God's Great Salvation ministry

God's Great Salvation ministry 446k followers 2.3m likes

17/11/2025

1 Wakorintho 2 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁴ Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
⁵ ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu.
⁶ Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii, wanaobatilika;
⁷ bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
⁸ ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana k**a wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu;

17/11/2025

1 Timotheo 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁵ Walakini mwisho wa agizo hilo ni upendo utokao katika moyo safi na dhamiri njema, na imani isiyo na unafiki.
⁶ Wengine wakiyakosa hayo wamegeukia maneno ya ubatili;
⁷ wapenda kuwa waalimu wa sheria, ingawa hawayafahamu wasemayo wala mambo yale wayanenayo kwa uthabiti.
⁸ Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, k**a mtu akiitumia kwa njia iliyo halali;
⁹ akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji,
¹⁰ na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;

17/11/2025

Waefeso 3 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.
⁸ Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;
⁹ na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;
¹⁰ ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;
¹¹ kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu.
¹² Katika yeye tunao ujasiri na uwezo wa kukaribia katika tumaini kwa njia ya kumwamini.
¹³ Basi naomba msikate tamaa kwa sababu ya dhiki zangu kwa ajili yenu, zilizo utukufu kwenu.
¹⁴ Kwa hiyo nampigia Baba magoti,

17/11/2025

Wagalatia 4 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁰ Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka.
¹¹ Nawachelea, isiwe labda nimejitaabisha bure kwa ajili yenu.
¹² Ndugu zangu, nawasihi, iweni k**a mimi, maana mimi ni k**a ninyi. Hamkunidhulumu kwa lo lote.
¹³ Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili;
¹⁴ na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea k**a malaika wa Mungu, k**a Kristo Yesu.
¹⁵ Ku wapi, basi, kule kujiita heri? Maana nawashuhudu kwamba, k**a ingaliwezekana, mngaling'oa macho yenu, mkanipa mimi.
¹⁶ Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli?

17/11/2025

Wagalatia 2 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Lakini wale wenye sifa ya kuwa wana cheo; (walivyokuwa vyo vyote ni mamoja kwangu; Mungu hapokei uso wa mwanadamu); nasema, hao wenye sifa hawakuniongezea kitu;
⁷ bali, kinyume cha hayo, walipoona ya kuwa nimekabidhiwa injili ya wasiotahiriwa, k**a vile Petro ya waliotahiriwa;
⁸ (maana yeye aliyemwezesha Petro kuwa mtume wa waliotahiriwa ndiye aliyeniwezesha mimi kwenda kwa Mataifa);
⁹ tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;

17/11/2025

Yohana 7 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²¹ Yesu akajibu, akawaambia, Mimi nalitenda kazi moja, nanyi nyote mnaistaajabia.
²² Musa aliwapa tohara; lakini si kwamba yatoka kwa Musa, bali kwa mababa; nanyi siku ya sabato humtahiri mtu.
²³ Basi ikiwa mtu hupashwa tohara siku ya sabato, ili torati ya Musa isije ikavunjika, mbona mnanikasirikia mimi kwa sababu nalimfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya sabato?
²⁴ Basi msihukumu hukumu ya macho tu, bali ifanyeni hukumu iliyo ya haki.

17/11/2025

Yeremia 9 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
²³ Bwana asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake;
²⁴ bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni Bwana, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana,
²⁵ Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapowaadhibu wote waliotahiriwa katika hali yao ya kutokutahiriwa;
²⁶ Misri, na Yuda, na Edomu, na wana wa Amoni, na Moabu, na wote wenye kunyoa denge, wakaao nyikani; maana mataifa hayo yote hawana tohara, wala nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa mioyo yao.

10/09/2025

1 Wathesalonike 1 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
³ Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.
⁴ Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu;
⁵ ya kwamba injili yetu haikuwafikia katika maneno tu, bali na katika nguvu, na katika Roho Mtakatifu, na uthibitifu mwingi; k**a vile mnavyojua jinsi zilivyokuwa tabia zetu kwenu, kwa ajili yenu.
⁶ Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu.
⁷ Hata mkawa kielelezo kwa watu wote waaminio katika Makedonia, na katika Akaya.
⁸ Maana kutoka kwenu neno la Mungu limevuma, si katika Makedonia na Akaya tu, ila na kila mahali imani yenu mliyo nayo kwa Mungu imeenea; hata hatuna haja sisi kunena lo lote.
⁹ Kwa kuwa wao wenyewe wanatangaza habari zetu, jinsi kulivyokuwa kuingia kwetu kwenu; na jinsi mlivyomgeukia Mungu mkaziacha sanamu, ili kumtumikia Mungu aliye hai, wa kweli;

10/09/2025

Waebrania 6 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁷ Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
⁸ bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
⁹ Lakini, wapenzi, ijapokuwa twanena hayo, katika habari zenu tumesadiki mambo yaliyo mazuri zaidi, na yaliyo na wokovu.
¹⁰ Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.
¹¹ Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho;

10/09/2025

Wagalatia 6 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁶ Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.
⁷ Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.
⁸ Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.
⁹ Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.
¹⁰ Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

10/09/2025

1 Wakorintho 9 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁴ Je! Hatuna uwezo wa kula na kunywa?
⁵ Hatuna uwezo kuchukua pamoja nasi mke aliye ndugu, k**a wao mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?
⁶ Au je! Ni mimi peke yangu na Barnaba tusio na uwezo wa kutokufanya kazi?
⁷ Ni askari gani aendaye vitani wakati wo wote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi?
⁸ Je! Ninanena hayo kwa kibinadamu? Au torati nayo haisemi yayo hayo?
⁹ Kwa maana katika torati ya Musa imeandikwa, Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Je! Hapo Mungu aangalia mambo ya ng'ombe?
¹⁰ Au yamkini anena hayo kwa ajili yetu? Naam, yaliandikwa kwa ajili yetu; kwa kuwa alimaye nafaka ni haki yake kulima kwa matumaini, naye apuraye nafaka ni haki yake kutumaini kupata sehemu yake.
¹¹ Ikiwa sisi tuliwapandia ninyi vitu vya rohoni, je! Ni neno kubwa tukivuna vitu vyenu vya mwilini?
¹² Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.
¹³ Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
¹⁴ Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili.

10/09/2025

1 Timotheo 5 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁷ Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.
¹⁸ Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake.
¹⁹ Usikubali mash*taka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.

Address

To Spread Gospel
Kilimani

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when God's Great Salvation ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share