ELCT Diocese of Meru

ELCT Diocese of Meru "KAZI YA MUNGU,MIKONO YETU"

Fursa ya ajira kwa wenye sifa....
11/05/2026

Fursa ya ajira kwa wenye sifa....

ZIARA YA MARAFIKIOfisi Kuu ya KKKT Dayosisi ya Meru ilipata fursa ya kutembelewa na Marafiki kutoka Kanisa la Kiinjili l...
06/05/2026

ZIARA YA MARAFIKI

Ofisi Kuu ya KKKT Dayosisi ya Meru ilipata fursa ya kutembelewa na Marafiki kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Bavaria, Ujerumani. Lengo la ziara ni kuimarisha uhusiano mzuri na wa muda mrefu.

Wageni waliongozwa na Baba Askofu Christian Kopp wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Bavaria na walipokelewa na Msaidizi wa Askofu, Mchungaji Ndelekwa Pallangyo kwa niaba ya Baba Askofu Elias Nasari.

"KAZI YA MUNGU, MIKONO YETU"

MKUTANO MKUU WA IDARA YA WANAWAKE NA WATOTO.Idara ya Wanawake na Watoto, Jimbo la Kusini lililo sehemu ya KKKT Dayosisi ...
04/05/2026

MKUTANO MKUU WA IDARA YA WANAWAKE NA WATOTO.

Idara ya Wanawake na Watoto, Jimbo la Kusini lililo sehemu ya KKKT Dayosisi ya Meru inafanya Mkutano wake Mkuu wa 11.

Mkutano unafanyika Usharika wa Kikatiti na ulifunguliwa rasmi tarehe 03/05/2026 katika Ibada iliyoongozwa na Msaidizi wa Askofu, Mchungaji Ndelekwa Pallangyo kwa niaba ya Baba Askofu Elias Nasari. Neno Kuu la Mkutano linatoka Isaya 41:13b "Usiogope; mimi nitakusaidia"

Mkutano utaendelea hadi tarehe 04/05/2026.

"KAZI YA MUNGU, MIKONO YETU"

KONGAMANO LA MAOMBIIdara ya Wanawake na Watoto ya KKKT Dayosisi ya Meru imeandaa kongamano kubwa la maombi ya Wanawake t...
23/04/2026

KONGAMANO LA MAOMBI

Idara ya Wanawake na Watoto ya KKKT Dayosisi ya Meru imeandaa kongamano kubwa la maombi ya Wanawake tarehe 22 hadi 24 Aprili 2026.

Ibada ya ufunguzi wa Kongamano iliongozwa na Msaidizi wa Askofu, Mchungaji Ndelekwa Pallangyo ambapo Neno Kuu litakaloongoza Kongamano hilo linatoka kitabu cha Mathayo Mtakatifu 11:28-30.

Kongamano linafanyika chuo cha ufundi stadi Mshik**ano. Washiriki ni Wanawake kutoka Sharika zote za KKKT Dayosisi ya Meru.

"KAZI YA MUNGU, MIKONO YETU"

02/04/2026

KARIBUNI

Mwaliko
28/03/2026

Mwaliko

IBADA YA SIKU YA BWANA, UZINDUZI NA UFUNGUZI WA MKUTANOIbada ya siku ya Bwana ya tarehe  22/03/2026 katika Usharika wa P...
23/03/2026

IBADA YA SIKU YA BWANA, UZINDUZI NA UFUNGUZI WA MKUTANO

Ibada ya siku ya Bwana ya tarehe 22/03/2026 katika Usharika wa Patandi iltawaliwa na matendo makuu ya baraka.

Mkutano Mkuu wa Idara ya Wanawake na Watoto Jimbo la Magharibi ulifunguliwa rasmi. Mkutano ulifunguliwa rasmi na Baba Askofu Elias Kitoi Nasari na unaongozwa na Neno Kuu kutoka Isaya 43:26.

Baba Askofu aliweka Jiwe la Pembe kwenye jengo la matumizi mbalimbali k**a ofisi, vyumba vya wageni, madarasa na maliwato. Jengo litakuwa na ghorofa mbili ambapo sakafu ya chini (ground floor) inatarajiwa kukamilika mwaka huu. Baba Askofu alisisitiza majengo ya Kanisa kuwa na miundombinu rafiki kwa wenye mahitaji maalum.

"KAZI YA MUNGU MIKONO YETU"

Fursa ya ajira kwa wenye sifa stahiki
18/03/2026

Fursa ya ajira kwa wenye sifa stahiki

IBADA YA SIKU YA BWANA NA UZINDUZIKatika Ibada ya Siku ya Bwana tarehe 15/03/2026, Usharika wa Duluti, Mtaa wa Hosiana; ...
16/03/2026

IBADA YA SIKU YA BWANA NA UZINDUZI

Katika Ibada ya Siku ya Bwana tarehe 15/03/2026, Usharika wa Duluti, Mtaa wa Hosiana; yalifanyika pia matendo ya baraka ya kuwekwa mawe ya msingi na uzinduzi wa Darasa la Shule ya Jumapili na Kengele na manara wake.

Ibada iliongozwa na Baba Askofu Elias Kitoi Nasari, Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Meru. Baba Askofu aliwapongeza Washarika kwa jitihada zao katika kuifanya kazi ya Bwana.

Katika Ibada hiyo ilifanyika harambee iliyoongozwa na Mkuu wa Jimbo la Kati, Mchungaji Abel Sawe Kaaya kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kuabudia lenye uwezo wa kubeba Watu 700 kwa wakati mmoja. Ujenzi wa jengo hilo umeanza. shilingi za Kitanzania milioni 40 ziliapatikana katika harambee hiyo.

"KAZI YA MUNGU, MIKONO YETU"

Fursa ya ajira kwa wenye sifa
03/03/2026

Fursa ya ajira kwa wenye sifa

Address

Leganga
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ELCT Diocese of Meru posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share