27/05/2026
Kwanini Tukambike?
1. Makambi Hutukaribisha Zaidi kwa Mungu.
Makambi hutupa nafasi ya kuondoka kwenye pilikapilika za maisha ili tupate muda wa maombi, kujifunza Neno la Mungu, na kutulia mbele zake.
“Tulieni mkajue ya kuwa mimi ni Mungu.”
— Zaburi 46:10
2. Makambi Hujenga Imani Yetu.
Kupitia mafundisho, mahubiri, na ushuhuda mbalimbali, maisha ya watu wengi hubadilika na kuimarishwa kiroho.
“Imani chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.”
— Warumi 10:17
3. Makambi Hujenga Umoja wa Waamini
Tunapokutana pamoja kambini, tunajifunza kupendana, kusaidiana, na kuombeana k**a familia moja ya Mungu.
“Tazama jinsi ilivyo vema na kupendeza ndugu wakae pamoja kwa umoja.”
— Zaburi 133:1
4. Makambi Hututenganisha kwa Muda na Mambo ya Dunia
Makambi hutusaidia kuweka kando shughuli za kawaida ili kumpa Mungu nafasi ya kwanza katika maisha yetu.
“Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu…”
— Mathayo 6:33
5. Makambi Huleta Mabadiliko ya Maisha
Wengi wameokoka, wameponywa majeraha ya moyo, na kupata nguvu mpya kupitia makambi ya kiroho.
“Mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya.”
— 2 Wakorintho 5:17
KARIBU MAKAMBI YA MWAKA HUU
Usikubali shughuli za maisha zikakunyima baraka za kiroho.
Biashara zitakuwepo, kazi zitakuwepo, lakini nafasi ya kukutana na Mungu ni ya muhimu zaidi.
Mwaka huu njoo:
ujifunze Neno la Mungu
uombe pamoja na wengine
ujengwe kiroho
upokee faraja na matumaini mapya
“Nami nitawapa ninyi moyo mpya…”
— Ezekieli 36:26
Karibu sana kwenye makambi ya mwaka huu.Mungu ana jambo jema kwa ajili yako.
🙏🙏🙏🙏