14/08/2026
MATENDO YA BARAKA - USHARIKA WA KILIMAMOJA
Tarehe 13/08/2026 yalifanyika matendo ya baraka Usharika wa Kilimamoja. Matendo hayo ni kuwekwa wakfu kiwanja cha Mtaa mpya, kuwekwa jiwe la msingi Mtaa wa Penuel, kuzinduliwa jengo la shule ya Jumapili na kuzinduliwa rasmi Usharika wa Kilimamoja. Matendo yote hayo yalifanywa na Baba Askofu Elias K. Nasari, Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Meru.
Baba Askofu aliwashukuru na kuwapongeza Wanakilimamoja kwa jinsi wanavyotekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya Dayosisi "Kazi ya Mungu, Mikono yetu". Pia aliwaomba Washarika na Viongozi wa Serikali kutoa maeneo zaidi kwa ajili ya ukuaji wa Kanisa.
"KAZI YA MUNGU, MIKONO YETU"