15/07/2024
https://chat.whatsapp.com/Dqx0rEt7lznGyLWIgHDlHc
*NUKUU YA LEO!* Tarehe 15/07/2024. Jumatatu.
*Katika Ufunuo 3, tunasoma hili, kwamba Kanisa la Laodikia, tumechorwa mojawapo ya picha zenye huzuni kuliko picha zote za Biblia nzima, Ufunuo 3, kwenye Kanisa la Laodikia. Makanisa mengine yote, kupitia Wakati wa Luther, na Nyakati Saba za Kanisa, kila mmoja, haikuninii, kasema kuhusu Yesu kuwa ndani ya kanisa, “Yeye aliye ndani ya kanisa.” Lakini katika Laodikia, Yeye alikuwa nje, akibisha, akijaribu kurudi ndani. Ni kitu cha kusikitisha namna gani kuwazia, kwamba, “Mwana wa Mungu, akibisha katika kanisa Lake Mwenyewe, akijaribu kurudi ndani.”*
*Lakini utajiri wa ulimwengu huu umepofusha macho yao. Si tu tajiri wa pesa, bali tajiri katika umaarufu, tajiri katika mambo ya ulimwengu, mahangaiko ya maisha, mpaka mmechangamana, na watu wenye elimu wameingia ndani na kuondolea mbali hiyo Punje, ile—ile Lulu yenye thamani kubwa. Lakini Mungu aliwachagua watu kimbele kuwa huko; mtu fulani anaenda kuwepo huko. Bali wao wanaikataa Hiyo. Si wote watakaofanya hivyo; baadhi yao wataipokea Hiyo. Sasa walimweka nje ya upendo wao, upendo wao wa Neno Lake.*
63-1116B - Uwekezaji
Rev. William Marrion Branham
________________________
*MKATE WA KILA SIKU*
_Wamtumainio Bwana ni k**a mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele._
*_Zaburi 125:1_*