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulubiwa? Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Je mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?.
Wagalatia 3:1-3.

Ukisoma vizuri sentensi za Paulo ambazo nyingi zipo katika mfumo wa maswali ni ishara kuwa,
Paulo mwenyewe alikuwa haamini kile ambacho alikiona kinatokea kwa Wagalatia,
Kwani alijua walivyoanza vizuri na Bwana, lakini hali yao ya mwisho ilikuwa ni mbaya tena ya mwilini. Kwa sababu hii Paulo akaugua sana rohoni, ndipo ikamlazimu kutumia lugha ngumu (kali) sana ili kuwasaidia.
Naam, kwa andiko hili tunajua kwamba mtu anaweza akaanza safari yake vizuri na kisha ak**aliza vibaya, ndiyo maana Mhubiri 7:8a naye anasema
"Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake…"

Ni huzuni kubwa sana kwa mtu aliyemjua Mungu halafu akarudi nyuma na kumaliza katika mwili. Mpendwa wangu jifunze kuchunga na kutunza mguu wako katika Bwana ukiwa makini wapi unakanyaga.
Ni vema tumruhusu Roho Mtakatifu atuongoze na kutufundisha njia itupasayo kuiendea, huku tukiwa watiifu na waaminifu kwake (Zaburi 32:8). Neno la Bwana na liongoze hatua zetu ndani yake kwa kuwa imeandikwa
"Neno la Bwana ni taa ya miguu yangu"
(Zaburi 119:105).

Asomaye na afahamu

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

SAA YA KUZAA IKIFIKA HAIZUILIKILUKA 2:6 Ikawa, katika kukaa huko, *siku zake za kuzaa zikatimia,* 7 akamzaa mwanawe, kif...
21/04/2026

SAA YA KUZAA IKIFIKA HAIZUILIKI

LUKA 2:6 Ikawa, katika kukaa huko, *siku zake za kuzaa zikatimia,*
7 akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika *hori ya kulia ng?ombe* , kwa sababu hawakupata nafasi katika *nyumba ya wageni*

Majira ya kuzaa yakifika huwa hayazuiliki...Ratiba ya Yusufu na Mariam haikuwa kuzaa nje ya mji wao inawezek**a walitamani iwe nyumbani kwao ila muda wa kuzaa ulipofika haikujalisha wapo wapi alitakiwa kuzaa.

Walitafuta mahali pazuri pa kujifungua hawakupata..wakajikuta wamepata mahali pasipofaa lakin kwa sababu saa ya kuzaa imefika hakukuwa na namna.

Nataka kusema na wewe kuwa muda wa kuzaa hauzuiliki....haijalishi wanajitahidi kwa namna gani kuhakikisha ...
Husomi
Huolewi/huoi
Huzai
Hupati kazi
Hufanyi biashara
Huduma yako haikui
Hupandishwi cheo
Nk....saa ikifika hata kwenye z**i la ng'ombe utazaa tuu..

Laiti k**a wale wenyeji wa mji wangejua Mariam anaenda kuzaa mfalme wa wafalme nadhani kila mtu angeng'ang'ania azalie nyumbani kwake wasingekubali azaliwe kwenye hori la ng'ombe

Kuna watu kwa sababu hawaoni thamani ya ulichokibeba hakuna anayekufuatilia ..hawana muda na wewe hawana nafasi ya kukupa.

Lakini nataka kukuambia kuwa saa ikifika wala hakuna wa kukuzuia, huko huko kwenye hori la ng'ombe watakuletea manemane na uvumba pia na dhahabu....kule kule horini Yesu walimletea na dhahabu kila mtu alitamani kwenda kumwona..hata Herode alitaka kwenda kumsujudia japo kinafiki...

Acha wakudharau ..saa ya kuzaaa ikifika watakutafuta...maana unachoenda kuzaaa ni cha thamani!!.

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

MAHALI ULIPO PANAVYOWEZA KUKUFANYA MTUMWA AMA SHUJAA WA MAISHA YAKO.Lengo la somo ni ili kukutafakarisha kwa kina juu ya...
09/04/2026

MAHALI ULIPO PANAVYOWEZA KUKUFANYA MTUMWA AMA SHUJAA WA MAISHA YAKO.

Lengo la somo ni ili kukutafakarisha kwa kina juu ya mahali ulipo ili kuona pana mchango kiasi gani katika kukufanikisha ama kukufelisha kwenye maisha yako,
Na uchukue Hatua.

Mahali ulipo ni maeneo mbalimbali ambayo kwa namna moja ama nyingine uwepo wako unahusika.
Yako maeneo mbalimbali ambayo uwepo wako unaweza ukahusika kwa namna mbalimbali.
mfano: familia,taasisi mbalimbali za kielimu, Dini(madhehebu mbalimbali) ama mazingira fulani.

Maeneo haya yote na hata ambayo sijayataja ile unahusika nayo, upo uwezekano mkubwa wa maeneo haya kukufanikisha ama kukufelisha.

"Yuko mfalme mmoja aliyekwenda kutembea mbugani yeye na mke wake pamoja na mtoto wao mdogo.
Wangali katika matembezi yao walivamiwa na watu wanaoishi katika mbuga hiyo,
katika kujiokoa mfalme na mke wake wakakimbia lakini mtoto wao ambae bado alikuwa mdogo akatekwa na watu wa hiyo jamii ya mbugani na kuondoka naye.
Yule mtoto wa mfalme akalelewa na watu wa porini, akakua katika yale mazingira ya porini na akaishi na yeye k**a mtu wa porini.
Na kwakuwa hakukuwa na mtu aliyemueleza kilichotokea juu ya maisha yake,
aliamini kabisa kuwa yeye pia ni sehemu ya ile jamii ya porini,
aliishi maisha ya taabu na kutegemea uwindaji k**a watoto wengine wa ile jamii.
Pamoja na haya yote kumbuka, huyu ni mtoto wa mfalme, na mtoto wa mfalme ni mfalme, na vyote vilivyopo kwenye nchi ya kifalme ni vya mfalme, Nini kinasababisha aishi maisha magumu,maisha ambayo sio asili yake?.
jawabu ni MAHALI ALIPO.

Mkumbuke Petro ambaye maandiko yanatuambia kuwa kivuli chake kiliponya wagonjwa, ila ukweli ni kuwa kabla hajawa chombo cha Bwana alikuwa mvuvi na si mvuvi tu bali alikuwa na maisha tofauti kabisa na vile Mungu alivyomkusudia, na laiti isingekuwa ni ujio wa Kristo kumrejesha kwenye asili yake, angebaki kuwa mvuvi milele.
Ni nini kilisababisha jibu ni Mahali alipo.

Mkumbuke mtume paulo ambaye ameandika karibu robo tatu ya vitabu vyote katika agano jipya, ukweli wa maisha ni kwamba isingekuwa ni kutokewa na Bwana, mahali alipo pangeificha hazina njema aliyokuwa amewekezewa na Mungu kwaajili ya watu wa mataifa pia kanisa,
Ni mahali alipokuwa ndio sababu.

Kumbuka swali la Nathanaeli aliposikia habari za Yesu, kilichomsumbua sio miujiza aliyokuwa anafanya Yesu ila ni mahali alipotoka, ndio maana akauliza je kuna kitu chema cha weza toka Nazareti?.
Watu wa Archeologist wanasema, Nazareti kilikuwa ni kijiji kidogo sana wakati ule, kilikuwa na nyumba kumi na moja tu,kwahiyo unaweza ona palikuwa kijijini kiasi gani,pia watu masikini ndio waliokuwa wanaishi huko.
Na hakunaga kitu chema kilichowahi toka Nazareti ndio maana Nathanael aliposikia habari za Yesu kuwa katoka nazareti ilibidi aulize imewezekanaje maana alishangaa inawezekana vipi hili litokee Nazareth.

Kumbe hata mtaa au kijiji au taifa unaloishi linaweza likachangia kwa namna moja ama nyingine kukuficha ukweli wa maisha yako na kukufanya uishi maisha ambayo haujapangiwa na Mungu.

Mkumbuke Gideon ambaye Mungu alimkusudia awe shujaa katika kizazi chake,lakini aliishi maisha ya kawaida sana,tena ya mateso, naye akiogopa na kujificha katika mapango k**a wengine, ijapokuwa YEYE NDIYE aliyekuwa jibu la changamoto iliyoikabili jamii yake ila hakujijua.
Nini kilisababisha asijijue?
Jibu ni Mahali alipokuwa.

Nini kinasababisha mahali ulipo pawe na uwezo wa kukufanya uwe mtumwa au shujaa wa maisha yako!

01. MAHALI ULIPO PANAWEZA KUKUFICHA UHALISIA WA MAISHA YAKO KWA KUKUZUIA USIJIJUE WEWE NI NANI.

Uhalisia wa maisha yako juu ya wewe ni nani ni ukweli wa maisha yako sawa na vile alivyokukusudia Mungu uwe.
Ni vile anavyokuona Mungu.

Yeremia 1:5
"Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa."

K**a hutaujua ukweli wa alivyokukusudia Mungu kiasi cha kuwaza kukuumba, huwezi kuuepuka huu mtego usababishwao na mahali ulipo.

Ni kwa Mungu pekee ndiko kuliko na kioo cha kujitazamia kuhusu uhalisia wa wewe ni nani.
Hii maana yake pasipo kujihusisha na Mungu wewe k**a mwanadamu utaishi ukijua kiwango unachokiishi ndicho kiwango cha uhalisia wa upaswavyo,
HUTAUJUA UKWELI.

Rejea kwa Mungu aliye asili yako ili urudi kwenye uhalisia wa upaswavyo sawa na
Mwanzo 1:26

02. MAHALI ULIPO HUAMUA AINA YA MAWAZO UTAKAYOKUWA NAYO JUU YA HATIMA YAKO.

Hivi unadhani ni aina gani ya mawazo anayoweza kuwa nayo mfungwa aliyeko gerezani tangu kuzaliwa kwake ama aliyezaliwa gerezani juu ya maisha yake ya baadaye!

Unadhani mtoto wa kifalme anayeishi katika jamii ya porini ama ya utumwani atakuwa na aina gani ya mawazo juu ya hatima yake!

Hivi ni aina gani ya mawazo unadhani atakuwa nayo mtu aliyezaliwa katika familia inayoamini katika mila,tamaduni, mambo ya matambiko, mizimu nk, juu ya uwepo wa Mungu halisi!

Yako maswali mengi sana, lakini lengo ni nataka uone kuwa, mahali mtu alipo,panauwezo wa kumtengenezea aina fulani ya mawazo ndani yake, na aina hiyo ya mawazo ndiyo ambayo humtengenezea mtazamo wa aina fulani, na huo mtazamo humjengea imani fulani juu yake,
na hiyo imani humpa kuamini katika kila kitu.

Leo hii tuna idadi ndogo sana ya watoto wa k**e wanaosoma masomo ya sayansi, si kana kwamba hawana uwezo, ila ni kwasababu katika jamii kuna mtazamo ambao umejengeka ya kwamba,masomo ya sayansi ni ya wanaume, sasa fikiri pamoja nami juu ya binti anayezaliwa katika hayo mazingira,
NI AINA GANI YA MAWAZO ANAYOWEZA KUWA NAYO JUU YA MASOMO YA SAYANSI?

Kumbuka;
Mawazo ni mkusanyiko wa taarifa(information) fulani ambazo zikiingia ndani ya ubongo wa mtu hutengeneza kitu kinachoitwa Mtazamo.

Huyu binti anayezaliwa katika jamii ya namna hii atakuwa na mtazamo upi juu ya haya masomo ya sayansi?.

Maandiko yanatuambia Yesu alitoka katika kijiji cha Nazareti,sifa juu ya kijiji hiki nimekupa mwanzoni, hebu fikiri pamoja nami,
Unadhani watoto waliozaliwa katika mazingira ya namna hii walikuwa na mawazo gani juu ya hatima zao!
Yamkini walizaliwa wakiwa na kitu kikubwa k**a ambacho Yesu alikuwa nacho unadhani walikitendea kazi?.

Naomba ufahamu kuwa:
"JESHI LA SIMBA LINALOONGOZWA NA KONDOO LINAWEZA KUSHINDWA NA JESHI LA KONDOO LINALOONGOZWA NA SIMBA"

Kinachokuongoza ama unachokiishi kikiwa dhaifu hakuna namna ya wewe kuwa hodari,
Utakuwa dhaifu tu.

Wito wangu juu yako katika kuuishi ukweli wa maisha yako, ni BADILI CHANZO CHA TAARIFA ili mtazamo na imani itakayojengeka ndani yako iwe ni ya kukufanya shujaa na si mtumwa.
Naam shida ni chanzo cha taarifa, kinachokufanya ujione ujionavyo.

Hosea 4:6
"Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa....

Umebarikiwa

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

Huwezi kuwa mshindi katika hii Dunia k**a hauna mwendelezo,Unaweza kuwa mwombaji mzuri lakini ukikosa mwendelezo utakuwa...
08/04/2026

Huwezi kuwa mshindi katika hii Dunia k**a hauna mwendelezo,

Unaweza kuwa mwombaji mzuri lakini ukikosa mwendelezo utakuwa mtu wa kupiga hatua moja mbele kisha unarudi nyuma,
Unaweza kuwa unasoma neno kwa muda mrefu lakini ukikosa mwendelezo utajikuta ulikotoka yaani nyuma.

HII DUNIA, INAHITAJI WATU WENYE MWENDELEZO WA KUENDELEA MBELE KILA SIKU PASIPO KURUDI NYUMA.

Shetani na mawakala wake sifa yao kubwa ni hawaishiagi njiani katika kutafuta kuharibu maisha yako.

K**a wanaotafuta kukurudishia nyuma hawachoki, kukosa kwako mwendelezo ni kuamua kuwapa ushindi wa kukurudisha nyuma.

Washindi ni wale wanaovumilia mpaka mwisho.

Unaweza usiwe mwombaji wa masaa mengi lakini una dakika 30 zako kila siku bila kuacha nakuhakikishia utapiga hatua kubwa kuliko yule anayeomba kwa msimu hata k**a anaomba masaa mengi,

Unaweza kuwa unasoma kila siku msitari mmoja bila kuacha nakuhakikishia utakuwa mshindi kuliko yule anayesoma sura nzima mara moja kwa week,

Mwendelezo ndio unaotoa ushindi.

Kukosa mwendelezo ni kujipa kibali cha kurudi kurudi nyuma.

Tafadhali sana,
Jiwekee mkakati wa kuamua kuwa na mwendelezo, ninachokuhakikishia ni utaona matokeo makubwa sana kwenye maisha yako.

Wakolosai 4:2
"Dumuni sana katika kuomba, mk**esha katika kuomba huku na shukrani"

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

Tafuta kwa Bidii kuujua ukuu wa Mungu kwenye maisha yako.Mashaka unayoyaona ndani yako ni kwasababu kuna ufahamu hauna j...
07/04/2026

Tafuta kwa Bidii kuujua ukuu wa Mungu kwenye maisha yako.

Mashaka unayoyaona ndani yako ni kwasababu kuna ufahamu hauna juu ya huyu Mungu anayeishi ndani yako ....

Wanafunzi wa Yesu wakati wanavuka kwenda ng'ambo , Upepo ulipovuma walijawa na mashaka kwasababu hawakujua ukuu wa Yesu waliyekuwa nae ....

Ukisoma Mathayo 8:27 Baada ya Yesu kukemea pepo na bahari zikamtii , Kila mmoja alianza kushangaa na kuuliza huyu mtu ni wa namna gani mpaka pepo na bahari za mtii ??

Maana yake walikuwa na Yesu ila hawakujua kuwa Yesu anauwezo wa kunyamanzisha Upepo wa bahari ...

Yesu yuko ndani yako lakini kwasababu haujui uwezo wake kwenye hiyo changamoto unayopitia ndio maana umejaa mashaka ....

Wale wanaojua uweza wa Yesu kwenye maisha yao huwa hawajawi na mashaka, maana wana uhakika na Mungu waliyenaye kuwa atatenda ...

Daudi anasema katika Zaburi 23:4
Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

alijua uweza wa Bwana ndio maana hata katika ya mauti anakiri akisema hatayaogopa mabaya maana anajua yeye yuko pamoja nae ...

Sikia nikwambie
"Yeye yuko pamoja na wewe nyakati zote ondoa mashaka ndani yako. Anasema Yeremia 32:27
“Mimi ndimi BWANA, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?

Halipo asiloliweza ondoa kabisa mashaka tambua ni Mungu anayeweza yote na atakusaidia kuvuka mpaka ng'ambo ya pili ...

Jumanne yako Imebarikiwa.

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

Ni week Mpya ambayo Bwana ametupatia ....Unapoianza hii week tembea na hili neno kutoka katika Warumi 8:37 "Lakini katik...
06/04/2026

Ni week Mpya ambayo Bwana ametupatia ....

Unapoianza hii week tembea na hili neno kutoka katika Warumi 8:37
"Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda."

Anasema Katika mambo Yote tunashinda na zaidi ya kushinda

Ni kweli kuna mambo yatainuka lakini utashinda ...

Adui atainua vikwazo lakini utashinda na zaidi ya kushinda ...

Mindset yako iwe na ushindi ndipo utajidhihirisha ....

Hautashindwa kupata wateja
Hautashindwa na Mitego ya adui
Hautashindwa kupiga hatua
Hautashindwa katika namna yoyote ...

Tembea kwa ujasiri ukijua week hii utashinda na zaidi ya kushinda ...

Week Yako imebarikiwa ...

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

FURAHA YAKO, MACHOZI YAO, KWANINI?.Niliwahi kusikia mfano wa  mwalimu aliyekuwa na tabia ya kumchapa mwanafunzi ambaye k...
02/04/2026

FURAHA YAKO, MACHOZI YAO, KWANINI?.

Niliwahi kusikia mfano wa mwalimu aliyekuwa na tabia ya kumchapa mwanafunzi ambaye kila siku ya shule alikuwa mchelewaji sugu.

Kila akimwona mwanafunzi yule kachelewa, mwalimu yule hakusita kumchapa bakora na kisha kumsema vibaya yule mtoto darasani mbele ya wenzake.

Siku moja yule mwanafunzi akawahi mapema shule. Wiki nzima mwalimu yule anamtafuta amchape bakora lakini mwanafunzi anawahi.

Sasa ikabidi amuulize mbele ya wenzake, imekuwaje mbona sasa anawahi?

Yule mwanafunzi, huku akilia akasema, siku zote nilikuwa nachelewa maana mama yangu alikuwa mgonjwa sana. Ni mimi peke yangu nilikuwa naishi naye. Katika hali yake ya ugoniwa hakuwa na mtu mwingine wa kumuugiza zaidi yangu.

Kila siku asubuhi nilipaswa kusafisha nyumba, kumpa dawa mama na kumuandalia hadi chakula cha mchana ndipo nije shule.

Mwanafunzi yule akahitimisha story hiyo kwa kusema, Wiki kadhaa zilizopita mama alifariki. Ndiyo maana sasa nawahi shule.

Yule mwalimu alilia sana. Akajilaumu kwanini hakumsikiliza yule mtoto na kujua kwanini kachelewa. Badala ya kufanyika faraja kwake akamuongezea maumivu.

SIKILIZA NIKUSHAURI,
Katika harakati zako za kutafuta, uwe makini sana usiumize wengine. Usikubali furaha yako iwe machozi kwa wengine. Wale unaowaumiza wanategemewa pia. Tena inawezekana wanategemewa sana.

Huyo unayemchongea ili afukuzwe kazi wewe upewe nafasi yake, laiti ungejua watu wangapi wanaomtegemea ungebadili mawazo yako mabaya.

Unataka afukuzwe kazi ili wewe uchukue nafasi yake. Umejiuliza kuna watu wangapi watakosa matibabu na wataweza kupoteza maisha wakikosa msaada wa fedha kwa huyo mtu?.

Umejiuliza kuna watoto wangapi wataacha shule huyo mtu akifukuzwa kazi.?

Kuna watu ambao wanafanya kazi lakini pesa yao inategemewa na watu wengi mno.

Mtu wa namna hiyo unapomuumiza, uwe na uhakika umeumiza watu wengi nyuma yake ambao huwajui. Machozi yao hayatakuacha salama.

Furaha yako isiwe machozi yao. Watazame wengine huku ukijua ana watu wanaomkubali sana na kumtegemea.
Kazia Tafakari hii kwa kusoma Waefeso 4:31-32
Usiumize watu. Furaha yako isiwe machozi kwa wengine.

Pastor Andrea Benedictor
TAG NIA NJEMA Bagamoyo
0713211635.

Address

NIA NJEMA BAGAMOYO
Bagamoyo
255

Telephone

+255713211635

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAG NIA NJEMA Bagamoyo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to TAG NIA NJEMA Bagamoyo:

Share