24/01/2024
WEWE YONA!
NINAWI UTAKWENDA AU UTAKIMBILIA TARSHISHI?
Kila mmoja wetu anao wito maalum tofauti na mwenzake hapa duniani; huyu hivi na yule vile. Huyu anatumwa NINAWI anaenda TARSHISHI kwa sababu kaona watu wengine wanaenda huko!
Tatizo la watu wengi kuishi kwenye matatizo, changamoto na shida zisizo koma au kukosa raha na furaha ya maisha hata k**a wana pesa, ni kwa sababu ya kuacha miito yao au makusudi ya wao kuja duniani na kukimbizana na majukumu ya watu wengine. Hili ni tatizo kubwa sana hususani hapa Afrika; watu wako kwenye Ofisi si zao. Ni kina Yona, yule wa kwenye Biblia. Wito wake ni kwenda NINAWI kuhubiri toba, yeye anakimbilia kwenye meli ya wafanyabishara kwenda TARSHISHI!
Baba ambaye anakimbia wito wake atatesa sana familia yake, mkewe na watoto wataishi kwenye shida, taabu na mateso kupita kawaida!
Mchungaji mmoja alinipigia simu kwa huzuni akiniambia "Mtu wa Mungu nisaidie mimi. Nina miaka 16 kwenye huduma mambo hayaendi kabisa, chakula shida na mahitaji mengine. Mke wangu kanikimbia, nisaidie, napitia majaribu makubwa sana. Nimefunga na kuomba, nimepakwa sana mafuta, lakini sioni mabadiliko, nataka niache huduma nirudi kijijini na familia maana hata umri unakwenda!"
Nilipokuja kumfuatilia kinyota nikagundua yeye ni 'born a leader' ambaye hakutakiwa kuwa muhubiri wa Injili Kanisani (Mchungaji) alitakiwa kuwa muhubiri wa Injili Serikalini na kwenye taasisi kwa sababu hatima yake na wito wake ulikuwa kufanya kazi za kiutawala!
Remember; Injili ni habari njema. Huyu pastor hakutakiwa kuwa Kanisani alitakiwa kuwa public figure kupitia Utawala Serikalini!
Ni Yona aliyeabiri meli kwenda TARSHISHI badala ya NINAWI!
Aliona wengine wanahubiri makanisani akapenda akaenda huko. Akakutana na Samaki mkubwa (nyangumi) akammeza!
Ndio maana anapitia yote anayoyapitia kwa miaka 16 mfurulizo kwenye kazi ya kichungaji!
Mwingine yuko Mbeya mjini.
Huyu alitakiwa kuwa Mwimbaji wa muziki akaenda kuanzisha Kanisa vijijini. Miaka zaidi ya 5 bila wafuasi!
Alipojitambua akabadili GIA angani akaanza kuimba Muziki wa Injili k**a basic call huku akichunga Kanisa.
Muda mchache baadaye akaanza kuona matokeo makubwa kupitia muziki. Akajenga, akanunua Prado, akajenga Kanisa lake, akapeleka watoto shule na wafuasi wakaanza kumfuata huko huko Kanisani kwake ili wasikilize nyimbo zake sio mahubiri wala mafundisho yake!
Truly, I tell you. Huyu Mchungaji Mwimbaji asingeshtuka, mpaka leo angekuwa pabaya sana. Life would have been very very hard and difficult.
Watu wengi ambao hawajashtuka, hawajajitambua, bado wanasota kwenye tumbo la nyangumi.
Wakijielewa nyangumi atawatapika, ili waende NINAWI kwenye wito wao.
Hakuna mtu anayeweza kutulia kwenye hii dunia bila kujua wito wake ni hupi. Wengi sana wanaangaika kutafuta pesa, hawapati na wanaopata wana presha, sukari, maradhi ya moyo na sonona, kwa sababu FEDHA SIO SULUHISHO kwa mtu aliyekumbia wito wake!
Mtu alitakiwa awe business man mzuri wa kusambaza maji mikoa mbalimbali na nje ya nchi, lakini cha ajabu yupo kwenye hema anaombea watu na kuwauzia maji!!!!
Ni Mfanyabishara aliyejivika joho la mtume au nabii!
A true prophet/ prophetess, never sell the so called 'spiritual commodities' ili apate hela. Wito wake haupo kwenye hela. Water selling prophets, oil selling apostles waacheni wanatafutia familia zao, sio wito wao ndio maana hawana raha pia.
Prophets of whom I know ni mountain men, ni watu wa faragha huko milimani; kula, kuvaa na kula bata town sio inshu zao hizo, nendeni mkafuatilie.
Nikisema hivyo utasikia watu wanang'aka "mbona tunapona?"
Mi sijasema hamponi, mnapona just because you believe!
Acha kuamini tuone k**a utapona!
Yote yawezekana kwake aaminiye. Wapo wanaopona kwa kwenda kwa waganga wakapiga manyanga na kuchezea tunguli wakaponywa.
Wapo wanaoponywa kwa kula mizizi, wengine kuchemsha majani ya miti fulani na wengine kwa kwenda hospitalini. Uongo???
Anyway, mada yetu ni YONA NA NINAWI, sio?
Tuendelee...
Ukigundua wito wako au kusudi lako la kuishi sio hicho unachojishughulisha nacho ujue umekosea, umeacha kwenda NINAWI umekimbilia TARSHISHI.
K**a huna raha na kazi yako hata k**a inakupa hela nzuri acha maana unapoteza muda, tafuta kujua kusudi lako maalum.
K**a unachofanya kinakupa amani, raha na furaha hata k**a hakikupi fedha nyingi komaa nacho maana ndio wito wako na mahitaji yako yote na ya familia yako yatapatikana humo humo.
Usiponielewa leo kesho ipo. Sio kila mtu ni fast learner. Wengine tuna vichwa ngumu, kuelewa haraka ni jaribu!
Somo litaendelea . . .
Ukitaka ushauri wowote wa masuala ya kiroho, inbox.!