17/05/2026
Bwana Yesu asifiwe mpendwa Wangu. Karibu katika Ibadan yetu ya leo Masaba Township MFA. Nitakuwa nikizungumza kuhusu ujumbe
"ASILI YAKO HAITAAMUA HATIMA YAKO", 1Mambo ya nyakati 4:9-10
Niukweli Asili YAKO inaweza kuwa mbaya ambayo hata huwezi taka kueleza Kwa watu. Ukaendelea kuivumilia hata kuamini ndivyo ulivyo pangiwa na Mungu, lakini nina neno juu yako, unaweza badili mwisho wako ukapendeza Kulikov mwanzo.
Mambo matatu yakuusaidia:
1.TAMANI KUISHI MAISHA YA HESHIMA
Biblia inasema Yabesi alikuwa Mwenye HESHIMA Kulikov ndugu make. Kitakacho kupa Haji ya kupokea yaliyo kwenye Hazina ya Mungu kwako, ni Maisha ya heshima. Jiheshimu, HESHIMA watu na zaidi umheshimu Mungu naye atakuheshimisha na HATIMA iliyo kuu. Mithali 8:17
2.ELEWA HATIMA YAKO NI MUNGU ANAIJUA
Haijalishi ulizaliwa wapi na wazazi gani au misingi ipi. Lewa Mungu alikuleta duniani wala sio nguvi za wazazi wako...Jer 1:4-5. Hivyo hukuja duniani kwa bahati mbaya, yeye alikujua na hata kukupangia HATIMA yako
3.MLINGANE MUNGU
Licha ya kuwa Mungu ametupangia HATIMA zetu na yuko tayari kutufikisha pale Jer 29.11. Sharti tuwe tumemwomba Mungu. Yeye ametuwekea HATIMA lakini adui anatukumbusha Asili yetu Mara Kwa Mara hata kutupofusha tusiione. Mambo hupenya mbingu na kutufikisha kwenye store ya Mungu ili tuelewe alichotuwekea
K**a alivyoomba Yabesi na Mungu akamtendea, niombi langu kuwa Mungu akutendee sawa na Mambo yako mbele yake; yeye akubariki, apanue mipaka yako, mkono wake uwe juu yako, na akulinde kutoka Kwa maovu. Ubarikiwe