Parokia ya Watakatifu Petro na Paulo Kijenge

Parokia ya Watakatifu Petro na Paulo Kijenge UKURASA HUU NI KWA AJILI YA MASUALA YA KANISA PEKEE HURUHUSIWI KUTUMA VITU AMBAVYO HAVIENDANI.

05/06/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA JUMAMOSI*

*JUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*06 JUNI 2026*
*-------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2 Timotheo, 4:1-8

Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake; lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho. Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako. Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.

*Neno La Bwana........*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 71:8-9, 14-17, 22

Kinywa changu kitajazwa sifa zako, Na heshima yako mchana kutwa.
Usinitupe wakati wa uzee, Nguvu zangu zipungukapo usiniache.

*(K)Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa*

Nami nitatumaini daima, Nitazidi kuongeza sifa zake zote.
Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa;

*(K)Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa*

Nitakuja na mambo ya ajabu ya Bwana MUNGU; Nitawakumbusha watu haki yako Wewe peke yako.
Ee Mungu, umenifundisha tokea ujana wangu; Nimekuwa nikitangaza miujiza yako hata leo.

*(K)Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa*

Nami nitakushukuru kwa kinanda, Na kweli yako, Ee Mungu wangu.
Nitakuimbia Wewe kwa kinubi, Ee Mtakatifu wa Israeli.

*(K)Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako Mchana kutwa*

*SHANGILIO*

Mathayo, 5:3

*Aleluya, Aleluya*

*Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao*

*Aleluya, Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 12:38-44

Yesu aliwaambia katika mafundisho yake: Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele katika karamu; ambao hula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu; hawa watapata hukumu iliyo kubwa. Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa. Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

*Neno La Bwana.........*

04/06/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA IJUMAA*

*KUMBU KUMBU YA MTAKATIFU BONIFASI ASKOFU SHAHIDI*

*JUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*05 JUNI 2026*
*-------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2Timotheo, 3:10-17

Wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na uvumilivu, na upendo, na saburi; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote. Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa. lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao; na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu. Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

*Neno La Bwana.........*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 119:157, 160-161, 165-166, 168

Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi,
Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
Jumla ya neno lako ni kweli,
Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.

*(K) Wana amani nyingi waipendao sheria yako*

Wakuu wameniudhi bure,
Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
Wana amani nyingi waipendao sheria yako,
Wala hawana la kuwakwaza.

*(K) Wana amani nyingi waipendao sheria yako*

Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako,
Na maagizo yako nimeyatenda.
Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako,
Maana njia zangu zote zi mbele zako.

*(K) Wana amani nyingi waipendao sheria yako*

*Shangilio*
Zaburi, 111:7, 8

*Aleluya, Aleluya*

*Maagizo yako yota Ee Bwana ni amini, Yamethibitika milele na milele*

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 12:35-37

Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu, alijibu, akasema, Husemaje waandishi ya kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi? Daudi mwenyewe alisema, kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako. Daudi mwenyewe asema ni Bwana; basi amekuwaje mwanawe? Na mkutano mkubwa walikuwa wakimsikiliza kwa furaha.

*Neno La Bwana........*

03/06/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA ALHAMISI*

*JUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*04 JUNI 2026*
*-------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2Timotheo, 2:8-15

Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi k**a inenavyo injili yangu. Nami katika hiyo nimeteswa hata kufungwa k**a mtenda mabaya; lakini neno la Mungu halifungwi. Kwa ajili ya hilo nastahimili mambo yote, kwa ajili ya wateule, ili wao nao waupate wokovu ule ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. Ni neno la kuaminiwa.
Kwa maana, k**a tukifa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia; k**a tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; k**a tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi; k**a sisi hatuamini, yeye hudumu wa kuaminiwa. Kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao. Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.

*Neno La Bwana.......*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 25:4-5, 8-10, 14;

Ee Bwana, unijulishe njia zako,
Unifundishe mapito yako,
Uniongoze katika kweli yako,
Na kunifundisha.

*(K) Ee Bwana, unijulishe njia zako*

Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu,
Nakungoja Wewe mchana kutwa.
Bwana yu mwema, mwenye adili,
Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Wenye upole atawaongoza katika hukumu,
Wenye upole atawafundisha njia yake.

*(K) Ee Bwana, unijulishe njia zako*

Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli,
Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.
Siri ya Bwana iko kwao wamchao,
Naye atawajulisha agano lake.

*(K) Ee Bwana, unijulishe njia zako*

*SHANGILIO*

Yohane, 8:12

*Aleluya, Aleluya*

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, asema, Bwana, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 12:28-34

Mmoja wa waandishi alifika kwa Yesu akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza? Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja. nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako k**a nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi. Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye; na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani k**a nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhabihu zote pia. Naye Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, alimwambia, Wewe hu mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.

*Neno La Bwana.........*

03/06/2026
02/06/2026

*๐ŸŸฃTAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA JUMATANO๐ŸŸฃ*

*๐ŸŸฃKUMBU KUMBU YA MTAKATIFU KAROLI LWANGA NA WENZAKE MASHAHIDI WA UGANDA๐ŸŸฃ*

*๐ŸŸฃJUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA MWAKA๐ŸŸฃ*

*03 JUNI 2026*
*------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2Timotheo, 1:1-3, 6-12

Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa ajili ya ahadi ya uzima ulio katika Kristo Yesu; kwa Timotheo, mwanangu mpendwa. Neema na iwe kwako, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
Namshukuru Mungu, nimwabuduye kwa dhamiri safi tangu zamani za wazee wangu, k**a vile nikukumbukavyo wewe daima, katika kuomba kwangu usiku na mchana.
Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Basi usiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, wala usinionee haya mimi mfungwa wake, bali uvumilie mabaya pamoja nami kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu; ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele, na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Kristo Yesu; aliyebatili mauti, na kuufunua uzima na kutokuharibika, kwa ile Injili; ambayo kwa ajili ya hiyo naliwekwa niwe mhubiri na mtume na mwalimu.
Kwa sababu hiyo nimepatikana na mateso haya, wala sitahari; kwa maana namjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kwamba aweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hata siku ile.

*Neno La Bwana.........*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 123:1-2

Nimekuinulia macho yangu,
Wewe uketiye mbinguni.
K**a vile macho ya watumishi
Kwa mkono wa bwana zao.

*(K) Nimekuinulia macho yangu, ee Bwana*

K**a macho ya mjakazi
Kwa mkono wa bibi yake;
Hivyo macho yetu humwelekea Bwana, Mungu wetu.
Hata atakapoturehemu.

*(K) Nimekuinulia macho yangu, ee Bwana*

*SHANGILIO*

Luka, 8:15

*Aleluya, Aleluya*

Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno la Mungu, na kulishika.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 12:18-27

Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, walimwendea Yesu, wakamwuliza na kusema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao. Basi kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao. Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika; hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye. Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.

Yesu akajibu, akawaambia, Je! hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu? Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa k**a malaika walioko mbinguni. Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahi- mu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.

*Neno La Bwana.......*

01/06/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA JUMANNE*

*JUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*02 JUNI 2026*
*-------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2Petro, 3:11-15, 17-18

Kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? Lakini, k**a ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, k**a vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa.
Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu, mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele. Amina.

*Neno La Bwana...........*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 90:2-4,10,16

Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia,
Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu.

*(K) Wewe Bwana, umekuwa makao yetu, kizazi baada ya kizazi*

Wamrudisha mtu mavumbini,
Usemapo, Rudini, enyi wanadamu.
Maana miaka elfu machoni pako
Ni k**a siku ya jana ikiisha kupita,
Na k**a kesha la usiku.

*(K) Wewe Bwana, umekuwa makao yetu, kizazi baada ya kizazi*

Siku za miaka yetu ni miaka sabini,
Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini;
Na kiburi chake ni taabu na ubatili,
Maana chapita upesi tukatokomea mara.

*(K) Wewe Bwana, umekuwa makao yetu, kizazi baada ya kizazi*

Utushibishe asubuhi kwa fadhili zako,
Nasi tutashangilia na kufurahi siku zetu zote
Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako,
Na adhama yako kwa watoto wao.

*(K) Wewe Bwana, umekuwa makao yetu, kizazi baada ya kizazi*

*SHANGILIO*

Mathayo,4:4

*Aleluya,Aleluya*

Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

*Aleluya.Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 12:13-17

Walituma kwa Yesu baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno. Hata walipofika walimwambia, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, wala hujali cheo cha mtu; kwa maana hutazami sura za watu; lakini katika kweli waifundisha njia ya Mungu. Je! Ni halali kumpa Kaisari kodi au siyo? Tumpe, tusimpe? Naye, akijua unafiki wao, akawaambia, Mbona mmejijaribu? Nileteeni dinari niione. Wakaileta. Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii na anwani hii? Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana.

*Neno La Bwana...........*

31/05/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA JUMATATU*

*MTAKATIFU YUSTINO SHAHIDI*

*JUMA LA TISA MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*01 JUNI 2026*
*==============*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

2Petro, 1:2-7

Neema na iwe kwenu na amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa, na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika sabauri yenu utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na ktika upendano wa ndugu, upendo.

*Neno La Bwana........*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 91:1-2, 14-16

Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu
Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu nitakayemtumaini.

*(K) Mungu wangu ninakutumaini*

Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
Kwa kuwa amekaza kunipenda
Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, kw akuwa amenijua jina langu.
Ataniita nami nitamwitikia.

*(K) Mungu wangu ninakutumaini*

Nitakuwa pamoja naye taabuni,
Nitamwokoa na kumtukuza;
Kwa siku nyingi nitamshibisha,
Nami nitamwonyesha wokovu wangu.

*(K) Mungu wangu ninakutumaini*

*SHANGILIO*

Zaburi, 130:5

*Aleluya, Aleluya*

Roho yangu inamngoja Bwana, na neno lake nimelitumainia.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko,12:1-12

Yesu alisema na Mafarisayo kwa mifano; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akazungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. Hata kwa wakati wake akatuma, mtumwa kwa wale wakulima, ili apokee kwa wakulima katika matunda ya mizabibu. Wakamtwaa, wakampiga, wakamtoa nje, hana kitu. Akatuma tena kwao mtumwa mwingine, na huyo wakamtia jeraha -za kichwa, wakamfanyia jeuri. Akamtuma mwingine, huyo wakamwua; na wengine wengi, hawa wakiwapiga na hawa wakiwaua. Basi alikuwa na mmoja bado, mwana mpendwa wake; huyu naye akamtuma kwao mwisho, akisema, Watamstahi mwanangu. Lakini wale wakulima wakasemezana, Huyu ni mrithi; haya, na tumwue, na urithi utakuwa wetu. Wakamk**ata, wakamwua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu. basi atafanyaje yule bwana wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. Hata andiko hili hamjalisoma, Jiwe walilolikataa waashi, hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni. Neno hili limetoka kwa Bwana, nalo ni ajabu machoni petu? Nao wakatafuta kumk**ata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.

*Neno La Bwana........*

30/05/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA DOMINIKA*

*SHEREHE YA UTATU MTAKATIFU*

*DOMINIKA BAADA YA PENTEKOSTE - MWAKA A. WA KANISA*

*31 MEI 2026*
*ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€ฯ€*

*๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง๐ŸŽง*
*๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ*
*MASOMO YA MISA*
*๐Ÿ’’๐Ÿ’’๐Ÿ’’๐Ÿ’’๐Ÿ’’๐Ÿ’’๐Ÿ’’*
*๐ŸŽผ๐ŸŽผ๐ŸŽผ๐ŸŽผ๐ŸŽผ๐ŸŽผ๐ŸŽผ*
*Kutoka,34 : 4-6, 8-9*
*Danieli, 3:52-56. (K) 52*
*2Wakorintho,13 :11-14*
*Ufunuo,1 :8*
*Yohane,3:16-18*
*๐ŸŽน๐ŸŽน๐ŸŽน๐ŸŽน๐ŸŽน๐ŸŽน๐ŸŽน*
*๐Ÿช—๐Ÿช—๐Ÿช—๐Ÿช—๐Ÿช—๐Ÿช—๐Ÿช—*

*SOMO LA KWANZA*

*Kutoka,34 : 4-6, 8-9*

Musa aliinuka na mapema asubuhi, naye akakwea katika mlima wa Sinai, k**a Bwana alivyomwamuru, akazichukua hizo mbao mbili za mawe mkononi mwake.

Bwana akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la Bwana. Bwana akapita mbele yake, akatangaza, Bwana, Bwana, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; Musa akafanya haraka, akainamisha kichwa chake hata nchi, akasujudu. Akasema, Ikiwa sasa nimepata neema mbele zako, Bwana, nakuomba, Bwana, uende kati yetu maana ni watu wenye shingo ngumu; ukasamehe uovu wetu na dhambi yetu, ukatutwae tuwe urithi wako.

*Neno La Bwana.......*

*WIMBO WA KATIKATI*

*Danieli, 3:52-56. (K) 52*

*(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele*

Umehimidiwa, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu:
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Limehimidiwa jina lako takatifu, tukufu;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

*(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele*

Umehimidiwa katika hekalu la fahari yako takatifu;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa juu ya kiti cha ufalme wako;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

*(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele*

Umehimidiwa utazamaye vilindi, uketiye juu ya makerubi;
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa katika anga la mbinguni
Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele.

*(K) Wastahili kusifiwa na kutukuzwa milele*

*SOMO LA PILI*

*2Wakorintho,13 :11-14*

Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfariji- ke, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. Sali- mianeni kwa busu takatifu. Watakatifu wote wawasalimu. Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu. na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.

*Neno La Bwana........*

*SHANG1LIO*

*Ufunuo,1 :8*

*Aleluya, Aleluya*

Atukuzwe Baba na
Mwana na Roho
Mtakatifu, Mungu
ambaye
yupo,aliyekuwako, na
atakayekuja.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

*Yohane,3:16-18*

Yesu alimwambia Nikodemu: Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhu- kumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.

*Neno La Bwana.......*

29/05/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA JUMAMOSI*

*JUMA LA NANE MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*30 MEI 2026*
*------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

Yuda, 1:20-25

Wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele. Wahurumieni wengine walio na shaka, na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.
Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu; Yeye aliye Mungu pekee, Mwokozi wetu kwa Yesu Kristo Bwana wetu; utukufu una yeye, na ukuu, na uwezo, na nguvu, tangu milele, na sasa, na hata milele. Amina.

*Neno La Bwana .......*

*WIMBO WA KATIKATI*

Zaburi, 63:1-5

Ee Mungu, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,
Nafsi yangu inakuonea kiu,
Mwili wangu wakuonea shauku,
Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.

*(K) Nafsi yangu inakuonea kiu, Ee Bwana*

Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu,
Nizione nguvu zako na utukufu wako.
Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai;
Midomo yangu itakusifu.

*(K) Nafsi yangu inakuonea kiu, Ee Bwana*

Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai;
Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
Nafsi yangu itakinai k**a kushiba mafuta na vinono;
Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.

*(K) Nafsi yangu inakuonea kiu, Ee Bwana*

*SHANGILIO*

Zaburi, 119:18

*Aleluya, Aleluya*

Unifumbue macho yangu niyatazame, maajabu yatokayo katika sheria yako.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko, 11:27-33

Yesu na wanafunzi walifika Yerusalemu; alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee, wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya? Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya. Ubatizo wa Yohane ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Nijibuni.
Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, K**a tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini? Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu. Waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohane kuwa nabii halisi. Wakamjibu Yesu, wakasema, Hatujui. Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.

*Neno La Bwana......*

28/05/2026

*TAFAKARI YA MASOMO YA MISA YA IJUMAA*

*JUMA LA NANE MWAKA A KIPINDI CHA KAWAIDA CHA KANISA*

*29 MEI 2026*
*------------------------*

*MASOMO YA MISA*

*SOMO LA KWANZA*

1 Petro, 4:7-13

Mwisho wa mambo yote umekaribia; basi iweni na akili, mkeshe katika sala. Zaidi ya yote iweni na juhudi, mkeshe katika sala. Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi. Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunungโ€™unika; kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; k**a mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. Mtu akisema, na aseme k**a mausia ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.
Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio katik yenu, unaowapata k**a moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho. Lakini k**a mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

*Neno La Bwana........*

*WiIMBO WA KATIKATI*

Zaburi,149:1-6,9

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,
Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.

*(K) Bwana awaridhia watu wake. au: Aleluya*

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

*(K) Bwana awaridhia watu wake. au: Aleluya*

Watauwa na waushangilie utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote.

*(K) Bwana awaridhia watu wake. au: Aleluya*

*SHANGILIO*

1 Petro,1:25

*Aleluya, Aleluya*

Neno la Bwana hudumu hata milele, na neno hilo ni neno jema lililohubiriwa kwenu.

*Aleluya,Aleluya*

*SOMO LA INJILI*

Marko,11:11-26

Yesu aliingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara.
Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipouiikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.
Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza na wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa; wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu. Akafundisha, akasema, Je! haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyangโ€™anyi. Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote walishangaa kwa mafundisho yake. Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.
Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mtini umenyauka toka shinani. Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. Yesu akajibu, akawaambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ngโ€™oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.
Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, ntkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu. Lakini k**a ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.

*Neno La Bwana........*

Address

Kijenge Box 3071
Arusha
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Parokia ya Watakatifu Petro na Paulo Kijenge posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share