Pastor Crispin Mdimi

Pastor Crispin Mdimi MSHAURI, MWALIMU NA KIONGOZI WA MAOMBI WA KANDA

04/02/2026

Super Migration

04/02/2026

Kilimanjaro

04/02/2026

Mount Kilimanjaro

25/01/2026
Kuna uhusiano mkubwa wa KIROHO Kati ya ardhi au eneo na watu wake. Ni rahisi kuona watu wanaoishi eneo fulani kuwa na ma...
23/01/2026

Kuna uhusiano mkubwa wa KIROHO Kati ya ardhi au eneo na watu wake. Ni rahisi kuona watu wanaoishi eneo fulani kuwa na mambo yanayofanana kuanzia tabia mpaka uchumi wao. Ndio sababu ukifatilia utagundua kuwa watu wa mtaa fulani hawafanani tabia na maisha na watu wa mtaa mwingine ipo siri kwa kiroho cha eneo.

Pia pamekuwa na shuhuda mbalimbali kuwa kuna watu wamewahi kuishi mtaa fulani wakawa na maendeleo, lakini walipotoka na kwenda eneo jingine kila kitu kikaharibika. Walipohama eneo la kwanza kwenda eneo jingine ndoa zikavurugika, biashara zikaharibika kazi zao zikaharibika. Sababu sio watu kubadilika tabia bali ni roho za kigeni zinazotawala kwenye ardhi hiyo mpya. Tatizo sio Hali ya kiuchumi ya nchi kubadilika Tatizo lipo kwenye hilo eneo jipya.

Leo nakupa siri hii ni kweli ardhi imebeba roho, ili uweze kutambua ni roho gani ipo kwenye eneo hilo angalia aina ya maisha wanayo ishi watu wa eneo hilo.

Mungu ameshusha UFUNUO kwetu tutakuwa na Maombi ya siku 11 za KUIKOMBOA ARDHI ili itoe mazao yake karibu sana jumapili hii. Wewe uliyeko mbali piga simu.

Mwl Mdimi
0689 488000

Ukiona Mambo Yako YAMEHARIBIKA Ujue Mahali Fulani Kuna Mtu ANAFANIKIWA.
17/01/2026

Ukiona Mambo Yako YAMEHARIBIKA Ujue Mahali Fulani Kuna Mtu ANAFANIKIWA.

USIFANYE MAMBO HAYA 2026.2. Kutokuwa Tayari Kusahihishwa.Kuna watu wengi wanaoamini kuwa hakuna mtu  mwingine anaweza ku...
29/12/2025

USIFANYE MAMBO HAYA 2026.

2. Kutokuwa Tayari Kusahihishwa.

Kuna watu wengi wanaoamini kuwa hakuna mtu mwingine anaweza kuwasahihisha hata wakikosea bado wanaona wako sahihi.

Mtu asiyetaka kusahihishwa hawezi kusaidiwa. Hakuna mwanadam asiyekosea. mwaka huu mpya uwe tayari kukosolewa ili ufike mbali

K**A UNATAKA KUFANIKIWA 2026 USIFANYE MAMBO HAYA"! 1. Kuishi bila Malengo Unapowinda Sungura wawili kwa wakati mmoja huw...
29/12/2025

K**A UNATAKA KUFANIKIWA 2026 USIFANYE MAMBO HAYA"!

1. Kuishi bila Malengo

Unapowinda Sungura wawili kwa wakati mmoja huwezi Pata hata mmoja. Mtu asiyekuwa na Malengo yupo k**a mtu anayekimbiza sungura wawili kwa wakati mmoja, hana mwelekeo na hana vipaumbele maishani. Anafanya kila kitu bila mpangilio

Mithali 17:24 "Hekima huwa machoni pake mwenye ufahamu; Bali macho ya mpumbavu huwa katika ncha za dunia"

Mpumbavu haoni mbele wala hatambui lengo lake anaangalia kila mahali lakini hajui aende wapi.
🤔 Shetani akitaka kuharibu maisha ya mtu huanza kwa kuvuruga MWELEKEO wake.

Kila jambo na wakati wake, ilikuwa ni miezi, wiki na hatimae zimebaki siku kupata kibali cha kumaliza mwaka. Maswali ya ...
29/12/2025

Kila jambo na wakati wake, ilikuwa ni miezi, wiki na hatimae zimebaki siku kupata kibali cha kumaliza mwaka. Maswali ya kujiuliza ni mambo magapi umejifunza mwaka huu na kwa kupitia maarifa hayo mangapin umeyafanyia kazi, Katika mapito na magumu uliyokutana nayo 2025 pia yafanye yawe darasa kwako na ukisha jifunze fanyia kazi ulichojifunza Ili uweze kupata matokeo chanya. Usipoyafanyia kazi mitihani k**a hiyo inaweza kujirudia tena kwa sababu hujafaulu.

Kanuni ya maisha inasema wazi mafanikio yako yamefichwa kwenye maarifa, na kwa kufanyia kazi maarifa hayo. hiki unachokijua leo usipokifanyia kazi maarifa hayo uliyopokea hayatakuwa na maana tena kwako na unakuwa hauna tofauti na mtu asiyejua. JIFUNZE NA FANYIA KAZI ULICHOJIFUNZA 2026 UTAKUWA MWAKA WAKO WA USHUHUDA.

Address

Arusha
00255

Telephone

+255658944227

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor Crispin Mdimi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share