19/07/2026
3. NYAKATI ZA KUMKUMBUSHA BWANA
Isaya 66:6 “ Sauti ya fujo itokayo mjini! Sauti itokayo hekaluni! Sauti ya Bwana awalipaye adui zake adhabu!”
Nyakati za kumkumbusha Bwana kisiwe kipindi cha kukaa kimya bali roho mtakatifu akuongoze. Kwa nini usimwache Mungu akaye kimya? Bali unamkumbusha Bwana Yesu maana tunajua Yeye ni mpaji wa vyote, maana sisi tunamtegemea Yeye
Isaya 43:26 “Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.”
Mungu anasema umkumbushe ili aone uzingativu wako katika kukiri au kutangaza yale ambayo Mungu unatamani akuridhie ili akupe ahadi na baraka zake. Kipindi cha kumkumbusha Bwana ni kipindi cha kuumba nini kitokee.
Katika nyakati za kumkumbusha Bwana ni nyakati za ibada yaani hupaswi kukosa katika ibada na mikesha. Nyakati hizi shetani anapambana kung’oa waliookoka warudi duniani hivyo hizi ni nyakati za kumtafuta Mungu kweli kweli.
Isaya 62:6 “Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu, Ngome yangu, sitatikisika sana.
©KIONGOZI WA KIROHO WA KANISA LA EFATHA - MTUME NOEL KAPINGA