25/07/2022
Je! Amri kuu ni ipi?
Amri zote kumi za Mungu kiuharisia ziko sahihi lakini ukizifuata kisheria zitakutia udini tu
Lengo kuu la Mungu ilikuwa ni kukombolewa kupitia amri hizi, amri zote za Mungu hufanyika rohoni tofauti na torati ukweli ni kwamba amri za Mungu ni nyingi Sana, lakini torati Mungu aliweka amri kuu kumi. Vipi hapo? Je, ni haki kushika amri kuu kumi tu? Hasha! hiwezi kuwa hivyo.
Nasema amri za Mungu ni nyingi tu kwamfano, kuna amri za talaka, kutoa zaka, kuhusu sadaka, utoaji, kusaidia yatima, wajane na maskini, kuhusu kufunga, kuhusu kuua, kunyanganya, uzinzi, viapo na kadhalika
Mpendwa unaonaje ukizifuata amri kumi tu na kuziacha zingine zote, mpendwa ukizifuata kwa muongozo wa Sheria hakika utaanguka maana biblia inasema katika kitabu cha wagalatia 3:10 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya Sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yalioandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye) soma WAEBRANIA 8:8-10 soma...
Basi amri kuu ni hii UPENDO na Yesu mwenyewe alisema katika mathayo 22:35-40 .35 mmoja wao, mwana sheria akamwuliza, akimjaribu. 36 mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?.37 Akamwambia , mpende Bwana Mungu wako Kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. 38 HII NDIYO AMRI ILIYO KUU TENA NI YA KWANZA 39 Na ya pili ya, yafanana nayo, nayo ni hii mpende jirani yako k**a nafsi yako. 40 katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii
UPENDO huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari, upendo haujivuni, haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake, hauoni uchungu , hauhesabu mabaya , haufurahii udhalimu, Bali hufurahi pamoja na kweli, upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote, palipo upendo hapana chuki, hapana wivu, hapana hasira, hapana vita, hapana uchawi, hapana masengenyo,hapana uadui, hapana ugomvi, hapana ukabira, hapana tamaa, hapana kujipenda, hapana kutelekezwa, hapana kesi,hapana uchoyo....
Nikihitimisha Yesu anasema katika kitabu cha YOHANA 14:15 mkinipenda, mtazishika amri zangu.
Mpendwa siri ni Yesu Kristo pekee mjue leo Kwa kutubu na kumaanisha kuziacha dhabi zako zote , kisha tafuta ubatizo sahihi, ambao ni ule wamaji tele na kwa jina la Yesu Kristo, na kujiunga na kanisa sahihi linalo ongozwa na Roho mtakatifu.